Mkanganyiko katika zoezi la sensa ni mavuno ya mbegu yaudini walioipanda CCM kwa manufaa yao bila kufiri matokeo yake MUNGU IBARIKI TANZANIA.Nadhani ni wakati muafaka wa kufikiri jinsi ya kuchukua hatua za kisheria juu ya hili jambo, kwani hapa ni sawa na kuwajengea chuki wananchi wenzao wa kabila la Kichaga. Kiasi kikubwa inaonekana kama Wachaga hawana haki vile ndani ya nchi hii. Unapochukua sulala la kisiasa na kulibandika juu ya kabila fulani, ni kutowatendea haki wanachi wa kabila husika.
Hii mbegu inayopandwa ni mbaya sana, na sijui itakapokutoa maua na punje hali itakuwa je! Lazima tupinge hii kwa nguvu zetu zote!
merci...
Leo tarehe 29.08.2012 niko hapa maeneo ya Lumumba Kariakoo , kuna rafiki yangu alinialika mlo wa mchana katika moja ya migahawa ya hapa Lumumba na kuwa kwangu hapa niomekutana na tukio ambalo nimeamua niliweke hadharani kabla halijatokea kwani naamini kabisa kuwa lengo la mpango huu ni kuendelea kutugawa taifa kwa misingi ya Ukabila jambo ambalo sikubaliani nalo kama ambavyo ninapinga kugawa watanzania kwa misingi ya udini .
Mwigulu Nchemba , juzi jumatatu amechapisha tisheti zenye maandishi ya M4C na ameweka maana kwenye hizo tisheti ambazo bado hazijaanza kugawanywa kuwa ni Movement 4 Chagga na ameweka maandishi makubwa kuwa changia Movement 4 Chagga (M4C), Zipo na zitaanza kugawanywa muda wowote .
Zoezi hili linaendena sambamba na operation ya Mwigulu ya kwenda Igunga eti kuelezea nini kilitokea mahakamani kwa wana Igunga , ziara hii imepangwa kuanza siku ya Jumamosi kwani alikuwa anasubiria FUSSO waliyonunua kwa shilingi milioni arobaini na tisa (49,000,000) na kuitengeneza kama za CDM ikamilike na walinunua vifaa Mlimani City tayari tangu wiki iliyopita.
Lengo la kuweka hapa ni kuwajulisha CDM wajue kuwa kuna mipango hiyo tayari imepangwa na inaendelea kutekelezwa , chukueni hatua .Aidha kuna vijana wenu watatu majina leo nayahifadhi wanafanya vikao vingi sana na Mwigulu na wa mwisho alipofika kwake wiki iliyopita alipewa shilingi laki nane , mara ya kwanza alipewa shilingi milioni tatu na huyu ametangaza rasmi kuwa atajiunga na CCM wakati wowote fuatilieni waliogombea Bavicha na kushindwa na hata mmoja aliweza kushinda ila anawahujumu nyie CDM.
Sikubaliani na mipango ya kuligawa taifa kwa misingi ya Udini na Ukabila hivyo nitaipinga sana hata kama mtanijua LIWALO NA LIWE.
NI MIMI MPIGA FILIMBI-
Mwigulu amekosea tu hiyo ni m4c maana yake no movement for catholic.
Mwigulu amekosea tu hiyo ni m4c maana yake no movement for catholic.
mbona sera za CDM muhashamu mapengo anazisapoti sana? kunani?Akili yako imeingiliwa na kile ilichokalia. Hebu rudi kawaida kwanza. Watanzania hawataki akili yenye mawazo ya kizushi, kizandikikichochezi, kichonganishi na mufilisi kama haya.
nakubalia na wewe ubaguzi haufai, lkn hayo yanatakiwa yaonekane kivitendo na sio kimaneno tu, nikuulize mbona cdm inamzonga sana zitto na sio Lissu, Mbowe, solaha, Mnyika au wengine wowote wale, ukinipa jibu kweli nitajua wewe unapinga ubaguzi vinginevyo utakuwa mnafiki. na tunakupotezea tu.UOMBEWE, kinachokusumbua ni PEPO TU: ukimuona SHEIKH ISSAH P utasaidiwa anaondoa mapepo na majini pia, na hata ukifika kwa MWINGILA nako utaombewa. ZINGATIA USHAURI ... kwani nchi hii ni yetu sote, tusibaguane
<br><br>Turudi nyuma na kukumbuka haya. Naona Mwigulu Nchemba Naibu Katibu Mkuu wa CCM naye ameingia kuchangia, anaweza kuingia hapa na kujibu pia maswali yanayomhusu?<br><br>PM<br>Naanza kuunganisha dots kuanzia matamshi ya juzi ya Nape na Wasira kuhusu CDM na tuhuma hizi kwa Mwigulu na vurugu za Polisi ktk mikutano ya CDM ktk mikoa ya Morogoro na Iringa. Kuna mchangiaji mmoja jana amedai mauaji na vurugu za Polisi ktk mikutano ya CDM inaratibiwa na Wasira na Mwingulu. Kwamba ndiyo wanaowashinikiza wakuu wa Polisi kuhakikisha mikutano ya CDM inahujumiwa.