Mwambie jamaa akulipe fedha ulizoomba mkeweNilikaza kuwa Sitembei na mkewe!!na kikao kikafanyika cha kutusuluhisha....Nyumba za wapangaji wengi ni nux tu...
Mwambie jamaa akulipe fedha ulizoomba mkeweNilikaza kuwa Sitembei na mkewe!!na kikao kikafanyika cha kutusuluhisha....Nyumba za wapangaji wengi ni nux tu...
Kaa mbali na huyo bidada,hata kama huna nia ya kula mzigo,Mumewe atakushuku tu,imeanzia kukopeshana pesa,itafika point huyo dada ataanza kukusimulia mambo yake,na Mumewe,zile siri za ndani zinazohusu Hari ya kipesa,na mateso anayopata,kabla hujashituka utaanza kumwachia pesa,Ili apike,dogo ale vzr,ikifika hapo Ngosha,unatafuta balaa la kupigwa panga,Kuna familia moja tumepanga wote ni vijana tu wana kama miaka 24 25 hivi wana mtoto mmoja ni familia yenye uchumi wa chini sana hii imefanya mtoto wao wa umri wa miaka kama mitatu hivi kua ana mendea chai kila siku asubuhi mida ya chai yupo kwangu
So hio ikafanya tukazoeana na mama yake. Maana mara nyingi mtoto wao anashinda kwangu, mumewe sina mazoea nae saana zaidi ya salam tu
Juzi kati hivi mida ya jioni huyu dada aliniita na akaomba nimkopeshe buku 5 me nikampa muda huo tunazungumza mume akawa kalejea home akakuta tunazungumza pale akapitiliza ndani bila salam
Kesho yake nikaja kuambiwa na mpangaji mwingine kua huyu dada alienikopa pesa alipigwa na mumewe, so moja kwa moja nikaunganisha dots
Nikaona ngoja nipunguze mazoea na huyu dada ijapokua ni mtu wa vimizinga mizinga sana
Baadae huyu kaka akawa anampiga mwanae akija kula kwangu but dogo hasikii akiamka tu huyu hapa so na sipendi kutia doa ndoa yao mda mwingine naweza kumpa chakula nikatoka nikakuta akabeba akaenda kulia kwao, na kiukweli hii familia msosi ni wa tabu,
Nakua na kamuunganiko fulani hivi jambo ambalo naliiona si zuri je niwe nafukuza huyu dogo ili nikate connection au nifanyaje?
Kaa mbali na familia ya mnyonge
Ulimkaza!Acha mazoea kabisa na wake za watu...mimi yalinikuta sakata Kama ilo mume alimbana mkewe(kwa kipigo heavy) aseme kweli kuwa nimemtongoza na mke naye akasupport kuwa nilikuwa namtongoza kweli. Mbona ugomvi mkubwa uliibuka! timbwili sio la nchi hii!! aah sema nikakaza
Kweli, naunga mkono hojaHuwezi kuhama kisa hiyo familia. Vizia siku huyo mume wake anatoka mfate muongee kiume, mwambie ukweli, utahama hadi lini