Mpangaji anahesabika ni mvamizi mara tu kodi yake inapoisha

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,308
5,460
Tarehe 5/10/2022 majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa kupitia Rufaa Na. 333/2019 kati ya Lawrence Magesa t/a Jopen pharmacy VS Fatuma Omary na Rimina Auction Mart wamesema kuwa pale mpangaji kodi yake inapoisha na akawa hajaondoka katika nyumba ama eneo la pango, basi hadhi yake inabadilika na anakuwa mvamizi(trespasser).

Kwa sheria zetu mvamizi anaweza kuondolewa ndani nyumba/eneo kwa nguvu yeye na mali zake bila hata kuhitaji notisi.

Na akiondolewa kwa nguvu yeye na mali zake hawezi kudai fidia ikiwemo ile ya kwamba nilikuwa na milioni 10 zangu ndani wakati naondolewa zimepotea.

Hukumu hii inasema hawezi kudai kwasababu kuendelea kwake kuwemo ndani wakati kodi yake imeisha ni makosa na hivyo hawezi kuwa mnufaika wa makosa yake mwenyewe(benefit from own wrongs).

Na huu ndio msimamo wa sheria hata kabla ya hukumu hii. Wapangaji wajifunze kuwa wapole kodi zao zinapokuwa zimeisha. Kodi inapoisha unapoteza haki za upangaji.

Kuhusu notisi ya kuondoka, mpangaji ambaye kodi yake imeisha hapewi notisi isipokuwa kama mkataba wake unasema hivyo.

Kama hausemi hivyo basi kodi ikiisha ni kuondoka, ama kuondolewa kwa nguvu, ama kuomba vinginevyo kutoka kwa mwenye nyumba/eneo.

Mahakama ya rufaa ndiyo mahakama kubwa na ya juu kuliko zote Tanzania, na ndiyo inaongea maneno haya.

Mwisho nasisitiza, ile habari ya kuondolewa kwa nguvu ukitegemea utasema milioni 10 yangu iliyokuwa kabatini nayo imepotea sahau. Ni maneno ya mitaani hayo achana nayo yatakupotezea muda.

Huwezi lipwa, kwani tangu kodi yako ilipoisha ulikuwa mvamizi na mvamizi halipwi manufaa na stahiki kama hizo.

Andiko la:
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255714047241
 
Ahsante kwa mada nzuri mkuu JanguKamaJangu na Mwanasheria Bashir Yakub

Kwenye mada umeeleza suala la notisi ya kuondoka,
"Kuhusu notisi ya kuondoka, mpangaji ambaye kodi yake imeisha hapewi notisi isipokuwa kama mkataba wake unasema hivyo."

Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 inasema tofauti na kilichoelezwa hapo juu

Kisheria, in absence of an express term in the contract, the law has provided implied terms which binds
the parties and applies in the same way as express terms.


Kifungu Na. 88 (2) (b) kinasema kuwa,

"There shall be implied In every lease covenants by the lessor with the lessee empowering the lessor to terminate the lease by serving a notice of intention to terminate the lease on the lessee where any rent is unpaid for one month after the due date for payment whether or not a demand in writing for payment has been made by lessor or an agent of the lessor."

Hivyo, inamaanisha kuwa hata kama mkataba usipoeleza suala la kupewa notisi, bado kupewa notisi ni "implied term" (ni lazima notisi itolewe)

Nimeambatanisha na Kesi ya Rufaa Na. 153 ya mwaka 2018 kati ya Abraham Migeto (Appelant) vs Issa Rajabu (Respondent)

Kesi hii iliamuliwa mwaka 2020 na Jaji M. P. Opiyo kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania (Land Division)

Nawasilisha
 

Attachments

  • Case 8 Lease conflict.pdf
    162.9 KB · Views: 60
Na huu ndio msimamo wa sheria hata kabla ya hukumu hii. Wapangaji wajifunze kuwa wapole kodi zao zinapokuwa zimeisha. Kodi inapoisha unapoteza haki za upangaji

Mwisho nasisitiza, ile habari ya kuondolewa kwa nguvu ukitegemea utasema milioni 10 yangu iliyokuwa kabatini nayo imepotea sahau. Ni maneno ya mitaani hayo achana nayo yatakupotezea muda.
Una mpangaji hajakulipa?
Naona umekuwa mkali kupitiliza
 
Ahsante kwa mada nzuri mkuu JanguKamaJangu na Mwanasheria Bashir Yakub

Kwenye mada umeeleza suala la notisi ya kuondoka,
"Kuhusu notisi ya kuondoka, mpangaji ambaye kodi yake imeisha hapewi notisi isipokuwa kama mkataba wake unasema hivyo."

Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 inasema tofauti na kilichoelezwa hapo juu

Kisheria, in absence of an express term in the contract, the law has provided implied terms which binds
the parties and applies in the same way as express terms.


Kifungu Na. 88 (2) (b) kinasema kuwa,

"There shall be implied In every lease covenants by the lessor with the lessee empowering the lessor to terminate the lease by serving a notice of intention to terminate the lease on the lessee where any rent is unpaid for one month after the due date for payment whether or not a demand in writing for payment has been made by lessor or an agent of the lessor."

Hivyo, inamaanisha kuwa hata kama mkataba usipoeleza suala la kupewa notisi, bado kupewa notisi ni "implied term" (ni lazima notisi itolewe)

Nimeambatanisha na Kesi ya Rufaa Na. 153 ya mwaka 2018 kati ya Abraham Migeto (Appelant) vs Issa Rajabu (Respondent)

Kesi hii iliamuliwa mwaka 2020 na Jaji M. P. Opiyo kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania (Land Division)

Nawasilisha
Kwenye hayo maelezo, imesemwa mwenye nyumba (lessor) anaweza kusitisha mkataba kwa notisi.
Sasa mpangaji ambae Kodi yake Imeisha kimsingi mkataba wake umefikia mwisho, hivyo hakuna haja ya mwenye nyumba kutoa notisi ili aondoke.
 
Kwenye hayo maelezo, imesemwa mwenye nyumba (lessor) anaweza kusitisha mkataba kwa notisi.
Sasa mpangaji ambae Kodi yake Imeisha kimsingi mkataba wake umefikia mwisho, hivyo hakuna haja ya mwenye nyumba kutoa notisi ili aondoke.
Upo sahihi mkuu

Ila pia maelezo yamesema kuwa notisi ni mwezi mmoja baada ya tarehe iliyopaswa kulipwa pesa ya pango

"...where any rent is unpaid for one month after the due date for payment"

Kwa uzoefu, NHC huwa wana huo utaratibu wa notisi

Pia tukumbuke kuwa muongozo huo ni kutoka kwenye Sheria Mama kuhusu mambo ya Ardhi nchini Tanzania

My Take:
Wakitaka mabadiliko hayo (yaliyoletwa kutokana na maamuzi ya kesi) yawe na athari basi kuwe na mabadiliko pia kwenye kifungu namba 88(2)(b) cha Sheria Mama ya Ardhi (Land Act No. 4 Cap 113 of 1999)
 
Tarehe 5/10/2022 majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa kupitia Rufaa Na. 333/2019 kati ya Lawrence Magesa t/a Jopen pharmacy VS Fatuma Omary na Rimina Auction Mart wamesema kuwa pale mpangaji kodi yake inapoisha na akawa hajaondoka katika nyumba ama eneo la pango, basi hadhi yake inabadilika na anakuwa mvamizi(trespasser).

Kwa sheria zetu mvamizi anaweza kuondolewa ndani nyumba/eneo kwa nguvu yeye na mali zake bila hata kuhitaji notisi.

Na akiondolewa kwa nguvu yeye na mali zake hawezi kudai fidia ikiwemo ile ya kwamba nilikuwa na milioni 10 zangu ndani wakati naondolewa zimepotea.

Hukumu hii inasema hawezi kudai kwasababu kuendelea kwake kuwemo ndani wakati kodi yake imeisha ni makosa na hivyo hawezi kuwa mnufaika wa makosa yake mwenyewe(benefit from own wrongs).

Na huu ndio msimamo wa sheria hata kabla ya hukumu hii. Wapangaji wajifunze kuwa wapole kodi zao zinapokuwa zimeisha. Kodi inapoisha unapoteza haki za upangaji.

Kuhusu notisi ya kuondoka, mpangaji ambaye kodi yake imeisha hapewi notisi isipokuwa kama mkataba wake unasema hivyo.

Kama hausemi hivyo basi kodi ikiisha ni kuondoka, ama kuondolewa kwa nguvu, ama kuomba vinginevyo kutoka kwa mwenye nyumba/eneo.

Mahakama ya rufaa ndiyo mahakama kubwa na ya juu kuliko zote Tanzania, na ndiyo inaongea maneno haya.

Mwisho nasisitiza, ile habari ya kuondolewa kwa nguvu ukitegemea utasema milioni 10 yangu iliyokuwa kabatini nayo imepotea sahau. Ni maneno ya mitaani hayo achana nayo yatakupotezea muda.

Huwezi lipwa, kwani tangu kodi yako ilipoisha ulikuwa mvamizi na mvamizi halipwi manufaa na stahiki kama hizo.

Andiko la:
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255714047241
dah mkuu anawaamsha waliyolala!!.
 
Upo sahihi mkuu

Ila pia maelezo yamesema kuwa notisi ni mwezi mmoja baada ya tarehe iliyopaswa kulipwa pesa ya pango

"...where any rent is unpaid for one month after the due date for payment"

Kwa uzoefu, NHC huwa wana huo utaratibu wa notisi

Pia tukumbuke kuwa muongozo huo ni kutoka kwenye Sheria Mama kuhusu mambo ya Ardhi nchini Tanzania

My Take:
Wakitaka mabadiliko hayo (yaliyoletwa kutokana na maamuzi ya kesi) yawe na athari basi kuwe na mabadiliko pia kwenye kifungu namba 88(2)(b) cha Sheria Mama ya Ardhi (Land Act No. 4 Cap 113 of 1999)
Kwahio kimsingi sheria inasema kua mpangaji anatakiwa apewe notice isyo pungua mwezi mmoja na mmiliki wa jengo ili aondoke na hakuna kitu chochote mwenye nyumba anacho weza kufanya kumtoa huyo mpangaji kwenye nyumba yake kabla ya huo muda kufika au ni mimi ndio nimeshindwa kuelewa mkuu?
 
Ahsante kwa mada nzuri mkuu JanguKamaJangu na Mwanasheria Bashir Yakub

Kwenye mada umeeleza suala la notisi ya kuondoka,
"Kuhusu notisi ya kuondoka, mpangaji ambaye kodi yake imeisha hapewi notisi isipokuwa kama mkataba wake unasema hivyo."

Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 inasema tofauti na kilichoelezwa hapo juu

Kisheria, in absence of an express term in the contract, the law has provided implied terms which binds
the parties and applies in the same way as express terms.


Kifungu Na. 88 (2) (b) kinasema kuwa,

"There shall be implied In every lease covenants by the lessor with the lessee empowering the lessor to terminate the lease by serving a notice of intention to terminate the lease on the lessee where any rent is unpaid for one month after the due date for payment whether or not a demand in writing for payment has been made by lessor or an agent of the lessor."

Hivyo, inamaanisha kuwa hata kama mkataba usipoeleza suala la kupewa notisi, bado kupewa notisi ni "implied term" (ni lazima notisi itolewe)

Nimeambatanisha na Kesi ya Rufaa Na. 153 ya mwaka 2018 kati ya Abraham Migeto (Appelant) vs Issa Rajabu (Respondent)

Kesi hii iliamuliwa mwaka 2020 na Jaji M. P. Opiyo kutoka Mahakama Kuu ya Tanzania (Land Division)

Nawasilisha
Haya Sasa,
wataalam wa sheria uwanja Ni wenu
 
Kwahio kimsingi sheria inasema kua mpangaji anatakiwa apewe notice isyo pungua mwezi mmoja na mmiliki wa jengo ili aondoke na hakuna kitu chochote mwenye nyumba anacho weza kufanya kumtoa huyo mpangaji kwenye nyumba yake kabla ya huo muda kufika au ni mimi ndio nimeshindwa kuelewa mkuu?
"Kimsingi sheria inasema kua mpangaji anatakiwa apewe notice isyo pungua mwezi mmoja na mmiliki wa jengo ili aondoke na hakuna kitu chochote mwenye nyumba anacho weza kufanya kumtoa huyo mpangaji kwenye nyumba yake kabla ya huo muda kufika"

Umeelewa mkuu sheria ndio inasema hivyo

Kuna kesi iliwahi kutokea, mwenye nyumba alimtoa kwa nguvu mpangaji
Mpangaji akashtaki, akashinda kesi

Mwenye nyumba alikata rufaa hadi mahakama kuu, lakini bado alishindwa kesi

Hivyo, ni jambo ambalo lipo kisheria kwenye sheria kuu ya Ardhi nchini Tanzania
 
"Kimsingi sheria inasema kua mpangaji anatakiwa apewe notice isyo pungua mwezi mmoja na mmiliki wa jengo ili aondoke na hakuna kitu chochote mwenye nyumba anacho weza kufanya kumtoa huyo mpangaji kwenye nyumba yake kabla ya huo muda kufika"

Umeelewa mkuu sheria ndio inasema hivyo

Kuna kesi iliwahi kutokea, mwenye nyumba alimtoa kwa nguvu mpangaji
Mpangaji akashtaki, akashinda kesi

Mwenye nyumba alikata rufaa hadi mahakama kuu, lakini bado alishindwa kesi

Hivyo, ni jambo ambalo lipo kisheria kwenye sheria kuu ya Ardhi nchini Tanzania

Naomba kueleweshwa hapo hyo notisi inamuhusu mpangaji ambaye kodi yake imeisha ama vip
 
Upo sahihi mkuu

Ila pia maelezo yamesema kuwa notisi ni mwezi mmoja baada ya tarehe iliyopaswa kulipwa pesa ya pango

"...where any rent is unpaid for one month after the due date for payment"

Kwa uzoefu, NHC huwa wana huo utaratibu wa notisi

Pia tukumbuke kuwa muongozo huo ni kutoka kwenye Sheria Mama kuhusu mambo ya Ardhi nchini Tanzania

My Take:
Wakitaka mabadiliko hayo (yaliyoletwa kutokana na maamuzi ya kesi) yawe na athari basi kuwe na mabadiliko pia kwenye kifungu namba 88(2)(b) cha Sheria Mama ya Ardhi (Land Act No. 4 Cap 113 of 1999)
Due date inatoka wapi wakati hakuna mkataba? Based on what? Mkataba ukiisha mpangaji hapaswi kulipa kodi yoyote bila mkataba mpya. Anajua atalipa kiasi gani ? Nahisi mikataba ya NHC haina end date ndio maana lazima watoe notisi.
 
Kwa maelezo haya, je unaweza kumfungulia mashitaka kwa kosa la criminal tresspass mpangaji aliyepitiliza muda wake baada ya notice ya kusitishwa upangishwaji wake kutolewa na yeye kukaidi kuondoka kwa wakati (kuendelea kukaa kwa mabavu) kituo cha polisi?
 
Back
Top Bottom