JanguKamaJangu
JF-Expert Member
- Feb 7, 2022
- 2,308
- 5,460
Tarehe 5/10/2022 majaji watatu wa Mahakama ya Rufaa kupitia Rufaa Na. 333/2019 kati ya Lawrence Magesa t/a Jopen pharmacy VS Fatuma Omary na Rimina Auction Mart wamesema kuwa pale mpangaji kodi yake inapoisha na akawa hajaondoka katika nyumba ama eneo la pango, basi hadhi yake inabadilika na anakuwa mvamizi(trespasser).
Kwa sheria zetu mvamizi anaweza kuondolewa ndani nyumba/eneo kwa nguvu yeye na mali zake bila hata kuhitaji notisi.
Na akiondolewa kwa nguvu yeye na mali zake hawezi kudai fidia ikiwemo ile ya kwamba nilikuwa na milioni 10 zangu ndani wakati naondolewa zimepotea.
Hukumu hii inasema hawezi kudai kwasababu kuendelea kwake kuwemo ndani wakati kodi yake imeisha ni makosa na hivyo hawezi kuwa mnufaika wa makosa yake mwenyewe(benefit from own wrongs).
Na huu ndio msimamo wa sheria hata kabla ya hukumu hii. Wapangaji wajifunze kuwa wapole kodi zao zinapokuwa zimeisha. Kodi inapoisha unapoteza haki za upangaji.
Kuhusu notisi ya kuondoka, mpangaji ambaye kodi yake imeisha hapewi notisi isipokuwa kama mkataba wake unasema hivyo.
Kama hausemi hivyo basi kodi ikiisha ni kuondoka, ama kuondolewa kwa nguvu, ama kuomba vinginevyo kutoka kwa mwenye nyumba/eneo.
Mahakama ya rufaa ndiyo mahakama kubwa na ya juu kuliko zote Tanzania, na ndiyo inaongea maneno haya.
Mwisho nasisitiza, ile habari ya kuondolewa kwa nguvu ukitegemea utasema milioni 10 yangu iliyokuwa kabatini nayo imepotea sahau. Ni maneno ya mitaani hayo achana nayo yatakupotezea muda.
Huwezi lipwa, kwani tangu kodi yako ilipoisha ulikuwa mvamizi na mvamizi halipwi manufaa na stahiki kama hizo.
Andiko la:
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255714047241
Kwa sheria zetu mvamizi anaweza kuondolewa ndani nyumba/eneo kwa nguvu yeye na mali zake bila hata kuhitaji notisi.
Na akiondolewa kwa nguvu yeye na mali zake hawezi kudai fidia ikiwemo ile ya kwamba nilikuwa na milioni 10 zangu ndani wakati naondolewa zimepotea.
Hukumu hii inasema hawezi kudai kwasababu kuendelea kwake kuwemo ndani wakati kodi yake imeisha ni makosa na hivyo hawezi kuwa mnufaika wa makosa yake mwenyewe(benefit from own wrongs).
Na huu ndio msimamo wa sheria hata kabla ya hukumu hii. Wapangaji wajifunze kuwa wapole kodi zao zinapokuwa zimeisha. Kodi inapoisha unapoteza haki za upangaji.
Kuhusu notisi ya kuondoka, mpangaji ambaye kodi yake imeisha hapewi notisi isipokuwa kama mkataba wake unasema hivyo.
Kama hausemi hivyo basi kodi ikiisha ni kuondoka, ama kuondolewa kwa nguvu, ama kuomba vinginevyo kutoka kwa mwenye nyumba/eneo.
Mahakama ya rufaa ndiyo mahakama kubwa na ya juu kuliko zote Tanzania, na ndiyo inaongea maneno haya.
Mwisho nasisitiza, ile habari ya kuondolewa kwa nguvu ukitegemea utasema milioni 10 yangu iliyokuwa kabatini nayo imepotea sahau. Ni maneno ya mitaani hayo achana nayo yatakupotezea muda.
Huwezi lipwa, kwani tangu kodi yako ilipoisha ulikuwa mvamizi na mvamizi halipwi manufaa na stahiki kama hizo.
Andiko la:
Na Bashir Yakub, WAKILI
+255714047241