Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 106,832
- 189,747
Katika Muendelezo wa Mikutano ya hadhara inayoendelea kwenye Oparesheni 255 ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) , ambayo sasa imeingia kwenye Mkoa wa Katavi, Tundu Lissu ameyataja mapungufu ya Maridhiano hadi sasa.
Akizungumza kwa kujiamini mbele ya Maelfu ya wananchi Lissu amesema kwamba , maana halisi ya maridhiano ni kuhakikisha kwamba Makandokando ya awali yaliyotokana na utawala wa kikatili wa awamu ya 5 yanaondolewa na kuanza ukurasa mpya.
Bali anashangazwa na kitendo cha washirika wa makandokando hayo kuendelea kupewa vyeo tena katikati ya naridhiano , Amemtaja IGP Camillius Wambura kama mpishi mkuu wa kesi zote za uongo zilizomkabili yeye mwenyewe , ambazo zimetupiliwa mbali mahakamani , anadai hakuna asiyejua upishi wa kesi za uongo wa Wambura , lakini aliteuliwa IGP
Tundu Lissu amefunguka kwamba Byakanwa ndiye aliyeharibu miundo mbinu ya Shamba la Kisasa la Freeman Mbowe , baada ya hapo akala shavu na kuwa RC wa Mtwara , na sasa ameteuliwa Balozi .
Lissu Amemtaja Ramadhan Kingai kama Mhalifu aliyetunga kila uongo kwenye kesi ya Ugaidi wa uongo iliyomkabili Mbowe, hata baada ya kesi hiyo kutupiliwa mbali Kingai akapandishwa Cheo , Lissu amedai kwamba katika wahalifu wa awamu ya 5 ni Sabaya Pekee aliyejaribu kushughulikiwa.
Tundu Lissu amependekeza Maridhiano ni lazima kweli yazingatie kuondoa matatizo pamoja na walioyaleta .
Akizungumza kwa kujiamini mbele ya Maelfu ya wananchi Lissu amesema kwamba , maana halisi ya maridhiano ni kuhakikisha kwamba Makandokando ya awali yaliyotokana na utawala wa kikatili wa awamu ya 5 yanaondolewa na kuanza ukurasa mpya.
Bali anashangazwa na kitendo cha washirika wa makandokando hayo kuendelea kupewa vyeo tena katikati ya naridhiano , Amemtaja IGP Camillius Wambura kama mpishi mkuu wa kesi zote za uongo zilizomkabili yeye mwenyewe , ambazo zimetupiliwa mbali mahakamani , anadai hakuna asiyejua upishi wa kesi za uongo wa Wambura , lakini aliteuliwa IGP
Tundu Lissu amefunguka kwamba Byakanwa ndiye aliyeharibu miundo mbinu ya Shamba la Kisasa la Freeman Mbowe , baada ya hapo akala shavu na kuwa RC wa Mtwara , na sasa ameteuliwa Balozi .
Lissu Amemtaja Ramadhan Kingai kama Mhalifu aliyetunga kila uongo kwenye kesi ya Ugaidi wa uongo iliyomkabili Mbowe, hata baada ya kesi hiyo kutupiliwa mbali Kingai akapandishwa Cheo , Lissu amedai kwamba katika wahalifu wa awamu ya 5 ni Sabaya Pekee aliyejaribu kushughulikiwa.
Tundu Lissu amependekeza Maridhiano ni lazima kweli yazingatie kuondoa matatizo pamoja na walioyaleta .