Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,480
- 30,152
Nimemsikiliza kwa makini Rais Samia Suluhu Hassan, akimpa "za uso" Spika Ndugai, kuhusu kile alichotufunulia ni kuwa ni mbio za Urais wa 2025, angalau kimebatizwa jina na hao mahasimu wake kuwa ni deni la Taifa linalohatarisha usalama wa nchi yetu kupigwa mnada.
Hoja pekee na ya nguvu niliyoisikia, ni pale aliposema kuwa mara tu baada ya kuapishwa kuwa Rais, alitembelewa na mtu mzito Sana wa CCM na kumnong'oneza kuwa Hongera zake na Pole nyingi.
Huyo mtu mzito akamfafanulia kuwa Hongera hiyo na Pole, ina maana kubwa, kuwa Kazi aliyonayo mbele ni ngumu Sana, kwa kuwa adui zake wa dhati, watakuwa ni wa upande wake wa kijani wenzie na wala siyo viongozi wa vyama vya upinzani!
Leo Mama katufafanulia kuwa ame-realize kuwa alichoambiwa na huyo mwanaccm mwenzie ni ya kweli kabisa na ndiyo yanayoendelea hivi sasa ndani ya CCM yake.
Ninachokiona Mimi ni kuwa mpambano huu mkali ambao kama nchi hatujawahi kuushuhudia, wa vita vya wenyewe kwa wenyewe maccm watupu, utawapa unafuu mkubwa na kupumua wa kuendesha shughuli zao za kisiasa, baada ya mateso makubwa ya muda mrefu, kwa vyama vya upinzani.
Hoja pekee na ya nguvu niliyoisikia, ni pale aliposema kuwa mara tu baada ya kuapishwa kuwa Rais, alitembelewa na mtu mzito Sana wa CCM na kumnong'oneza kuwa Hongera zake na Pole nyingi.
Huyo mtu mzito akamfafanulia kuwa Hongera hiyo na Pole, ina maana kubwa, kuwa Kazi aliyonayo mbele ni ngumu Sana, kwa kuwa adui zake wa dhati, watakuwa ni wa upande wake wa kijani wenzie na wala siyo viongozi wa vyama vya upinzani!
Leo Mama katufafanulia kuwa ame-realize kuwa alichoambiwa na huyo mwanaccm mwenzie ni ya kweli kabisa na ndiyo yanayoendelea hivi sasa ndani ya CCM yake.
Ninachokiona Mimi ni kuwa mpambano huu mkali ambao kama nchi hatujawahi kuushuhudia, wa vita vya wenyewe kwa wenyewe maccm watupu, utawapa unafuu mkubwa na kupumua wa kuendesha shughuli zao za kisiasa, baada ya mateso makubwa ya muda mrefu, kwa vyama vya upinzani.