Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,427
- 154,271
Hivi sasa wanandoa wa Marekani hawako tayari tena kujiapiza kwamba, wataishi na mume hadi kifo kije kiwatengenishe. Badala yake, wengi hutaka kujiapiza kwa kusema, "tutaishi kwa shida na raha, uzima na maradhi, kama tu penzi litaendelea kuwepo."
Kwa sababu maandiko ya dini ya Kikristo kwa mfano, hayawezi kubadilishwa katika jambo kama hilo, wanandoa wengi wameamua kutofunga ndoa zao kanisani na badala yake hufungia mahali pengine.Hii ni ili kukwepa kutamka kwamba, wataishi hadi kifo kiwatenge, wakati wanaona kabisa watu wengi wamechanganyikiwa na hawajui tena maana ya kupenda.
Kila bibi harusi anaogopa kujiapiza kwa kauli hizo zenye kumfunga. Inaelezwa kwamba, woga huo unatokana na kile kinachoonekana majumbani, kwamba, ndoa nyingi hazina kuaminiana na zinatisha kwa visa na mikasa. Inaelezwa na watu wanaopenda kuyachukulia mambo kimkabala na mila na desturi kwamba, utaratibu huu mpya wa kukwepa kusema, "hadi kifo kitutenge," wakati wakufunga ndoa na badala yake kusema kitu kama, "naahidi kuwa mwaminifu kwako, kama tu penzi bado lipo," huenda utadhoofisha ndoa nyingi.Raisi wa Muungano wa Makanisa Katoliki na haki za binadamu, William Donahue, amesema, kubadili kiapo hicho na kusema, "kama tu penzi litaendelea kuwepo," ni sawa na kuweka masharti kupenda, jambo ambalo litafanya kupenda kupoteze maana yake ya asili. Amesema kupenda hakuwezi kuwekewa masharti. Kiongozi wa utafiti huu Mary Jo Gallegos amesema, kwa hivi sasa ambapo watu wa mila na imani mbalimbali wanakutana na kuoana, mambo ya kuambiana hadi kifo kitutenge, hayawezi kuwa na nguvu.Mama huyo ameendelea kusema, hakumbuki kwa mara ya mwisho ni lini alimsikia mwanamke mwenye kufunga ndoa, akiahidi kwamba, atampenda mumewe hadi kifo kije kiwatenge.
Anazidi kusema, hakuna jambo kama hilo kwa sababu, wengi wamegundua kwamba, huko ni kujitwisha mzigo ambao mtu hawezi kuubeba.Amezidi kusema kwamba, watu wengi sasa wanaiona hali halisi na wanajua ukweli mkubwa zaidi katika ndoa. Amesema wale walio kwenye ndoa ya pili au ya tatu, wanajua ukweli mkubwa zaidi kuliko wale walio kwenye ndoa ya kwanza au ambao hawajaingia kwenye ndoa kabisa. Jambo la maana anasema, ni kwa wanandoa wote kuamini kwamba, wataishi kwa amani hadi kufa, lakini wakijua lolote linaweza
kutokea.
Huko Marekani, nusu ya ndoa huishia kwenye talaka.Hata hivyo kiwango hicho kimeshuka, baada ya wengi kuamua kuwekana kinyumba au kuwa vimada badala ya kufunga ndoa. Hivi sasa wapenzi huishi pamoja kwa miaka mitatu au zaidi kabla hawajaamua kama wafunge ndoa au hapana. Kila mmoja anamwogopa mwenzake, haamini kwamba, anampenda.Sharon Naylor, ambaye ni mtunzi wa kitabu cha Your Special Wedding Vows (Kiapo Maalum kwa Ndoa Yako) anasema amewahi kusikia bibi harusi akiapa siku ya ndoa yake kwa kusema, "hadi pale muda wetu wa kuwa pamoja utakapoisha."
Anasema kiapo kama hiki ni sahihi kwani kuapa kwa kitu ambacho huna uhakika wa kukiweza au ambacho unajua siyo kweli, ni kujitendea haki.Mabadiliko haya katika kuapa siku ya ndoa yanaashiria kwamba, taasisi inayoitwa ndoa inaendelea kupambana na mabadiliko ambayo hatimaye yataiporomosha na watu wataanza kuishi kama wanyama wengine. Inaelezwa pia kwamba, huenda ni kutokana na ubabe wa wanaume ambao umewabadili wanawake na sasa wameanza kuitazama ndoa kama kifungo.
Kwa sababu maandiko ya dini ya Kikristo kwa mfano, hayawezi kubadilishwa katika jambo kama hilo, wanandoa wengi wameamua kutofunga ndoa zao kanisani na badala yake hufungia mahali pengine.Hii ni ili kukwepa kutamka kwamba, wataishi hadi kifo kiwatenge, wakati wanaona kabisa watu wengi wamechanganyikiwa na hawajui tena maana ya kupenda.
Kila bibi harusi anaogopa kujiapiza kwa kauli hizo zenye kumfunga. Inaelezwa kwamba, woga huo unatokana na kile kinachoonekana majumbani, kwamba, ndoa nyingi hazina kuaminiana na zinatisha kwa visa na mikasa. Inaelezwa na watu wanaopenda kuyachukulia mambo kimkabala na mila na desturi kwamba, utaratibu huu mpya wa kukwepa kusema, "hadi kifo kitutenge," wakati wakufunga ndoa na badala yake kusema kitu kama, "naahidi kuwa mwaminifu kwako, kama tu penzi bado lipo," huenda utadhoofisha ndoa nyingi.Raisi wa Muungano wa Makanisa Katoliki na haki za binadamu, William Donahue, amesema, kubadili kiapo hicho na kusema, "kama tu penzi litaendelea kuwepo," ni sawa na kuweka masharti kupenda, jambo ambalo litafanya kupenda kupoteze maana yake ya asili. Amesema kupenda hakuwezi kuwekewa masharti. Kiongozi wa utafiti huu Mary Jo Gallegos amesema, kwa hivi sasa ambapo watu wa mila na imani mbalimbali wanakutana na kuoana, mambo ya kuambiana hadi kifo kitutenge, hayawezi kuwa na nguvu.Mama huyo ameendelea kusema, hakumbuki kwa mara ya mwisho ni lini alimsikia mwanamke mwenye kufunga ndoa, akiahidi kwamba, atampenda mumewe hadi kifo kije kiwatenge.
Anazidi kusema, hakuna jambo kama hilo kwa sababu, wengi wamegundua kwamba, huko ni kujitwisha mzigo ambao mtu hawezi kuubeba.Amezidi kusema kwamba, watu wengi sasa wanaiona hali halisi na wanajua ukweli mkubwa zaidi katika ndoa. Amesema wale walio kwenye ndoa ya pili au ya tatu, wanajua ukweli mkubwa zaidi kuliko wale walio kwenye ndoa ya kwanza au ambao hawajaingia kwenye ndoa kabisa. Jambo la maana anasema, ni kwa wanandoa wote kuamini kwamba, wataishi kwa amani hadi kufa, lakini wakijua lolote linaweza
kutokea.
Huko Marekani, nusu ya ndoa huishia kwenye talaka.Hata hivyo kiwango hicho kimeshuka, baada ya wengi kuamua kuwekana kinyumba au kuwa vimada badala ya kufunga ndoa. Hivi sasa wapenzi huishi pamoja kwa miaka mitatu au zaidi kabla hawajaamua kama wafunge ndoa au hapana. Kila mmoja anamwogopa mwenzake, haamini kwamba, anampenda.Sharon Naylor, ambaye ni mtunzi wa kitabu cha Your Special Wedding Vows (Kiapo Maalum kwa Ndoa Yako) anasema amewahi kusikia bibi harusi akiapa siku ya ndoa yake kwa kusema, "hadi pale muda wetu wa kuwa pamoja utakapoisha."
Anasema kiapo kama hiki ni sahihi kwani kuapa kwa kitu ambacho huna uhakika wa kukiweza au ambacho unajua siyo kweli, ni kujitendea haki.Mabadiliko haya katika kuapa siku ya ndoa yanaashiria kwamba, taasisi inayoitwa ndoa inaendelea kupambana na mabadiliko ambayo hatimaye yataiporomosha na watu wataanza kuishi kama wanyama wengine. Inaelezwa pia kwamba, huenda ni kutokana na ubabe wa wanaume ambao umewabadili wanawake na sasa wameanza kuitazama ndoa kama kifungo.