Moyo Ulojeruhiwa, Kupenda tena ni kazi?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,474
39,987
Moyo ulojeruhiwa, kuponywa kwake ni kazi,
Hasa ulodhulumiwa, kutwa hujaa majonzi,
Ule ulosalitiwa, hutiririka machozi,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?


Moyo ulojeruhiwa, daima huwa na kovu,
Kila ukishituliwa, huwa kama nyumba mbovu,
Nyumba inapovujiwa, ndivyo uzidi ubovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Moyo ulojeruhiwa, hauishi maumivu,
Huhisi kukataliwa, hukwepa tonesha kovu,
Hofu ya kukatiliwa, huwa kama gari bovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
 
haya Mzee Mwanakijiji..........................karibu
hizi broken hearted zimekuwa nyingi kweli nowadays,
hebu wasiliana na Mbu, nae amekuja na ''KUHARIBIWA MAISHA''
 
Moyo ukijeruhiwa , dawa yake hii hapa

Ukijeruhiwa moyo wako unakuwa very devastating na ukijaribu kuwa sawa tenaaaa can seem almost impossible, unakuwa hauwezi kumwamini mtu tena na sometimes unajiuliza "Is there anybody worthy of loving?" Ni kweli kabisa kama utakuwa muwazi kwako mwenyewe na open yourself up for healing and refrain from bitterness

1. Take time to heal, uhusiano ukiisha ni vizuri ukae single for a bit until you can put all the pieces of what happened
to relationship in perspective. Give youself time to mourn the loss of the relationship and figure what was done.
Time will take away the pain if you just wait it out.

2.Usijilaumu kabisa kuwa uhusiano umekufa, uhusiano umefail sababu wote wawili hamjakubaliana na matakwa yenu
ukijilaumu sana itakupa unnecessary grief, kwa hiyo acha kabisa kujilaumu mwenyewe

3.Ongea na marafiki na ndugu waliokaribu sana na wewe, waeleze kuhusu uhusiano na kilichotokea kwako chote,
Sometimes you are too close to the situation to see what is really going on and close friend and family could
offer a differing opinion...unaweza kuongea hata na watu wazima waliopitia mambo mengi katika maisha na ukapata
ushauri
4.Na usi generalise all relationships eti ziko sawa, hii hata humu kwetu MMU ipo mtu analaumu group fulani na kuwaungani
sha wote,kuwa positive na open to new things, na ujue kuwa watu wote hawafanani kabisa, jua kabisa mtu mwingine
atakayekuja katika maisha yako atakuwa tofauti na hatakuumiza hisia zako kama aliyepita. Ganaralization only keeps
you from ever and forever happiness

5.Believe in love, love is real na ina exist na sababu you had heart broken once haimaanishi itatokea ten kila mara
unapokutana na mtu. kumbuka mtu wako atakayekupenda na kukufanya uwe happy yupo mahala katulia tuli
anasubiria muda tu ufike, Optimism is key

6.Date for the sake of dating. have fun, go out ,screw up and never regret and do not pressure yourself to
find love, Sio kila uhusiano will turn into love. Furahia maisha na watu wengine na u relax your mind and body,
You cant get your heart broken if you just having fun and feeling out the relationship

Sorry MM sijakujibu ki malenga malenga ngoja nijipange
 
Moyo ukijeruhiwa , dawa yake hii hapa

Ukijeruhiwa moyo wako unakuwa very devastating na ukijaribu kuwa sawa tenaaaa can seem almost impossible, unakuwa hauwezi kumwamini mtu tena na sometimes unajiuliza "Is there anybody worthy of loving?" Ni kweli kabisa kama utakuwa muwazi kwako mwenyewe na open yourself up for healing and refrain from bitterness

1. Take time to heal, uhusiano ukiisha ni vizuri ukae single for a bit until you can put all the pieces of what happened
to relationship in perspective. Give youself time to mourn the loss of the relationship and figure what was done.
Time will take away the pain if you just wait it out.

2.Usijilaumu kabisa kuwa uhusiano umekufa, uhusiano umefail sababu wote wawili hamjakubaliana na matakwa yenu
ukijilaumu sana itakupa unnecessary grief, kwa hiyo acha kabisa kujilaumu mwenyewe

3.Ongea na marafiki na ndugu waliokaribu sana na wewe, waeleze kuhusu uhusiano na kilichotokea kwako chote,
Sometimes you are too close to the situation to see what is really going on and close friend and family could
offer a differing opinion...unaweza kuongea hata na watu wazima waliopitia mambo mengi katika maisha na ukapata
ushauri
4.Na usi generalise all relationships eti ziko sawa, hii hata humu kwetu MMU ipo mtu analaumu group fulani na kuwaungani
sha wote,kuwa positive na open to new things, na ujue kuwa watu wote hawafanani kabisa, jua kabisa mtu mwingine
atakayekuja katika maisha yako atakuwa tofauti na hatakuumiza hisia zako kama aliyepita. Ganaralization only keeps
you from ever and forever happiness

5.Believe in love, love is real na ina exist na sababu you had heart broken once haimaanishi itatokea ten kila mara
unapokutana na mtu. kumbuka mtu wako atakayekupenda na kukufanya uwe happy yupo mahala katulia tuli
anasubiria muda tu ufike, Optimism is key

6.Date for the sake of dating. have fun, go out ,screw up and never regret and do not pressure yourself to
find love, Sio kila uhusiano will turn into love. Furahia maisha na watu wengine na u relax your mind and body,
You cant get your heart broken if you just having fun and feeling out the relationship

Thanks for the tips, nakubaliana na zote isipokuwa hiyo ya sita, maana katika kuscrew up unaweza kujikuta unapoteza hata reputation yako.

Nafikiri jambo la msingi ni kuruhusu pain, maana that is what makes us human, we feel happiness, pain, love.

With time, the pain will go away, only the scar will ramain.
 
Thanks for the tips, nakubaliana na zote isipokuwa hiyo ya sita, maana katika kuscrew up unaweza kujikuta unapoteza hata reputation yako.

Nafikiri jambo la msingi ni kuruhusu pain, maana that is what makes us human, we feel happiness, pain, love.

With time, the pain will go away, only the scar will ramain.
Ndio wataalam wa saikologia sasa, na unaposema screw sio ile tu uanyofikiri, hilo neno lina maana nyingi mkuu
 
kuna mijitu huku kitaa inajiita ''the heart breaker'' sijui inafikiri sifa!!
 
Moyo ukijeruhiwa , dawa yake hii hapa

Ukijeruhiwa moyo wako unakuwa very devastating na ukijaribu kuwa sawa tenaaaa can seem almost impossible, unakuwa hauwezi kumwamini mtu tena na sometimes unajiuliza "Is there anybody worthy of loving?" Ni kweli kabisa kama utakuwa muwazi kwako mwenyewe na open yourself up for healing and refrain from bitterness

1. Take time to heal, uhusiano ukiisha ni vizuri ukae single for a bit until you can put all the pieces of what happened
to relationship in perspective. Give youself time to mourn the loss of the relationship and figure what was done.
Time will take away the pain if you just wait it out.

2.Usijilaumu kabisa kuwa uhusiano umekufa, uhusiano umefail sababu wote wawili hamjakubaliana na matakwa yenu
ukijilaumu sana itakupa unnecessary grief, kwa hiyo acha kabisa kujilaumu mwenyewe

3.Ongea na marafiki na ndugu waliokaribu sana na wewe, waeleze kuhusu uhusiano na kilichotokea kwako chote,
Sometimes you are too close to the situation to see what is really going on and close friend and family could
offer a differing opinion...unaweza kuongea hata na watu wazima waliopitia mambo mengi katika maisha na ukapata
ushauri
4.Na usi generalise all relationships eti ziko sawa, hii hata humu kwetu MMU ipo mtu analaumu group fulani na kuwaungani
sha wote,kuwa positive na open to new things, na ujue kuwa watu wote hawafanani kabisa, jua kabisa mtu mwingine
atakayekuja katika maisha yako atakuwa tofauti na hatakuumiza hisia zako kama aliyepita. Ganaralization only keeps
you from ever and forever happiness

5.Believe in love, love is real na ina exist na sababu you had heart broken once haimaanishi itatokea ten kila mara
unapokutana na mtu. kumbuka mtu wako atakayekupenda na kukufanya uwe happy yupo mahala katulia tuli
anasubiria muda tu ufike, Optimism is key

6.Date for the sake of dating. have fun, go out ,screw up and never regret and do not pressure yourself to
find love, Sio kila uhusiano will turn into love. Furahia maisha na watu wengine na u relax your mind and body,
You cant get your heart broken if you just having fun and feeling out the relationship

Sorry MM sijakujibu ki malenga malenga ngoja nijipange
As im going through this, nina imani itanisaidia sana, uko juu gaga
 
Moyo ulojeruhiwa, kuponywa kwake ni kazi,
Hasa ulodhulumiwa, kutwa hujaa majonzi,
Ule ulosalitiwa, hutiririka machozi,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?


Moyo ulojeruhiwa, daima huwa na kovu,
Kila ukishituliwa, huwa kama nyumba mbovu,
Nyumba inapovujiwa, ndivyo uzidi ubovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Moyo ulojeruhiwa, hauishi maumivu,
Huhisi kukataliwa, hukwepa tonesha kovu,
Hofu ya kukatiliwa, huwa kama gari bovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)

Unachosema ni kweli, mzee mwanakijiji
Inaumiza akili, na ni vizuri umehoji
mwanadamu kwa asili, kujeruhiwa hakubali
Moyo ukijeruhiwa, dawa yake kusamehe.

Ni vigumu kuponyeka, ukigoma kuachilia
Nasema kwa uhakika, kwani nimeshuhudia
Wale walofadhaika, waweza kufurahia
Moyo ukijeruhiwa, dawa yake kusamehe

Namkumbuka Asia, jinsi alivyoumizwa
Alipotoswa na kulia, mtaa ulishangwazwa
kathubutu kwachilia, leo moyo umepozwa
Moyo ukijeruhiwa, dawa yake kusamehe
 
Moyo ulojeruhiwa, kuponywa kwake ni kazi,
Hasa ulodhulumiwa, kutwa hujaa majonzi,
Ule ulosalitiwa, hutiririka machozi,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?


Moyo ulojeruhiwa, daima huwa na kovu,
Kila ukishituliwa, huwa kama nyumba mbovu,
Nyumba inapovujiwa, ndivyo uzidi ubovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Moyo ulojeruhiwa, hauishi maumivu,
Huhisi kukataliwa, hukwepa tonesha kovu,
Hofu ya kukatiliwa, huwa kama gari bovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)


kwa nyongesa tu yero.................
WHAT SHOULD WE DO?
What should we do​
If love is dead​
And trust buried?​
As people love today​
And hate tomorrow as they alway:​
Should we say allas!​
Whence our pride divorce?​
A man likes a woman and woo​
A woman loves a man through​
A priest stands for God as to vow​
Today's matrimonial​
Is tomorrow's break-up proposal​
Should I had a toast​
For today's divorce?​
What do you mean​
When say you love someone​
Tenderly like a shinning moon​
A huge wedding party in vain​
A costly honey moon​
Why to do all these​
While the end is divorce?​
As in thy heart no love​
Dig not thy own grave​
To be as docile as a slave​
If not patient​
Nor tolerant​
Leave it, don't force​
For it will end up by divorce​
Your love is but hate​
Its foe is but jealousy​
Yours is not love, but desires​
Why wed if love isn't there​
And why promise, is not life?​
Fool not the heavens with thy passion​
Since to God divorce is not written.​
12/01/2005​
Dar Es Salaam, Tz​
 
kuna mijitu huku kitaa inajiita ''the heart breaker'' sijui inafikiri sifa!!

Kuumizwa kubaya....nyie acheni,hebu ona hii.....................

THE LIE:
The little maiden in the dark room ready to die​
Bitter and desperate for the denay:​
Her love squeezed her for the lie​
The day and night long, dreams and cry​
For she was blinded by the lie:​
10/02/2005​
 
Kuumizwa kubaya....nyie acheni,hebu ona hii.....................

THE LIE:
The little maiden in the dark room ready to die​
Bitter and desperate for the denay:​
Her love squeezed her for the lie​
The day and night long, dreams and cry​
For she was blinded by the lie:​
10/02/2005​
Yote maisha
 
Unachosema ni kweli, mzee mwanakijiji
Inaumiza akili, na ni vizuri umehoji
mwanadamu kwa asili, kujeruhiwa hakubali
Moyo ukijeruhiwa, dawa yake kusamehe.

Ni vigumu kuponyeka, ukigoma kuachilia
Nasema kwa uhakika, kwani nimeshuhudia
Wale walofadhaika, waweza kufurahia
Moyo ukijeruhiwa, dawa yake kusamehe

Namkumbuka Asia, jinsi alivyoumizwa
Alipotoswa na kulia, mtaa ulishangwazwa
kathubutu kwachilia, leo moyo umepozwa
Moyo ukijeruhiwa, dawa yake kusamehe
Uko juu sana malenga
 
Moyo ukijeruhiwa , dawa yake hii hapa

Ukijeruhiwa moyo wako unakuwa very devastating na ukijaribu kuwa sawa tenaaaa can seem almost impossible, unakuwa hauwezi kumwamini mtu tena na sometimes unajiuliza "Is there anybody worthy of loving?" Ni kweli kabisa kama utakuwa muwazi kwako mwenyewe na open yourself up for healing and refrain from bitterness

1. Take time to heal, uhusiano ukiisha ni vizuri ukae single for a bit until you can put all the pieces of what happened
to relationship in perspective. Give youself time to mourn the loss of the relationship and figure what was done.
Time will take away the pain if you just wait it out.

2.Usijilaumu kabisa kuwa uhusiano umekufa, uhusiano umefail sababu wote wawili hamjakubaliana na matakwa yenu
ukijilaumu sana itakupa unnecessary grief, kwa hiyo acha kabisa kujilaumu mwenyewe

3.Ongea na marafiki na ndugu waliokaribu sana na wewe, waeleze kuhusu uhusiano na kilichotokea kwako chote,
Sometimes you are too close to the situation to see what is really going on and close friend and family could
offer a differing opinion...unaweza kuongea hata na watu wazima waliopitia mambo mengi katika maisha na ukapata
ushauri
4.Na usi generalise all relationships eti ziko sawa, hii hata humu kwetu MMU ipo mtu analaumu group fulani na kuwaungani
sha wote,kuwa positive na open to new things, na ujue kuwa watu wote hawafanani kabisa, jua kabisa mtu mwingine
atakayekuja katika maisha yako atakuwa tofauti na hatakuumiza hisia zako kama aliyepita. Ganaralization only keeps
you from ever and forever happiness

5.Believe in love, love is real na ina exist na sababu you had heart broken once haimaanishi itatokea ten kila mara
unapokutana na mtu. kumbuka mtu wako atakayekupenda na kukufanya uwe happy yupo mahala katulia tuli
anasubiria muda tu ufike, Optimism is key

6.Date for the sake of dating. have fun, go out ,screw up and never regret and do not pressure yourself to
find love, Sio kila uhusiano will turn into love. Furahia maisha na watu wengine na u relax your mind and body,
You cant get your heart broken if you just having fun and feeling out the relationship

Sorry MM sijakujibu ki malenga malenga ngoja nijipange

Umeiweka vizuri sana!
 
Ila wapo wazee wa kufariji wajane anaweza akakusahaulisha ndani ya muda mfupi na ukajilaumu why hukumjua mapema.
 
Moyo ulojeruhiwa, kuponywa kwake ni kazi,
Hasa ulodhulumiwa, kutwa hujaa majonzi,
Ule ulosalitiwa, hutiririka machozi,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?


Moyo ulojeruhiwa, daima huwa na kovu,
Kila ukishituliwa, huwa kama nyumba mbovu,
Nyumba inapovujiwa, ndivyo uzidi ubovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Moyo ulojeruhiwa, hauishi maumivu,
Huhisi kukataliwa, hukwepa tonesha kovu,
Hofu ya kukatiliwa, huwa kama gari bovu,
Moyo ukijeruhiwa, huponywa kwa dawa gani?

Na. M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)

Dawa ya penzi ni penzi,tafuta wako mpenzi,
siwe kama yake inzi,yalonuka kuyaenzi,
panda mpaka kimawenzi,tafuta wako kipenzi,
Moyo ukijeruhiwa,dawa yake ndio wewe,

Akija kumwaga mboga,na wewe mwaga ugari,
wako kama kwenye mbuga,mwaga sera kifahari,
wenye shingo ka ya twiga,watanashati mahiri,
Moyo ukijeruhiwa,dawa yake ndio wewe,

Usitafute mchawi,mganga wake mapenzi,
siende hata malawi,sera zako tegemezi,
mwimbie sandakalawi,lazima kwite mpenzi,
Moyo ukijeruhiwa,dawa yake ni wewe,

Ngoja nilitue nanga,usiniite mbeya,
Nikamuone ma manga,kule aliko kyeya,
Nitapita hata Tanga,mwanakijiji oyeya,
Moyo ukijeruhiwa,dawa yake ni wewe.........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom