Moyo Ulioonja Maumivu

SEHEMU YA 36

Maumivu aliyokuwa ameyapata yalikuwa ni mara tano ya yale ambayo angeyapata mke wake. Aliumia, hakutamani kuona mke wake huyo akiumia kama atakavyoumia, alitamani kuona akiishi maisha ya furaha, yasiyokuwa na maumivu hata kidogo.

Siku ya kwanza ikapita, Theo hakuondoka hospitalini, taarifa zilianza kuzagaa mitandaoni kwamba Violeth alijifungua usiku uliopita lakini hakukuwa na mtu aliyepata taarifa kuwa mtoto mmoja alifariki dunia.

Theo hakutaka kumtaarifu mtu yeyote yule, na hata alipoongea na ndugu zake aliwaambia kwamba alijifungua salama kabisa. Alihitaji kumuona mke wake akifumbua macho na kuzungumza naye, ampe taarifa hiyo ili wajue ni kwa namna gani wangewaambia wananchi.

Siku hiyo ndiyo ambayo Violeth alipoyafumbua macho yake kitandani pale. Alionekana kuchoka mno, kitu cha kwanza kilichokuja kichwani mwake ni watoto wake, alijua alijifungua, alihitaji kuwaona wote wawili.

Akaangalia pembeni, kulikuwa na mtoto mmoja wa kike, lakini upande mwingine hakukuwa na mtoto. Haraka sana Theo akasimama na kumfauata mke wake mahali pale.

“Mume wangu! Nimejifungua....tumepata watoto mapacha mume wangu...wa kiume ataitwa Harry na wa kike ataitwa Rachel...” alisema Violeth kwa sauti ya chini, hakujua kilichotokea, badala ya Theo kumjibu, machozi yakaanza kumtoka hali iliyoanza kumtisha Violeth kitandani pale. |
|
|

Je, nini kitaendelea?
Tukutane siku nyingine.
 
Naenda kulia mkuu ..hii long waiting sio ya nchi hii
Tumwite tartiiibu.. . .... ...

Atakuja tu...
Maana .... Tevie haongei ila wakati mwingine..
Itakuwa kazongwa ..mambo mengi na usawa huu wa jiwe... ... ngoma nzito...inabidi kujipinda!
 
SEHEMU YA 36

Maumivu aliyokuwa ameyapata yalikuwa ni mara tano ya yale ambayo angeyapata mke wake. Aliumia, hakutamani kuona mke wake huyo akiumia kama atakavyoumia, alitamani kuona akiishi maisha ya furaha, yasiyokuwa na maumivu hata kidogo.

Siku ya kwanza ikapita, Theo hakuondoka hospitalini, taarifa zilianza kuzagaa mitandaoni kwamba Violeth alijifungua usiku uliopita lakini hakukuwa na mtu aliyepata taarifa kuwa mtoto mmoja alifariki dunia.

Theo hakutaka kumtaarifu mtu yeyote yule, na hata alipoongea na ndugu zake aliwaambia kwamba alijifungua salama kabisa. Alihitaji kumuona mke wake akifumbua macho na kuzungumza naye, ampe taarifa hiyo ili wajue ni kwa namna gani wangewaambia wananchi.

Siku hiyo ndiyo ambayo Violeth alipoyafumbua macho yake kitandani pale. Alionekana kuchoka mno, kitu cha kwanza kilichokuja kichwani mwake ni watoto wake, alijua alijifungua, alihitaji kuwaona wote wawili.

Akaangalia pembeni, kulikuwa na mtoto mmoja wa kike, lakini upande mwingine hakukuwa na mtoto. Haraka sana Theo akasimama na kumfauata mke wake mahali pale.

“Mume wangu! Nimejifungua....tumepata watoto mapacha mume wangu...wa kiume ataitwa Harry na wa kike ataitwa Rachel...” alisema Violeth kwa sauti ya chini, hakujua kilichotokea, badala ya Theo kumjibu, machozi yakaanza kumtoka hali iliyoanza kumtisha Violeth kitandani pale. |
|
|

Je, nini kitaendelea?
Tukutane siku nyingine.

Ubarikiwe sana Shunie
 
Tumwite tartiiibu.. . .... ...

Atakuja tu...
Maana .... Tevie haongei ila wakati mwingine..
Itakuwa kazongwa ..mambo mengi na usawa huu wa jiwe... ... ngoma nzito...inabidi kujipinda!
Naenda kulia mkuu ..hii long waiting sio ya nchi hii
kama ni me huko bafuni unaenda kulia machozi ya simba!
Kweli arosto .... acha nikajililie zangu bafuni mie
Toka mwanzo nilitoa taarifa hii ndio arosto yenyewe sasa mvumilie tu
 
Mkweee!! Nimekuja kimya kimya mpaka nimekukuta hapa,,vipi kwema? Ahsante Sana kwa rubudani
 
SEHEMU YA 37

Theo alibaki akimwangalia mke wake pale kitandani alipokuwa. Moyo wake ulimuuma mno, swali alilomuumiza likamfanya kuanza kukumbuka kila kitu kilichotokea. Machozi yalianza kujaa machoni mwake lakini hakutaka kuyaruhusu yatiririke mashavuni mwake kwa kuwa aliamini mke wake angegundua kila kitu.

Violeth aliendelea kumwambia mume wake kuhusu watoto wake, aliamini kwamba alijifungua salama kabisa lakini baada ya kutuliza macho yake usoni mwa Theo, akagundua kulikuwa na kitu kilitokea kwani lisingekuwa jambo jepesi kwa mwanaume ambaye mkewe alijifungua salama kuwa na muonekano ule aliokuwanao.

Akamuuliza tatizo lilikuwa nini, Theo hakutaka kumwambia ukweli, alibaki kimya lakini mke wake huyo hakutaka kunyamaza, alihisi kulikuwa na kitu na alikuwa tayari kuambiwa kwani hali ile ilimtia hofu mno.

“Kuna nini mume wangu?” aliuliza Violeth huku akimwangalia Theo.
“Hakuna kitu!” alijibu Theo kwa kujikaza.
“Mbona macho yako mekundu hivyo? Ulikuwa unalia ama?” aliendelea kuuliza mwanamke huyo.

Theo akashindwa kuvumilia kabisa, machozi yake yakaanza kutiririka mashavuni mwake kitu kilichomshtua mno Violeth ambaye alihisi kulikuwa na jambo fulani ambalo mume wake hakutaka kumwambia.

“Hapana! Kuna tatizo! Kwanza nataka kuwaona wanangu,” alisema Violeth huku akimwangalia mume wake, hakuishia hivyo tu bali akataka kuinuka, haraka sana daktari aliyekuwa pembeni akamsogelea na kumzuia.

“Violeth! Subiri, usiinuke,” alisema daktari kwani alijua kama angeinuka basi angeuchomoa mpira uliokuwa ukipitisha maji kwenda kwenye mishipa yake.
“Niambieni kuhusu wanangu!” alisema Violeth kwa sauti kubwa.


“Subiri kwanza...” alimtuliza daktari.
Ilikuwa vigumu sana kwa Violeth kutulia, alihitaji kitu kimoja tu mahali hapo, kuwaona watoto wake.

Alimwambia daktari kwamba asingeweza kutulia hata kidogo, alifika hospitalini hapo kwa lengo la kujifungua, kazi hiyo ilifanyika hivyo alihitaji kujua ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom