marybaby
JF-Expert Member
- Apr 11, 2017
- 3,260
- 9,193
Shangazi hiyo sauti yantisha mi pia.!SEHEMU YA 31
Alipoona amechoka, akausogelea mlango na kuanza kuugonga, alihitaji ufunguliwe ili aone kile kilichokuwa kimeendelea humo..
“Dokta! Fungua mlango...fungua mlango...” alisema Theo huku machozi yakianza kumtoka, aliisikia sauti moyoni mwake ikimwambia kuna moja limetokea, inawezekana mke wake akawa amefariki ama watoto wake.
Alijitahidi kuipinga sauti hiyo kwa nguvu kubwa, haikupingika, iliendelea kumwambia hivyohivyo kitu kilichomfanya kuwa na hofu zaidi na zaidi.
Baada ya dakika kadhaa za kugonga mlango ule, mara ukafunguliwa na kukutanisha macho yake na daktari.
Kwa muonekano wa mtu huyo tu ulimwambia kulikuwa na jambo kubwa lililokuwa limetokea huko, alionekana tofauti, kama kweli mke wake alijifungua salama, inamaanisha daktari huyo angeonekana kuwa na furaha na si kama alivyokuwa.
“Nini kinaendelea?” aliuliza Theo huku akimwangalia daktari huyo ambaye alionekana kuwa na jambo zito moyoni mwake ila hakutaka kumwambia mahali hapo.
“Naomba twende ofisini kwangu,” alijibu daktari huyo.
“Subiri kwanza. Naomba uniambie! Amejifungua salama?” aliuliza Theo huku akianza kutetemeka kwa hofu, kijasho chembamba kikaanza kumtoka, mwili wake ulikuwa ukitetemeka kana kwamba alikaa sehemu iliyokuwa na baridi kali.
“Naomba twende tukaongee,” alisema daktari yule.
Hakuwa na jinsi, yeye na marafiki zake wakaanza kuelekea kule ofisini kwa daktari, aliogopa, alimuomba Mungu kusiwe na habari mbaya ya kupewa, aliujua moyo wake, kwa jinsi ulivyompenda Violeth, kama angeambiwa mke wake amekufa basi maumivu ambayo angeyasikia yangekuwa makubwa mno.
Walipofika ndani ya ofisi hiyo, wakakaa kwenye viti na kuanza kuangaliana. Moyo wa Theo ulikuwa kwenye maombezi mazito, hakukuwa na siku ambayo alikuwa akimuomba Mungu kama siku hiyo.
“Theo....tumejitahidi sana, mke na watoto wako wamekufa...” aliisikia sauti hiyo moyoni mwake, sauti ambayo ilimtisha mno.
Je, nini kitaendelea?
Tukutane siku nyingine.