Moto wateketeza mabanda ya biashara Mwenge TRA

Gulwa

JF-Expert Member
Jun 16, 2008
9,729
14,740
Moto mkubwa umewaka nyuma ya TRA Mwenge na kuteketeza kabisa vifaa na mali mbambali ziloOkuwemo kwenye vibanda vya biashara.

Kitu kilichonisikitisha ni simu za zimamoto kutokupokelewa haraka kama inavyotakiwa. Hata walipopatikana walichelewa kufika eneo la tukio mpaka wananchi wakaamua kujitosa na kupambana na moto ili usilete madhara makubwa zaidi.

Nimejiuliza maswali mengi kuhusu tukio la leo. Hivi badala ya kununua madege mengi yanayotumiwa na watanzania wachache kwanini yasinunuliwe magari ya zimamoto ya kutosha na kusambazwa maeneo mbalimbali ya miji ili kuokoa mali za wananchi zisiteketee kwa moto?
 
Tuma ka picha tuone palipoungua.
Kuna mwana anabanda lake hapo na nimemkopa😂😂😂 kwaiyo nijiandae kwa foleni za simu zake.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom