Moto Ndani ya CC: Mbowe azuiwa ku-chair kikao!

MBOWE WEWE BANA ACHA ZAKO, KWANZA SIASA HUIWEZI, ACHILIA MBALI NA HAKUNA CHOCHOTE ULICHOFANYA KUWASHAWISHI WATU KWAMBA KWELI UNA NIA YA UONGOZI, HIVI HADI HIVI SASA UMEFANYA NINI WEWE MBOWE ?? SIASA SIO KITU KIDOGO TU, KWANZA UMRI WAKO HUO BADO TU UNAOTA KUWA RAIS WA TANZANIA HIVI KARIBUNI ?? IN MY OPINION YOU HAVE ANOTHER 15 YEARS NDIO UANZE KUFIKIRIA HUO URAIS !

BORA WATU WA ZITTO(MGAWANYIKO USHATOKEA) WALIVYOMUOMBA MBOWE ASIWE MWENYEKITI WA MKUTANO, HUYU JAMAA NDIO TUNATEGEMEA AWE RAIS WETU KWELI ONE DAY ?? YAANI ANASHINDWA HATA KUWA PUNCTUAL BANA ? JE INA MAANA ALICHELEWA KUWA BRIEFED NA HICHO KIKAO MPAKA ACHELEWE AU ? KAMA ALITOKA UGHAIBUNI MAPEMA NA ALIJUA JUMAMOSI NDIO KIKAO, KWA NINI ASINGEONYESHA MFANO KWA KUFIKA MAPEMA KULIKO WENGINE ? AU NDO MAMBO YA BOSI AKICHELEWA RUKSA ? MIE SIFAGILII HIZI TABIA WAZEE, NAJUA KUNA WENGINE MTANIRUKIA, LAKINI POA SEMENI MAANA NAMI NINA UHURU WA KUONGEA JUST LIKE ANYBODY ELSE !

KWA KUWA HUKUFANYA CHOCHOTE KUMSHAWISHI MTANZANIA WA KAWAIDA KUKUCHAGUA, BASI KIDOGO UNGEFIKA KWENYE KIKAO MAPEMA NA KUWEKA KWENYE CURRICULUMN VITAE YAKO KWAMBA ULIHUDHURIA KIKAO MAPEMA, LAKINI WEE UNACHELEWA TU, CV ITAJAA KWELI ?? teh teh.

haya bana mheshimiwa mbowe, wee endelea tu kufika late kwenye vikao bila sababu maalum, na onyesha ubaguzi wako kwa kutokuwa nyutro !

nasubiri tu habari zaidi maana tumeambiwa tukae tyun-di na nikipata hizo habari nitaendelea na wewe mheshimiwa mbowe !

SOMA MAKINI MANENO MEKUNDU ! sikumaanisha wafuasi wake, am dealing with him !
hata hivyo kuna mtabiri mmoja JF kaniambia wafuasi wake watakuja kufurika hapa kutokana na nilichoandika ! so hey........! lets roll the dice.
 
KADA.....

BANA wewe hulali?au ndio umetoka kuFUNGA GROCERRY KINONDONI hivi sasa?

hahahahaha where we dare to talk openly!!!!!!
 
Chadema chatoa baraka kwa Zitto kuendelea katika kamati ya madini *Wangwe asema Kamati Kuu ikiamua yeye hana nongwa
* Wafurahia Machunde kujitoa Kamati ya Madini

Na Kizitto Noya (Mwananchi)


CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetoa baraka zake kwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe kuendelea kuwa mjumbe wa Kamati ya Madini, iliyoteuliwa na Rais Jakaya Kikwete.


Habari kutoka ndani ya kikao cha Kamati Kuu kilichofanyika katika hoteli ya Keys jijini Dar es Salaam, zilisema kuwa Kabwe ataendelea kushiriki katika kamati hiyo, ili kuendelea kutekeleza sera ya chama hicho ya kupitia upya mikataba ya madini.


Hata hivyo, taarifa rasmi ya kikao hicho kilichoongozwa na Makamu Mwenyekiti, Mzee Said Mzee, inatarajiwa kutolewa leo saa 5:00 asubuhi katika Makao Makuu ya chama hicho.


Akizungumza na Mwananchi Jumapili mara baada ya kikao hicho, Mbunge wa Tarime ambaye alikuwa mstali wa mbele kumpinga Kabwe, alisema ameridhika na maamuzi ya Kamati Kuu ingawa hakutaka kuingia kwa undani kwa madai kuwa taarifa rasmi ingetolewa leo.


Hata hivyo, Kabwe mwenyewe alipopigiwa simu muda mfupi baadaye, hakutaka kulizungumzia na kudai kuwa kikao kilikuwa bado kinaendelea na kingemalizika leo saa 5.00 asubuhi.


Mapema, chama hicho kilitangaza kuweka kiporo tamko la kamati kuu hadi leo, kutokana na kuchelewa kuanza kwa Kikao cha Kamati Kuu ya Chama hicho.


Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk Willibrod Slaa aliwaambia waandishi wa habari katika ufunguzi wa kikao hicho kilichofanyika kwenye ukumbi wa hoteli ya Keys jijini Dar es Salaam kuwa taarifa ya kikao hicho isingepatikana jana kutokana na kikao kuchelewa kuanza kwa kumsubiri mwenyekiti wake Freeman Mbowe.


"Kama tungeanza saa 4:00 tuliyokuwa tumepanga tungetoa taarifa hiyo leo (jana) lakini tumechelewa kuanza kwa kumsubiri mwenyekiti ambaye tulipowasiliana naye hivi karibuni alisema amekwama Nairobi, hivyo taarifa tutaitoa kesho (leo)," alisema Dk Slaa saa 5:45 asubuhi jana.


Hata hivyo, Dk Slaa alisema kuwa kikao hicho chenye agenda moja, kimeitishwa kuchambua Kamati ya Madini na siyo kujadili uteuzi wa Kabwe katika kamati ya madini ya Rais Jakaya Kikwete.


Alisema mjadala wa Kabwe umeibuka kama sehemu ya mbinu za baadhi ya wanasiasa kutaka kuhamisha hoja ya msingi iliyoanzishwa na Chadema kuhusu ufisadi kwa kukitengenezea chama hicho mgogoro.


Kwa mujibu wa Dk Slaa Chadema haina mgogoro unaohusiana na uteuzi wa Zitto bali ina mgogoro wa Kamati yenyewe ambayo baadhi ya wajumbe wake wamebainika kuchangia katika mapungufu yanayolalamikiwa kwenye sekta ya madini.


"Watu wamehamisha mjadala wetu kutoka kwenye ufisadi kwenda kwa Zitto lakini Chadema bado tuko kwenye msimamo wetu kwamba agenda sio Zitto ni Kamati" alisema Dk Slaa.


Alisema hata kama kumekuwa na mawazo tofauti baina ya viongozi wa Chadema kuhusu suala la Zitto na Kamati, tofauti hizo sio mgogoro bali ni kukua kwa demokrasia ndani ya chama na mwisho wa tofauti hizo ni kauli itakayotolewa na Kamati Kuu iliyokutana jana.


Alikitaka kikao hicho kuichambua kwa makini kamati hiyo, hasa historia ya wajumbe wake na kutoa msimamo kuhusu suala hilo kwa lengo la kuendeleza mapambano dhidi ya ufisadi.


Alibainisha kuwa msimamo wa awali wa watendaji wakuu wa chama kwamba kamati hiyo inatakiwa kuboreshwa, umeanza kuzaa matunda kwa mmoja wa wajumbe waliokuwa wamelalamikiwa, Peter Machunde, kuamua kujitoa mwenyewe.


Alisema Chadema iliona uwepo wa Machunde, Mary Kejo na Salome Makange kunatia doa katika kamati hiyo kwa kuwa wamekuwa na historia inayowaondolea imani katika kamati hiyo.


Dk Slaa alisema kuwa Aprili 7 mwaka jana Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi, alimtambulisha Peter Machunde bungeni kuwa ni rafiki yake wa karibu na mfanyakazi wa kampuni yake binafsi ya Vatex Financial Services jambo ambalo linatia shaka kwamba ataweza kupitia mikataba iliyowekwa na rafiki yake Karamagi na kuitoa kasoro.


Aliendelea kuwaambia wajumbe wa kikao hicho kuwa katika kashfa ya IPTL, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji Patrick Rutabanzibwa aliwahi kutoa ushahidi wa kiapo mahakamani kuwa mmoja wa wajumbe alitaka kutoa rushwa ili mkataba huo uendelezwe jambo ambalo pia ni shaka juu ya uwepo wake kwenye kamati.


Alisema mjumbe mwingine amewahi kuwa mshauri wa mikataba ya madini hivyo hawezi kubadilisha ushauri wake katika mikataba hiyo na kupendekeza ushauri mwingine.


Dk Slaa aliwataka wajumbe wawili waliobaki kufuata nyayo za Peter Machunde na kujitoa katika kamati ili kulinda hadhi zao kwani madai yanayotolewa na chama hicho ni ya kweli yanayoweza kutolewa ushahidi popote.


"Ingawa nimeanza kupata taarifa kwamba wengine watajitoa kabla ya kuanza kwa vikao vya kamati hii, ni vyema wakatangaza hivyo sasa kwani sisi (Chadema) tumejitosheleza kiushahidi na nyaraka tunazo," alisema.


Machunde alitangaza kujiuzulu ujumbe wa kamati hiyo juzi kwa kile alichodai kuwa ni ubabaishaji na upotoshaji wa taarifa unaofanywa na Chadema.


Katika hatua nyingine, Dk Slaa, alielezea matatizo anayokumbana nayo katika kuongoza mapambano dhidi ya ufisadi, kuwa ni makubwa lakini hayawezi kubadili msimamo wake.


Alisema achilia mbali vitisho alivyopewa na baadhi ya watu aliowatuhumu kwa ufisadi kwamba watamfikisha mahakamani, baadhi ya vigogo wa serikali walimweka kitimoto katika bunge lililomalizika Novemba 16 mwaka huu kumtaka atoe sababu za kusambaza mkataba wa siri wa Buzwagi.


Alisema ingawa viongozi hawa na wale aliowatuhumu kwa ufisadi walimtishia kumshtaki, haamini kwamba anaweza kwenda mahakamani kwa kuwa anachosema ni ukweli na wala si kuwachafulia watu majina.
 
KADA.....

BANA wewe hulali?au ndio umetoka kuFUNGA GROCERRY KINONDONI hivi sasa?

hahahahaha where we dare to talk openly!!!!!!

hehee, unanikumbusha jamaa mmoja, anaitwa chesko mzee wa matunda, huyu jamaa alikuwa hana kazi ya kufanya zaidi ya kupiga simu kwenye vituo vya radio !
 
Mwenyekiti kazuia kuendesha kikao? Kwani Katiba ya Chadema inasemaje?

mifarakano ndani ya chama ndo chanzo ANGALAU wanachama wa Chama cha maendeleo na demokrais(CCMD)wanakataa tofauti zao ndani ya chama ! kila mtu anataka kuwa head wa chama, sasa huko chadema hakukaliki utafikiri wamekalia upupu !
 
KADA.....

kwi kiw kwi kwi WANAPOSHINDWA HOJA HULETA VIOJA.najiuliza kama habari hii ungeileta wewe KADA ingesemwa ohhhhh yule KADA tu analeta mambo ya CCM,angeileta MTU WA PWANI angesemwa ndio wale wale watoto wa wakubwa,angeleta ES angeeambiwa anaipenda CCm,leo imeletwa na SHETANi jina lake limekuwa issue jamani kwa nini inakuwa hivi.....

YA WENZAO MIDOMO JUUUU YA KWAO KIMYA

Heeh heeh

Mnakula kunywa na kuvaaa. Siku zinaenda, vya bure kupenda kupewa, wanaume kama....

Kwa mipasho, tutakoma mwaka huu. Au sio rizki?

Bahati ya Zitto na CHADEMA hamuwezi kuziba, ametoa Mungu wala hawajaiba, kama mnaweza pandeni juu mkazibe!

Mlisema ooooh wanafarakana, sasa jiandaeni kubadili kauli

Mseme msemayo, yote ni bureeeeee, kwani mapenzi- hayana shuleeee. Yawenzenu midomo juu lakini yetu hamyasemi..

Asha
 
JUST IN CASE YOU MISSED IT !!

HIKI NDICHO KINAONGELEWA HAPA !!

Kwanza kikao kilichelewa kuanza kwasababu Mwenyekiti alichelewa kuwasili. Kimeanza. Watu wa upande wa Zitto wameomba Mwenyekiti Mbowe asiwe mwenyekiti wa kikao kwasababu ameonyesha dhahiri kwamba hayupo neutral. Makamu wa Mwenyekiti ndiye Mwenyekiti wa kikao hadi sasa. Nitawaletea habari kadri ninavyotumiwa text kutoka ndani ya kikao.

Shetani wenu.


(NA SI VINGINEVYO)!!!!!!!!!1
 
MBOWE WEWE BANA ACHA ZAKO, KWANZA SIASA HUIWEZI, ACHILIA MBALI NA HAKUNA CHOCHOTE ULICHOFANYA KUWASHAWISHI WATU KWAMBA KWELI UNA NIA YA UONGOZI, HIVI HADI HIVI SASA UMEFANYA NINI WEWE MBOWE ?? SIASA SIO KITU KIDOGO TU, KWANZA UMRI WAKO HUO BADO TU UNAOTA KUWA RAIS WA TANZANIA HIVI KARIBUNI ?? IN MY OPINION YOU HAVE ANOTHER 15 YEARS NDIO UANZE KUFIKIRIA HUO URAIS !

BORA WATU WA ZITTO(MGAWANYIKO USHATOKEA) WALIVYOMUOMBA MBOWE ASIWE MWENYEKITI WA MKUTANO, HUYU JAMAA NDIO TUNATEGEMEA AWE RAIS WETU KWELI ONE DAY ?? YAANI ANASHINDWA HATA KUWA PUNCTUAL BANA ? JE INA MAANA ALICHELEWA KUWA BRIEFED NA HICHO KIKAO MPAKA ACHELEWE AU ? KAMA ALITOKA UGHAIBUNI MAPEMA NA ALIJUA JUMAMOSI NDIO KIKAO, KWA NINI ASINGEONYESHA MFANO KWA KUFIKA MAPEMA KULIKO WENGINE ? AU NDO MAMBO YA BOSI AKICHELEWA RUKSA ? MIE SIFAGILII HIZI TABIA WAZEE, NAJUA KUNA WENGINE MTANIRUKIA, LAKINI POA SEMENI MAANA NAMI NINA UHURU WA KUONGEA JUST LIKE ANYBODY ELSE !

KWA KUWA HUKUFANYA CHOCHOTE KUMSHAWISHI MTANZANIA WA KAWAIDA KUKUCHAGUA, BASI KIDOGO UNGEFIKA KWENYE KIKAO MAPEMA NA KUWEKA KWENYE CURRICULUMN VITAE YAKO KWAMBA ULIHUDHURIA KIKAO MAPEMA, LAKINI WEE UNACHELEWA TU, CV ITAJAA KWELI ?? teh teh.

haya bana mheshimiwa mbowe, wee endelea tu kufika late kwenye vikao bila sababu maalum, na onyesha ubaguzi wako kwa kutokuwa nyutro !

nasubiri tu habari zaidi maana tumeambiwa tukae tyun-di na nikipata hizo habari nitaendelea na wewe mheshimiwa mbowe !


Kada Pumba
Kwani wewe ndege haijawahi kuwa delayed ukachelewa connection yako inayofuata? Au umezoea madaladala!

Kitendo cha Mbowe kuacha kikao nyeti kama hicho kiongozi na makamu wake mpaka yeye alipofika na kuendelea kuongoza kikao ni ishara ya demokrasia na kuaminiana. Ingekuwa ni handsome boy JK na tabia yake ya kuchelewa masaa mengi bado asingempa kiti Malecela wakati huo, sijui Msekwa. Jk kwa woga wake, pamoja na kuwa ni Rais Vasco Da Gama lakini kila kikao cha chama chenye hisia za mivutano ya hoja tu lazima awepo mwenyewe, akichelewa vikao huwa vinasubirishwa.

Hebu acha zako, mlisema watafarakana,wamewasakama. Sasa mmekosa hoja mnazua vioja.
Mtajiju mwaka huu, endeeleni kuitangaza CHADEMA tu

Asha
 
mifarakano ndani ya chama ndo chanzo ANGALAU wanachama wa Chama cha maendeleo na demokrais(CCMD)wanakataa tofauti zao ndani ya chama ! kila mtu anataka kuwa head wa chama, sasa huko chadema hakukaliki utafikiri wamekalia upupu !

as usual you becoming more a spinner than the spinners themselves.. but well, now people know..what "kada Mpinzani" really means.. kazi ya kada ni kupinga hata ukweli ukimtumbulia macho kama mjusi aliyebanwa na mlango..
 
JUST IN CASE YOU MISSED IT !!

HIKI NDICHO KINAONGELEWA HAPA !!

Kwanza kikao kilichelewa kuanza kwasababu Mwenyekiti alichelewa kuwasili. Kimeanza. Watu wa upande wa Zitto wameomba Mwenyekiti Mbowe asiwe mwenyekiti wa kikao kwasababu ameonyesha dhahiri kwamba hayupo neutral. Makamu wa Mwenyekiti ndiye Mwenyekiti wa kikao hadi sasa. Nitawaletea habari kadri ninavyotumiwa text kutoka ndani ya kikao.

Shetani wenu.



(NA SI VINGINEVYO)!!!!!!!!!1

Kada Pumba

Nimeona wenyewe mmeibadili hii mada mkaleta 'vidole juu', nikahisi labda mnataka tuwajadili 'watoto sio rizki'.

Hii habari ya Shetani kama ingekuwa kweli si ndio ingekuwa habari kubwa ya magazeti ya leo?

Shetani alimdanganya Eva, na Eva akamdanganya Adamu kula tunda la mti wa katikati.

Sijui shetani wetu huyu anataka kutupeleka wapi na habari yake hii?

Asha
 
pole kwa yaliyokukuta, mada ni kwamba mbowe got kicked out of ze meeting, na sasa kuna makundi chadema na wapinzani kwa ujumla, ingawa hawataki kukubali. wape pole wenzako !
 
pole kwa yaliyokukuta, mada ni kwamba mbowe got kicked out of ze meeting, na sasa kuna makundi chadema na wapinzani kwa ujumla, ingawa hawataki kukubali. wape pole wenzako !

R u a saint or an insane?, i tend to be believe that u r z later, please convice me dat u r z former!
 
naona mzee mwanakijiji wamegusa pabaya,
karibu tukupe kadi ya chama cha mapinduzi!
hili nimetumwa
 
am just wondering kama mbowe will make a good come back maana hata afanye nini sasahivi huyu jamaa sijui kama atainuka, maana ni kama vile alijipiga konzi mwenyewe na sasa anatafuta mchawi !

makundi ndani ya chadema chanzo chake ni nini haswa ?? wengine wanadai kwamba, wengi wao mule wanataka vyeo vya juu ndani ya chama, wengine hawajafurahishwa na sifa walizopata zitto, na slaa.
je wapinzani kuzidi kumomonyoka ??
 
Heeh heeh

Mnakula kunywa na kuvaaa. Siku zinaenda, vya bure kupenda kupewa, wanaume kama....

Kwa mipasho, tutakoma mwaka huu. Au sio rizki?

Bahati ya Zitto na CHADEMA hamuwezi kuziba, ametoa Mungu wala hawajaiba, kama mnaweza pandeni juu mkazibe!

Mlisema ooooh wanafarakana, sasa jiandaeni kubadili kauli

Mseme msemayo, yote ni bureeeeee, kwani mapenzi- hayana shuleeee. Yawenzenu midomo juu lakini yetu hamyasemi..

Asha

DADA ASHA.....

umenikosha sana kwa vipande vyako,unanikumbusha HOME SWEET HOME znz island.
 
Hii habari imetoka kwenye gazeti lao la Tanzania Daima la leo. Ukiisoma kwa makini, hasa kwenye maeneo niliyoweka bold, utaona hawa jamaa wamekwisharusha taulo ulingoni wakati bado mpambano mbichii. Sasa kama haka ka-dhoruba ndio kanawafanya hivi, itakuwaje huko mbele?

---Asanteni. Na, ambaye hajawahi kurubuniwa na shetani, hata kuiba cookie, na awe wa kwanza kupinga jina langu. Shetani wenu in JF.


CCM, JK waitega CHADEMA kinamna

na Charles Mullinda

SASA ni dhahiri kwamba jitihada za vyama vya upinzani kukipoka madaraka Chama Cha Mapinduzi (CCM), katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 au hata 2015 ziko kitanzini.

Ukweli huu unadhihirishwa na dhoruba iliyokikumba Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) hivi karibuni, baada ya Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho, Kabwe Zitto, kuteuliwa na Rais Jakaya Kikwete kuwa mmoja wa wajumbe wa kamati ya kupitia upya mikataba ya madini.

Wafuatiliaji wa masuala ya kisiasa ya hapa nchini, wameeleza kuwa ingawa CHADEMA imefanikiwa kumaliza tofauti zilizojitokeza baina ya viongozi wa chama hicho waliokuwa wakivutana kuhusu uteuzi wa Kabwe, mvutano huo umeipa mwanya CCM wa kubaini mbinu za kuisambaratisha.

Maoni tofauti yaliyotolewa kwa Tanzania Daima Jumapili na wafuatiliaji wa siasa za nchini kwa takriban wiki nzima sasa yameonyesha kuwa, CCM itamtumia zaidi Mwenyekiti wake, Rais Jakaya Kikwete kuhakikisha mkakati wake wa kuibomoa ngome ya kambi ya upinzani unafanikiwa.

Habari zinaeleza kuwa magwiji wa fitina za kisiasa ndani ya CCM wameishauri kumsogeza karibu zaidi na Serikali, Zitto, mmoja wa wanasiasa wenye ushawishi kwa kumpangia majukumu mengi mazito ya kitaifa, lakini yenye masilahi bora kwake binafsi.

Kwamba Zitto ambaye sasa nyota yake inang’ara, ndiye anayelengwa kwa nia ya kumfanya silaha muhimu ya kuisambaratisha CHADEMA, chama ambacho kwa sasa kinaoneka kuwa na nguvu kwa upande wa Tanzania Bara, si suala la mjadala wala la siri.

Ukweli kuhusu hali hiyo ulianza kujionyesha mapema na hasa baada ya mbunge huyo kijana kulitikisa Bunge na taifa kwa hoja yake kudai kuundwa kwa kamati teule ya kuchunguza utiwaji saini mkataba wa Buzwagi, hoja ambayo iliwalazimisha wabunge wa CCM kuungana na kumsimamisha kufanya kazi za Bunge ili kuinusuru serikali.

Mbali na Zitto ambaye tayari uteuzi wake katika kamati ya kupitia upya mikataba ya madini nusura ukisambaratishe chama hicho, wengine wanaolengwa kushughulikiwa kwa staili kama ya Zitto ni pamoja na Mkurugenzi wa Vijana wa CHADEMA, John Mnyika na vijana wengine kadhaa wanaoonekana kuinyima raha serikali.

“Watashirikishwa kwa karibu sana katika shughuli mbalimbali za kitaifa, wataangaliwa kimasilahi, watateuliwa katika nafasi nyingine nyeti, nadhani unajua, nafasi kama iliyoachwa na Kabuye (Phares, aliyekuwa Mbunge wa Bihalamuro Magharibi) ipo wazi, nafasi kama hizi zitaelekezwa kwa wanasiasa hawa vijana, watakuwa ‘busy’, najua mwanzo watakuwa wagumu, lakini masilahi mazuri watakayoyapa kwa kazi watakazopewa yatawalainisha tu,” hiyo ni kauli ya kada mashuhuri mwenye ushawishi ndani ya CCM wakati akizungumza na gazeti hili hivi karibuni.

Wachambuzi wanaeleza kuwa wanaamini CCM inaweza kufanikiwa kwa kutumia mkakati huu, kwa sababu wanasiasa vijana wa CHADEMA mbali na kuwa wasomi wazuri na wenye upeo wa kutosha katika kuchanganua mambo, bado wanaweza kuelemewa na majukumu mengi ya kitaifa watakayopewa na serikali pamoja na ya chama chao.

“Najua wengi wanashangazwa na hatua ya rais, kuonyesha dhamira ya dhati ya kushirikiana na viongozi wa kambi ya upinzani katika shughuli mbalimbali za kitaifa, lakini ninakuhakikishia kuwa Rais Kikwete ni mtu makini, anajua anachokifanya.

“… Usidhani kwamba hawa wapinzani wanaoteuliwa wanaachwa tu wafanye wanavyotaka, wanawekwa katika kamati ambazo hawawezi kufurukuta, na hata katika kazi nyingine za kitaifa, watakuwa wakiangaliwa kwa jicho makini, litakalo kuwa likiwadhibiti kufika katika maeneo nyeti yanayoweza kusababisha madhara kwa serikali ya CCM,” anaeleza kada mwingine wa CCM.

Wafuatiliaji wa masuala ya kisiasa walieleza zaidi kwamba, tayari CCM imekwisha kubaini kuwa si rahisi kuwarubuni kwa fedha wanasiasa inaowakusudia, hivyo imejipanga katika kuwapatia marupurupu makubwa katika kazi zao ambayo inaaminika yatayeyusha taratibu ujasiri na ugumu wa mioyo yao.

Walidokeza zaidi kwamba, wasaidizi wa Rais Kikwete wameelekezwa kuwapanga wapinzani hao kusafiri na rais katika safari zake za nje, hususan atakazokuwa akifanya katika mataifa makubwa, huko pia watahusishwa katika shughuli mbalimbali za kitaifa, lakini kamwe ziara hizo hazitatumiwa kushawishi kwa fedha kuwabadili misimamo yao.

“CCM haishindwi kitu, mimi ni mwanamageuzi mkubwa lakini hilo nalitambua, CHADEMA si chama cha kwanza cha upinzani kutikisa katika siasa za nchi hii, kulikuwa na NCCR- Mageuzi, leo imebaki historia, kuna CUF, nguvu zake sasa zimewekwa shakani. Sasa ni zamu ya CHADEMA, haina muda itapita tu, suala ni muda, tuipe muda.

“Na hivi ndiyo imeanza kushughulikiwa. CCM imejua udhaifu wa viongozi wa CHADEMA, itautumia huo kuimaliza, mwaka 2009 haitakuwa na nguvu kama ilizonazo sasa”, alisema mmoja wa wanafunzi wa chuo kikuu aliyehudhuria mdahalo wa siku ya wanafunzi wa vyuo vikuu Jumapili iliyopita, uliofanyika katika Ukumbi wa DDC.

Habari zaidi zinaeleza kuwa, sambamba na CCM kuanza kuishughulikia kambi ya upinzani ili kupunguza makali yake wakati wa uchaguzi mkuu wa 2010, kuachwa nje ya safu ya juu kabisa ya uongozi wa chama kwa baadhi ya makada waliomsadia Rais Kikwete kuingia ni hatua, ni moja ya hatua anazozichukua (Kikwete) kuelekea uchaguzi mkuu ujao.

Mmoja wa makada wanaotajwa zaidi kuwa huenda rais ameamua kuwaacha nje ya sekretariati ya chama hicho akiwa na sababu maalumu ya kuanza kupanga upya safu yake ya ushindi ya 2010 ni Rostam Aziz, anaelezwa kuwa bingwa wa mikakati ya chinichini ambaye atasafisha makovu yaliyoachwa 2005.

Rostam Aziz, mmoja wa makada wa CCM wasomi, mwenye akili za kuzaliwa na anayeaminika kuwa na ukwasi wa kutosha ni mmoja kati ya watu wanaotajwa kuwa walishiriki kwa karibu kampeni zilizowaingiza madarakani marais Benjamin Mkapa, na baadaye Kikwete.

Rostam ambaye mafanikio yake kibiashara kwa baadhi ya wachambuzi wa mambo yamekuwa yakichukua nafasi kubwa ya mjadala hasa wanaorejea historia yake kibiashara tangu akiwa mfanyabiashara wa kununua ngozi hadi sasa anapoaminika kuwa na ukwasi wa kutosha ni nguzo muhimu ndani ya CCM, hivyo kuachwa kwake katika serikali kunaelezwa kuwa ni mbinu za Rais Kikwete kuanza kujipanga upya kabla ya 2010 na hasa katika mkakati wa kuwamaliza wapinzani.

Wasiwasi kwamba Rostam ndiye atakayesimamia operesheni hiyo, zinaanza kuonyesha dalili zake hivi sasa kwani yeye ndiye mwanasiasa anayewasiliana kwa karibu na wanasiasa wote vijana ndani ya CHADEMA na hata CUF wanaoonyesha mwelekeo wa kukitikisa chama hicho tawala.

Aidha, uamuzi wa mwanasiasa na mfanyabiashara huyo maarufu kuwa na hisa katika vyombo kadhaa vya habari nchini kama Mwananchi Communications Ltd na Habari Corporation, unatajwa kuwa moja ya nguzo kuu atakazotumia kukiimarisha chama tawala na wakati huo huo kuvisambaratisha vyama vya upinzani vitakavyoonekana kutoa upinzani makini.

http://www.freemedia.co.tz/daima/2007/11/25/habari2.php
 
Sasa wale waliokuwa wanasema Zitto asiingie kwenye Kamati wajitoe CHADEMA ama sivyo nao tuwaite mambumbumbu wa kufuata nidhamu ya Chama. Hapa Mbowe kapigwa bao na huu ndio mwisho wa ndoto yake ya kuwa Rais wa Jamhuri yetu. Watatudanganya viini macho leo kwamba yameisha na CHADEMA iko moja lakini nyongo zishatumbuka na udhaifu wao sasa uko bayana. Mbowe ana ego kubwa, Zitto ana ego kubwa, Baregu ana ego kubwa, Wangwe ana ego kabambe na Tundu Lissu ana ego kubwa. Hayawezi kuisha leo.

Shetani wenu.
 
kada na wenzake vibar5aka walio kazini hapa WAMEAIBIKA!!!!!!!!!!

TUAMBIENI MAMILIONI MANGAPI MMETUMIA KUFANYA PROPAGANDA..ZA KUWAFANYA WATU WAAMINI WATU WA CHADEMA WANA GOGORO KUBWA,,....

DADA ASHA WAIMBIE....

"..acha maneno katika nyumba za watu mama ...acha umbea katika nyumba za watu babaa...!!

wakielewana mtabaki na aibu........."
 
Back
Top Bottom