Moto mkubwa wateketeza mapipa ya lami wilayani Kilosa

figganigga

JF-Expert Member
Oct 17, 2010
25,490
54,884
Kuna ajali ya moto ilitokea Jumapili juni 18 huko kilosa.Moto uliwaka katika jengo la [HASHTAG]#UJENZI[/HASHTAG] leo jioni ulio sababishwa na wapika [HASHTAG]#Rami[/HASHTAG]
19366308_1954412488125144_4769748789848547195_n.jpg

Mashine azijafikiwa na moto nakuna Mali yeyote ilio teketea ilakunakijana mmojatu muda wa tukio alikuwa anajalibu kuuzima moto kwabahati mbaya akatereza ila akupoteza maisha walimuwaisha hospital

======

mapipa.jpg

Moto mkubwa wateketeza mapipa ya lami wilayani Kilosa yaliyokuwa yamehifadhiwa katika ofisi za ujenzi wilayani humo huku jitihada za jeshi la polisi na wananchi za kuokoa mapipa hayo zikigonga mwamba licha ya kufanikiwa kuudhibiti moto kutoteketeza karakana ya ofisi hiyo.

Wakizungumza na ITV mashuhuda wa tukio hilo wamesema wameshangazwa na kuibuka kwa moto huo ambao wameeleza chanzo cha moto huo na jinsi walivyofanikiwa kuokoa magari mabovu yaliyokuwa jirani na moto huo.

Mkuu wa wilaya ya Kilosa Adam Mgoyi akiwemo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo kesi Mkambara wamewashukuru wananchi kwa ushirikiano walionyesha katika kuokoa mali za serikali.
 
Back
Top Bottom