Moshi: Mwalimu na Wanafunzi 2 wapandishwa kizimbani kwa kuchoma Mabweni ya shule

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,499
9,279
Moshi. Ofisi ya Taifa ya mashtaka nchini Tanzania imewafikisha mahakamani watuhumiwa watatu wakiwemo wanafunzi wawili kwa tuhuma za kuhusika katika matukio ya kuchoma moto mabweni ya shule za sekondari za Uchira na Ebeneza Sango zilizopo Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 5, 2020 mkurugenzi wa utenganishaji wa shughuli za mashtaka na upelelezi wa ofisi hiyo, Oswald Tibabyekomya amesema walifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Moshi jana na leo.

Amesema katika tukio la uchomaji moto bweni la shule ya sekondari ya wasichana Uchira ofisi hiyo imefungua mashtaka ya kuongoza genge la uhalifu yanayowahusu washtakiwa wawili ambapo mmoja ni mwanafunzi na mwingine ni mwalimu, Abdallah Ramadhani. Haya hivyo, Tibabyekomya hakutaja majina ya wanafunzi hao.

Amebainisha kuwa katika tukio jingine la kuchoma moto bweni la shule ya Ebeneza Sango, mashtaka yamefunguliwa kwa mwanafunzi wa shule hiyo.

"Kulingana na upelelezi uliofanyika mpaka sasa kichocheo kikubwa cha matukio haya ni mahusiano mabaya na ushawishi wa vikundi rika visivyofaa mashuleni.”
 
Kama ndio wahusika sheria ifuate mkondo wake. Pia upelelezi ufanyike kuona kama kuna chanzo kingine cha ajari ya moto
 
Walichoma sana shule za kiislamu, sasa wanajichomea wenyewe. Akili za kipumbavu hizo.
 
Moshi. Ofisi ya Taifa ya mashtaka nchini Tanzania imewafikisha mahakamani watuhumiwa watatu wakiwemo wanafunzi wawili kwa tuhuma za kuhusika katika matukio ya kuchoma moto mabweni ya shule za sekondari za Uchira na Ebeneza Sango zilizopo Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Alhamisi Novemba 5, 2020 mkurugenzi wa utenganishaji wa shughuli za mashtaka na upelelezi wa ofisi hiyo, Oswald Tibabyekomya amesema walifikishwa katika mahakama ya hakimu mkazi Moshi jana na leo.

Amesema katika tukio la uchomaji moto bweni la shule ya sekondari ya wasichana Uchira ofisi hiyo imefungua mashtaka ya kuongoza genge la uhalifu yanayowahusu washtakiwa wawili ambapo mmoja ni mwanafunzi na mwingine ni mwalimu, Abdallah Ramadhani. Haya hivyo, Tibabyekomya hakutaja majina ya wanafunzi hao.

Amebainisha kuwa katika tukio jingine la kuchoma moto bweni la shule ya Ebeneza Sango, mashtaka yamefunguliwa kwa mwanafunzi wa shule hiyo.

"Kulingana na upelelezi uliofanyika mpaka sasa kichocheo kikubwa cha matukio haya ni mahusiano mabaya na ushawishi wa vikundi rika visivyofaa mashuleni.”
Ushawishi wa Vikundi rika Mwalimu + Mwanafunzi?
 
Kama kuna watu wa kutoa ushahidi watoe mapema haki ipatikane kwa wahanga wa moto na watuhumiwa isije baada ya muda ikaanza vurugu tena za kutaka mambo ambaya hayaeleweki
 
Wapewe dhabu kali sana...



Cc: mahondaw
Utakua una umwa wewe, wapewe adhabu kali kwani umethibitisha ni wao walichoma hizo shule?!

Polisi Tanzania hii wanakamata yeyote kisha wanamlazimisha akubali kosa, kwasababu hawajui kuchunguza.

Na akikataa atapigwa mpaka akubali.
 
Duuuuh sheria ifuate mkonndo wake, but haki itendeke ktk sheria hyo
 
Miss Bad news katika uboura wako..!!
But, nakupongeza sana Miss Zomboko maana wewe ni miongoni mwa members wachache walioweza kujibrand au kuspecialize kwenye kitu fulani tu hapa JF.
Whenever I see your thread..I gat to see Bad news
 
Back
Top Bottom