Kama kawadia yangu napenda kula raha kila wakti noti zikijaa mfukoni. Jana nilikuwa Morogoro kwenye hotel ya Mbunge Shabib, inaitwa MORENA, njiani kabisa pale Msamvu. Hotel Porsche sana! Kilichonishangaza, maji ni ya kumwaga ukilinganisha na maisha yetu ya Dar. Lakini pia Moro maji ni shiiida, kila kona watu wanazunguka na madumu mekundu. Nikaanza kutafuta nini na wapi Morena anapata maji.
Maji ya Morena yanatoka MORUWASA kinyume na taratibu za ugawaji maji mijini. MORENA amepewa bomba la inchi 4 peke yake wakati majirani wanahangaika na maji ya kunywa. Huu ndo ufisadi wa wafanyabiashara kama Shabib kwa kushirikiana na taasisi ya serikali, MORUWASA. MORENA anapewa bomba ambalo kawaida hutumika kuwapa maji wateja wasiopungua maelfu!
Nchi imejifia tu! Eti Shabib na wenzake ktk biashara ya hotel, wana hadhi kuliko taratibu za MORUWASA!
Maji ya Morena yanatoka MORUWASA kinyume na taratibu za ugawaji maji mijini. MORENA amepewa bomba la inchi 4 peke yake wakati majirani wanahangaika na maji ya kunywa. Huu ndo ufisadi wa wafanyabiashara kama Shabib kwa kushirikiana na taasisi ya serikali, MORUWASA. MORENA anapewa bomba ambalo kawaida hutumika kuwapa maji wateja wasiopungua maelfu!
Nchi imejifia tu! Eti Shabib na wenzake ktk biashara ya hotel, wana hadhi kuliko taratibu za MORUWASA!