Morogoro: Wagonjwa watembea na drip mkononi wakitafuta maji!

QUALITY

JF-Expert Member
Sep 27, 2010
853
115
Ndugu zangu,
tayari Serikali mpya ya CCM imeanza kutekeleza mikakati ya maisha bora kwa kila mtanzania. Leo katika taarifa ya habari saa 2 usiku kupitia ITV, imeripotiwa kuwa Hospitali ya mkoa wa Morogoro haina maji na hivyo wagonjwa wanatoka na drip mkononi kwenda kutafuta maji nje ya hospitali. Naye mbunge wa morogoro Aboud, amethibitisha hilo.

Wenzetu mlio Morogoro, jaribu kutuwekea picha ya baadhi ya wagonjwa waliokuwa wakitafuta maji na mtuwekee hapa kuonesha reality.

Maswali ya kujiuliza:
1. je kweli serikali inawajali wananchi katika hali hiyo?
2. je ni kweli kuwa hospitali haina hela za kuhakikisha maji yapo?
3. Hayo ni sehemu ya maisha bora?
4. Au kikwete hajatengeneza indicators za maisha bora ndo maana maswali yanakuwa mengi kwake?

Nawasilisha
 
Pamoja na mito yote ya mkoani morogoro eti hakuna maji duu ccm oneeni huruma wananchi!court of hague itafurika wana ccm very soon
 
Hivi si nilisoma gazeti jana aboud kaenda hospitali kuangalia matatizo waliyonayo? Ina maana alaienda kuuza sura???????? Na kutafuta abiria wa aboud bus service? Ccm bwana kweli inaweka vioyo kweli! Wamulize sugu mbeya kapta wapi vitanda mbeya, au lema arusha kapata wapi ambulance na trekita na kusomesha sekondari vijana 500 waliofaulu, au wenje mwanza anafuta ada za sekondari, au vincent nyerere -anafakamia barabara kama ahana akili nzuri na kusomesha watoto 100, -hivi abudi anawaza nini? Au pancha na break ziligoma kwenye mabsi?
 
Back
Top Bottom