Morogoro: Stand ya Daladala kuhamishiwa kilomita 2+ kutoka katikati ya mji ni kero kwa Wananchi

Faana

JF-Expert Member
Dec 12, 2011
31,685
32,993
Ndugu wanajamvi,

Nimefika mjini Morogoro kwenye hekaheka zangu nikashangazwa na kitendo cha kuhamishia stand ya daladala kutoka katikati ya mji na kuipeleka karibu na Chuo Kikuu cha Sokoine umbali wa kama Km 2+.

Ni jambo jema kuboresha huduma kwa jamii kutokana na kukua kwa mji, lakini viongozi wa jambo husika hawakaushirikisha mawazo ya wananchi katika kufikia maamuzi ya jambo walilofanya.

Daladala zinazoingia na abiria waendao kufuata mahitaji katikati ya mji wanashushwa mbali na mji na kulazimika kukodi bajaji na pikipiki ili wafike katikati ya mji kitendo ambacho kinawaongezea gharama wananchi ambao wengi wao ni wa kipato cha chini.

Bajaji ambazo ndiyo msaada wa haraka nazo zimeondolewa katikati ya mji na kulazimu wananchi kutembea umbali mrefu kwenda kutafuta usafiri wa kuunganisha ili waende waendako, mathalani mtu atokaye Msamvu kwenda Bigwa analazimika kuchukua pikipiki kwenda mpaka mjini kati ndipo apate daladala ya kwenda Bigwa.

Changamoto ni nyingi sana, nashauri mamlaka husika zishirikishe mawazo ya wananchi ili kuondoa usumbufu unaoendelea kujitokeza mapaka sasa na kuathiri kwa kiasi kikubwa majukumu ya watu na kuwaongezea gharama za maisha wananchi wa kipato cha chini.

Ikumbukwe kuwa maamuzi yalifanywa na viongozi bila kushirikisha wananchi, lakini viongozi hao hawakuvaa viatu vya wananchi husika ili nao wapate feelings ambazo wananchi wanazipata kwa sasa kwakuwa viongozi husika hawatumii daladala, laiti wangekuwa wanatumia daladala wangeona adha hizo na huenda wasingechukua uamuzi waliochukua.

Nawasilisha
 
Huu mtindo wa hovyo mno , ina maana kila stend ikibanana mnahamisha, ikibanana tena mnahamisha mwisho watafika Dodoma au Iringa Kwa kuhamisha hamisha. Kwa nn wasijenge nyingine karbu wakatenganisha Tu route, huku zikabaki za kwenda kule na stemd mpya zikabaki za route nyingine kuliko kupeleka watu pori.
 
Huu mtindo wa hovyo mno , ina maana kila stend ikibanana mnahamisha , ikibanana tena mnahamisha mwisho watafika Dodoma au Iringa Kwa kuhamisha hamisha, Kwa nn wasijenge nyingine karbu wakatenganisha Tu route, huku zikabaki za kwenda kule na stemd mpya zikabaki za route nyingine kuliko kupeleka watu pori
Upo sahihi kabisa, kama wananchi wangekuwa wanashirikishwa katika maamuzi ingesaidia sana kupata mawazo mbadala lakini ni watu wachache hujifungia ndani na kutoa maamuzi, mbaya zaidi wanaotoa maamuzi hawatumii usafiri wa daladala, ni watu wanatumia usafiri wa serikali kwahiyo ni ngumu kuonja adha wanayopata wananchi.
 
Kuhamisha stand haiepukiki, ni moja ya matokeo ya maendeleo na ukuaji wa miji.

Ya Dar es Salaam ilikua Kisutu, ikahamia Ubungo zilikua km9 toka mjini. Sasa imetoka Ubungo imepelekwa Mbezi Luis km26 toka mjini na bado watu wanadunda tu.

Usiogope mabadiliko.
 
Kuhamisha stand haiepukiki, ni moja ya matokeo ya maendeleo na ukuaji wa miji.

Ya Dar es salaam ilikua kisutu, ikahamia ubungo zilikua km9 toka mjini. Sasa imetoka ubungo imepelekwa mbezi Luis km26 toka mjini na bado watu wanadunda tuu

Usiogope mabadiliko

Upo sahihi, lakini kinacholalamikiwa ni utaratibu wa kuwafikisha abiria katikati ya mji ambako ndiko mahitaji muhimu yalipo, kwa mfano mtu anayetoka Msamvu kwenda Polisi, Hospital, anashushiwa Masika na ili apate bus la kwenda Msamvu ni lazima aende huko porini umbali sawa na Msamvu.

Nashauri magari yaruhusiwe kushusha na kupakia abiria katikati ya mji bila kufanya maegesho ya zaidi ya dakika kwakuwa wapo wenye matatizo mbalimbali yakiwemo ya kiafya na hawana uwezo wa kukodi pikipiki na bajaji kwenda mpaka huko porini ili wakapande mabasi ya kwenda Msamvu, Kihonda na Tungi.
 
1606813091028.png

Msaada katika kuionyesha kwenye ramani tafadhali Ahyan
 
Eneo la SUA ila ni mbele ya Mafiga Secondary... mkabala na kituo cha mafuta T.O.T pembeni mwa barabara iendayo Iringa... ukiwaambia watu SUA direct.. unawachanganya
Kwahiyo hapo iliyokuwa stendi ya daladala wanajenga nini?
 
Nchi hii haijawahi kuwa na mipango , Tulipohamishwa kutoka Mnazi mmoja na Kisutu kupelekwa ubungo tukajua yameisha , sasa ni hivi ni Mbezi Luis , lakini nakuapia haitoisha miaka mingi tutapelekwa Kibaha .
 
Wanapeleka kalibu na viwanja vyao, huu ni ujinga kabisa na ni kama serikali pia haina mipango ya mda mrefu, yani kimji kama Lamadi ya Mwanza pia wanaamisha wakati stendi ndo imechangamsha mji.
 
Kuhamisha stand haiepukiki, ni moja ya matokeo ya maendeleo na ukuaji wa miji.

Ya Dar es salaam ilikua kisutu, ikahamia ubungo zilikua km9 toka mjini. Sasa imetoka ubungo imepelekwa mbezi Luis km26 toka mjini na bado watu wanadunda tuu

Usiogope mabadiliko
Hata Ubungo Tanesco pale chini palikua na Stendi ya Daladala sahivi iko mbezi Luis kitambo sana pale pamebaki gofu tu.

Na mwendokasi itafika Kibaha.
 
Kuhamisha stand haiepukiki, ni moja ya matokeo ya maendeleo na ukuaji wa miji.

Ya Dar es salaam ilikua kisutu, ikahamia ubungo zilikua km9 toka mjini. Sasa imetoka ubungo imepelekwa mbezi Luis km26 toka mjini na bado watu wanadunda tuu

Usiogope mabadiliko
Kuna tofauti ya kuamisha kuepusha misongamano na kuamisha imradi tu mna mamlaka, jua hii tofauti kwanza.
 
Daladala hawana nidhamu. Unaonaje trafick jam inayosababishwa na daladala kupaki nje ya stand wakisubiria wateja? Kwani ni wapanda daladala tu ndio wanafanya shughuli za kiuchumi Morogoro?

Mwanakulitafuta, mwana kulipata.
 
Kuhamisha stand haiepukiki, ni moja ya matokeo ya maendeleo na ukuaji wa miji.

Ya Dar es salaam ilikua kisutu, ikahamia ubungo zilikua km9 toka mjini. Sasa imetoka ubungo imepelekwa mbezi Luis km26 toka mjini na bado watu wanadunda tuu

Usiogope mabadiliko
Tatizo hatunaga longterm plan ina maana hko nako kukibana watahamisha mama D

Lazima tujitahidi tuwe na mipango endelevu.

Ova
 
Back
Top Bottom