Morogoro: Serikali kumpima mtoto anayedhaniwa kuwa na kipaji cha hesabu

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,000
9,862
Mtoto Charles Mathias Mbena(6) mkazi wa Kibungo Juu, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ameonesha kipaji cha hesabu ambapo anaweza kujumlisha na kutoa hesabu za makumi na malaki bila kutumia karatasi.

Mtoto huyo anayesoma darasa la awali katika Shule ya Msingi Nyigwa ametakiwa kufanyiwa majaribio ili kumpeleka katika Shule na darasa analostahili.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Emmanuele Kalobelo amesema wamegundua ana kipaji hivyo watamfanyia majaribio.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala ameelezea azma yao ya kuboresha mazingira ya Shule ya Msingi Nyigwa kwa kuijengea madarasa manne mbali na mawili ambayo yanamaliziwa na Mkurugenzi.



Pia soma: Serikali yaagiza mtoto Charles Mathias arushwe darasa kutoka Chekechea hadi Primary, Babu Tale aahidi kumlipia ada
 
Katika hatua nyingine Katibu Tawala ameelezea azma yao ya kuboresha mazingira ya Shule ya Msingi Nyigwa kwa kuijengea madarasa manne mbali na mawili ambayo yanamaliziwa na Mkurugenzi wa Mkoa
Mnaboresha madarasa kama zawadi kwakuwa amepatikana mtoto mwenye kipaji hapo? Shule zisizo na watoto wenye kipaji waendelee ku suffer
Je, mna mpango gani wa kuibua vipaji vingine zaidi ya hicho katika maeneo mengine?
 
Africa kichwa ya mwenda hazimu km ntoto ana kipaji basi bas ni rahis sn kuelewa uyo inabod afundishwe ktk special school ndan ya mwaka mmoja tu ashamaliza form six upo chuo anapiga computer engineering hawa ndio huwa wanakujaga vumbua vitu sababu kwao ni rahoc kuelewa kitu.
 
Mnaboresha madarasa kama zawadi kwakuwa amepatikana mtoto mwenye kipaji hapo? Shule zisizo na watoto wenye kipaji waendelee ku suffer
Je mna mpango gani wa kuibua vipaji vingine zaidi ya hicho katika maeneo mengine?
Tanzania karibu watoto wengi ni vipaji sema mazingira mabovu tuu shule hazina madarasa wala walimu ukiona picha ya shule ya huyo mtoto utadhani ilipigwa sudani kusini na wakurugenzi wapo wakipitisha Vocha za V 8 ya milion 400.
 
Kumpima? Wanampimaje? Kwanini hivyo vipimo wasivisambaze kwenye mashule yote ili tupimane wote?

Hizi Siasa shida sana, sitashangaa badala ya waalimu na wataalamu kumpima ukashangaa mbunge, mkuu wa mkoa na mkuu wa wilaya ndio wapimaji wakuu (bila kusahau makamera na waandishi wa habari). Kupeana stress tu, na presha katika umri mdogo
 
Mtoto Charles Mathias Mbena(6) mkazi wa Kibungo Juu, Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro ameonesha kipaji cha hesabu ambapo anaweza kujumlisha na kutoa hesabu za makumi na malaki bila kutumia karatasi.

Mtoto huyo anayesoma darasa la awali katika Shule ya Msingi Nyigwa ametakiwa kufanyiwa majaribio ili kumpeleka katika Shule na darasa analostahili.

Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro, Mhandisi Emmanuele Kalobelo amesema wamegundua ana kipaji hivyo watamfanyia majaribio.

Katika hatua nyingine Katibu Tawala ameelezea azma yao ya kuboresha mazingira ya Shule ya Msingi Nyigwa kwa kuijengea madarasa manne mbali na mawili ambayo yanamaliziwa na Mkurugenzi.
Umaskini wa muafrika uko kwenye akili yake.
 
Back
Top Bottom