Yaani ndugu nchi hii kuna matatizo makubwa, sasa mtu anazungumza as if yeye mama angekuwepo ndiyo moto usingewaka??Wakati anaondoka moto ulikuwa unawaka ama la?
Alimradi kila mtu anaweza kukamata keypad na kuandika anachopenda.Yaani ndugu nchi hii kuna matatizo makubwa, sasa mtu anazungumza as if yeye mama angekuwepo ndiyo moto usingewaka??
Au hata kama angekuwepo yeye ndiyo jeshi la zimamoto angeenda kuuzima.
Everyday is Saturday...............................
Kuna watu ndani ya system hawamtaki Mama! Na haya majanga ni msg sema sisi bado hatusanuki tu!!HIZI NI HUJUMA AU?
mbona majanga yanazidi kila kukicha?
Enzi Za JP.
Upuuzi mwingi tulikuwa tumeusahau!
Tulibaki kulia na mambo madogo sana (Inshu za wanasiasa)
Lakini, Maisha Yalienda Vizuri pasi na Shida!
Huyu Mama Huyu??
Moto mkubwa umeunguza na kuteketeza kituo kikubwa kabisa chenye mitambo maalumu ya kupokea, kupoza na kusambaza Umeme kuelekea Mikoa ya Morogoro, Dar es salaam, Tanga na Kilimanjaro
Moto huo bado haujazimika hadi sasa na juhudi za kuuzima zinaendelea
Hadi sasa chanzo cha moto huo hakijulikani
View attachment 1877226
ITV
Joel 2: 10 - 17
10: Nchi inatetemeka mbele yao; mbingu zinatetemeka; jua na mwezi hutiwa giza, na nyota huacha kuangaza; 11naye BWANA anatoa sauti yake mbele ya jeshi lake; maana matuo yake ni makubwa sana; kwa maana yeye ni hodari atekelezaye neno lake; kwa kuwa siku ya BWANA ni kuu, yenye kitisho sana; naye ni nani awezaye kuistahimili?
12 Lakini hata sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea; 13rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema, naye hughairi mabaya. 14N’nani ajuaye kwamba hatarudi na kugeuka, na kutuachia baraka nyuma yake, naam, sadaka ya unga, na sadaka ya kinywaji, kwa BWANA, Mungu wenu?
15Pigeni tarumbeta katika Sayuni,
Takaseni saumu, kusanyeni kusanyiko kuu;
16 Kusanyeni watu, litakaseni kusanyiko,
Kusanyeni wazee, kusanyeni watoto,
Na hao wanyonyao maziwa;
Bwana arusi na atoke chumbani mwake,
Na bibi arusi katika hema yake.
17 Hao makuhani, wahudumu wa BWANA, na walie
Kati ya patakatifu na madhabahu,
Na waseme, Uwaachilie watu wako, Ee BWANA,
Wala usiutoe urithi wako upate aibu,
Hata mataifa watawale juu yao;
Kwani waseme kati ya watu, Yuko wapi Mungu wao?
WATANZANIA, HAYA MABAYA YANATUPATA SISI NA WATOTO WETU KWA SABABU TUMEMWACHA MUNGU, TUMEKATAA KUTAMBUA UKUU WAKE UWEZA WAKE ULIOTUPITISHA KATIKA MAMBO MENGI TANGU MWANZO WA TAIFA HILI. TUMRUDIE MUNGU ATUREHEMU. KILA MATU ASEME NA WATU WANYUMBANI MWAKE. TUUNGAME DHAMBI ZA TAIFALETU ILI MUNGU ATUSAMEHE NA KUMUAMURU MALAIKA WA KISASI CHA MUNGU ARUDISHSE UPANGA WAKE ALANI MWAKE.
Bahati mbaya kanuni ya Mungu, viongozi mara nyingi huwa ni wa mwisho. Angalia hapa.Si heri aadhibiwe kiongozi Sasa dagaa tuna ubaya gani?
La huyu mama jamani.Bahati mbaya kanuni ya Mungu, viongozi mara nyingi huwa ni wa mwisho. Angalia hapa.
1 Mambo ya Nyakati 21:1-17
Shetani akajitokeza kuwataabisha Waisraeli, akamshawishi Daudii awahesabu watu. Hivyo, Daudi akamwambia Yoabu na wale makamanda wengine,
“Nendeni mkawahesabu Waisraeli, kutoka Beer-sheba mpaka Dani. Nileteeni ripoti ili nijue idadi yao.” Lakini Yoabu akasema, “Mwenyezi-Mungu na awaongeze Waisraeli mara mia kuliko walivyo sasa! Bwana wangu mfalme, kwani hawa wote si watumishi wako? Kwa nini basi unataka kufanya jambo ambalo litawatia Waisraeli katika hatia?”
Lakini tamko la mfalme lilikuwa na nguvu zaidi dhidi ya Yoabu.
Hivyo, Yoabu akaenda katika nchi yote ya Israeli, kisha akarejea Yerusalemu. Yoabu akampelekea mfalme Daudi idadi ya watu:
Katika Israeli yote, kulikuwamo wanaume 1,100,000, wenye ujuzi wa kutumia upanga;
na katika Yuda kulikuwamo watu 470,000, wenye ujuzi wa kutumia upanga. Lakini Yoabu hakuwahesabu Walawi na Wabenyamini, kwa sababu alichukizwa sana na amri ya mfalme.
Mungu hakupendezwa na jambo hilo kwa hiyo akaiadhibu Israeli. Daudi akamwambia Mungu,
“Nimetenda dhambi kubwa kwa tendo hili nililolifanya! Lakini nakuomba unisamehe mimi mtumishi wako, kwani nimefanya jambo la kipumbavu kabisa.” Basi, Mwenyezi-Mungu alisema na Gadi, mwonaji wa Daudi, akamwambia,
“Nenda umwambie Daudi kwamba mimi Mwenyezi-Mungu ninampa mambo matatu. Ajichagulie mojawapo nami nitamtendea.” Hivyo Gadi akamwendea Daudi na kumwambia,
“Mwenyezi-Mungu anasema hivi: Jichagulie mojawapo:
Njaa ya miaka mitatu, au
miezi mitatu ya maangamizi kutokana na maadui zako ambapo upanga wa maadui zako utakushinda; au
siku tatu ambapo Mwenyezi-Mungu atawashambulia kwa upanga wake, awaletee maradhi mabaya nchini, na malaika wake apite kuwaangamiza katika nchi nzima ya Israeli.
Sasa amua, ni jibu lipi nitakalompa yeye aliyenituma.” Daudi akamjibu Gadi,
“Nimeingia katika mashaka makubwa! Lakini afadhali niadhibiwe na Mwenyezi-Mungu kwani yeye ana huruma sana. Ila nisianguke katika mkono wa mwanadamu.” Basi, Mwenyezi-Mungu akawaletea Waisraeli maradhi mabaya, ambayo yalisababisha vifo vya Waisraeli 70,000. Halafu Mungu akatuma malaika aende kuuharibu Yerusalemu; lakini kabla hajafanya hivyo, Mwenyezi-Mungu akageuza nia yake na kumwambia malaika huyo aliyetekeleza maangamizi, “Basi, yatosha!”
Malaika alikuwa amesimama karibu na uwanja wa kupuria nafaka wa Ornani, Myebusi. Daudi akainua macho yake, akamwona huyo malaika wa Mwenyezi-Mungu amesimama kati ya mbingu na dunia, naye ameunyosha upanga wake juu ya Yerusalemu tayari kuuangamiza.
Hapo Daudi na wazee wote walikuwa wamevaa mavazi ya gunia, wakaanguka kifudifudi. Daudi alimwambia Mungu, “Je, si mimi niliyetoa amri watu wahesabiwe? Ni mimi niliyetenda dhambi na kufanya uovu. Lakini kondoo hawa wamefanya nini? Nakusihi sana, ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wangu, mkono wako uwe dhidi yangu na dhidi ya jamaa ya baba yangu, lakini maradhi haya mabaya yasiwapate watu wako.”