Morogoro Mjini: Abood atawasaidia nini bungeni?

Magezi

JF-Expert Member
Oct 26, 2008
3,359
692
Mimi nimesikitishwa sana na wananchi na wakazi wa mkoa wa Morogoro kwa kuchagua mwarabu (Aziz Abood) awe mbunge ili hali tunajua kabisa walitutesa wakati wa ukoloni, wametuibia sana na hawalipi kodi.

Warguru mnamatatizo gani??? au ni kutokuwa na elimu????
 
Morogoro na Tabora ni kama wamelaaniwa kwa wadosi, kulikua na Yule wa Mvomero, kuna yule wa GAIRO, na sasa Abood, na ikumbukwe zama za SHAMIM kHAN, ni watu wasi na msaada wowote, na kwambia hawana msaada wowote
 
Morogoro na Tabaro ni kama wamelaaniwa kwa wadosi, kulikua na Yule wa Mvomero, kuna yule wa GAIRO, na sasa Abood, na ikumbukwe zama za SHAMIM kHAN, ni watu wasi na msaada wowote, na kwambia hawana msaada wowote

Kweli mkuu sitegemei abood aache biashara zake alafu aka hangaikie wananchi ambao maisha yamepinda kinoma.
 
Kweli mkuu sitegemei abood aache biashara zake alafu aka hangaikie wananchi ambao maisha yamepinda kinoma.

Abood kama walivyo wafanya biashara wenzake, hawana nia ya kuwasaidia WATANZANIA, WANAENDA KUTETEA MASLAHI YA WAFANYA BIASHARA WENZAO, Shabiby miaka 5 iliopita alistick kulalamikia asilimia ya kodi kwenye mafuta. hakuwa na hoja dhidi ya watu maskini, hakuwapigania wala kuwatetea, hawa si wazalendo wa Moyo wala wa Kuigiza, ni wachumia tumbo kwa maslahi yao.
 
Someni historia vizuri mtajua kuwa mwarabu alitumika kama middleman kwenye biashara ya utumwa waafrika tulienda utumwani bara la amerika na ulaya na kwenye mapinduzi ya viwanda huko ulaya na amerika ndio ukawa ukomo wa biashara ya utumwa. Pengine kuna chuki nyingine zaidi ya hiyo ila kwa suala la utumwa hapana au labda hayo majina yao AZIZI/AHMED/SADIQ na sio CHRISTOPHER etc
 
Ndugu Zangu Acheni kumchanganua Mtu kwa Tabaka Lake i.e Mwarabu Mnaonekana Hamjaendelea Utawala wa Kiarabu ulipita karne nyingi zilizopita -- Kweli yeye ni mfanyabiashara, kuna watu wengine weusi lakini hawajafanya kitu chochote jimboni kwao Mr. Mkulo Jirani yake amefanya nini jimboni mwake?

Tafadhani Nchi yetu Ni ya Kila Raia wa kila RANGI acheni hayo... Mimi ni shabiki wa Chadema lakini sipendi kubaguana kwa Rangi ni mbaya
Mfano Mzuri Mohamed Dewji; Ameiimarisha Singida Mjini zaidi ya Lau Masha Nyamagana na naona nyie mngeona bora kudhalilishwa na Lau?

Angalia America as long as you are a Citizen you can apply for any position... Kuna wahindi Magavana; ndio maana nchi hii inaendelea na nadhani Tanzania ni same... Hatujali matabaka ya rangi, dini au kabila. WE ARE VERY DIFFERENT COMPARING WITH OTHER AFRICAN NATIONS, WE HAVE 2 BE PROUD AND STOP LUNATIC THINKING...
 
Abood kama walivyo wafanya biashara wenzake, hawana nia ya kuwasaidia WATANZANIA, WANAENDA KUTETEA MASLAHI YA WAFANYA BIASHARA WENZAO, Shabiby miaka 5 iliopita alistick kulalamikia asilimia ya kodi kwenye mafuta. hakuwa na hoja dhidi ya watu maskini, hakuwapigania wala kuwatetea, hawa si wazalendo wa Moyo wala wa Kuigiza, ni wachumia tumbo kwa maslahi yao.

Mkuu umenena kwali nakumbuka hata kwenye kikao cha budget kila akichangia utamsikia akisema (((((MIMI KAMA MDAU))))) Yani Hawa watu wa TABORA MOROGORO sijui wataelimika lini kwani,,Hawa waarabu na wahindi siko zote hawajawahi fikiria kumsaidia Mtanganyika wao wanachuma tu na kwenda kulia CANADA na Ulaya,, ndo hawa hawa ni vinara wawizi,uhujumu,,watoa rushwa wakubwa na ndo wanatumalizia TEMBO wetu miongoni mwa hawa wahindi na waarabu utajiri wao umetokana na pembe za ndovu,,,,,,wanapoona pa kujifichia ni Bungeni,,
 
Watu wa Morogoro mjini wanapenda sana pilau! Huyo Aboud huwapa pilau na lorry la kubebea maiti kwenda Kuzikia....!
 
Labda wanawashangaa rangi za ngozi zao na kuwaona bora kuliko wao..
 
Mimi nimesikitishwa sana na wananchi na wakazi wa mkoa wa Morogoro kwa kuchagua mwarabu (Aziz Abood) awe mbunge ili hali tunajua kabisa walitutesa wakati wa ukoloni, wametuibia sana na hawalipi kodi.

Warguru mnamatatizo gani??? au ni kutokuwa na elimu????

Kaka mi sijaipenda hii ilivyokaa. Sababu ya Azizi kuwa mwarabu si sababu tosha ya kum-disqualify yeye kuwatumikia watanzania.

Embu tuache kuweka tofauti za kirangi ama dini ama kabila,ishu ya msingi ni uwezo wa Aziz kuweza kuwatumikia wanchi(Devotion) akaacha biashara zake ambazo najua ki uhakika zinahitaji muda. Mimi ni mweusi na mkristo, ila siwezi kumyima kura mtu mweupe Mwislam kama ana uwezo wa kunifanya mimi kufika pale ninapoona.So ishu za udini na rangi hazitakiwi kuletwa hapa,cha msingi tuongelee uzalendo kama Obama alivyomzalendo kwa America ingawa ni Mweusi!

Wakristo,waislam,weupe,weusi yeyote yule kama anaweza apewe nafasi.Sipingi wazo lako kuwa Abood hana uwezo wa kuongoza hasha,napinga dhana yako ya kum disqulify kwa sababu warabu walihusika kwenye utumwa!

Mbona kuna watu kibao ambao si weusi ingawa ni watanzania wanaweza kuongoza nchi kwa uzalendo utafikiri babu zao walitoka milima ya usambaa!!Tuchague maneno ya kusema,tusije kuta tunapandikiza mbegu za ubaguzi ambazo jirani zetu wa soutth wanahangaika nazo mpaka sasa!!
 
Mimi nimesikitishwa sana na wananchi na wakazi wa mkoa wa Morogoro kwa kuchagua mwarabu (Aziz Abood) awe mbunge ili hali tunajua kabisa walitutesa wakati wa ukoloni, wametuibia sana na hawalipi kodi.

Warguru mnamatatizo gani??? au ni kutokuwa na elimu????

Now i know i have arrived at the home of great thinkers! so pathetic

Did you think before posting that?
 
Nenda Morogoro ijumaa ukaone watu wanavyoshuka toka milimani kupewa misaada na wakuu wa mji kama kina Abood ndio unaweza kupata picha halisi ya hali yetu ilivyo. Guys, tumehimizane na kusaidiana kuondoa ujinga maana vinginevyo, tutaendelea kuota ndoto tu.
 
Kaka mi sijaipenda hii ilivyokaa. Sababu ya Azizi kuwa mwarabu si sababu tosha ya kum-disqualify yeye kuwatumikia watanzania.

Embu tuache kuweka tofauti za kirangi ama dini ama kabila,ishu ya msingi ni uwezo wa Aziz kuweza kuwatumikia wanchi(Devotion) akaacha biashara zake ambazo najua ki uhakika zinahitaji muda. Mimi ni mweusi na mkristo, ila siwezi kumyima kura mtu mweupe Mwislam kama ana uwezo wa kunifanya mimi kufika pale ninapoona.So ishu za udini na rangi hazitakiwi kuletwa hapa,cha msingi tuongelee uzalendo kama Obama alivyomzalendo kwa America ingawa ni Mweusi!

Wakristo,waislam,weupe,weusi yeyote yule kama anaweza apewe nafasi.Sipingi wazo lako kuwa Abood hana uwezo wa kuongoza hasha,napinga dhana yako ya kum disqulify kwa sababu warabu walihusika kwenye utumwa!

Mbona kuna watu kibao ambao si weusi ingawa ni watanzania wanaweza kuongoza nchi kwa uzalendo utafikiri babu zao walitoka milima ya usambaa!!Tuchague maneno ya kusema,tusije kuta tunapandikiza mbegu za ubaguzi ambazo jirani zetu wa soutth wanahangaika nazo mpaka sasa!!

marshal hongera hakika umenena,hawa wabaguzi watoe ubaguz wao humu jamvini,wakumbuke kua dhambi ya ubaguzi itawaandama mpaka kwenye makaburi yao,hata mwalimu nyerere alisema,hakika wote wenye ubaguzi wajue hiyo nilaana itawaandama,tanzania haina ubaguz,tusibagau nduguzetu weupe,angalia dadazetu wangapi wakiswahili wameolewa nawatu weupe,je wale watotowao ambao cc niwajombazetu nawenyewe tuwabague.
 
Tatizo ni shule tu, jamaa kawanunulia pombe na vijikhanga basi wakaona ndo wamepata kila kitu!
 
Someni historia vizuri mtajua kuwa mwarabu alitumika kama middleman kwenye biashara ya utumwa waafrika tulienda utumwani bara la amerika na ulaya na kwenye mapinduzi ya viwanda huko ulaya na amerika ndio ukawa ukomo wa biashara ya utumwa. Pengine kuna chuki nyingine zaidi ya hiyo ila kwa suala la utumwa hapana au labda hayo majina yao AZIZI/AHMED/SADIQ na sio CHRISTOPHER etc

Again! Watanzania bado tumebobea ktk uvivu wa kufikiria! hatuna kasumba ya kujiuliza hivi ni kwa nini kitu fulani kitokee? ili tufanye tathmini ya chanzo na hatimaye kufikia utatuzi ( problem solving), hilo kwa kweli ni Zero!. Kuna mtu anatoa kura yake sababu ya kumuogopa mtu(because of their status), kuna hao watatoa sababu ya udini, kuna hao wa sababu he/she is good looking, kuna wanaotoa sababu ya kasumba ya ubabaikiaji, kuna hao wanaotoa sababu ya njaa zao bila ya kujiuliza mara mbili!. Hii ni laana tena kubwa sana na itachukua muda kutokomeza kasumba hii!

Ee Mungu utupe nguvu ya kuwaelimisha watanzania wenzetu ili wote kwa pamoja tusonge mbele! leo young peoples of England are marching up just because the new coalition wameongeza student fees 3 times higher na wamesema wamekuwa betrayed na new coalition where majority of students voted for. They decided not to vote again for the two parties in the next election!
 
Mimi ninachofikiria ni kwamba kuna wabunge ambao ni wa rangi yetu weusi lakini nao pia hakuna walichotufanyia hata wanaoingia mikataba feki ni wenzetu weusi.

Mimi nasimamia utendaji wa kazi na sio rangi ya mtu, kwani hata viwanda vya morogoro vilijengwa kwa nguvu ya yule waziri wa rangi ya Azizi akiwa waziri wa fedha na ndio waliomsaidia Mwl kuleta uhuru ila kwa kuwa historia haiwaandiki watz wengi hatujui hilo.

Kwa kuhusu Azizi mi nadhani tumpime kwa utendaji wake na sio rangi yake na kwa kweli sisi tulio nje ya tz tunaona jinsi gani inauma unavyobaguliwa kwa rangi yako,hivyo wana jf huu ni wakati wetu chadema kusonga mbele na sio kuangalia rangi ya mtu,kwani inanipa tabu saana je ktk chama chetu akija mwanachama wa rangi ya abood je tutamtupa nje? tubadilike wa tz

mapinduziiiiiiiiiiii daimaaaaaaaaaaaa
 
People:

Demokrasia ina gharama zake. Kwa kihistoria tu Morogoro sio watu wabaguzi. Mbunge wa kwanza ni Oscar Kambona. Hivyo mtu yoyote anayeweza kujieleza na kuchaguliwa bila kujali kabila lake, rangi yake au dini yake. Kitu hiki nyinyi watu wa majimbo mengine mshindwa kukifikia.
 
Swala la uarabu wa Abood halina msingi.
Nitazungumzi kuhusu biashara ya watumwa. Ndugu zangu, kwa nini tunaendelea kukumbutia historia iliyopotoshwa? Katika biashara ya watumwa, mwarabu alikuja KUNUNUA watumwa. Kabla hatujamlaani mwarabu kwa kufanya hivyo, tujiulize; je, ni nani alimuuzia mwarabu hao watumwa? Huyo ndio wa kumlaani. Kwa sababu huyo muuzaji ana uhusiano wa kindugu kabisa na yule anayemuuza - amedhihirisha roho mbaya mara elfu zaidi ya yule aliyekuja kununua.
Laana kwa machifu wote waliouza ndugu zao!
 
Back
Top Bottom