Morogoro: Kuna sehemu kunajengwa msikiti mkubwa unaopakana ukuta na kanisa, Je hii imekaaje?

Siku wakileta shida watakaoleta shida Sheria ichukue mkondo wake.., so long as mipango miji ramani inayonyesha hio sehemu ni ya Taasisi...

Kama wamevamia hao na wale wanaovamia mitaani kwenye makazi na kujenga nyumba za ibada kama uyoga nao washughulikiwe... Tukienda kwa kufuata Sheria za Nchi mbona mambo yatakwenda tu bila shida...

Sidhani kama kuna sheria kwamba Uzio wa Taasisi A hauruhusiwi kuwa na Uzio wa Taasisi B iwapo inapoishia A ndio mali ya A..., Ila kuna sheria ya chochote kinachofanyika A au B kisiwabughuzi watu wa A, B C au hata wapita njia
 
Hakuna tabu.. muhimbili, huku msikiti huku kanisa, alfajiri kama mbili nimeswalia pale, msikitini tunaendelea na yetu na huko kanisani wanaendelea na yao.
 
Lile eneo naona ni mwendo wa taasisi tu. Hospitali, kanisa, msikiti, chuo, shule 'mixa' magereza.

So far sio rahisi kusitisha kujenga msikiti kwa kuwa kuna kanisa pembeni ya eneo lao.

Watavumiliana na kutatua kero ndogo ndogo endapo zitajitokeza miongoni mwao.
 
Lazima wa msikiti watahama tu!

Maana mapepo hayawezi kukaa sehemu moja na Yesu
 
9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom