Moral Authority: Mnyika amuombe msamaha Mzee Kikwete, au amuunge mkono Rais Magufuli hadharani kwa niaba ya CHADEMA

Azizi Mussa

JF-Expert Member
May 9, 2012
9,172
7,428
Mara kadhaa tumezungumzia kuhusu umuhimu wa ‘moral authority’ na tukasema hii ni jambo la msingi sana kwa kiongozi au chama chochote pengine kuliko mambo mengine yote. Mada hii inaendelea kufafanua umuhimu wa jambo hili na linavyofanya kazi kwa namna chanya au hasi.

Wakati, Mzee Kikwete akiwa Rais, alikuwa akisisitiza mara kwa mara kuhusu kufuata taratibu na sheria zilizokuwepo wakati wake na kutotumia madaraka nje ya sheria. Pia alipenda uhuru wa watu, ushirikishwaji, ushirikiano miongoni mwa vyama, maridhiano n.k.

Kutokana na tabia yake hivyo (ambayo lengo la uzi huu si kujadili kama ilikuwa hasi au chanya), Mnyika ambaye kwa sasa ni katibu mkuu wa CHADEMA, alitangaza hadharani kwamba mzee Kikwete alikuwa ni “Dhaifu”.

Hoja ilikuwa ni kwa nini Mzee Kikwete hakuwa anatumia mamlaka yake kama Rais kusukuma maamuzi kwenye mambo mbali mbali ama iwe kwa mujibu wa sheria au nje ya sheria; kinyume chake anasema ‘sheria na taratibu zifuatwe’. Kauli hiyo ya Mnyika haikuwahi kukanushwa na yeye mwenyewe au chama chake.

Sasa basi, ikiwa Mnyika na chama chake bado wanaamini kwamba hiyo ilikuwa ni sahihi, ‘It is ok’ lakini kama hawaamini hivyo; sioni ni kwa nini wasijitokeze hadharani na kumuomba msamaha mzee Kikwete?

Lakini kwa upande mwingine, kama bado wanaamini kwamba hiyo ilikuwa ni kweli na sahihi kabisa; hakuna sababu ya kutojitokeza hadharani na kumuunga mkono Mh. Rais Magufuli kwa kuwa sasa anaonekana anatekeleza hoja nyingi za akina Mnyika wa zama za Mzee Kikwete.

Mtu anaweza kujiuliza ni nini hiki? Maana yake nini? Ili iwe nini? Kwa faida ya nani? n.k. Hii ni muhimu sana kwa sababu zifuatazo;-

Kwanza msingi mkuu wa uongozi ni fikra; ni kipi unaamini ni kizuri na kipi unaamini ni kibaya na unaowaongoza wakuelewe hivyo. Kama utakuwa hueleweki unaamini kipi kizuri na kipi kibaya, unapoteza ‘moral authority’ na ukiongea kitu kabla ya watu kuangalia uzuri wake au ubaya wake; watafikiria kwanza unapata wapi ‘moral authority’ ya kusema unachosema?

Nitoe mfano, Shekhe au Mchungaji, ni lazima kwanza aeleweke anaamini pombe ni nzuri au ni mbaya. Kama wakati flani anasema pombe mbaya, wakati fulani anasema nzuri, kama anasema mbaya kwa mfano halafu watu wakiacha anawapinga anataka wanywe, wakianza kunywa tena anasema mbaya waache; watu hawatawaza ubaya au uzuri wa pombe kwanza bali watawaza kwanza shekhe au mchungaji huyo anapata wapi ‘Moral authority’ ya kuwaeleza uzuri au ubaya wa pombe?

Pili, kama ni vizuri pale viongozi wa CCM wanapokosea wakakubali na kukiri kisha kujisahihisha; kwa nini pia ninyi msione umuhimu wa kukubali na kukiri hadharani pale mnapokosea ili kujenga ‘precedence’?

Tatu, ili watu wenye utulivu wa akili wakuchukulie serious, ni lazima waelewe na wajiridhishe; unaamini nini na huamini nini, unaunga mkono nini na huungi mkono nini, na wewe unafanya nini ili iwe nini.

Kama hayo hayako wazi, maana yake hata muelekeo wa taasisi unayoongoza utakuwa haueleweki na hautabiriki “Uncertain” na hapo kinachofuata ni “Total failure”, na ni vigumu mtu kuku/kuwaamini kwenye jambo lolote, na usipoaminika ‘then what is there?'

Nne, ni vizuri kujifunza kutokana na matukio, na katika hili kuona umuhimu wa; kwanza kujiridhisha kabla ya kusema au kufanya jambo kama kweli unaamini juu ya unachosema au kufanya na pili, ikiwa unashauri au kukosoa mtu mwingine; kutumia lugha ambayo baadae haitakuhukumu.

Hili ni muhimu katika kuhakikisha kwamba hujutii maamuzi yako kesho na kesho kutwa.

Sasa najua kuna watu watakuja hapa kuuliza kwa nini haya usiwaambie CCM, ni sawa tu maana kila mtu na kichwa chake.

Mwisho, ni ukweli pekee unaoweza kuwa na manufaa ya muda mrefu, hata hivyo huu ni ushauri tu.
 
Mtu anaweza kusema “ahhh hizo zilikuwa siasa tu!” lakini kama ndivyo; basi mtu huyo atakuwa anatuambia kuwa ulikuwa ulaghai, na kama ulikuwa ulaghai na wahusika hawajutii, kwa nini sasa ifikiriwe kwamba, leo na kesho haitakuwa kama jana?

Binafsi si amini kama ni jambo la busara kwa watu wenye utulivu wa akili kuamini kuwa siasa za ‘ulaghai’ (bila kujali nani anafanya) ndio inapaswa kuwa ‘future’ ya Tanzania.Ndio maana tunafikiri kuyasema haya ni muhimu.
 
Mara kadhaa tumezungumzia kuhusu umuhimu wa ‘moral authority’ na tukasema hii ni jambo la msingi sana kwa kiongozi au chama chochote pengine kuliko mambo mengine yote. Mada hii inaendelea kufafanua umuhimu wa jambo hili na linavyofanya kazi kwa namna chanya au hasi.

Wakati, Mzee Kikwete akiwa Rais, alikuwa akisisitiza mara kwa mara kuhusu kufuata taratibu na sheria zilizokuwepo wakati wake na kutotumia madaraka nje ya sheria. Pia alipenda uhuru wa watu, ushirikishwaji, ushirikiano miongoni mwa vyama, maridhiano n.k.

Kutokana na tabia yake hivyo (ambayo lengo la uzi huu si kujadili kama ilikuwa hasi au chanya), Mnyika ambaye kwa sasa ni katibu mkuu wa CHADEMA, alitangaza hadharani kwamba mzee Kikwete alikuwa ni “Dhaifu”.

Hoja ilikuwa ni kwa nini Mzee Kikwete hakuwa anatumia mamlaka yake kama Rais kusukuma maamuzi kwenye mambo mbali mbali ama iwe kwa mujibu wa sheria au nje ya sheria; kinyume chake anasema ‘sheria na taratibu zifuatwe’. Kauli hiyo ya Mnyika haikuwahi kukanushwa na yeye mwenyewe au chama chake.

Sasa basi, ikiwa Mnyika na chama chake bado wanaamini kwamba hiyo ilikuwa ni sahihi, ‘It is ok’ lakini kama hawaamini hivyo; sioni ni kwa nini wasijitokeze hadharani na kumuomba msamaha mzee Kikwete?

Lakini kwa upande mwingine, kama bado wanaamini kwamba hiyo ilikuwa ni kweli na sahihi kabisa; hakuna sababu ya kutojitokeza hadharani na kumuunga mkono Mh. Rais Magufuli kwa kuwa sasa anaonekana anatekeleza hoja nyingi za akina Mnyika wa zama za Mzee Kikwete.

Mtu anaweza kujiuliza ni nini hiki? Maana yake nini? Ili iwe nini? Kwa faida ya nani? n.k. Hii ni muhimu sana kwa sababu zifuatazo;-

Kwanza msingi mkuu wa uongozi ni fikra; ni kipi unaamini ni kizuri na kipi unaamini ni kibaya na unaowaongoza wakuelewe hivyo. Kama utakuwa hueleweki unaamini kipi kizuri na kipi kibaya, unapoteza ‘moral authority’ na ukiongea kitu kabla ya watu kuangalia uzuri wake au ubaya wake; watafikiria kwanza unapata wapi ‘moral authority’ ya kusema unachosema?

Nitoe mfano, Shekhe au Mchungaji, ni lazima kwanza aeleweke anaamini pombe ni nzuri au ni mbaya. Kama wakati flani anasema pombe mbaya, wakati fulani anasema nzuri, kama anasema mbaya kwa mfano halafu watu wakiacha anawapinga anataka wanywe, wakianza kunywa tena anasema mbaya waache; watu hawatawaza ubaya au uzuri wa pombe kwanza bali watawaza kwanza shekhe au mchungaji huyo anapata wapi ‘Moral authority’ ya kuwaeleza uzuri au ubaya wa pombe?

Pili, kama ni vizuri pale viongozi wa CCM wanapokosea wakakubali na kukiri kisha kujisahihisha; kwa nini pia ninyi msione umuhimu wa kukubali na kukiri hadharani pale mnapokosea ili kujenga ‘precedence’?

Tatu, ili watu wenye utulivu wa akili wakuchukulie serious, ni lazima waelewe na wajiridhishe; unaamini nini na huamini nini, unaunga mkono nini na huungi mkono nini, na wewe unafanya nini ili iwe nini.

Kama hayo hayako wazi, maana yake hata muelekeo wa taasisi unayoongoza utakuwa haueleweki na hautabiriki “Uncertain” na hapo kinachofuata ni “Total failure”, na ni vigumu mtu kuku/kuwaamini kwenye jambo lolote, na usipoaminika ‘then what is there?'

Nne, ni vizuri kujifunza kutokana na matukio, na katika hili kuona umuhimu wa; kwanza kujiridhisha kabla ya kusema au kufanya jambo kama kweli unaamini juu ya unachosema au kufanya na pili, ikiwa unashauri au kukosoa mtu mwingine; kutumia lugha ambayo baadae haitakuhukumu.

Hili ni muhimu katika kuhakikisha kwamba hujutii maamuzi yako kesho na kesho kutwa.

Sasa najua kuna watu watakuja hapa kuuliza kwa nini haya usiwaambie CCM, ni sawa tu maana kila mtu na kichwa chake.

Mwisho, ni ukweli pekee unaoweza kuwa na manufaa ya muda mrefu, hata hivyo huu ni ushauri tu.
Rubbish

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mara kadhaa tumezungumzia kuhusu umuhimu wa ‘moral authority’ na tukasema hii ni jambo la msingi sana kwa kiongozi au chama chochote pengine kuliko mambo mengine yote.
Duh, Aziz Musa leo unaongelea morality na mambo ya moral authority?!.
Nilikuona mahali kwenye mambo ya morality ngoja nikukumbushe...

wewe aliekuambia kwamba uliemtaja hapo juu alikataa kuhudhuria kikao ni nani?huvi unajua ukibadilisha neno moja tu kwenye maelezo flani unaweza kuharibu maana yote?
Dada
Kwani wewe ndiyo Julianza Shonza? Au wewe ndiyo yule jembe aliyekuwa na boda boda akiwahi kikao pale MIC?
Embu soma hii kitu hapa chini kutoka release ya BAVICHA jana. Ndo utajua wewe si saizi yangu dada.
ee ndo mimi.
Sasa mtu unayeweza kujifanya wewe ni fulani, which is immoral kwa mwanamume kujifanya ni mwanamke, kaka Kaka Wakudadavua wengi humu wakidhani ni mwanamke, halafu leo ukazungumzia morality!.
Msalimie yule dada Bethlehem wa enzi zile
P
 
Vile vile ni jambo lisilotegemewa kwa mtu anayejielewa afikiri eti Tanzania yenye mafanikio itapatikana kwa watu kuunga mkono chama B eti tu kwa sababu wamechoka chama A. Imani ya namna hiyo haitegemewi kwa mtu anayefikiri sawa sawa.

Ndio maana tunasisitiza, ni vyema vyama vya upinzani vikatumia akili, muda, na nguvu kubwa kujitathmini vyenyewe kwanza kabla havijawanyoshea vidole wengine.
 
Trump miaka ya zamani alikuwa akimsifia sana Hillary Clinton lakini 2016 alimtukana sana kwenye kampeni hadi Leo anamtukana, Obama 2009 alikana kuyakubali mapenzi ya jinsia moja lakini 2012 alikiri kuyakubali, Mwaka 2015 mgombea JPM alikuwahakikishia wanafunzi wa vyuo vikuu kuwa hawatacheleweshewa mikopo 2019 tunaona viongozi wa wanafunzi wanafukuzwa kisa mikopo.
Kwahiyo usipende kuyaamini maneno ya wanasiasa
 
Trump miaka ya zamani alikuwa akimsifia sana Hillary Clinton lakini 2016 alimtukana sana kwenye kampeni hadi Leo anamtukana, Obama 2009 alikana kuyakubali mapenzi ya jinsia moja lakini 2012 alikiri kuyakubali, Mwaka 2015 mgombea JPM alikuwahakikishia wanafunzi wa vyuo vikuu kuwa hawatacheleweshewa mikopo 2019 tunaona viongozi wa wanafunzi wanafukuzwa kisa mikopo.
Kwahiyo usipende kuyaamini maneno ya wanasiasa
Swala sio kuwaamini au kutokuwaamini, suala ni kwamba kutokuwa waaminifu ni sahihi? na kama si sahihi, mtu mmoja asiye muanifu anapata wapi moral authority ya kumkabili mwenzake kwa kukosa uaminifu? na kama ni sahihi, ipo haja ya mtu kulalamikia au kulaumu, au kupinga au kukosoa jambo lolote lifanywalo na mwanasiasa?
 
Mara kadhaa tumezungumzia kuhusu umuhimu wa ‘moral authority’ na tukasema hii ni jambo la msingi sana kwa kiongozi au chama chochote pengine kuliko mambo mengine yote. Mada hii inaendelea kufafanua umuhimu wa jambo hili na linavyofanya kazi kwa namna chanya au hasi.

Wakati, Mzee Kikwete akiwa Rais, alikuwa akisisitiza mara kwa mara kuhusu kufuata taratibu na sheria zilizokuwepo wakati wake na kutotumia madaraka nje ya sheria. Pia alipenda uhuru wa watu, ushirikishwaji, ushirikiano miongoni mwa vyama, maridhiano n.k.

Kutokana na tabia yake hivyo (ambayo lengo la uzi huu si kujadili kama ilikuwa hasi au chanya), Mnyika ambaye kwa sasa ni katibu mkuu wa CHADEMA, alitangaza hadharani kwamba mzee Kikwete alikuwa ni “Dhaifu”.

Hoja ilikuwa ni kwa nini Mzee Kikwete hakuwa anatumia mamlaka yake kama Rais kusukuma maamuzi kwenye mambo mbali mbali ama iwe kwa mujibu wa sheria au nje ya sheria; kinyume chake anasema ‘sheria na taratibu zifuatwe’. Kauli hiyo ya Mnyika haikuwahi kukanushwa na yeye mwenyewe au chama chake.

Sasa basi, ikiwa Mnyika na chama chake bado wanaamini kwamba hiyo ilikuwa ni sahihi, ‘It is ok’ lakini kama hawaamini hivyo; sioni ni kwa nini wasijitokeze hadharani na kumuomba msamaha mzee Kikwete?

Lakini kwa upande mwingine, kama bado wanaamini kwamba hiyo ilikuwa ni kweli na sahihi kabisa; hakuna sababu ya kutojitokeza hadharani na kumuunga mkono Mh. Rais Magufuli kwa kuwa sasa anaonekana anatekeleza hoja nyingi za akina Mnyika wa zama za Mzee Kikwete.

Mtu anaweza kujiuliza ni nini hiki? Maana yake nini? Ili iwe nini? Kwa faida ya nani? n.k. Hii ni muhimu sana kwa sababu zifuatazo;-

Kwanza msingi mkuu wa uongozi ni fikra; ni kipi unaamini ni kizuri na kipi unaamini ni kibaya na unaowaongoza wakuelewe hivyo. Kama utakuwa hueleweki unaamini kipi kizuri na kipi kibaya, unapoteza ‘moral authority’ na ukiongea kitu kabla ya watu kuangalia uzuri wake au ubaya wake; watafikiria kwanza unapata wapi ‘moral authority’ ya kusema unachosema?

Nitoe mfano, Shekhe au Mchungaji, ni lazima kwanza aeleweke anaamini pombe ni nzuri au ni mbaya. Kama wakati flani anasema pombe mbaya, wakati fulani anasema nzuri, kama anasema mbaya kwa mfano halafu watu wakiacha anawapinga anataka wanywe, wakianza kunywa tena anasema mbaya waache; watu hawatawaza ubaya au uzuri wa pombe kwanza bali watawaza kwanza shekhe au mchungaji huyo anapata wapi ‘Moral authority’ ya kuwaeleza uzuri au ubaya wa pombe?

Pili, kama ni vizuri pale viongozi wa CCM wanapokosea wakakubali na kukiri kisha kujisahihisha; kwa nini pia ninyi msione umuhimu wa kukubali na kukiri hadharani pale mnapokosea ili kujenga ‘precedence’?

Tatu, ili watu wenye utulivu wa akili wakuchukulie serious, ni lazima waelewe na wajiridhishe; unaamini nini na huamini nini, unaunga mkono nini na huungi mkono nini, na wewe unafanya nini ili iwe nini.

Kama hayo hayako wazi, maana yake hata muelekeo wa taasisi unayoongoza utakuwa haueleweki na hautabiriki “Uncertain” na hapo kinachofuata ni “Total failure”, na ni vigumu mtu kuku/kuwaamini kwenye jambo lolote, na usipoaminika ‘then what is there?'

Nne, ni vizuri kujifunza kutokana na matukio, na katika hili kuona umuhimu wa; kwanza kujiridhisha kabla ya kusema au kufanya jambo kama kweli unaamini juu ya unachosema au kufanya na pili, ikiwa unashauri au kukosoa mtu mwingine; kutumia lugha ambayo baadae haitakuhukumu.

Hili ni muhimu katika kuhakikisha kwamba hujutii maamuzi yako kesho na kesho kutwa.

Sasa najua kuna watu watakuja hapa kuuliza kwa nini haya usiwaambie CCM, ni sawa tu maana kila mtu na kichwa chake.

Mwisho, ni ukweli pekee unaoweza kuwa na manufaa ya muda mrefu, hata hivyo huu ni ushauri tu.
Kwa akili yako ndogo kwa sasa hivi sheria zinafuatwa?wafanyakazi hawapandishwi madaraja,hawapewi nyongeza,madeni hawalipwi,nauli za likizo hawapewi,vyama vya siasa hawaruhusiwi kufanya siasa,mkwamo wa uchaguzi sirikali za mita,wafanyakazi kuachishwa kazi bila utaratibu,watu kutekwa na kufunguliwa mashtaka ya uongo ya uhujumu uchumi,kufanya manunuzi bila ya utaratibu,watanzania tunaona japo mnatufanya mambulula,!!!!!
 
Kwa akili yako ndogo kwa sasa hivi sheria zinafuatwa?wafanyakazi hawapandishwi madaraja,hawapewi nyongeza,madeni hawalipwi,nauli za likizo hawapewi,vyama vya siasa hawaruhusiwi kufanya siasa,mkwamo wa uchaguzi sirikali za mita,wafanyakazi kuachishwa kazi bila utaratibu,watu kutekwa na kufunguliwa mashtaka ya uongo ya uhujumu uchumi,kufanya manunuzi bila ya utaratibu,watanzania tunaona japo mnatufanya mambulula,!!!!!
Uwe unasoma mada uelewe kabla ya kuchangia, mada mahindi wewe unajadili maharage
 
Swala sio kuwaamini au kutokuwaamini, suala ni kwamba kutokuwa waaminifu ni sahihi? na kama si sahihi, mtu mmoja asiye muanifu anapata wapi moral authority ya kumkabili mwenzake kwa kukosa uaminifu? na kama ni sahihi, ipo haja ya mtu kulalamikia au kulaumu, au kupinga au kukosoa jambo lolote lifanywalo na mwanasiasa?
Wanasiasa kama wachezaji mpira tu, kuna jamaa yangu alikuwa akimpenda sana Beckham David siku alipohama Man U mshikaji aliugua na ilimchukua miezi mingi kuamini, Siasa ni mchezo ambao unaenda na upepo wa ajenda, kwa suala la kumkebehi JK hata humu watu wengi walikuwa wakimponda sana waulize Leo vipi wanamuonaje Mkwere? Watatamani arudi Magogoni.
 
Duh, Aziz Musa leo unaongelea morality na mambo ya moral authority?!.
Nilikuona mahali kwenye mambo ya morality ngonja nikukumbushe...

Msalimie yule dada Bethlehem wa enzi zile
P
Mkuu muda wote nimekuwa na kuheshimu sana nikiamini wewe ni verified user, lakini siku hizi unajivunjia hesima mkuu.

Nakushauri badilika ndugu yangu. Hapa mjadala unahusu jambo la msingi la kimantiki, wewe unatafuta njia ya kunidhalilisha au kunifanya nionekane sifai halafu mwishowe ulichoandika hata hakieleweki. Acha hizo broo! haziwezi kuwa na faida kwa mtu yoyote, jitahidi kurudi kwenye standard yako ya kutoa mada za kuelimisha jamii. Umekubwa na nini mkuu?

By the way hata kama nimekosea, au ninakosea au nitakosea; mimi bado ni binadamu na sio kamili. Ila hiyo haifanyi hoja ya msingi isiwe hoja kwa sababu mimi nina udhaifu A,B,C.Ndio maana tunaelimishana, kukosoana, kueleweshana na kujisahihisha.

Acha hizo mkuu, otherwise labda kama una shida nyinge lakini katika hili huna hoja ya msingi mkuu inawezekana dhamira yako ndio imekupotosha.
 
Mtu anaweza kusema “ahhh hizo zilikuwa siasa tu!” lakini kama ndivyo; basi mtu huyo atakuwa anatuambia kuwa ulikuwa ulaghai, na kama ulikuwa ulaghai na wahusika hawajutii, kwa nini sasa ifikiriwe kwamba, leo na kesho haitakuwa kama jana?

Binafsi si amini kama ni jambo la busara kwa watu wenye utulivu wa akili kuamini kuwa siasa za ‘ulaghai’ (bila kujali nani anafanya) ndio inapaswa kuwa ‘future’ ya Tanzania.Ndio maana tunafikiri kuyasema haya ni muhimu.

Halafu ww Azizi ukae kwa kutulia na acha kufundisha watu siasa za woga. Aombe msamaha ili iweje? Alichokisema Mnyika kuhusu JK alisema sawa, inaonekana unataka kuonyesha kuwa JK alikuwa ni mwema sana kisa unamfananisha na huyu. Ukweli nini kuwa JK alikuwa dhaifu na huyu ni katili, sifa zote hazitakiwi. Usitake kufunika udhaifu wa JK kwa ukatili wa Magu. Kama umechoka kutoa ushauri piga kimya, au kama vipi mwambie JK atoke aombe msamaha kutekwa na kuteswa kwa Ulimboka, ili tuone uungwana wa JK unaotaka kutuonyesha anao.
 
Halafu ww Azizi ukae kwa kutulia na acha kufundisha watu siasa za woga. Aombe msamaha ili iweje? Alichokisema Mnyika kuhusu JK alisema sawa, inaonekana unataka kuonyesha kuwa JK alikuwa ni mwema sana kisa unamfananisha na huyu. Ukweli nini kuwa JK alikuwa dhaifu na huyu ni katili, sifa zote hazitakiwi. Usitake kufunika udhaifu wa JK kwa ukatili wa Magu. Kama umechoka kutoa ushauri piga kimya, au kama vipi mwambie JK atoke aombe msamaha kutekwa na kuteswa kwa Ulimboka, ili tuone uungwana wa JK unaotaka kutuonyesha anao.
Hayo yote hapo juu unasema wewe halafu unadai nasema mimi.
 
Lakini kwa upande mwingine, kama bado wanaamini kwamba hiyo ilikuwa ni kweli na sahihi kabisa; hakuna sababu ya kutojitokeza hadharani na kumuunga mkono Mh. Rais Magufuli kwa kuwa sasa anaonekana anatekeleza hoja nyingi za akina Mnyika wa zama za Mzee Kikwete.

Kuna uzi leo niliandika umuhimu wa watu kuwa na knowledge ya "crtical thinking" hapa naona mfano mwingine wa kukazia point yangu. Kikwete kuitwa au kuwa "dhaifu" ilimhusu yeye JK. JPM kutekeleza baadhi ya hoja za CDM hai sababishi yeye kuungwa mkono hasa kama ana "madhaifu" makubwa hasa ukija kwenye mambo ya utawala bora na dhana yake ya serikali kufanya kazi na serikali.
 
Back
Top Bottom