Monitoring thread: John Pombe Magufuli katika Awamu ya Nne

mTz

JF-Expert Member
Aug 20, 2006
282
22
Wakuu, tujaribu kuupitia utendaji wa Magufuli katika awamu ya nne na kwa kuanzia naanza na makala hii kutoka gazeti la Tanzania Daima

==========

JANA vyombo vya habari nchini vimechapisha taarifa za ajabu. Taarifa hizi zinasema Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Pombe Magufuli, ametishiwa kuuawa na waandishi wa habari.

Waandishi anaowatuhumu ni Mhariri Mtendaji wa Habari Corporation, John Bwire, Mhariri wa Rai, Muhingo Rweyemamu na mwandishi wa Rai, Neophitius Kyaruzi. Ametoa taarifa polisi Dodoma Julai, mwaka huu na kupewa RB namba DO/IR/3085/2006.

Katika mashitaka yake, anasema wahariri hao na mwandishi huyo wamemtishia kwa kutumia SMS kuwa watamuua.

Wao katika utetezi wanasema waliwasiliana naye kupata ufafanuzi juu ya taarifa za barabara ya Usagara hadi Geita, zilizoonyesha kuwa kuna mahali hakutenda kwa usahihi, hali iliyoitia serikali hasara.

Magufuli ni waziri aliyepata heshima kweli katika utawala wa Awamu ya Tatu. Aliaminika kutokana na utoaji wa takwimu zilizowavutia wananchi kuona yu kiongozi makini mwenye kustahili heshima, kwani aliwatumikia wananchi kwa mujibu wa matakwa yao. Alipata kusema ametishiwa maisha katika awamu iliyopita na akapewa ulinzi.

Hata hivyo, kitendo cha Magufuli sasa kudai waandishi wa habari wanataka kumuua, sisi kimetutia wasiwasi. Kimetutia wasiwasi, na Magufuli kwa wadhifa wa ofisi ya umma anayoishikilia tunapaswa kumjadili na kuhoji, amekuwaje hadi anapata fikra na kutenda maajabu kama haya?

Magufuli amekuwa waziri wa kwanza duniani au pengine kiongozi anayepaswa kuingizwa kwenye vitabu vya historia kuthubutu, kudai na kutamka kuwa waandishi wanataka kumuua. Haijapata kutokea duniani mwandishi akataka kumuua kiongozi yeyote.

Waandishi ndio huuawa mara nyingi na takwimu na kumbukumbu zilizo katika fikra zetu sahihi zinaonyesha kuwa mwandishi hawezi kabisa hata kufikiri kumuua mtu, bali wao ndio wamekuwa wakiwindwa.

Hatuwezi kumhukumu moja kwa moja, lakini magazeti yameeleza walichofanya wahariri hao na kauli ya Magufuli na uamuzi wake.

Sisi tunapendekeza uchunguzi wa kesi hii usiishie kwenye kuchunguza SMS, Magufuli na waandishi tajwa, wote wafanyiwe uchunguzi wa akili pia, kuthibitisha kama wanao uwezo na wanaendelea kufanya kazi kwa matarajio ya jamii na taaluma wanazozitumikia; uandishi na siasa.

Bila hivyo, hatudhani kama tutapata jibu sahihi. Inawezekana kama waandishi hawa wemefikia hatua ya kumwinda waziri wamuue, basi wachunguzwe huenda wana matatizo ya akili. Wakibainika waondolewe katika kazi hii kabla hawajaliteketeza taifa, lakini pia Magufuli naye apimwe akili. Ikithibitika kuwa hajatishiwa, ametunga na ana akili timamu, aadhibiwe kwa mujibu wa sheria.


CHANZO: Tanzania Daima
 
Ina maana J.Pombe si mtandao ? Maana nijuavyo mimi habari Corp ni mali ya wana mtandao wapo akina RA na Jenerari ndiyo maan hata mambo ya maana hayandikwi. Sasa naomba kujua kwamba kama si mwana mtandao then nitafakari madai yake. Kuna mwenye majibu anisaidie ?
 
Mugishagwe
Pombe siyo mtandao, na hao mtandao wana mpango wa kumuondoa kwenye uwaziri wachukue wao hiyo wizara. Ni yeye na mwenzake Mramba wizara zao zinahitajika na matandao.
 
Mugishagwe
Kama mtandao umeenea mpake kwenye media basi tumekwisha! Ndio maana sasa kwenye magazeti hakuishi headings kama "Kikwete Mwisho" "Kikwete Kiboko" "Haijapata Kutokea". Wananchi wanachotaka kuona ni uchambuzi wa kina kuhusu utendaji kazi wa serikali ili ambapo pana makosa wakosolewe na penye mafanikio wapewe hongera.

Katika pitapita zangu mtandaoni nilikumbana na hii article,

In Bed With State

Source: http://home.ripway.com/2005-4/290382/mapenzi.doc

Tanzania is perhaps the only country in the region with four sports dailies and no less than seven titles that thrive on sheer pornography. Ernest Mpingajira explains why.

In a free media environment, why would the Press keep mum when the president travels in a reconditioned jet for which the taxpayer forked out twice what would have cost a brand new aircraft? Or, why would the Tanzanian media look the other side when the government purchases junk radar equipment at a time when airport security has become a matter of international concern since 9/11?

The answers are never easy to come by until one delves into the cosy relationship between media practitioners and the powers that be in Tanzania.

In April this year, two very experienced editors, Said Nguba and Mhingo Rweyemamu, committed what amounted to professional impropriety. They manipulated a picture of former OAU secretary-general, Dr Salim Ahmed Salim, and cast him as a member of an Islamic terrorist group Hizbu.

At the time this happened, Dr Salim was running neck and neck for the Chama Cha Mapinduzi presidential nomination against the eventual victor, Jakaya Kikwete. Dr Salim looked set to win the nomination to vie for the presidency in the October 30 General Election.

Within the CCM ranks, Dr Salim's encroachment on Kikwete's turf was a major threat and his wings had to be clipped at whatever cost.The offensive picture was fished out of the archives, manipulated and published on page one of Mwananchi Kiswahili daily. It portrayed Dr Salim as a racist and an Arab supremacist who masterminded the assassination of Zanzibar's first president, Abeid Amani Karume.

Foremost diplomat
Naturally, Dr Salim protested, but the damage had been done. For the time being, Tanzania's foremost diplomat will never shake off this tag for the rest of his political life. The two Mwananchi editors, Nguba and Rweyemamu, were given their marching orders by the employer but for Dr Salim, the die had been cast; he lost to Kikwete, who is likely to become Tanzania's president in the October polls. But rather than feel ashamed of the unorthodox conduct of the two editors against his opponents, Kikwete has rewarded Nguba by appointing him his press secretary. He is touted to become permanent secretary in the ministry of information and broadcasting upon Mr Kikwete's ascendancy to power.
Nguba took up his new role with gusto; his first clean up move was to rid the local media of people deemed to be hostile to CCM. He has his searchlight focused on foreign journalists who have in the recent past questioned everything from state firms using taxpayer's money to run paid adverts in the media to support CCM and its presidential candidate.

Curious foreign journalists appeared to give voice to Tanzania's often-timid opposition parties. They went further and questioned why CCM was using state-owned media to campaign for its candidates. Questions about why the CCM had hit the campaign trail before parliament is prorogued and the National Electoral Commission (NEC) gives the green light for start of campaigns angered CCM mandarins. They cracked the whip. The result was the expulsion of the gung-ho journalists who had begun asking the party to observe the law that it had so brazenly broken in the past.

Unless you are spreading the ruling party's propaganda, the standard rule in the Tanzanian industry media is "never scratch beneath the surface." Make a mistake of forcing CCM to account for its activities and the repercussions would be unbearable.

In June, a columnist with one of Tanzania's widely read weeklies, Rai, Jabbir Idrissa, dared tread the unbeaten path. In an incisive analysis of the sporadic election violence in Zanzibar, the writer accused CCM of heavy-handedness. CCM reacted swiftly: he was branded an alien and threatened with being stripped of citizenship. He was temporarily barred from writing anything about the isles. Of course, Jabbir Idrissa was born in Zanzibar and is in possession of a press card that allows him to travel to any part of Tanzania.
The government relented on its threat only after the intervention of Amnesty International and the International Press Institute.

Idrissa's run-in with the authorities was, however, not as nasty as say what befell the country's top journalist, Jenerali Ulimwengu, in the early years of President Benjamin Mkapa's presidency. Having campaigned for Mkapa to win the 1995 General Election, Ulimwengu, a media owner, felt betrayed by Mkapa's partiality to sleaze.

Mkapa, with whom Ulimwengu worked at the Daily News (Tanzania's oldest English daily) in the 1970s alongside Kenya's Philip Ochieng, did not take kindly to Ulimwengu's bare-knuckled criticism of entrenched graft in the government. He responded by stripping Ulimwengu of his Tanzanian citizenship, claiming the latter was a Tutsi from neighbouring Rwanda. Like a marionette, Ulimwengu was tweaked rudely into line. He plays it safe these days lest he is deported.

Ulimwengu's once flourishing stable of newspapers was denied government advertisements. Private firms that advertise in newspapers deemed to be hostile to the government, too, risk the wrath of the powers that be if they place ads in the "hostile" publications. To this day, Ulimwengu's Habari Corporation, the second largest media house in Tanzania, survives on a shoestring budget and there are no indications that it will pick up the pieces soon because CCM looks set to retain power.

The flipside of the journalists and media houses being marked by the government is that praise- singing publications carry many government adverts. Taking the cue from the government, private firms also place adverts only in newspapers the government does business with. Papers that write positively about opposition politics also risk being sidelined by the government.

Investors in the media industry know full well that circulation revenue alone cannot sustain a newspaper, and the more advertising the better.

The risk of losing government adverts sends a clear message: see nothing, say nothing; the gravy train will come your full way. Scratch beneath the surface, expose the underside and your nose will be bloodied.

With this stick and carrot (call it club and pie) method, the government has managed to clamp down on the media so much that Tanzania is perhaps the only country in the region with four sports dailies and no less than seven titles that thrive on sheer pornography!

In sports and pornography, journalists and investors rarely cross the government's path. In all, Tanzania has more than 15 dailies and over 30 weeklies, which are published in the commercial capital of the country, Dar es Salaam, but their content is invariably hymnal – praise be to the government!

Radio and TV stations, which number more than 25 and spread over the country, fair no better. They are no more than tools for individual's self-glorification. It would be presumed that pornographic and seminar/workshop journalism have taken root in Tanzania because the industry wants to steer clear of political and investigative reporting, which ordinarily drive circulation in other parts of the world. Compared with Uganda and Kenya, where the media – sometimes even the state-owned media – hold the government of the day to account, Tanzania's media portrays itself as part of the government.

Even after the country shed its socialist cloak, the Fourth Estate has not played its public watchdog role. Except in the case when Ulimwengu took President Mkapa's government to task over the brazen theft of public utilities by people close to him, the industry is yet to wake up to its core role of informing the public. Hence the citizens lack an impartial vehicle of information, and political repression is a reality.

Tyrannical
Unbeknown to the outside world, Mkapa is one of those African leaders who do not brook criticism – however, fair. His tyrannical tendencies are something most Tanzanians talk about in muted tones.

So intimidated are political leaders and the media that those within the ruling party cannot change allegiance to the opposition for fear being persecuted. And to stay on the lee side of government fire, many journalists are members of the ruling party.

Some are retained to paint a rosy picture of CCM and its leaders. And overzealous ones like Said Nguba and Mhingo Rweyemamu are assured of plum appointments. In this situation it is difficult to expect a lot from journalists and media owners who expect to be cuddled by their government.

After Mark Bomani, a former CCM stalwart who passed on in April this year, leaked to the media how his party had made questionable purchases of aircraft and airport equipment, one would have expected the media to take the cue and peek into the government's other shady deals.

And they are many: from questionable disposal of state firms, houses, issuance of mining licences, awarding of plum contracts to firms associated with the big shots in the government, etc to arm-twisting officials to approve questionable decisions.

Whereas Tanzania is a goldmine for stories that speak for the downtrodden, the poor, the marginalised and the disenfranchised, few stories seriously tackle these themes. Runaway graft at all levels of society has given Dar es Salaam the nickname of Bongo - implying that you only need to be crafty to make it in life.
 
Sam ,

Mimi wala sitaudhunika hata kidogo wakimwondoa huyo Magufuli . Ni nani asiyefahamu ya kuwa yeye ndiye aliye kuwa architect wa kuuza nyumba za serikali kwa bei ya chini kabisa pale oysterbay ? Ni nani asiyejua mpango wake wa kunya'nganya walala hoi viwanja vyao !

Mimi nikiwa mmoja wa victim wa policy mbovu za huyu bwana nitafurahi sana kama wanamtandao watamwondoa !
 
Rufiji

Mbunifu wa uuzaji wa Nyumba za Serikali siyo Magufuli bali Mkapa akishirikiana na wanaomzunguka.

Si unajua nyumba nyingi zilikwenda kwa akina nani.

Magufuli mwanzoni alikataa kata infact kuendana na habari za ndani huu mfumo ulianza mara baada ya fununu kuwa anataka kurudisha nyumba za Serikali Serikalini akama alivyokuwa amefanya kwa magari kwani nyumba nyingi zilikuwa zinamilikiwa na viongozi kama mali zao.

Jaribu kujiuliza kwa nini nyumba nyingi hazikuuzwa kwa kupitia wizara yake.

Pia kumbuka skendo ya Prof. Sarungi na aliyekuwa anakaa kwenye nyumba aliyonunua kukataa, magufuli baada ya kupigia simu alisema kuwa "Nyumba za Serikali siyo nyumba za Wizara yeye anafuata maagizo ya Serikali"

Pamoja na Magufulu kuwa na mapungufu yake, nadhani ni mmojawapo wa viongozi wachache wachapakazi na hufanya kazi ya kweli kama hawapati pingamizi kutoka serikalini.
 
Nitaridhika akiondolewa Mramba sio magufuli.

Mramba ni kiongozi mchovu asie na jipya na amekuwa na sera ya upendeleo katika maeneo ya kwao. Katumia parcent kubwa ya bajeti ya wizara kujenga barabara za kwao.

Kaondoa kipimo cha kisasa bandari/mpakani ambacho kingeweza kuvuta biashara ya nchi nyingi kapeleka mpaka wa holili kwa vile ni karibu na jimboni kwake hivyo potential business nyingi zimepotea.

Magufuli ni kiongozi nadhani shupavu asiesita kufanya maamuzi magumu. Sijui kama ni mtandao au la lakini nadhani anafaa kuendelea kutokana na mageuzi anayoyafanya ardhi.

tumpe muda then tutamjadili baadae.
 
Uuzwaji wa nyumba za serikali ni wa serikali nzima ya BM akiwemo JK ambaye hapa mnasema ni mkombozi na ana nyumba ya kununua sasa leo kumpa lawama juu ya hizo bwana Pombe ni kumuonea JK anayo na alificha hadi last minutes .Je ndiyo usafi wa JK ?
 
Gazeti la Rai la Alhamisi [Oct 5 - Okt 11] limekuja na habari yenye kichwa hicho hapo juu.

Dondoo ni kuwa:

Wakala wa majengo, taasisi iliyo chini ya wizara ya Miundo mbinu, imemuuzia nyumba bwana Musa Joseph Magufuli (mdogo wake waziri Magufuli) huku akiwa na mkataba ambao unaonyesha angefanya kazi kwa miezi mitatu tu (26/09/2005 - 31/12/2005). Nyumba aliyouziwa iko ubungo, na ameuziwa kwa Tshs. 1.5M (!). Wakati anapewa ajira hiyo (Afisa tawala, business support unit), bwana Musa alikuwa na bado ni mwanafunzi wa masters UDSM. Alipoanza kazi tu akaanza kushughulikia ununuzi wa nyumba na within one month akawa na nyaraka zote muhimu za kumiliki nyumba hiyo. Wahadhiri wake UDSM wamesema kwa ratiba ya masomo yake ilivyokuwam masomo na kazi visingewezekana. Bwana Musa Magufuli aliacha kazi siku mbili kabla ya mkataba kwisha, akiwa na nyumba!

Mpo hapo? Sijui waziri atatuambiaje katika hili. Otherwise makeke yoote yale ya nyumba za NHC etc itakuwa anatuzuga tu.. nae yumo. ... labda aseme huyu ndugu alichakarika kivyake katika hili suala na yeye hakuhusika.
 
Mzee Kulikoni,

Heshima yako mkuu, habari hii ni nzuri sana katika kuonyesha unafiki wa viongozi wetu,

But, hili gazeti ambalo sasa hivi tunafahamu kuwa liko chini ya influence ya Rostam, linatupa wasi wasi pia pale tu linapomripoti ndugu ya Magufuli tu, ambaye si mtandao kama Rostam na wengineo, na kuwaacha viongozi wa juu ambao wamegawana hizi nyumba kwa bei ya bureeee, au poa!

Mbona wasiseme JK mwenyewe aliponunua moja ya hizo nyumba na bei aliyolipa? Otherwise ni a very good point!
 
OK, the file is as attached.

i244_MagufuliPage1.jpg

i245_MagufuliPage2.jpg
 
Jamani tukisema tunaambiwa tunatetea watu, ila sioni Magufuli anaingiaje hapa ila kama tutapewa ushahidi kuwa alishinikiza mdogo wake auziwe nyumba hiyo. Vinginevyo wa kushutumiwa ni huyo bwana mdogo na hao waliomuajiri.

Hata hivyo tumeshasema kuwa zoezi lote la uuzaji nyumba lilikuwa ni bomu hata kama aliyeuziwa nyumba hiyo aliishi humo umri wake wote wa ajira. Na ni kweli tusingetegemea mtu yeyote mwenye uchungu wa nchi yetu aafiki au ashiriki kwenye kununuwa nyumba hizo. Binadamu huwa wanajisahau wanapopandwa na tamaa.

Hawa Rai wasimfuatie mtu mmoja mmoja bali walicharukie zoezi lote na zirudishwe nyumba zooooooote.
 
Yule mama niliyewaambia kuwa anasema nyumba alipewa na mungu. Yule mlokole ambaye nilisema labda mungu wake ni mkapa!

Huyo mama naye ni mdogo wake na MAGUFULI.ALINIAMBIA MWENYEWE!LAKINI NI CVIL SERVANT WA SERIKALI OFISI YA MAKAMU WA RAIS(MAZINGIRA) RAIS.

KWA HIYO ZOEZI HILI LA UUZWAJO WA NYUMBA SIYO SAHIHI JAPO WATU HUMU WANATETEA MASLAHI YAO, MARA WANASEMA NYUMBA ZILIKUWA ZIMECHOKA ETC!
 
Kwa nchi zilizoendelea, hii ya Mussa kama ni kweli basi Magufuli hata kama hakuhusika inabidi AJIUZULU.
Ni vigumu kuthibitisha kuhusika au kutohusika.

Upande mwingine wa shilingi unanionyesha kuwa kuna mawaziri wawili ambao ndio magazeti bongo yanafuatilia utendaji kazi zao. Mramba na Magufuli. Why? simpo sio mtandao. Sasa kwa stahili hii namuona Magufuli hana hatia, ni njama tu za kutaka kumuonyesha si mtu safi.

Hili ndio linanikera zaidi lazima kuwe na fair playing ground. Sio mimi nikitaka kucheza uwanja haumwagiliwi maji, ila Kulikoni (mfano) akicheza basi uwanja unamwagiliwa maji!. Ndio haya tunakataa.

FD
 
Ndiyo hapa unaona ukweli wa kikatuni cha Wakenya na waandishi wa Habari wa Tanzania na Mtandao .Sasa utasemaje wakenya wanatukana wakati ni kweli wanafanay yale yale ambayo wanasema wametukanwa nayo ?
 
Unayosema Fduni ni kweli lakini mtenda kosa kakosa na mrudia kosa vilevile,kwa hiyo Magufuli ninaamini you're responsible person .......tunahitaji maelezo
 
Waziri Magufuli, amewapa rungu wananchi la kuwapiga nalo watakaobainika kutaka kuwadhulumu ardhi yao bila kuwapa fidia. Aliwakabidhi rungu hilo wananchi wa kijiji cha Zinga, Bagamoyo.

Rungu lenyewe ni sheria namba nne na tano ya mwaka 1999 inayosema "...Lazima kila mwananchi atakayetoa ardhi kwa ajili ya kupimwa au kuendelezwa kulipwa fidia kwa wananchi......"

"Ishikeni kwa umakini mkubwa sheria hiii ya ardhi namba nne na tano, ili atakapokuja mtu na kupima ardhi yako kwa ajili ya maendeleo bila kukupa fidia uidai," Katika kudhuhirisha kuwa hana utani na kazi yake Magufuli, aliwanyanyua Afisa ardhi wa Wilaya hiyo, pamoja na mkuu wa idara ya upimaji ardhi wa UCLASS, ambaye ni mkandarasi katika kupima mradi wa viwanja 3000 wa mwaka 2003 ambao bado haujakamilika, kujibu malalmiko ya wananchi juu ya ucheleweshaji wa kukabidhiwa viwanja vyao!

&

Mbunge wa CCM wa jimbo la Temeke, ambaye aliwahi kulalamikiwa na wananchi wa jimbo kuhusu matatizo ya maji, juzi amezindua kisima kipya cha maji kwa wananchi hao ambao aliwaahidi wakakti wa kampeni za uchaguzi, zilizopita, katika kata ya Azimio kule Tandika!

Katika sherehe hiyo pia mbunge Mtemvu, aliwaonya baadhi ya watu wenye tabia ya kuchafua vyanzo vya maji na kusema kuwa wanastahili kuchukuliwa hatua kali za kisheria!

Source: Alasiri October 26, 2006.
 
Wasema nyumba 8,000 kauza kwa mkono wake mwenyewe
-Apuuza maonyo ya wataalamu
-Mafaili ya Sundi na Musa aliyabeba kwapani


ALIYEKUWA Waziri wa Ujenzi, John Magufuli, katika Serikali ya awamu ya tatu, aliteka madaraka na kuwa mwenyekiti wa zoezi la kuuza nyumba za serikali ambazo hadi sasa, zimeshauzwa 8,288 imefahamika.

Habari zilizopatikana ndani ya wakala wa Majengo ya Serikali (TBA), zimethibitishia Rai wiki hii kwamba Magufuli alihakikisha anashiriki kama Mwenyekiti katika zoezi zima la kuuza nyumba, ambalo kimsingi lilistahili kusimamiwa na Mtendaji Mkuu wa TBA.

Kwa mujibu wa vyanzo kadhaa vya habari ndani ya TBA, Magufuli alifanya kila aina ya ‘fujo’ katika zoezi la kuuza nyumba hizo, wakati mwingine akibatilisha maamuzi yaliyofanywa na Kamati ya TBA ya kuuza nyumba hizo, akiwapangia watu nyumba kwa utashi wake na wakati mwingine akiwakemea wale wote waliomshauri kinyume na matakwa.

Ni chini ya utaratibu huo, habari zinaeleza kwamba Magufuli, aliyabeba yeye mwenyewe mafaili ya ndugu zake; Musa Magufuli ambaye ni mdogo wake, na Sundi Malomo ambaye ni mzazi mwenzake na kuwalazimisha watendaji wa TBA wafuate matakwa yake katika kuwapatia nyumba ndugu zake hao.

Habari hizo zinaeleza kwamba awali Mtendaji Mkuu wa TBA alimshauri Magufuli kwamba suala la mauzo ya nyumba kwa ndugu zake ni kinyume cha utaratibu. Hata hivyo, imeelezwa kwamba Magufuli alilazimisha huku akisema mdogo wake hana tatizo kwa sababu alikuwa tayari mfanyakazi wa Serikali.

Musa aliajiriwa kwa mkataba wa miezi mitatu, baada ya mwezi mmoja akauziwa nyumba na baada ya miezi miwili akaacha kazi.

“Kwa upande wa Sundi, kwanza ilikuwa Sundi auziwe nyumba moja kwa moja. Lakini Magufuli alipoonywa akashtuka na kusema suala hilo aachiwe yeye mwenyewe. Na ndipo akaibuka na jina la Stanley Manongi kwamba ndiye mnunuzi halisi na baba yake Sundi,” vinasema vyanzo hivyo vya habari, vingine ambavyo vilishiriki moja kwa moja katika mchakato wa uuzaji nyumba hizo.

Habari hizo zinaendelea kueleza kwamba baadaye, Sundi alishtuka akitilia shaka uaminifu wa Manongi, kwamba angeweza kumdhulumu nyumba hiyo.

“Ndipo Magufuli aliibuka na mpango wa Sundi kuwa mtoto wa Manongi na mrithi wake na kisha kwa kuhakikisha kwamba hakuna dhuluma yoyote, mtoto wa Sundi naye akarithishwa na kama mrithi wa pili,” chanzo hicho cha habari kinaeleza.

Chini ya sheria ya Executive Agency Act No. 30 ya mwaka 1997, TBA ilipewa madaraka yote ya kuuza nyumba za Serikali, kujenga nyumba mpya, kuzikarabati zilizopo pamoja na kugawa nyumba za madaraja A, B na C kwa wafanyakazi wa Serikali.

Sheria hiyo inaipa mamlaka ya kipekee ya kufanya shughuli zote bila kuingiliwa na chombo chochote.

Chini ya sheria hiyo, Waziri anaruhusiwa kuteua wajumbe wa bodi ya ushauri watakaomshauri Katibu Mkuu wa Wizara juu ya namna nzuri ya TBA kusimamia mamlaka yake.

Hadi Machi mwaka huu, wajumbe hao walikuwa ni J. Kijazi, E. Lipambila, E. Lugwisha, Msangi, E. Mwakalinga, D. Kisasi, P. Ncheye, F. Werema na A. Bukuku.

Hata hivyo, sheria haitoi nafasi yoyote kwa Waziri kusimamia shughuli za uuzwaji au upangaji wa nyumba za serikali.

Mtendaji Mkuu wa TBA Togolayi Makumba Kimweri, alipoulizwa kupitia kwa Katibu Muhtasi wake, alimwambia mwandishi wa Rai aandike maswali kisha asubiri kuruhusiwa kuingia ndani ya ofisi.

Hata hivyo, baada ya kusubiri kwa muda wa saa moja, mwandishi alipokwenda kuuliza akaambiwa kwamba Kimweri tayari alikwishaondoka ofisini kupitia mlango wa nyuma na asingeweza kurudi ofisini.

Lakini baadhi ya wafanyakazi wa TBA wameiambia Rai kwamba kinachoandikwa kwenye magazeti kuhusu ushiriki wa Magufuli kuuza nyumba za Serikali ni kidogo mno kuliko hali halisi.

Kama ilivyokuwa kwa mdogo wake Musa, waziri Magufuli alishinikiza mtoto wa dada yake anayeitwa James Doto Mgosha auziwe nyumba za serikali kwa kumtengenezea ajira ya muda mfupi katika TANROADS.

Tofauti na Musa, Doto ameuziwa nyumba hiyo kwa jina la mtu mwingine lakini anaishi katika nyumba hiyo, namba 64 iliyopo Kinondoni Flats.

Habari kutoka TBA zinaonyesha jina la mtu mwingine (tunalihifadhi) kuwa ndiye aliyeuziwa nyumba hiyo mtu huyo alipata kupitia utaratibu wa Magufuli kupeleka jina lake kwenye wakala wa majengo na kulazimisha apewe nyumba.

Alipoulizwa kwa njia ya simu, Doto alisema suala la ajira na nyumba waulizwe waliomwajiri na kumpa nyumba. Akakata simu.

Mfanyakazi mwingine alieleza Rai kwamba msichana mwingine (jina tunalihifadhi) akiwa na miezi minne tu kazini alipelekwa na Magufuli katika Wakala wa Majengo akilazimisha auziwe nyumba hata kabla ya kuthibitishwa kazini. Nyumba hiyo iko Block A, Ocean Road.

Hata hivyo, habari hizo zinaeleza kwamba msichana huyo ambaye hadi sasa anaishi na wazazi wake, ameipangisha nyumba hiyo kwa mfanyakazi mmoja wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa na analipwa kwa dola za kimarekani.

“Kuuza nyumba za serikali sawa, lakini kweli katika mtindo huu? Sisi tunaoshiriki kuzikagua na kuziratibu tukiomba hatupati, lakini wengine wanaingia serikalini miezi miwili wanapata nyumba. Na wengine hata si wafanyakazi, wanapata, hii si sahihi, alilalamika mfanyakazi mmoja aliyeandikia Rai kwa njia ya barua pepe.

Hadi Machi mwaka huu Wakala wa Majengo wa Serikali (TBA) walishauza nyumba 8,288 ambazo hata hivyo zilitakiwa kuuzwa kwa watumishi wa serikali.

Katika mauzo hayo, Serikali ilitarajia kupata jumla ya shilingi 60,016,556,439.00. Hata hivyo hadi sasa Serikali imepata shilingi 22,684,108,115.08.

Kwa sasa, Serikali imebakiwa na nyumba 1,098 zinazosimamiwa na TBA. Kati ya hizo, nyumba 692 zimetengwa kwa wafanyakazi wa Serikali, nyumba 675 kama tied quarters, nyumba 111 zinatumika kama Rest House za Serikali, wakati nyumba 40 zinatumika kama state lodges. Nyumba 24 zinatumika kama ofisi na nyingine 29 ni kama karakana na bohari.


Chanzo: Rai Nguvu ya Hoja: Toleo Namba 682
 
Back
Top Bottom