Monica Ngenzi Mbega atangaza rasmi kutetea kiti chake cha ubunge

Kupiga kelele sana bungeni haina maana kuwa Mbunge ni mzuri. Kinachotakiwa ni kufuatilia kero za wapiga kura wake ni kuwapa mlisho nyuma wa jinsi mambo yanavyokwenda au yanavyotatilowa!!!!! Porojo nyingi hazimsaidii mpiga kura!!!!
 
Nanu

Naungana na wewe kuhusu kelele za bungeni. Pili, lazima ikumbukwe kwamba kwa kuwa mkuu wa mkoa tayari anakuwa upande wa serikali, kama ilivyo kwa mawaziri. Hata siku moja mkuu wa mkoa (Lukuvi, Nsekela, Mbega) hawezi akasimama bungeni kuuliza swali juu ya jimbo lake, kwani anatakiwa kuwasiliana na waziri husika kwa njia tofauti.

Kwa hiyo, kama ilivyokuwa kwa mawaziri, wabunge ambao ni wakuu wa mikoa tuwahukumu kwa waliyoyafanyia majimbo yao na sio kwa kelele za bungeni. Wako baadhi ya wabunge wenye kelele sana bungeni, lakini majimboni kwao hawatakiwi kabisa.
 
Mpingo,
Ni njia gani hizo ambazo wabunge wa aina ya mama Mbega wanawasiliana na Mawaziri,kwa jinsi nijuavyo matumizi na mipango ya maendeleo kama ujenzi wa barabara,madaraja,viwanja vya ndege nk hujadiliwa bungeni na bajeti zake lazima ziungwe mkono na wabunge.

Wabunge wa majimbo husika ndio wanaweza kuileza serikali mahitaji ya wanajimbo bungeni ili wabunge wengine washawishike kuunga mkono hoja,sasa hizo njia zingine ni zipi.

Isije ikawa kama ile hoja aliyoibua Selelii bungeni alipohoji ujenzi wa barabara katika jimbo fulani wakati bajeti yake haikupitishwa na bunge.

Jambo jingine, unaweza kuona baadhi ya miradi katika jimbo ukafikiri ni juhudi za mbunge na kumbe ni misaada kutoka benki ya dunia na wafadhili wengine.
 
Jana Mheshimiwa mkuu wa mkoa wa kilimanjaro na mbunge wa Iringa mjini kaweka wazi nia yake ya kutetea jimbo lake, Mama huyu ambaye hakubaliki sana kwenye jimbo lake kiasi cha watu kuamini kuwa hupita kiccm jana ametangaza kuwa anagombea tena.
Akiongea kwa kujisifu eti kuwa ukuu wa mkoa alioupata ndio mafanikio na ni kitu cha kujivunia kwa wananchi wa Iringa kwa kuwa wao kumchagua kwake kumemfanya aonekane na rais na kupewa nafasi hiyo ya ukuu wa mkoa. amerbainisha msimamo wake jana kwenye mkutano ulioandaliwa na taasisi ya ISICO kati yake na wnanchi.
yawezekana hali na wakati ukawa umempita lakini yawezekana pia alikuwa mjanja kuuwahi wakati so in 1995 alikuwa before time na sasa yuko on time watazamaji wantazama off time. hii inanipa shaka kama kweli forum hii ina members ambao ni critical thinkers au critical thingers au critical singers?
kuna watu hawawapendi wake wa kaka zao lakini cha ajabu eti kaka zao wanawapenda wake zao nadhani ingekuwa ni vema na wao wakaoa wake zao wanaowapenda na kukaa kimya.
tunahitaji kufanya tafiti hata kwa kutumia judgemental sampling lakini tutumie wapiga kura (prospective) badala ya kuja na mawazo ya kimtandao.
nimeona kuna kila juhudi za kuwahimiza wanawake kugombea kupitia majimbo badala ya viti maalum sasa sijui walio na nia ya kugombea na ambao ni tayari wapo wanapigwa vijembe sasa sijui ni kina nani hao wahimizwa.
ikumbukwe mama huyu alikuwa viti maalum lakini kwa kuona anaweza kugombea na akanadi sera na kujieleza akagombea jimbo baada ya kipindi kimoja tu wapo ambao wameng'ang'ania viti maalum mpaka wakapelekea kuweka utaratibu wa ukomo wa viti maalum hii ni kituko.
monica kama alivyo mtanzania mwingine anayo haki ya kugombea; kushinda au kushindwa ni haki ya wapiga kura kuamua na ni wajibu wake kukubali matokeo na ni wajibu wa wananchi kupiga kura; madhari keshatangaza nia yake wale wanaodhani hafai basi waibukekugombea au kutafuta ushawishi kwa wengine wagombee otherwise story ya chura itajirudia kila siku hapa.
kila tusemalo na tunalotaka ni vema tukafanya utafiti badala ya haka kamtindo ka mi staki arudi mjengoni, utafanyaje na wapiga kura wamemchagua?
regards;
 
Falesy,
Kwamba alikuwa viti maalumu kisha akaamua kugombea jimboni hiyo siyo issue,tatizo letu hapa ni uwezo wake wa kudeliver kama mwakilishi wa watu wa Manispaa ya Iringa,hapa hatusemei ushabiki au tumetumwa na watu fulani.

Binafsi sina tatizo na Mama Mbega,tatizo langu ni majukumu aliyonayo,yamekuwa mengi kiasi kwamba yamekuwa mzigo kwake.Manispaa ya iringa inahitaji mtu mwenye uwezo wa kushughulikia changamoto zinazolikabili jimbo,na mtu huyo anahitaji kuwa na muda wa kutosha wa kukutana na wananchi,kujadiliana nao jinsi ya kutatua matatizo mbalimbali nk.Sasa mtu yupo Kilimanjaro atasikiliza matatizo yetu saa ngapi?
 
Mkuu hebu fafanua hapo kupita KICCM ndiyo kupitaje? na je hii ina athari gani kwa wananchi wasiomkubali?. Maana hapa tuelewane mapema kuwa njia yoyote isiyo ya kuchaguliwa kihalali na wananchi ni CRIMINAL act which needs to be stoped. Tulisihalalishe misamiati ya uvunjaji wa sheria, siku wananchi wakichoka patakuwa hapatoshi
kupita kiccm maana yake ni kupitishwa na chama kuwa mbunge na siyo kuchaguliwa na wananchi, yaani hupita kwa kuibiwa kura ok!
 
Falesy,
Kwamba alikuwa viti maalumu kisha akaamua kugombea jimboni hiyo siyo issue,tatizo letu hapa ni uwezo wake wa kudeliver kama mwakilishi wa watu wa Manispaa ya Iringa,hapa hatusemei ushabiki au tumetumwa na watu fulani.

Binafsi sina tatizo na Mama Mbega,tatizo langu ni majukumu aliyonayo,yamekuwa mengi kiasi kwamba yamekuwa mzigo kwake.Manispaa ya iringa inahitaji mtu mwenye uwezo wa kushughulikia changamoto zinazolikabili jimbo,na mtu huyo anahitaji kuwa na muda wa kutosha wa kukutana na wananchi,kujadiliana nao jinsi ya kutatua matatizo mbalimbali nk.Sasa mtu yupo Kilimanjaro atasikiliza matatizo yetu saa ngapi?
hata kabla ya kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa huyu mama alikuwa ni mgumu mno kukutana na wananchi wake, kwa kweli ukuwajiwa uchumi wa iringa ni wa kasi hivyo unahitaji wabunge waliochangamka wanaoweza kuwatetea wananchi na kuhakikisha maendeleo ya kweli yanapatikana kama alivyo mheshimiwa lukuvi ambaye anawajibika mno kwa wananchi wake na wananchi wanaziona juhudi zake ila siyo huyu mama jamani!
 
nimeona kuna kila juhudi za kuwahimiza wanawake kugombea kupitia majimbo badala ya viti maalum sasa sijui walio na nia ya kugombea na ambao ni tayari wapo wanapigwa vijembe sasa sijui ni kina nani hao wahimizwa.
;
kwa hiyo bwana falesy unataka useme kwa vile ni kinamama tukae kimya hata kama hawawajibiki? kisa haki sawa ndo tunyamaze? irirnga inahitaji mtu wa kuleta maendeleo awe wa kiume au wa kike lakini siyo mtu wa kujali tumbo lake
 
Kupiga kelele sana bungeni haina maana kuwa Mbunge ni mzuri. Kinachotakiwa ni kufuatilia kero za wapiga kura wake ni kuwapa mlisho nyuma wa jinsi mambo yanavyokwenda au yanavyotatilowa!!!!! Porojo nyingi hazimsaidii mpiga kura!!!!
hatuna maana kuwa apige kelele bungeni ila tuna maanisha awajibike wananchi kwa kusaidia kuibua miradi kama tunavyojua miradi haiwezi kutekelezwa kama mbunge haitetei sawasawa.mfano kama Lukuvi anavyopigania ujenzi wa barabara ya iringa dodoma, yaani kama yeye akinyamaza kimya itachukua mda selikali kutekeleza, hinyo ndivyo huyu mama anatakiwa awe
 
Back
Top Bottom