Money Matters: Maendeleo, Ubunifu, Maadili na Kujitegemea

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Bob Mkandara, ni mtu ambaye amejikwamua kiubunifu na kujijenga kiuchumi. Ni juhudi zake mwenyewe na kutokukata tamaa au kutafuta njia nyepesi na rahisi kujipatia pesa kukimu maisha yake ndiko kulikonifanya nimtumie kama mfano kuhusu mada yangu mpya.

Sisi kama Taifa, tunatatizo moja kubwa ambalo linabidi tulifanyie kazi kwa mwendokasi wa mwanga na tusiendekeze kusubiri kesho kama tulivyoafanya kwa miaka 46!

Tatizo hili ni fedha.

Fedha, Nyerere na Azimio walisema, si msingi wa maendeleo, bali ni kitendea kazi cha kuleta maendeleo na msukumo wa kuimarisha maisha ya binadamu.

Sisi kama Taifa, hatujajua ni thamani ya pesa kwa kuwa tumelelewa kwa kusaidiwa pesa za misaada au kupokea mishahara lakini si kwa ajili ya uchapaji kazi au ubunifu.

Katika moja ya vitu tunavyojitahidi kukwepa kuvizungumzia ni matunda bora ya Ujamaa na Azimio la Arusha. Tumekimbilia kulaani kuangamia kwa viwanda na uzalishaji mali, huku tumesahau kuwa viwanda na mashirika haya, yalitumia mapato (fedha), kujenga middle class ya Tanzania ambayo ilihemea kuajiriwa na kupewa mshahara na marupurupu mengi, bila kuwa wabunifu wa kuongeza Tija au Ufanisi katika uzalishaji mali.

Pesa tunazo na utajiri tunao, lakini hatuna maadili ya kutuadabisha katika utumiaji wa fedha, hatuna mipango mizuri ya kuongeza fedha kwa kutumia uzalishaji mali na ubunifu, Hatuna uwezo wa kutumia vyanzo vyetu wenyewe kujizalishia mali na kuongeza fedha katika mifuko yetu na kuishia kuwa ombaomba.

Nimetaja vitu vitatu hapo juu. Maendeleo, Maadili na Kujitegemea. Fedha inaweza kupatikana kama jamii in nia ya kweli kuwa na maendeleo ambayo yanakwenda sambamba na maadili ili kujijengea kuwa Taifa na jamii inayojitegemea. Utashangaa ni jinsi gani maneno haya matatu yameweza kujenga sentenso nzuri sana ya kujjipa tumaini.

Umasikini, Unyonge, Uhujumu na Ufisadi, ni matokeo ya kutokuwa wawajibifu katika kuzalisha mali, kutunza thamani ya mali na fedha, kukosekana kwa dhamira ya uchapa kazi na kukosa ubunifu katika kuzalisha na kujipatia fedha.

Tumezoea kupewa vya dezo na kama ule wimbo wa "Kasimu", tunajua kuzitumbua fedha, lakini hatujui jinsi gani ya kuwa wazaishaji wa pesa hizi.

Ukosefu wa maadili ambao umeanzia katika oungozi, umeteremkia katika jamii. Kila mtu anataka pesa, na za haraka haraka, hatutaki kufanya kazi, hatutaki kuwa wabunifu, lakini twataka tuishi kwa neema ya kutafuna jibini na mkate wa kukaanga.

Nimegusia kuanguka kwa mashirika katika kujenga tabaka la kati (middle class). ni ukweli usiofichika kuwa kukosekana kwa ubunifu wa kuongeza ufanisi kulichangia kuanguka kwa mashirika na viwanda. La zaidi, kutolewa holela kwa ajira bila kuangalia na kujihoji kama kuongezeka huku kwa ajira kunawiana na uzalishaji mali na mapato.

Sisi kama Taifa, tulibahatika kujijenga kwa juhudi za kufadhiliwa na si kufanya kazi kwa kujituma au kuwa wabunifu wa vianzo vipya vya kazi au kuendeleza na kupanua vile tulivyorithi kutoka kwa mkoloni.

Hivyo basi, wakati tunapigana vita vya ufisadi ambavyo msingi wake mkuu ni tamaa na uvivu wa kuchapa kazi na kukimbilia kushiba haraka haraka, inabidi tujihoji nafsi kama jamii na Taifa.

Je tukishawafunga Mafisadi wote na kuing'oa CCM, ndi mwanzo wa neema na kutajirika? ndio mwanzo wa kuondoa umasikini na kuleta ubunifu, uwajibikaji, uchapakazi hodari, umakini na udhibiti ili tuiongeze mapesa na kuweza kuwa na huduma bora za jamii na kuwa Taifa linalojitegemea?

Jiulze kibinafsi, je mimi ni mbunifu, mchapa kazi, mwajibikaji, mwadilifu na najua thamani ya pesa na naweza kuizalisha marudufu na kudhibiti isipotee thamani?

Ndio maana namtolea wasifu Bob Mkandara. Yeye ni mmoja katika laki katika Taifa letu.

Ni mpaka pale ambapo tutaanza kujielimisha jinsi ya kutumia pesa na kuwa na malengo muhimu na kutumia pesa hizi kwa malengo ya muhimu na si kutumia tuu kwa kuwa zipo au tutapewa hundi la MDC kutoka kwa Marekani, WB, EU na IMF ndipo tunaweza kuleta maendeleo na kuweza kujitegemea. Kinyume cha hilo, tutaendelea kuwa "Kasimu bin Matanuzi" na hata wakija CUF na CHADEMA, tutaendelea kuzitumbua na kutokujali kuwa pesa, yahitaji kuitumikia.

"Kwa jasho la uso wako utakula chakula" Mwanzo 3:19, sisi tunahemea jasho la wenzetu ndio maana hatuna uchungu na pesa!
 
Naomba niambatanishe hii makala ya Mzee Mtei. Utaona kuwa Watanzania bado hatujui masuala hya pesa!


Edwin Mtei



MATAMSHI na maamuzi ya serikali ya hivi karibuni, yanaashiria ama hatuna washauri wa kiuchumi na fedha au tunapuuza ushauri huo. Nitatoa mifano michache:
Vyama vya wafanyakazi vikiongozwa na wakuu wao walitangaza kwamba walitaka kiwango cha chini cha mshahara kiwe sh 315,000 kwa mwezi. Mazungumzo yaliendelea baina ya waajiri na wafanyakazi, Serikali ikisimamia majadiliano kwa mujibu wa sheria.
Pia kulikuwa na tishio kwamba watumishi wake wangegoma kama kiwango cha sh 85,000 hakingepandishwa mpaka sh 315,000.
Sijasoma majibu ya serikali yaliyochambua madai haya ya wafanyakazi. Nilitegemea uchambuzi kuonyesha uwezekano wa nyongeza kiasi hicho, ukifafanua haja ya kutoa motisha kwa waajiriwa, tija kazini, athari za ongezeko kubwa katika mfumko wa bei na uwezo wa waajiri kulipa.
Katika mazingira ya utawala bora unaozingatia haki na uendeshaji wa uchumi endelevu, nilitegemea Wizara ya Mipango na Uchumi, Wizara ya Fedha na Wizara ya Kazi wangekaa na kuchambua kwa makini na kuonyesha ni kiwango gani cha chini kingeweza kuidhinishwa ili uzalishaji uendelee na papo hapo wafanyakazi wa kima cha chini waweze kumudu maisha.
Uchambuzi wa aina hii ulikuwa unafanywa katika enzi za awamu ya kwanza, na Rais Nyerere alikuwa anatangaza kila Mei Mosi, kima cha chini cha mshahara. Kima hiki kilizingatia mfumko wa bei tangu Mei mwaka uliopita, ukuaji wa uchumi na ongezeko la tija katika muda husika.
Baada ya uchambuzi huo mazungumzo baina wa wadau wote, yaani wafanyakazi, waajiri na serikali wangefuata ushauri unaotokana na huo uchambuzi yakinifu. Lakini miezi hii ya karibuni Waziri wa Kazi, John Chiligati, alikubaliana na wadau kadhaa na kutamka kima cha chini cha sh 150,000 na papo hapo kusema kuwa katika sekta fulani walipwe hata sh 315,000 kwa mwezi.
Wakati waajiri kadhaa walipoeleza kwamba tija ya viwanda vyao haiwezi kukidhi kiwango hicho na wafanyakazi wakagoma, waziri alitoa amri kwamba waajiri ni lazima walipe kiwango kilichofikiwa kisheria na pia hawawezi kufunga viwanda vyao! Kama Tanzania hatutaki kurudia mtindo ule wa ruzuku kutoka Hazina ya Serikali ili wafanyakazi wasiwafungie mameneja wao viwandani, basi ni lazima tupime hoja zote za wadau, wakiwemo waajiri na wafanya kazi. Ni umbumbumbu kutoa amri eti kiwanda kiendelee kama hutoi ruzuku.

Hata katika mashamba huwezi kulazimisha mkulima mkubwa alipe sh 85,000 kwa mwezi kama mazao yake hayakidhi kiwango hicho. Ama mkulima huyo atapunguza vibarua au ataacha kupalizi, kupiga dawa, kutia mbolea au kunyweshea.
Matokeo ni kwamba uchumi utaathirika. Hakuna yeyote anayefaidika kwa kutoa maagizo na amri za kisiasa zisizotekelezeka. Mfano mwingine ni matangazo yaliyotolewa na Serikali mwisho wa wiki kuwa kima cha chini serikalini kitakuwa sh 100,000 kwa mwezi kuanzia Januari mosi mwaka huu wa 2008.

Ghasia, Waziri anayehusika amesema watumishi wamekubaliana na uamuzi huo, na kwamba ongezeko hilo litagharimu Serikali sh 200 bilioni kwa mwaka. Lakini ameendelea kueleza kwamba serikali haina fedha katika bajeti yake ya sasa, bali wafanyakazi ni lazima wasubiri hadi Julai 2008 wakati bajeti ya mwaka 2008/2009 itakapoidhinishwa!
Magazeti yameeleza kwamba viongozi wa watumishi serikalini wamekubali kwa shingo upande, na wanasubiri.
Jambo linalotia wasiwasi ni kwamba kumekosekana ushauri wa kiuchumi na fedha hapa tena.
Kama kweli wafanyakazi wanahitaji nyongeza hiyo wamekubalije kusubiri? Malipo ya malimbikizo ya miezi sita yakilipwa Julai mosi, yatatibua mfumko wa bei kwa namna ambayo uchumi wa Tanzania wote utaathirika? sh 100,000,000,000 (bilioni mia moja) zikiingia katika mzunguko wa fedha siku moja, ni vurugu tupu; hasa kwa vile wahusika ni wafanyakazi wa kima cha chini ambao wamesubiri na wametaabika kwa muda mrefu? Bei zitapanda kiasi cha kumfadhaisha mfanyakazi.
Bidhaa zitakuwa adimu kiasi kwamba ongezeko hilo halitamsaidia mfanyakazi aliyepata ongezeko. Wananchi wengine watapandishiwa bei za bidhaa za kawaida wanunuazo. Hapa naona serikali imekosa tena ushauri thabiti wa kiuchumi. Kama ni lazima kurekebisha kima cha chini, basi mishahara hiyo ianze kulipwa Januari 2008. Inajulikana kwamba serikali haitozi fedha zote za kodi zinazoidhinishwa siku ile ile bajeti inapoanza kutumika. Inakopa. Kwa hiyo inaweza kukopa Januari 2008, kama itakavyokopa Julai, 2008. Kwa hiyo, kama serikali ni lazima irekebishe kima cha chini, basi Bunge liidhinishe fedha hiyo ya nyongeza katika kikao cha Januari 2008. Hii itamaanisha kila mwezi, kuanzia Januari 2008, sh 16.7 bilioni zinaingizwa katika mzunguko wa fedha nchini na labda kwa utaratibu huo tutaweza kujirekebisha polepole, badala ya kuingiza kwa mkupuo mmoja sh 100 bilioni Julai mosi.
 
REV Kishoka!

Mtu mwenye Utu, ubinaadamu, Maadili na "Atawei Pesa" kwani zitakuwa na Thamni ya maendeleao kwakwe, familia na Taifa lake.

Mtu asiye na Utu, ubinaadamu, Maadili, Pesa zitammaliza yeye, familia yake na taifa lake..Kamwe asiziguse.

UTU ni Maadili ya kiutu, Utu ni Ubinaadamu na maendeleo yake. Utu ni Kujitegemea. Utu ni heshima na umakini katika kujitafutia riki kwa kujitegemea kwa jasho lako.

Kutokijitegemea sio UTU, Kutokuwa na Maadili sio utu, Kutokijieheshimu,Sio UTU, Kutukuwa muadilifu sio utu, PESA ni Kwa ajili Ya UTU. Kama huna UTU kimbia PESA kama Ukoma. Kimbia Pesa wewe, familia yako na Taifa. Kwani hata Ukizitwaa zitakukimbiza kukuondoa kwenye utu..maana ndipo zilipokukuta.

Hatuhitaji PESA kwanza ili tuendelee Tunahitaji UTU na Maadili yake kwanza!!
 
Hapa kuna mambo mazito na ya msingi sana..

Tukiwaondoa mafisadi wote, then what?

...offcourse tutakuwa tumesave pesa zetu ambazo zitasaidia maendeleo,wewe vipi tena unafikiri hapa tunapiga kelele za bure bila expectation yeyote? hayo ndio mambo ya kuona watu vilaza wapiga kelele tuu bila purpose.
 
Hapa kuna mambo mazito na ya msingi sana..

Tukiwaondoa mafisadi wote, then what?

I will have to echo Mzee Mtei on this. We need competent economists and financial/money managers in our country who will be complimented by efficient auditors and accountants to make sure that what is planned, is being used according to the plans and any irregular spending needs to be addressed.

Financial/Money Matters need to be a priority in education system in Tanzania. if I recall well, it wa Mungai who decided that it was not useful to teach commerce and accounting in general education.

I would suggest that parallel to civic studies in primary education, they should introduce money matters in primary school. This will teach our kids and grand children the value of money and how to be thrifty and focus to be hard workers to create wealth and not wait until purbety or late teens to teach them an important aspect of their lives.
 
Hivi pesa zote za EPA, Meremeta, Minara ya dhahabu, IPTL, Richmond, ATCL na TRC kwa ujumla zinaweza kufikia asilima ngapi ya bajeti yetu na hasa kile kifungu cha fedha za maendeleo?
 
Mods,

Naomba muunganishe hii mada na ile thread ya Umasikini wetu; Matumizi na matanuzi.
 
Back
Top Bottom