Monduli: Waziri Jumaa Awezo akuta maji hayatoki kisa Sh. elfu 50, amtumbua Meneja mbele ya Wananchi

YEHODAYA

JF-Expert Member
Aug 9, 2015
36,908
51,904
WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amefanya ziara ya kikazi katika wilaya ya Monduli mkoani Arusha na kukuta wananchi hawapati maji kutokana na changamoto mbali mbali hali iliyopelekea kuchukua hatu ya kumsimamisha kazi Meneja wa mradi wa maji wa RUWASA Nevill D. Msaki.

 
Hivi jamani pammoja na juhudi na hatua zinazochukuliwa bado kuna uzembe hivi wa hali ya juu. Na kwa nini hassa??? Mbunge kwanza ulikua wapi hadi mradi wa mabioloni unachezewa? Mkuu wa mkoa na hadi wa wilaya? Hadi waziri aje ndio haya madudu ya shughulikiwe?

Binafsi natoa maoni ADHABU ya watu kama hawa wazembe na wezi inabidi ipandishwe, watu hawaogopi, wanajua wakitumbuliwa tayari wameshajiwekezea huko mahela chungu nzima kwahiyo maisha yao yataendelea kunyooka, na akiletwa mwingine nae ataendelea na uzembe na wizi huohuo, hadi atakaposhtukiwa tiari kashakula mabilioni. watu hawa ni kuwaweka ndani si chini ya miaka 10 na hakuna kununua kifungo. Wallahi bada ya hapo hakuna atakaye thubutu kuleta madudu hayo.
 
Daaa yaan mp@k mkubw@ aje
Umeona hadi naibu waziri walivyomzungusha kwenye kisima tu ohh funguo hazipo

Mradi wanasema ulishakabidhiwa kwa wananchi kumbe uongo

maji ohh yanatoka kote kumbe sehemu kiduchu

Oh hapa hayatoki sababu zilikosekana elfu 50 kwenye akaunti kuna mamilioni!!! nk

Yaani huyo meneja asipodakwa na TAKUKURU watakuwa hawajui kazi yao
 
Umeona hadi naibu waziri walivyomzungusha kwenye kisima tu ohh funguo hazipo

Mradi wanasema ulishakabidhiwa kwa wananchi kumbe uongo....
Alaf mtuu anakuja analalamik serikal.ya ccm angal watendaj wa serikal ndio wanachafua hakika mh rais anakz ngum sna
 
Hivi jamani pammoja na juhudi na hatua zinazochukuliwa bado kuna uzembe hivi wa hali ya juu. Na kwa nini hassa??? Mbunge kwanza ulikua wapi hadi mradi wa mabioloni unachezewa? Mkuu wa mkoa na hadi wa wilaya? Hadi waziri aje ndio haya madudu ya shughulikiwe?
Yaani kuna watu vichwa ngumu acha kabisa.Raisi unamwona hadi anakonda. Ana delegate akiwaamini alio delegate madaraka chini lakini wapi!! upigaji pesa uko palepale na uongo pale pale!! Naibu waziri asingekuwa makini akaipokea hiyo ripoti ndio ilikuwa imetoka hiyo.

Mijizi imeshajua raisi anawaamini sana mawaziri kwa hiyo imehamia kwa mawaziri kuwa ukimudu kumdanganya waziri atampelekea ripoti raisi kuwa kila kitu kiko sawa itaishia hapo.Hao ndicho walitaka kufanya.Ila wamekwaa kisiki Naibu waziri yuko ngangari kagoma kudanganyika!

Hebu fikiria hawa watu kipindi kilichopita cha kutofuatiliwa walivyotupiga pesa ni hatari.Hivi sasa wanafuatiliwa kwa nguvu bado vichwa vigumu tu
 
Alaf mtuu anakuja analalamik serikal.ya ccm angal watendaj wa serikal ndio wanachafua hakika mh rais anakz ngum sna
Hao ndio utakuta wanabweka mishahara iongezwe kila siku kazi wanayofanya ndio hiyo ya kuhakisha wananchi hawapati maji.Mishahara kila mwezi wanapewa na migari mizuri na nyumba lakini maji hayatoki !!!!
 
WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amefanya ziara ya kikazi katika wilaya ya Monduli mkoani Arusha na kukuta wananchi hawapati maji kutokana na changamoto mbali mbali hali iliyopelekea kuchukua hatu ya kumsimamisha kazi Meneja wa mradi wa maji wa RUWASA Nevill D. Msaki.
kuna uzembe hapa kwakweli. mpaka kiongozi aje ndio waruke ruke. wanashindwaje ku solve tatizo dogo kama hilo
 
Hivi jamani pammoja na juhudi na hatua zinazochukuliwa bado kuna uzembe hivi wa hali ya juu. Na kwa nini hassa??? Mbunge kwanza ulikua wapi hadi mradi wa mabioloni unachezewa? Mkuu wa mkoa na hadi wa wilaya? Hadi waziri aje ndio haya madudu ya shughulikiwe?....
Juhudi zinachukuliwa kwenye makaratasi na kwenye vyombo vya habari, field ni tofauti kwani pesa hazifiki kwa wakati na zikifika hazitoshi
 
kuna uzembe hapa kwakweli. mpaka kiongozi aje ndio waruke ruke. wanashindwaje ku solve tatizo dogo kama hilo
Wahusika wapigwe chini tu waajiriwe wengine hao wazembe waende wakatafute shughuli zingine za kufanya
 
Hao ndio utakuta wanabweka mishahara iongezwe kila siku kazi wanayofanya ndio hiyo ya kuhakisha wananchi hawapati maji.Mishahara kila mwezi wanapewa na migari mizuri na nyumba lakini maji hayatoki !!!!
Si ndio hap.sio poa kiukwel kwa hil hat kma.mh rais akiwa mkal ni halal.kwa huu utumbo
 
Hivi jamani pammoja na juhudi na hatua zinazochukuliwa bado kuna uzembe hivi wa hali ya juu. Na kwa nini hassa??? Mbunge kwanza ulikua wapi hadi mradi wa mabioloni unachezewa? Mkuu wa mkoa na hadi wa wilaya? Hadi waziri aje ndio haya madudu ya shughulikiwe?..
kuna watu ugoi goi ni tatizo la kuzaliwa nalo.

yaani kama hapo kasimamishwa ndio akili zinarudi sasa.
 
WAZIRI wa Maji, Jumaa Aweso, amefanya ziara ya kikazi katika wilaya ya Monduli mkoani Arusha na kukuta wananchi hawapati maji kutokana na changamoto mbali mbali hali iliyopelekea kuchukua hatu ya kumsimamisha kazi Meneja wa mradi wa maji wa RUWASA Nevill D. Msaki.
Mkuu hiyo elfu 50,000 inahusiana na nini? Sijaiona kwenye post yako...!
 
Kwann hii nchi imekuwa hvy mpak watumbuliwe ndio kujitambuaa asee wanakera mh rais anakz kwel.kwel
ukianza kuhesabu viongozi waandamizi ni wengi mno, follow up inakiwa ngumi, ila kuna vilaza wengi sana.

kila mtu akisimama vyema alipo, hi nchi itakuwa moto sana.
 
Juhudi zinachukuliwa kwenye makaratasi na kwenye vyombo vya habari, field ni tofauti kwani pesa hazifiki kwa wakati na zikifika hazitoshi
Kwa hiyo hiyo elfu 50 walikuwa wakisubiri itoke hazina?

Mbunge ana mamilioni ya pesa za mfuko wa jimbo.Mshahara anapokea milioni 11 kashindwa kutoa elfu 50 wananchi wake wapate maji?

Huyo mtaalamu mwingine mbona kasema kuna mamilioni kwenye akaunti? kuchomoa hapo elfu 50 imeshindikana?

Halmashauri pia imeshindwa kutoa elfu 50?

Hata wangewaomba wananchi wachangie hata mia tano mia tano mbona ingepatikana kirahisi tu?

Kwa nini walidanganya kuwa mradi ulishakabidhiwa kwa wananchi na maji yanatoka wakati si kweli?
 
Kabla ya kuhukumu fuatilia mzee, Meneja anatikiwa kukusanya mapato na hajavunja sheria anafuata muongozo wa Wizara unaomtaka kukusanya mapato na kuwakatia maji ambao hajalipa bill, ulitaka afanye kama sio uonevu?
 
Back
Top Bottom