Mollel na Laizer waachiwa huru: Demokrasi ndani ya CCM imebakwa?

Mafuchila

JF-Expert Member
Apr 29, 2006
751
65
Mahakama hatimaye imewaachia huru wabunge wawili waliotuhumiwa kwa rushwa ya uchaguzi, hali iliyopelekea wabunge hao wawili kukosa haki yao ya msingi ya kugombea kama wanachama wa CCM katika uchaguzi uliopita. Kitendo hicho kimetokana na maombi ya TAKUKURU kuitaka mahakama ifute kesi hiyo kwa kutokuwa na nia ya kuendelea nayo, kesi ambayo ilishawaumiza wabunge hao kwa CC kutengua ugombea wao. Kitendo hiki bila shaka hakiashirii mwisho mwema wa siasa zetu, hasa ukizingatia kuwa kesi hiyo ilihusishwa sana na shinikizo la kisiasa kwa TAKUKURU. Binafsi naona kesi hii imeshusha hadhi ya TAKUKURU kwa mara nyingine tena. Bila shaka hatua madhubuti zinapaswa kuchukuliwa, ili vita dhidi ya wala rushwa na mafisadi isitumike kama fimbo ya kuwaadhibu wale ambao wanatofautiana kimaslahi ndani ya mfumo wetu wa siasa. Naomba kuwasilisha hoja.


Wabunge CCM waachiwa




na Mustafa Leu, Arusha



MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha, jana, imewaachilia huru wabunge wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha, na wanachama tisa wa CCM waliokuwa wakikabiliwa na tuhuma za rushwa.

Wabunge hao ni Elisa Mollel wa Arumeru Magharibi na Lekule Laizer wa Longido, Mkoa wa Arusha, pamoja na Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Arusha, Daniel ole Porokwa.

Wengine ni mjumbe wa mkutano wa wilaya, mkoa na taifa wa chama hicho, John Ndelilio Pallangyo na mjumbe wa Wilaya ya Arumeru, Abraham Zellote Kaaya na Katibu wa Kata ya Longido, Emmanuel Luka Laizer.

Pia wamo Ndewirwa Soori Mbise, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Nkoaranga na mjumbe CCM mkoa na taifa, Charles Akyoo, Ofisa Mtendaji Kata ya User River pamoja na Abubakari Shekalaghe ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM, Kata ya User River.

Akitoa uamuzi wa kuwaachia huru, Hakimu wa mahakama hiyo, George Ndabagoye alisema kesi hiyo imefutwa baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), kuomba ifutwe.

"Kutokana na maombi hayo ya Takukuru, mahakama imekubaliana nayo na inafuta kesi hiyo ya jinai kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 9 ya mwaka 1985 na washitakiwa wako huru," alisema hakimu Ndabagoye.

Wakizungumza mara baada ya kuachiwa huru, Mbunge wa Longido, Lekule Laiser aliishukuru mahakama kwa kuwatendea haki na kufutilia mbali kesi hiyo aliyosema kuwa ni ya kisiasa.

"Tumepoteza muda mwingi wa kazi za kuwatumikia wananchi, tumefika mahakamani kwa muda wa mwaka sasa hakuna siku kesi imesikilizwa, tunasikitika sana kwa hayo, lakini leo tumeona haki ikitendeka," alisema Laizer.

Alisema ingawa majina yao awali yalichafuliwa kutokana na kadhia hiyo, lakini sasa ni sura nyingine ya wananchi na wanachama wa chama cha mapinduzi kujua ukweli wa tuhuma dhidi yao.

Naye Mbunge wa Arumeru Magharibi, Elisa Mollel alisema suala lao limechukua muda wa mwaka mzima, lakini hakuna hata siku waliyoulizwa kitu. "Kama sisi tunafanyiwa hivyo itakuwaje kwa wananchi wa kawaida?" alihoji Mollel.

Alieleza kuwa Takukuru hawakuwa na ushahidi wowote katika shauri hilo, na kwamba ni mambo ya kisiasa ndiyo yaliwafikisha mahakamani.

Wabunge hao pamoja na watuhumiwa wengine, walikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa madai ya kutoa rushwa wakati wa kampeni za uchaguzi ndani ya CCM.

Laizer alikuwa akiwania nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha wakati Mollel alikuwa akiwania nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC), kupitia mkoa huo.

Hata hivyo, watuhumiwa hao baadaye walifutwa kuwania nafasi hizo kutokana na kesi hiyo ya jinai iliyokuwa ikiwakabili.

Source: Tanzania Daima 5/07/2008
 
Waliosafishwa na mahakama wanatakiwa wawe wazi na kutueleza ni akina nani waliowapakazia shutuma hizo ili watu hao wajulikane kwa wananchi maana hawana tofauti na mafisadi wanaorudisha nyuma maendeleo ya taifa letu.
 
Waliosafishwa na mahakama wanatakiwa wawe wazi na kutueleza ni akina nani waliowapakazia shutuma hizo ili watu hao wajulikane kwa wananchi maana hawana tofauti na mafisadi wanaorudisha nyuma maendeleo ya taifa letu.

Infact ni mafisadi walio nyuma ya mpango mzima wa kuwaondoa wanachama wenzao kwenye kinyang'anyiro cha uchaguzi, isivyo halali. Lakini hili sio tu linatushtua, lakini linaonyesha ni jinsi gani taasisi nyeti kama TAKUKURU inavyoweza kutumika vibaya kuumiza watu, badala ya kufanya kazi yake halali ya kukamata mafisadi.
 
Mahakama hatimaye imewaachia huru wabunge wawili waliotuhumiwa kwa rushwa ya uchaguzi, hali iliyopelekea wabunge hao wawili kukosa haki yao ya msingi ya kugombea kama wanachama wa CCM katika uchaguzi uliopita. Kitendo hicho kimetokana na maombi ya TAKUKURU kuitaka mahakama ifute kesi hiyo kwa kutokuwa na nia ya kuendelea nayo, kesi ambayo ilishawaumiza wabunge hao kwa CC kutengua ugombea wao. Kitendo hiki bila shaka hakiashirii mwisho mwema wa siasa zetu, hasa ukizingatia kuwa kesi hiyo ilihusishwa sana na shinikizo la kisiasa kwa TAKUKURU. Binafsi naona kesi hii imeshusha hadhi ya TAKUKURU kwa mara nyingine tena. Bila shaka hatua madhubuti zinapaswa kuchukuliwa, ili vita dhidi ya wala rushwa na mafisadi isitumike kama fimbo ya kuwaadhibu wale ambao wanatofautiana kimaslahi ndani ya mfumo wetu wa siasa. Naomba kuwasilisha hoja.


Wabunge CCM waachiwa




na Mustafa Leu, Arusha



MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Arusha, jana, imewaachilia huru wabunge wawili wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Arusha, na wanachama tisa wa CCM waliokuwa wakikabiliwa na tuhuma za rushwa.

Wabunge hao ni Elisa Mollel wa Arumeru Magharibi na Lekule Laizer wa Longido, Mkoa wa Arusha, pamoja na Mwenyekiti wa UVCCM, Mkoa wa Arusha, Daniel ole Porokwa.

Wengine ni mjumbe wa mkutano wa wilaya, mkoa na taifa wa chama hicho, John Ndelilio Pallangyo na mjumbe wa Wilaya ya Arumeru, Abraham Zellote Kaaya na Katibu wa Kata ya Longido, Emmanuel Luka Laizer.

Pia wamo Ndewirwa Soori Mbise, Ofisa Mtendaji wa Kata ya Nkoaranga na mjumbe CCM mkoa na taifa, Charles Akyoo, Ofisa Mtendaji Kata ya User River pamoja na Abubakari Shekalaghe ambaye ni Katibu Mwenezi wa CCM, Kata ya User River.

Akitoa uamuzi wa kuwaachia huru, Hakimu wa mahakama hiyo, George Ndabagoye alisema kesi hiyo imefutwa baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU), kuomba ifutwe.

"Kutokana na maombi hayo ya Takukuru, mahakama imekubaliana nayo na inafuta kesi hiyo ya jinai kwa mujibu wa kifungu cha sheria namba 9 ya mwaka 1985 na washitakiwa wako huru," alisema hakimu Ndabagoye.

Wakizungumza mara baada ya kuachiwa huru, Mbunge wa Longido, Lekule Laiser aliishukuru mahakama kwa kuwatendea haki na kufutilia mbali kesi hiyo aliyosema kuwa ni ya kisiasa.

"Tumepoteza muda mwingi wa kazi za kuwatumikia wananchi, tumefika mahakamani kwa muda wa mwaka sasa hakuna siku kesi imesikilizwa, tunasikitika sana kwa hayo, lakini leo tumeona haki ikitendeka," alisema Laizer.

Alisema ingawa majina yao awali yalichafuliwa kutokana na kadhia hiyo, lakini sasa ni sura nyingine ya wananchi na wanachama wa chama cha mapinduzi kujua ukweli wa tuhuma dhidi yao.

Naye Mbunge wa Arumeru Magharibi, Elisa Mollel alisema suala lao limechukua muda wa mwaka mzima, lakini hakuna hata siku waliyoulizwa kitu. "Kama sisi tunafanyiwa hivyo itakuwaje kwa wananchi wa kawaida?" alihoji Mollel.

Alieleza kuwa Takukuru hawakuwa na ushahidi wowote katika shauri hilo, na kwamba ni mambo ya kisiasa ndiyo yaliwafikisha mahakamani.

Wabunge hao pamoja na watuhumiwa wengine, walikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa madai ya kutoa rushwa wakati wa kampeni za uchaguzi ndani ya CCM.

Laizer alikuwa akiwania nafasi ya Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha wakati Mollel alikuwa akiwania nafasi ya ujumbe wa Halmashauri Kuu (NEC), kupitia mkoa huo.

Hata hivyo, watuhumiwa hao baadaye walifutwa kuwania nafasi hizo kutokana na kesi hiyo ya jinai iliyokuwa ikiwakabili.

Source: Tanzania Daima 5/07/2008

Mahakama ifute UAMUZI HUO MARA MOJA!

Kwani hawajui kuwa TAKUKURU INA WAJUMBE WA MAFISADI NDANI NA BUNGE LILISHAWAHI KUJULISHWA? Nani asiyejuwa kuna kilio kuhusu TAKUKURU?

Halafu huyu jaji anafuta kesi kwa amri ya chombo ambacho chenyewe kina MASWALI LUKUKI YA KUJIBU?

Wabunge wazalendo ingilieni kati uamuzi huo utenguliwe kwani ni maamuzi ya kisiasa kwa vile UKWELI NI KUWA PESA WALIZOTUMIA KWENYE RUSHWA NI ZA EPA!
 
Waishitaki Takururu kama iliwaweka danguroni kwa muda wa mwaka mmoja bila ya kuitwa hata siku moja na mahakama nayo ilikuwaje ikawaweka watu ndani mwaka mmoja wakati jalada la kesi hakuna.
Lazima hawa warudi kudai fidia.
 
Waishitaki Takururu kama iliwaweka danguroni kwa muda wa mwaka mmoja bila ya kuitwa hata siku moja na mahakama nayo ilikuwaje ikawaweka watu ndani mwaka mmoja wakati jalada la kesi hakuna.
Lazima hawa warudi kudai fidia.

TAKUKURU iliwaweka matatani na sasa inawasafisha na hivyo hawawezi kuwashitaki!
Mwenye tatizo ni huyo hakimu aliyesikiliza maneno ya TAKUKURU kabla haijafanyiwa marekebisho na wajumbe hao wa wanamtandao kuondolewa humo na wao kujumuishwa kwenye ufisadi...Kina Hosea nk!
 
Kama kuna mtu alitegemea hawa jamaa watafikishwa kokote basi alikuwa anaota. Ni sawa na mtu kufikiri mafisadi wa EPA. Richmond , meremeta na wengine watafikishwa mahakani na haki itendeke. Hapa TZ kuna watu wakifanya uhalifu hawaendi gerezani, lakini kama ukifanya wewe..............
 
Nalilia taifa langu!

Mahakama kawaida ina-kanuni moja!!! kwamba lazima uhakikisha bila shaka... beyond doubt!!!

Kwa maana hiyo yawezekana wakawa wamefanya lakini ikashindikana kuthibitisha bila kuwa na mashaka...

Hivyo wanaachiwa huru!!! The fact kwamba mahakama imefanya kazi yake... Utawala bora Umezingatiwa...

Sidhani ni jambo ya hekima ati kurudi nyuma kusema... nani kasema lile au lile... otherwise taifa hili linaonekana ni la wambea ...
 
Kasheshe,

nakubaliana na wewe, lakini tunachotaka kusikia ni kwanini TAKUKURU wameomba kufuta kesi? Je hawakuwa na ushahidi wa kutosha kuwashtaki? Je wameomba kufuta ili kulinda "heshima" ya serikali?
 
Nalilia taifa langu!

Mahakama kawaida ina-kanuni moja!!! kwamba lazima uhakikisha bila shaka... beyond doubt!!!

Kwa maana hiyo yawezekana wakawa wamefanya lakini ikashindikana kuthibitisha bila kuwa na mashaka...

Hivyo wanaachiwa huru!!! The fact kwamba mahakama imefanya kazi yake... Utawala bora Umezingatiwa...

Sidhani ni jambo ya hekima ati kurudi nyuma kusema... nani kasema lile au lile... otherwise taifa hili linaonekana ni la wambea ...

Huu ushaidi uliopo...Mahakama yetu ikileta MIZENGWE..BASI NA MIMI NITAFUNGUWA MASHITAKA DHIDI YA SERIKALI YETU!

Na nimeshasema haki isipofuatwa...Hapa wengine tushajitoa MUHANGA KITAMBO!

Najuwa MKONO WA MFISADI NI MREFU..NA HAPA USA WAKO NA WANA MASLAHI!

Kila mtu anajuwa kazi ninayoifanya hapa jf ni ya hatari!

Na hivyo ninaomba Mungu kila siku wailinde FAMILIA YANGU NA WAZALENDO WENGINE WALIOKO NYUMA YA MPAMBANO HUU WA UHURU!
 
Kama kuna mtu alitegemea hawa jamaa watafikishwa kokote basi alikuwa anaota. Ni sawa na mtu kufikiri mafisadi wa EPA. Richmond , meremeta na wengine watafikishwa mahakani na haki itendeke. Hapa TZ kuna watu wakifanya uhalifu hawaendi gerezani, lakini kama ukifanya wewe..............

Nakuunga mkono 100% maana swali la kujiuliza wameshinda kihalali ama ni kifisadi maana katika nchi hii ya kitu kidogo na watu wadogo haki inanunuliwa na kila kitu pesa tuu.
 
Nakuunga mkono 100% maana swali la kujiuliza wameshinda kihalali ama ni kifisadi maana katika nchi hii ya kitu kidogo na watu wadogo haki inanunuliwa na kila kitu pesa tuu.

Mnaota ndoto za mchana!
Hii ni jf...!Hakuna kusafishana hapa! Not under wazalendo's WATCH!
 
Nakuunga mkono 100% maana swali la kujiuliza wameshinda kihalali ama ni kifisadi maana katika nchi hii ya kitu kidogo na watu wadogo haki inanunuliwa na kila kitu pesa tuu.

Kevo,'
Nasikia walishtakiwa kifisadi. Kulikuwa na mkono wa Lowassa pale. Kuna mwingine anashangaa kama Takukuru ilishaingiliwa na mafisadi---nenda kaangalie UWT.
 
Sijakupata kidogo mkuu.Ufafanuzi please?

Originally Posted by Kevo
Nakuunga mkono 100% maana swali la kujiuliza wameshinda kihalali ama ni kifisadi maana katika nchi hii ya kitu kidogo na watu wadogo haki inanunuliwa na kila kitu pesa tuu.

Pale unapodai kuwa hakuna atakaye jaribu kupambana na UFISADI KWANI WANA PESA NA KESI ITAISHA!
Hapo ni kuwavunja wananchi MOYO!
Wfanye hivyo...Kuna ile COALITION YA KUFUNGUA KESI YA EPA!
Na mimi nina OPTION YA KUISHTAKI SERIKALI!
Sasa wewe ukiwa na mawazo kuwa watashinda...Umekosea!

Na hii ni kwasababu kauli yako hapo juu iliunga mkono kauli hii hapa chini ya BONGOLANDER AMBAYO BINAFSI NAIPIGA VITA KABISA!

Originally Posted by Bongolander
Kama kuna mtu alitegemea hawa jamaa watafikishwa kokote basi alikuwa anaota. Ni sawa na mtu kufikiri mafisadi wa EPA. Richmond , meremeta na wengine watafikishwa mahakani na haki itendeke. Hapa TZ kuna watu wakifanya uhalifu hawaendi gerezani, lakini kama ukifanya wewe..............
 
Wapokea rushwa kutoka CCM wanaombewa waachiwe na TAKUKURU!! Hayo maombi yalitoka kweli TAKUKURU au Ikulu? TAKUKURU wanasema hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo bila kutoa sababu zozote za msingi!! Kama kawaida ya TAKUKURU kwa mara nyingine tena wamewaangusha Watanzania. Hizi kesi ndogo ndogo za wala rushwa zinawashinda, kesi kubwa dhidi ya akina Mkapa, Mramba, Lowassa, Karamagi, Chenge, Msabaha na wengineo wataziweza kweli?

TAKUKURU bora ifutwe tu kwa sababu Watanzania hatuoni umuhimu wowote wa kuwa na taasisi hiyo ambayo imeshindwa kazi.
 
Wapokea rushwa kutoka CCM wanaombewa waachiwe na TAKUKURU!! Hayo maombi yalitoka kweli TAKUKURU au Ikulu? TAKUKURU wanasema hawana nia ya kuendelea na kesi hiyo bila kutoa sababu zozote za msingi!! Kama kawaida ya TAKUKURU kwa mara nyingine tena wamewaangusha Watanzania. Hizi kesi ndogo ndogo za wala rushwa zinawashinda, kesi kubwa dhidi ya akina Mkapa, Mramba, Lowassa, Karamagi, Chenge, Msabaha na wengineo wataziweza kweli?

TAKUKURU bora ifutwe tu kwa sababu Watanzania hatuoni umuhimu wowote wa kuwa na taasisi hiyo ambayo imeshindwa kazi.

Kabla ya kufutwa wafunguliwe mashtaka kwani wamekuwa wakifanya kazi za kuwatetea na kuwasafisha MAFISADI KWA KUTUMIA PESA ZA KODI YA MWANANCHI PAMOJA NA NYINGINEZO ZINAZOTOKA KWA WAFADHILI ZA KUPAMBANA NA RUSHWA!

Tunataka mahesabu yote ya PESA WANAZOPEWA KUYALINDA MAFISADI...PESA AMBAZO NI MAMILIONI YA DOLA..BUNGE LIFANYE KAZI YAKE LA SIVYO MAMBO NI MBAYA!

NA PIA TUNATAKA BUNGE LIZIJADILI RIPOTI ZOTE ZA EPA, MADINI NK...ILI MASWALI YAJIBIWE NA SHERIA ICHUKUWE MKONDO WAKE!

KAMA NI SHERIA...BASI NDIYO ITAWASAFISHA NA KAMWE SI PROPAGANDA ZA KUWA WATU HAWAKUZALIWA MAFISADI!

HAKUNA ALIYEZALIWA JAMBAZI LAKINI HAINA MAANA KUWA JAMBAZI HALIFIKISHWI KUNAKO SHERIA...SIMPLY KWASABABI HAKUZALIWA JAMBAZI!
 
Mimi nilishajua tu kwamba kesi hii itakwisha kwa jinsi ilivyokwisha. Hata siku moja hawa ccm ambao ni watoa rushwa wakubwa hawawezi kushitakiwa na kufungwa. Kwanza wao si wa kwanza kutoa rushwa. Na hatuwezi kusema they were innocent kwa sababu tu hawakutiwa hatiani. Bado nitaendelea kuamini kuwa walitoa rushwa na walikamatwa kweli, ila kama kawaida ili kulinda heshima ya chama cha wezi Takukuru wameamriwa kuiondoa kesi mahakamani.
Kama wakina Laizer wanataka tuamini kuwa they were innocent waje hapa watupe ushahidi na waeleze kwa vipi walikamatwa?. Na who was behind kukamatwa kwao? Na je wako tayari kushitaki au kudai fidia kwa kuharibiwa majina yao? Sisi tutapima na kuona ukweli ulipo.
Si hivyo nitabaki kuamini kesi imetupwa ili kukilinda chama cha majambazi na wezi wenzao.
 
Waungwana na hasa Mushi,

Mbona mnakuwa wasahaulifu namna hii? Je mmesahau kuwa tuhuma hizi kuwa hawa jamaa walitoa Rushwa zilipandwa na Vigogo wa CCM ili Mollel na Laizer wapakwe madoa na kuondolewa Kugombea viti vya NEC CCM?

Je mmesahau kuwa Mollel na Laizer wanajulikana ni maadui wa Lowassa na ilikuwa kampeni marudufu karibu kukigawa CCM mkoani Arusha ili kuhakikisha watu wa Lowassa wanaingia NEC?

Je mmesahau baada ya tuhuma za Ufisadi zilizosababisha Kikwete kuvunja Baraza la Mawaziri kutokana na Lowassa kujiuzulu kwa tuhuma za Richmond, zilisababisha kikao cha NEC na CC Butiama kiwe mshike mhike baada ya baadhi ya Wajumbe kuhoji iweje Watuhumiwa wa Ufisadi Lowassa, Chenge, Karamagi, Mramba, Msabaha na Rostam waendelee kuwa wajumbe wa NEC na CC huku wanatuhuma za kuhujumu Taifa na kwa nini hawavuliwi huo ujumbe na kuwekewa pingamizi kama Mollel na Laizer walivyofanyiwa?

Ukweli ni kuwa Kesi hii ilikuwa ya Haramu, TAKUKURU walitumiwa na CCM kupaka matope kina Mollel, Laizer na wenzao ili Uchaguzi wa CCM Arusha ufanyike kwa matakwa ya Lowassa na wenzake.

Wakulaumiwa si Mahakama, ni TAKUKURU kwa kukimbilia kushitaki kina Mollel na Laizer kwa jambo la uzushi na ushahidi wa kuzusha huku wanawaachia kina Chenge wanapeta!

Hii ni aibu kubwa kwa CCM na kama jinsi tunavyoshupalia Wangwe afukuzwe, basi sasa mpira uwageukie CCM.

Hili ni doa na tuwapake matope na mavi ya farasi, ng'ombe na nguruwe CCM iendelee kunuka Rushwa!

Kwa nini CCM iliogopa kuwaufukuza Ujumbe wa NEC na CC Lowassa, Chenge, Msabaha, Karamagi, Mramba na Rostam huku wakiwa na tuhuma? Je CCM kinaliambia nini Taifa ikiwa kinafanya mambo kwa Upendeleo na kugawanya wanachama?

Jee CCM ni mali ya Lowassa, Chenge, Msabaha, Karamagi na Rostam au ni mali ya wanachama Wakulima na Wafanyakazi wa Tanzania?
 
Mamilioni Ya Dola Alizopewa Kikwete Kwa Madai Ya Kupigana Na Rushwa Ni Ya Kulinda Rushwa!

Nimeshawambia Kuwa Hii Issue Nitawafikishia Na Ama Nimeshawafikishia Wamarekani Kuwa Hayo Mabilioni Wanayompa Kikwete Si Ya Kupigana Na Rushwa Na Ufisadi...Bali Kuulinda Na Kujilinda Kwani Wao Ndio Mafisadi!

Mafisadi Wapewe Vipi Pesa Za Kujilinda Na Kina Bush Na Sisi Tunyamaze?

Wananchi Nao Wasinyamaze Kwani Takukuru Wanalipwa Kwa Jasho Lao PIA Lakini Wanawalinda Viongozi Mafisadi Kwa Kutumia Jasho La Wananchi Na Kusaidiwa Na Mkaburu Waliye Mwuzia Nchi!
 
Back
Top Bottom