Moja ya sifa za Spika wa Bunge popote Duniani ni kuweza kuunganisha Wabunge kuwa kitu kimoja

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
1. Unapoona pale Bunge linashindwa kuweka maridhiano kati ya Wabunge kwa jambo dogo, jua Spika ni tatizo!

2. Unapoona Spika anatoa maamuzi ya haraka na ya jazba ya jambo lililopaswa kupelekwa na kujadiliwa kwanza na kamati za bunge ujue ni vigumu sana kuleta umoja wa wabunge.

Bahati nzuri, mimi ni mfuatliliaji na mtizamaji kupitia media mbalimbali za mabunge ya nchi za Jumuia ya madola nk.

Mfano Bunge la Uingereza, Kenya, Uganda, Afrika ya Kusini nk. Mojawapo ya kazi kubwa ya Spika ni kuwaweka Wabunge sawa pale hoja zinapokinzana ha hata inapotokea kuvurugana au kugomea bunge. Mfano issue ya Brexit pale bunge la England lilipokuwa likijadili jambo hilo. Au bunge la Kenya pale walipoparaganyika kuhusu issue ya Raisi na Makamu wake kushtakiwa ICC.

Tuliona pia pale Uganda issue ya majuzi kuhusu Raisi Museveni kuweka muswada wa kurefusha umri wa Rais.

Kwa mifano hii mitatu kwa mtu aliyefuatilia,angegundua tofauti ya aina ya uendeshaji wa bunge letu katika judgements hasa za spika, weledi na uthamini wa wabunge na Mabunge hayo niliyoyataja.

Hapa kwetu, ni mara nyingi Spika analoose self control ya jambo dogo ambapo Kamati za Bunge zingeweza kumsaidia na bunge likaendelea vyema na mambo ya msingi!

Mfano. Spika,bila kutaja msingi wa hoja anasema" Piga ua pamoja na Corona iliyopo,lazima bajeti zote zipitiwe na hakuna kusimama na hakuna mbunge kuondoka " Wakati huo huo, Waziri wa Afya yuko bungeni na anatoa maelekezo kuwa" Inapotokea mtu kapatikana na Corona case, lazima walioshiriki nae karibu wasakwe wawekwe karantini"!

Kwa case kama hii mfano,inatokea Mbunge ndani ya Bunge kaugua Corona,what next? Je, hapo kwa akili ya kawaida kama Spika,tegemea mpasuko wa Bunge ambao hauna tofauti na ule wa Brexit,kuwa tutoke au tubaki?

Nilitaraji hapa Spika ( kwa hoja na ushauri) aunganishe bunge na Wabunge ili maamuzi ya busara yafanyike! Tukumbuke, Wizara imeshatamka hatua za kuchukua, Spika naye alishatamka hakuna kutoka!

Hili,nasikitika na sina uhakika kilichofanyika kati ya Wabunge ndiyo njoa sahihi ya mshikamano wa Kibunge.

Kauli za utengano zilionekana waziwazi,wengine wakatoka,wengine wakabaki! Hata hivyo,viti vilionekana wazi zaidi kuashiria kuna waliotoka kimyakimya!

Madhara yake tumeyaona:-
1. Spika na KUB kutupiana lawama na maneno yasiyofaa!
2. Wabunge baadhi kufukuzwa uanachama na kuongeza mtafaruku wa Bunge.
3. Kudaiana kirudisha posho ( ambalo ni jambo la aibu kabisa)
4. Huenda hili lisiishie hapo,hata familia za wabunge, wapiga kura, wanachama wa vyama vya wabunge hao, chama chao nk. vikaingia katika mizozo isiyokuwa ya lazima.

Kwa maoni yangu, mambo kama haya yangeweza kuepukika pale tuu awali, ambapo nguvu ya Spika ingetumika ipasavyo kuunganisha bunge na Wabunge kwa ujumla wake bila kujali tofauti ya vyama.
 
..Ndugai anapinga kila hoja au ushauri unaotolewa na wapinzani.

..pia wakati wa mijadala anaruhusu wabunge wa ccm wawatukane wachangiaji wa kambi ya upinzani.

..Spika ajaye anatakiwa asiwe mbunge wa kuchaguliwa. Atafutwe Mtanzania msomi anayeheshimika agombee nafasi hiyo.
 
Tii sheria na kanuni za bunge bila shuruti hicho ndicho kiunganishi ukiambiwa fika kikao cha bunge kama unavyotakiwa usianze kumwambia Spika ohhh Mimi siji kwenda zako naenda ji lock down na Joyce mukya! Ukienda posho urudishe bunge haliwezi gharimia lockdown yako na Joyce mukya
 
Tii sheria na kanuni za bunge bila shuruti hicho ndicho kiunganishi ukiambiwa fika kikao cha bunge kama unavyotakiwa usianze kumwambia Spikav ohhh Mimi siji kwenda zako naenda ji lock down na Joyce mukya
Haya tena! Watetezi wa tabia hii ya Ndugai, ndiyo wa aina yako! Kazi tunayo!
 
Inategemea ni wabunge wa aina gani kwa mfano wabunge wahuni wasiojielewa Kama wa chadema inakuwa ngumu
 
Inategemea ni wabunge wa aina gani kwa mfano wabunge wahuni wasiojielewa Kama wa chadema inakuwa ngumu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu Chopa, hapo ndipo tunapofeli kwa kuangalia ni "Mbunge gani" badala ya kutizama ni "hoja gani". Na hili ndilo Spika wetu anapaswa kuondokana nalo na kulijenga Bunge letu kuwa la umoja zaidi! Hizi hoja mbili kinzani za Spika na Waziri wa Afya ndizo chanjo cha tuliyoyaona na tatakayoendelea kayaona zisipofanyika jitihada nyinginezo!
 
Binafsi pia ninafuatilia sana mabunge mbalimbali duniani hasa Kenya, India, India, USA nk. Shida ya maspika toka Tanzania ni kujivika uccm Zaidi kuliko kuwa kama kiongozi wa wabunge wote. Ndugai ndiye amekuja kuonekana ni dhaifu Zaidi labda pengine kutokana na utawala uliopo madarakani kuonekana kutojali sana mihimili mingine ya dora kiasi kwamba wakuu wa mihimili ya bunge na mahakama wanapokea maagizo tu toka kwa mhimili wa utawala. Bunge hili la 11 ndilo pengine linaonekana kufeli zaidi kutekeleza wajibu wake kutokana na mgawanyiko mkubwa kati ya kambi ya upinzani ni wale wa chama tawala. wabunge wa ccm wao muda wote wanaonekana kusifia tu kile kinachofanywa na serikali. wote sasa ni kuunga mkono tu hata vitu vinavyoonekana vinahitaji mjadala mpana. wapinzani nao sasa wamejikita kukosoa tu kila kitu. Kwa hapa ilitakiwa spika asimame kati na kuleta umoja ndani ya bunge. Badala yake naye kasimama kwenye upande wa wale wanaosifia kila kitu.

Tatizo kubwa linalopelekea haya ni sheria kukipa chama nguvu zaidi ya kumwajibisha mbunge kuliko mpiga kura. Mbunge hana hofu na mpiga kura bali chama maana ndicho kinachoweza kumfuta uanachama na hatimaye akakosa na ubunge. Mpiga kura hana la kumfanya mbunge asiyetekeleza majukumu yake mpaka asubiri uchaguzi mwingine ajaribu kumwajibisha kwenye sanduku la kura ambazo nazo pia sio mwamuzi wa mwisho maana anayetangaza matokeo ndiye mwamuzi wa mwisho kwa mjibu wa hizi siasa zetu. Kwa hali hii unaona hata Ndugai analazimika kufuata maagizo ya chama zaidi kuliko matakwa ya bunge.

Ndugai amejishushia Zaidi heshima yake binafsi na pia kwa bunge hili kutokana na udhaifu mkubwa ulioonekana kwenye chombo hiki. Baadhi ya maoni ya wadau wanasema ni bora tusiwe na mhimili wa bunge tu maana ni kama kitengo cha mhimili wa utawala. Ukisikiliza michango ya wabunge wengi wa ccm dakika zote anazopewa ni kumsifu rais kisha anamponda Mbowe na kuunga mkono kwa asilimia 100. Mbunge anatoka Tunduru, Ileje, Handeni, Kasulu, Rorya, Bahi au Mvomero ambako kote huko changamoto ziko kibao na wananchi wangependa mbunge wao azichambue vizuri na kuzieleza lakini utakuta mbunge husika anavyosifia yalyopo huko utadhani ni kama Tokyo Japan japo nako yapo ya kukosoa. Ni heri anayekosoa kitu kuliko anayesifia kila kitu. Na wapinzani wengi ukiwasikiliza wanakosoa vitu vyenye mantiki (japo sio wote) kuliko vinavyosifiwa na wabunge wa ccm.
 
Hawajaanza kutoka kwa ndugai walianza zamani tangu kwa makinda so job asibebeshwe mzigo
Binafsi pia ninafuatilia sana mabunge mbalimbali duniani hasa Kenya, India, India, USA nk. Shida ya maspika toka Tanzania ni kujivika uccm Zaidi kuliko kuwa kama kiongozi wa wabunge wote. Ndugai ndiye amekuja kuonekana ni dhaifu Zaidi labda pengine kutokana na utawala uliopo madarakani kuonekana kutojali sana mihimili mingine ya dora kiasi kwamba wakuu wa mihimili ya bunge na mahakama wanapokea maagizo tu toka kwa mhimili wa utawala. Bunge hili la 11 ndilo pengine linaonekana kufeli zaidi kutekeleza wajibu wake kutokana na mgawanyiko mkubwa kati ya kambi ya upinzani ni wale wa chama tawala. wabunge wa ccm wao muda wote wanaonekana kusifia tu kile kinachofanywa na serikali. wote sasa ni kuunga mkono tu hata vitu vinavyoonekana vinahitaji mjadala mpana. wapinzani nao sasa wamejikita kukosoa tu kila kitu. Kwa hapa ilitakiwa spika asimame kati na kuleta umoja ndani ya bunge. Badala yake naye kasimama kwenye upande wa wale wanaosifia kila kitu.

Tatizo kubwa linalopelekea haya ni sheria kukipa chama nguvu zaidi ya kumwajibisha mbunge kuliko mpiga kura. Mbunge hana hofu na mpiga kura bali chama maana ndicho kinachoweza kumfuta uanachama na hatimaye akakosa na ubunge. Mpiga kura hana la kumfanya mbunge asiyetekeleza majukumu yake mpaka asubiri uchaguzi mwingine ajaribu kumwajibisha kwenye sanduku la kura ambazo nazo pia sio mwamuzi wa mwisho maana anayetangaza matokeo ndiye mwamuzi wa mwisho kwa mjibu wa hizi siasa zetu. Kwa hali hii unaona hata Ndugai analazimika kufuata maagizo ya chama zaidi kuliko matakwa ya bunge.

Ndugai amejishushia Zaidi heshima yake binafsi na pia kwa bunge hili kutokana na udhaifu mkubwa ulioonekana kwenye chombo hiki. Baadhi ya maoni ya wadau wanasema ni bora tusiwe na mhimili wa bunge tu maana ni kama kitengo cha mhimili wa utawala. Ukisikiliza michango ya wabunge wengi wa ccm dakika zote anazopewa ni kumsifu rais kisha anamponda Mbowe na kuunga mkono kwa asilimia 100. Mbunge anatoka Tunduru, Ileje, Handeni, Kasulu, Rorya, Bahi au Mvomero ambako kote huko changamoto ziko kibao na wananchi wangependa mbunge wao azichambue vizuri na kuzieleza lakini utakuta mbunge husika anavyosifia yalyopo huko utadhani ni kama Tokyo Japan japo nako yapo ya kukosoa. Ni heri anayekosoa kitu kuliko anayesifia kila kitu. Na wapinzani wengi ukiwasikiliza wanakosoa vitu vyenye mantiki (japo sio wote) kuliko vinavyosifiwa na wabunge wa ccm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Chopa, hapo ndipo tunapofeli kwa kuangalia ni "Mbunge gani" badala ya kutizama ni "hoja gani". Na hili ndilo Spika wetu anapaswa kuondokana nalo na kulijenga Bunge letu kuwa la umoja zaidi! Hizi hoja mbili kinzani za Spika na Waziri wa Afya ndizo chanjo cha tuliyoyaona na tatakayoendelea kayaona zisipofanyika jitihada nyinginezo!
Tatizo wabunge wa chadema wao kila kinachofanywa na serikali wanapinga ni kama waliambiwa na mwenyekiti wao pingeni kila kitu kiujumla sio kila mbunge wa upinzani alikuwa ana pinga kila kitu kama Hawa wa Sasa wa chadema unategemea nini Tena hapo? Nadhani ndugai Yuko sawa bila hivyo kusingefanyika lolote bungeni,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo wabunge wa chadema wao kila kinachofanywa na serikali wanapinga ni kama waliambiwa na mwenyekiti wao pingeni kila kitu kiujumla sio kila mbunge wa upinzani alikuwa ana pinga kila kitu kama Hawa wa Sasa wa chadema unategemea nini Tena hapo? Nadhani ndugai Yuko sawa bila hivyo kusingefanyika lolote bungeni,

Sent using Jamii Forums mobile app
Na wabunge wa ccm nao wanasifia kila kitu kinachofanywa na serikali. Je kazi ya mbunge ndiyo hiyo ya kusifia kila kitu? Bunge mfu kabisa hili.
 
Back
Top Bottom