Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,806
- 11,968
Taasisi ya Tiba ya Mifupa Muhimbili (MOI) imeeleza mpango wake wa kuanza kutibu maradhi ya Kifafa kwa kutumia vifaa (Mashine) maalumu ya Upasuaji wa Ubongo na Uti mgongo kwa muda mfupi.
Dkt. Lemeri Mchome ambaye ni Daktari Bingwa wa Upasuaji kutoka MOI amesema kutokana na Mashine hizo zilizowasili nchini, Taasisi hiyo inatarajia kuja na Mpango wa Matibabu kwa wenye maradhi ya Kifafa ambayo yametajwa kuongezeka kutokana na Majeruhi wa ajali hasa za kichwani.
Hayo yamebainika katika mafunzo yanayoendeshwa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha Marekani jijini Dar es Salaam ambapo washiriki ni Madaktari na wauguzi zaidi ya 200 kutoka nchi 14 tofauti.
Akifafanua, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Asha Said Abdullah amesema mafunzo hayo yanategemewa kuongeza ujuzi katika upasuaji wa Mishipa ya Fahamu, Milango ya Fahamu, Ubongo, Vibyongo pamoja na Uti wa Mgongo.
Ameeleza kuwa mafunzo hayo yameenda pamoja na upasuaji kwa wagonjwa wenye matatizo ya Uti wa Mgongo na Ubongo ambapo umefanyika kupitia vifaa vipya hivyo viwili vyenye thamani ya Tsh. Bilioni 2 vilivyoletwa Nchini na Weill Cornell.
“MOI itaweka historia kwa Afrika Mashariki kwa kuwa na vifaa hivyo vya kisasa, tunawashukuru Weill Cornell kwa vifaa na mafunzo wanayofanya.
“Tumepunguza gharama za kuwapeleka wagonjwa wetu nje ya Nchi, kama wangefanyiwa upasuaji Nje ya Nchi kila upasuaji mmoja ungegharimu Tsh. Milioni 25 lakini kwa kuwa wamefanyiwa hapa gharama yake ni takribani Tsh. Milioni 5 kwa mgonjwa,” anasema Dkt. Asha Said Abdullah.
Upande wa Dkt. Khamis Shaban ambaye ni Mratibu wa Ndani wa Mafunzo hayo kutoka MOI ameeleza kuwa mafunzo hayo yanatambulika kimataifa licha ya kufanyika kwa zaidi ya miaka 10.
Aidha, Profesa Rogers Hart wa Weill Cornell amesema “Vifaa vilivyoletwa vitarahisisha sana upasuaji, tulikuwa tunafanya kwa muda mrefu, mfano tulikuwa tunafanya upasuaji mmoja kwa saa tatu, sasa hivi tutakuwa tunafanya kwa saa moja, hapo imeongeza ufanisi.”
Naye, Profesa Rogers Hart wa Weill Cornell amebainisha kuwa “Tunawapa mafunzo kwa ajili ya kufanya upasuaji ambapo wagonjwa hawatakuwa na ulazima wa kwenda Nje ya nchi kwa ajili ya matibabu ya upasuaji.”
Dkt. Lemeri Mchome ambaye ni Daktari Bingwa wa Upasuaji kutoka MOI amesema kutokana na Mashine hizo zilizowasili nchini, Taasisi hiyo inatarajia kuja na Mpango wa Matibabu kwa wenye maradhi ya Kifafa ambayo yametajwa kuongezeka kutokana na Majeruhi wa ajali hasa za kichwani.
Hayo yamebainika katika mafunzo yanayoendeshwa kwa ushirikiano na Chuo Kikuu cha Weill Cornell cha Marekani jijini Dar es Salaam ambapo washiriki ni Madaktari na wauguzi zaidi ya 200 kutoka nchi 14 tofauti.
Akifafanua, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa MOI, Dkt. Asha Said Abdullah amesema mafunzo hayo yanategemewa kuongeza ujuzi katika upasuaji wa Mishipa ya Fahamu, Milango ya Fahamu, Ubongo, Vibyongo pamoja na Uti wa Mgongo.
Ameeleza kuwa mafunzo hayo yameenda pamoja na upasuaji kwa wagonjwa wenye matatizo ya Uti wa Mgongo na Ubongo ambapo umefanyika kupitia vifaa vipya hivyo viwili vyenye thamani ya Tsh. Bilioni 2 vilivyoletwa Nchini na Weill Cornell.
“MOI itaweka historia kwa Afrika Mashariki kwa kuwa na vifaa hivyo vya kisasa, tunawashukuru Weill Cornell kwa vifaa na mafunzo wanayofanya.
“Tumepunguza gharama za kuwapeleka wagonjwa wetu nje ya Nchi, kama wangefanyiwa upasuaji Nje ya Nchi kila upasuaji mmoja ungegharimu Tsh. Milioni 25 lakini kwa kuwa wamefanyiwa hapa gharama yake ni takribani Tsh. Milioni 5 kwa mgonjwa,” anasema Dkt. Asha Said Abdullah.
Upande wa Dkt. Khamis Shaban ambaye ni Mratibu wa Ndani wa Mafunzo hayo kutoka MOI ameeleza kuwa mafunzo hayo yanatambulika kimataifa licha ya kufanyika kwa zaidi ya miaka 10.
Aidha, Profesa Rogers Hart wa Weill Cornell amesema “Vifaa vilivyoletwa vitarahisisha sana upasuaji, tulikuwa tunafanya kwa muda mrefu, mfano tulikuwa tunafanya upasuaji mmoja kwa saa tatu, sasa hivi tutakuwa tunafanya kwa saa moja, hapo imeongeza ufanisi.”
Naye, Profesa Rogers Hart wa Weill Cornell amebainisha kuwa “Tunawapa mafunzo kwa ajili ya kufanya upasuaji ambapo wagonjwa hawatakuwa na ulazima wa kwenda Nje ya nchi kwa ajili ya matibabu ya upasuaji.”