Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,646
Mkuu lengo lako hasa ni kupotosha? Anza na mtiririko huu ndipo utamwelewa Paulo alivyoandika..
1 Basi Myahudi ana ziada
gani? Na kutahiriwa kwafaa
nini?
2 Kwafaa sana kwa kila njia.
Kwanza kwa kuwa
wamekabidhiwa mausia ya
Mungu.
3 Ni nini, basi, ikiwa baadhi
yao hawakuamini? Je!
Kutokuamini kwao kutaubatili
uaminifu wa Mungu?
4 Hasha! Mungu aonekane
kuwa amini na kila mtu
mwongo; kama ilivyoandikwa,
Ili ujulike kuwa una haki katika
maneno yako, Ukashinde
uingiapo katika hukumu.
5 Lakini, ikiwa udhalimu wetu
waithibitisha haki ya Mungu,
tuseme nini? Je! Mungu ni
dhalimu aletaye ghadhabu?
(Nasema kwa jinsi ya
kibinadamu.)
6 Hasha! Kwa maana hapo
Mungu atawezaje kuuhukumu
ulimwengu?
7 Lakini, ikiwa kweli ya Mungu
imezidi kudhihirisha utukufu
wake kwa sababu ya uongo
wangu, mbona mimi ningali
nahukumiwa kuwa ni mwenye
dhambi?
8 Kwa nini tusiseme (kama
tulivyosingiziwa, na kama
wengine wanavyokaza kusema
ya kwamba twasema hivyo),
Na tufanye mabaya, ili yaje
mema? Ambao kuhukumiwa
kwao kuna haki.
Nilisema....... Watu wanaiona aya lakini wanajifanya hamnazo. Hivi wewe huoni kuwa kumbe utukufu wa Mungu umejidhihirisha kwa uongo wa mtu? Yaani mtu anaongopa kuhusu Mungu!!!!