zamani1116
Member
- Oct 24, 2017
- 25
- 6
Uislamu hauko hivi...usiwe unaongea maneno ya kusikia vijiweni fuatilia ukweli ,ukweli utakufanya uwe na mawazo chanya....Bora trump awapige vita tu... mtu anajilipua ili aue watu ni mtu wa kukaa nae kweli?
Uislamu hauko hivi...usiwe unaongea maneno ya kusikia vijiweni fuatilia ukweli ,ukweli utakufanya uwe na mawazo chanya....Bora trump awapige vita tu... mtu anajilipua ili aue watu ni mtu wa kukaa nae kweli?
Fred...Kiukweli mi kwenye suala la dini sipendi kuchangia sana kwa sababu kila mtu atazungumzia dini yake na wengine kuponda dini ya mwenzake.
Ila napenda kuwa muwazi kuwa marekani haipendi kabisa dini ya kiislam kwa sababu zao na inataka sana support ya nchi nyingi.
Vile vile waislam na waarab hawawapendi wamarekani kwa sababu ya kutengwa na kushutumiwa hasa katika misimamo yao ya kidini.
Mi nadhani chimbuko la uhasama huu ni kwa sababu mmarekani anataka kutawala dunia, kujiweka kuwa yeye ni polisi wa dunia, kukandamiza nchi za kiarabu ili ziwe chini yake na kuweza ku-explore vizuri mafuta.
Na kwa kuwa mafuta ndo yanaifanya nchi za kiarabu kuwa na maendeleo, hata hela yake kuwa juu zaidi ya dollar, basi hapo ndo vita ya biashara,kiuchumi na kimaendeleo huanzia hapo na ndo chanzo cha nchi za kiarabu kuwekewa masharti na marekani au kushambuliwa ili zisinyanyuke kuizidi marekani na ndo vita vya mara kwa mara na kunyang'anywa mafuta na kudhoofishwa.
Ila kwa kuwa jamii ya kiislam huwa na hasira za haraka na kuwa aggressive ukizungumzia dini au jambo lolote la dini, na hata wao kwa wao kugombana kisa kushutumiana jambo pasipo kufanyia research au kuwa na subira, hapo ndo marekani anapochezea karata yake na bila ajizi marekani anafanikiwa sana kwa hilo. Kumbuka kuwa vita vyote hivi tunavyoshuhudia, basi niliyoyaeleza hapo juu tactic hyo hutumika.
Pia ikumbukwe kuwa marekani nayo hutumia kufunika history ya viongozi wa kiislam, basi hapo ndo utashangaa kuona wasomi wa kiislam nao hawataki historia hizo zipotezwe na sababu hiyo ndo ndugu yangu hapa mohamed said anaitetea sana kila sehemu.
Nahitimisha kwa kusema kuwa nawaasa ndugu zangu waislam, historia iliyopita haina nafasi katika ulimwengu huu wa science na technology. Hebu fanyeni km libya, ambapo kiongozi wao alietolewa madarakani, hakuangalia na kukazania historia bali aliweza kujenga shule nyingi, kusomesha wananchi wake wengi na hivyo watu hao kuishi vizuri,kuendeleza nchi, huku wakiwa wamesoma.
Ningependa tushindane kuhusu dini zetu kwa maendeleo. Wakristo waliachiwa sana properties nyingi na wamisionari kama vile nyumba, shule, makanisa, mahospital na vitega uchumi kibao.
Tuachane na mashindano ya kusaka historia maana kipindi hiki ni cha technolojia, anzisheni shule nyingi, vitega uchumi vingi, shule nyingi, somesheni watoto wenu wengi sana, mjenge na sehemu nyingi sana za ibada. Changisheni hata hela sehemu za ibada kama wakristo ili mshindane kwa maendeleo na si kwa historia huku elimu mkiwa nyuma sana.
Na mtaeleweka na mtaonekana kuwa mna busara, kuliko baadhi yenu kushika bunduki, kujitoa mhanga, mabishano ya siasa na mengineyo yasiyo na tija.
Ila hongera mkuu kwa kazi nzuri unayoifanya japokuwa marekani walikutafsiri kivingine. Suala la kila siku kuwa na negative thinking kuwa mnaonewa, toeni vichwani mwenu maana mtashindwa kupata maendeleo wakati wengine wakiendelea kuwazidi, najua kwa hilo mtaendelea na kuwazidi hata wazungu.
Mwaipungu,Inshaallah Allah akuepushe na fitina. Uisalamu nikusema kwl hata ukichukiwa Allah atakulinda inshallah.
Its absolutely true that Tanzanian history has been cooked by some few mad people but the true history still lies in minds of a few intellects. Muslims played 90% to to independence of Tanzania of today and if it wasn't them, then I think it would have come later than 1961. Just to shade in some light I wish people ask themselves where did this freedom fighter we hear today come from? What is his history? Its just fragments of his history but the truth still lies out there. Anyway I wish people dig up the history of TAA, they would just know how cooked history is today.Mwaipungu,
Nilikuwa nawashangaza walimu wangu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam
walipokuwa wanasomesha historia ya utaifa wa Tanganyika.
Nilikuwa nawaeleza mambo wenyewe wanashangaa na nikiwaambia kuwa
ikiwa wanataka kusomesha uongo na waendelee lakini mimi haya majina
ninayowapa ndiyo wazalendo waliomtia Mwalimu Nyerere katika siasa za
kudai uhuru Dar es Salaam na huko majimboni.
Nikawa nawaeleza pia yote yaliyotokea baada ya uhuru kupatikana mwaka
wa 1961 na kuwapa fikra zangu kwa nini wao leo wanasomesha historia siyo.
Nilikuwa nalichangamsha sana darasa na walimu walinipenda.
Mwaipungu,
Nilikuwa nawashangaza walimu wangu Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam
walipokuwa wanasomesha historia ya utaifa wa Tanganyika.
Nilikuwa nawaeleza mambo wenyewe wanashangaa na nikiwaambia kuwa
ikiwa wanataka kusomesha uongo na waendelee lakini mimi haya majina
ninayowapa ndiyo wazalendo waliomtia Mwalimu Nyerere katika siasa za
kudai uhuru Dar es Salaam na huko majimboni.
Nikawa nawaeleza pia yote yaliyotokea baada ya uhuru kupatikana mwaka
wa 1961 na kuwapa fikra zangu kwa nini wao leo wanasomesha historia siyo.
Nilikuwa nalichangamsha sana darasa na walimu walinipenda.
Dah umeongea vizuri sanaTuthibitishie kuwa waliokukamata ni wakristo,naona mmejengewa misingi ya chuki,na kulalamika ndo maana kila kitu mtakitazama kwenye misingi ya dini,Leo hii waislamu wanazikimbia nchi zao sababu ya chuki za kuuwana waislamu Kwa waislamu wanakimbilia kwenye nchi za makafiri wakaonyeshwe Upendo, kwann wasiende kwenye nchi za waislamu wenzao? Imetoka list ya Wauza unga majina mengi ni waislamu rejea gazetini mtasema sasa wanaondamwa ni waislamu? Hapana msisingizie dini panapo maovu kujifichia kupata popularity km alivofanya Osama na Makundi ya kigaidi. Me ni mkristo kabla sijasoma habari za uchunguxi niliamini ugaidi na uislamu ni kitu kimoja baada ya kuujua ukweli, kumbe uislamu hauna uusiano na ugaidi, dhana ya ugaidi imeingizwa na Freemasons ktk uislamu rejea history ya ugaidi ulianza lini, nani waanzilishi, na nn ajenda yake kuelekea new world order,soma history ya mapinduzi ya Irani,soma kuhusu vita vya msalaba nk.lengo la ugaidi kwanza ni kuusambaratisha uislamu, kupata mafuta Kwa mabadilishano ya silaha, kuifanya middle east isitulie Kwa usalama wa Israel,na kujipatia himaya ya kidunia Kwa kujifichia kwenye dini, na wenye kujua ajenda kuu ya ugaidi ni viongozi wakuu wa Makundi hayo na si wapiganaji wao hawaelewi chochote wameaminishwa wanapigania dini.Sababu ukitaka waislamu wachinjane waaminishe wanapigania dini,kumbe wapo kutimiza matakwa ya Freemasons toka magharibi. Shida kubwa ya waislamu wengi wameshajijengea dhana ya tunaonewa,tunadhulumiwa ukimgusa muislam hata Kwa mambo nje ya dini anakimbilia kwenye dini tunaonewa sababu tu waislamu. Ukiwaambia mnaonewa nn hawajui inakuwa sawa na wimbo wa taifa Kwa kila moja.Cha msingi ondoeni ile dhana tunaonewa,tunachukiwa nk sababu hakuna MTU ashawahi zuiwa fanya yake ya halali Kwa kufuata sheria sababu ya dini yake.
Chizcom,ogopa halama hzi * alafu #
kwa nini * ina simama mfano:umejaribu kutafuta jamii ikuelewe kwa mda mrefu.
# ina simama mfano:kutokana na jamii kuto kuelewa umbaki kwa nini mimi.
zama iliyo kwa ndugu zetu waislamu wana # inayo wasumbua kuona kila jambo wao wanakandamizwa kutokana na wakristo.
mfano:mkoloni mwarabu alipo kuja hapa hakuja kwa misingi ya kufungua shure ndo maana shule zote tanganyika ni mishionari na wakoloni wajerumani na waingereza.kikubwa zaidi mwarabu tunacho shukuru kueneza dini na biashara zake.zama iliyo jengwa na mwarabu ndiyo ilipelekea hata babu zetu wanatuambia kipndi icho shule za kikoloni ndizo zilikuwa zimeletwa na wamisionari na wajerumani,wingereza wao waliona kuwa zimekuja kuwabadilisha dini na kuzuia watoto kusoma .ndo maana miaka ya nyuma na kidogo unakuta wasomi ni wengi wakristo si kwa udini kama nilivo toka kukuelezea nyuma hapo.
sitaki kufikia dini yoyote kwa lengo la kuchafua.# hii ndiyo iliyobaki kwa waislamu wengi kuona kama walionewa na kupandikiza chuki kwa watu wengi,na hata ukienda kwenye miazara mingi,# ndiyo inapandikizwa sana.
ni jukumu la waislamu kuelewa wapi palipo fanya kuonekana #.ndio maana unaona waislamu wengi nao wanajikita kwenye elimu siyo kama hile historia kwa ufupi niliyo kuwa nayo tu.
wote wamoja tujue nchi yetu si kutengana kwa rangi.
Mwaipungu,Its absolutely true that Tanzanian history has been cooked by some few mad people but the true history still lies in minds of a few intellects. Muslims played 90% to to independence of Tanzania of today and if it wasn't them, then I think it would have come later than 1961. Just to shade in some light I wish people ask themselves where did this freedom fighter we hear today come from? What is his history? Its just fragments of his history but the truth still lies out there. Anyway I wish people dig up the history of TAA, they would just know how cooked history is today.
Sherrif...Ina maana hata akina Max Mmuya na Mohammed Bakari walikuwa wakipindisha ukweli?
Mkuu kwa kweli umefanya jambo kuu la tarehe hii ya leo 9 desemba. Natamani kila mtu ajaribu kusoma hii historia.Mwaipungu,
Tunaweza kuangalia hapa kwani jicho halisahau kile jicho la camera liliona:
UHURU DAY: TUWAKUMBUKE MASHUJAA WA UHURU WA TANGANYIKA
Selemani Mamba
Shujaa wa Maji Maji
Sultan Abdulrauf Songea Mbano wa Songea
Shujaa wa Maji Maji
Kushoto aliyesimama ni Ally Kleist Sykes, na kulia kwake ni
Abdulwahid Kleist Sykes, mbele kushoto ni Kleist Sykes
Mbuwane na Abbas Kleist Sykes. Katika hawa aliye hai ni Abbas.
Ukoo huu umeacha kumbukumbu nyingi kwa maandishi katika harakati za
kuunda African Association 1929 na kuunda TANU 1954. Picha hii imepigwa
mwaka wa 1942 Abdul aliporudi Dar es Salaam kutoka Lower Kabete Kenya
alipokuwa akipata mafunzo ya kijeshi katika King's African Rifles kabla
hajakwenda Burma kujiunga na Burma Infantry. Angalia utaona Abdul amevaa
sare ya Jeshi la Mfalme wa Uingereza. Ilikuwa akiwa Burma Vita Vya Pili Vya Dunia
(1938 - 1945) ndipo alipoamua kuwa 6th Battalion iliyokuwa na askari kutoka
Tanganyika waunde TANU wakirudi Tanganyika kudai uhuru.
Ufunguzi wa Jengo la African Asociation 1933 jengo lililojengwa na uongozi wa
Kleist Sykes kati ya 1929 - 1933 na hapa ndipo ilipoundwa TANU 1954 wanae
wawili Abdul na Ally wakiwa waasisi wa chama hicho.
Waasisi wa TANU 1954
Baraza la Wazee wa TANU chini ya Mwenyekiti wake Sheikh Suleiman Takadir 1955
Hamza Kibwana Mwapachu 1913 - 1062
Kushoto: Dossa Aziz, Julius Nyerere, Abdulwahid Sykes na Lawi Sijaona
katika dhifa ya kumuaga Nyerere safari ya pili UNO 1957
Kushoto: Bi. Tatu bint Mzee, wa tatu Julius Kambaraga Nyerere
wa tano Bi. Titi Mohamed wanamsindikiza Mwalimu Nyerere
Uwanja wa Ndege safari ya UNO 1955
Kulia: Bi. Titi Mohamed, Clement Mohamed Mtamila, Sheikh Suleiman Takadir, Julius Nyerere
Nyuma kulia: John Rupia, Rajab Diwani na Mama Maria Nyerere
nime furahi sana kunielewesha itabidi nikutafute tufanikishe historia na kutafuta ukweliChizcom,
Tatizo ni kuwa huifahamu historia ya Pwani ya Afrika ya Mashariki na Waarabu.
Waarabu hawakuchukua koloni lolote.
Waislam ndiyo watu wa kwanza kuweka msingi wa elimu hizi sehemu zetu kupitia
madras na ndiyo walikuwakuwa wanajua zle 3Rs yaani Reading, Writing and Arithmetic.
Ishumi kalieleza hili vizuri bahati mbaya nimesahau ''paper'' yake na mwaka.
Lakini Waislam baada ya uhuru walifanya juhudi za elimu na walianza kujenga shule na
waliweka hadi jiwe la Chuo Kikuu kupitia East African Muslim Welfare Society (EAMWS).
EAMWS ina historia yake pekee na nimeieleza katika Sehemu ya Tatu ya kitabu cha Abdul
Sykes na ni historia iliyojaa simanzi.
Hutoweza kujadili historia ya Uislam na Waislam Tanzania bila kusoma historia hii ya EAMWS
na vipi ilikuja kupigwa marufuku na serikali mwaka wa 1968 na serikali ikawaundia Waislam
BAKWATA.
Huu ndiyo ikawa mwisho wa juhudi za Waislam katika kujenga shule na mradi wa Chuo Kikuu
ukafa.
Mambo yalianza wakati sasa narudi Dar es Salaam na ndege ya Emirates iliyokuwa inatua usiku. Inaelekea maofisa wa pasi pale uwanjani walikuwa na taarifa zangu mapema na walikuwa wakinisubiri kwa hamu kubwa kwani nilipotoa pasi yangu kwa afisa wa pasi hapo ndipo shughuli za kunishughulikia zilipoaanza.
Mimi sikuwa na hili wala lile. Nikawa namuona yule dada aliyekuwa kwenye kile kizimba akikukurika na pasi yangu akiitia katika mashine na kuitoa mara kadhaa. Fikra iliyonijia kwa haraka ilikuwa mashine ni mbovu na harakati zile zilikuwa ni kurekebisha mitambo.
Kumbe sivyo wahusika nadhani walikuwa wanahakikisha kuwa mimi ndiyo huyo waliokuwa wakimwinda na kumsubiri na sasa kapatikana, kaingia mwenyewe kwenye mtego na kanasa. Yule afisa wa pasi akanambia nikae pembeni natakiwa kwa mahojiano na watu wa usalama.
Hofu haikuwa imeniingia kwa kuwa nilikuwa natambua kuwa harakati dhidi ya ugaidi zilikuwa zimepamba moto na labda nilitakiwa kwa mahojiano mafupi kutaka kujua nyendo zangu. Sikujua wala kutarajia kuwa mshtuko mkubwa ulikuwa unanisubiri.
Nilichukuliwa hadi kwenye chumba kimoja na hapo niliwakuta maofisa wa usalama watatu wakanikaribisha kwa taadhima kisha wakanambia kuwa niko chini ya ulinzi kwa kuwa zimewafikia taarifa zangu kuwa mimi nasafirisha mihadarati. Mpaka hapa sikuwa na hofu bado ilinijia picha kuwa yawezekana wamefananisha majina.
Niliwaambia huenda Mohamed Said muuza madawa ya kulevya siyo mimi niliye mbele yao. Wakaniambia kwa kujiamini kabisa kuwa taarifa zao ni madhubuti muuza unga ni mimi na wamekuwa wakinifuatilia siku nyingi. Hapo ndipo walipotoa pasi yangu na kuniomba niitambue kama hiyo pasi ni yangu au la. Niliwajibu kuwa hakika hiyo ndiyo pasi yangu khasa.
Wakaniamuru sasa tutoke twende nikachukue mizigo yangu ili wafanye upekuzi wa mihadarati katika mizigo niliyotokanayo Tehran. Hapo ndipo nilipojuwa kuwa niko katika lindi kubwa la matatizo na ubongo wangu ukaanza kufanya kazi kwa haraka huku nikisoma dua kumuomba Allah ulinzi wake kwani kwa hakika nilijua kama ni njama zimekamilika na leo imefika siku yangu.
Nikajiuliza itakuwaje watakapotoa madawa kwenye mizigo yangu. Nikaanza kufikiri vichwa vya habari vya magazeti yatakavyopambwa na habari zangu. Ikanijia yakini kuwa watu wa usalama wameniwekea madawa ya kulevya katika mizigo yangu ili waniangamize na maadui zangu wapumzike na shari yangu.
Nilimgeukia yule ofisa mkuu aliyekuwa ananihoji nikamwambia kuwa sitokubali kugusa mizigo yangu bila kuwapo mashahidi isijekuwa mizigo yangu ishawekewa hayo madawa ya kulevya kwani nilikotoka Tehran mizigo ilikuwa imekaguliwa na ilikuwa salama.
Hoja yangu kubwa kwao ilikuwa kupata uhakika kutoka kwao kuwa wananijua vizuri kiasi cha kuthibitisha kuwa kweli mie ni msafirishaji wa madawa ya kulevya. Jibu nililopewa ni kuwa wao wanafanya kazi kutokana na taarifa zilizowafikia. Wakasema, “Sisi tunazo taarifa zako kamili kuwa wewe ni msafirisha madawa ya kulevya.”
Nikawauliza,“Baada ya kupata taarifa hizo zangu nyie mmechunguza kutafuta ukweli?” Wakasema, “Ndiyo maana leo tumekukamata.” Nikawaambia, “Si kweli kama kwa sababu mie nafahamika Dar es Salaam takriban kwingi maana ndio nilikozaliwa na kukulia. Hapo Kariakoo ukiwaambia watu kuwa Mohamed ni “Mzungu wa Unga” kila mtu atacheka maana huo kwao ndugu zangu ni mzaha mbaya.”
Walitaka kujua nilkwenda kufanya nini Iran. Niliwaambia nilialikwa na serikali ya huko kuhudhuria mkutano. Wakataka kujua vipi nilipata mwaliko. Nikawajibu kuwa hilo swali sina jibu labda waiulize serikali ya Iran. Nikawaeleza kuwa mbona siku zote napita hapo uwanjani nikenda sehemu tofauti duniani kwa mialiko na kutoa mada sijakamatwa kimezidi nini katika hii safari ya Iran?
Niliwaeleza kuwa miezi michache iliyopita nilikuwa Chuo Kikuu Cha Ibadan kwa mwaliko tena mkutano umefadhiliwa na serikali ya Marekani na wamenipa na tiketi toka Dar es Salaam hadi Lagos na kuniweka hoteli na kunilipa fedha.
“Mbona hamkunikamata wakati ule?” Nikafungua mlango mwingine nikawaambia, “Nakuapieni nyie msingethubutu kumkamata Mkristo anaetoka Vatican mkutanoni. Lakini kwa kuwa mie ni Muislam sina wa kunitetea. Nchi hii nani atakuuliza kwa kumnyanyasa Muislam?” Walishtuka na wakawa wanyonge sana wakasema si kweli kuwa naponzwa na dini yangu.
Baada ya kukurukakara nyingi na mabishano makubwa kuhusu mie kukubali kufanyiwa upekuzi wa mizigo yangu alikuja binti mmoja katika wao na yeye akanihakikishia kuwa wao ni serikali na sio wahuni. Hawathubutu kuniwekea dawa katika mizigo yangu hivyo akanisihi sana kwa upole nikubali ili wajitoe wasiwasi na wataniachia endapo hakuna kitu.
Niliomba apatikane shahidi wa kushuhudia mizigo yangu kabla ya kufanyiwa upekuzi lakini hakuna mtu aliyekubali kuchukua dhima ile katika maofisa waliokuwa kazini pale uwanja wa ndege usiku ule. Upekuzi ukafanyika hadi mwilini. Hakuna kitu. Wakanipela katika choo maalum cha kutolea madawa kwa njia ya haja kubwa.
Nikakataa kujisaidia pale. Ilikuwa ndio mara yangu ya kwanza kuona choo kama kile. Choo chenyewe ni cha aluminium. Tofauti na vyoo vya pale ambavyo siku zote ni vichafu, hiki kilikuwa kisafi sana kiasi mtu unaweza hata kutengewa chakula na akala bila ya kuhisi kinyaa.
Nilitegemea wataweka ahadi yao kuwa ikiwa hawatakuta madawa ya kulevya katika mizigo yangu watanirejeshea uhuru wangu wataniachia niende nyumbani. Haikuwa hivyo. Wakanirudisha ofisini kwao. Sasa wakaacha madawa ya kulevya wakahamia katika vitabu na “audio cassette” nilizokuwa nimepewa kama zawadi kule Tehran wakaniluliza kwa nini naingiza vitu vile khasa kanda za Khomeni na vitabu vyake nchini. Nikawauliza, “Kwani kanda na vitabu vya Khomeni haviruhusiwi kuingizwa Tanzania?
Likandamwasada,WATU WADINI KAMA NINYI MNYONGWE TU, YANI UNAKAMATWA UNASEMA KWA 7BU NI MUISLAMU
Chizcom,nime furahi sana kunielewesha itabidi nikutafute tufanikishe historia na kutafuta ukweli
Sherrif...Kwa mtaji huu naona kuna mengi sana yamechujwa katika historia Ya taifa hili
Motive ni ipi?
Sherrif...
Baada ya kupatikana uhuru kulifanyika Muslim Congress mbili mwaka wa 1962 na 1963
na Waislam chini ya East African Muslim Welfare Society (EAMWS) wakaja na mpango
wa elimu kwa vijana wa Kiislam kwani ukoloni uliwakandamiza sana Waislam katika elimu.
Kiongozi wa mipango hii alikuwa Mufti Sheikh Hassan bin Amir na Tewa Said Tewa.
Hakuna ambae hakutambua nguvu ya Waislam katika kupambana na ukoloni.
Hii ilitia hofu serikali iliyokuwa madarakani.
Matokeo yake ni kuvunjwa kwa EAMWS na kuundwa BAKWATA bila ridhaa ya Waislam
na Sheikh Hassan bin Amir akafukuzwa nchini na kurudishwa kwao Zanzibar.
Historia hii ikawa inaogopwa hadi leo na laiti kama si kwa Allah kunipa taufiq ya kuiandika
historia hii katika kitabu cha Abdul Sykes historia hii isingekuja kujulikana.
Wewe msukununu, jenga uislamu achana na ukatoliki.