Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,787
- 30,083
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Utaitaja vipi Historia ya Tanganyika / Tanzania bila kuwataja Waislam? Au huelewi kuwa wao ndio walioanzisha harakati za Uhuru?Jamii Forums thread za huyu mwanazuoni mnaziweka mahali si pake hizi ziwekwe katika Forums za dini. Hapa hatuletewi historia bali tunaambiwa masuala ya elimu ahera.
Sijaona hata thread moja ya huyu nguli inayowahusu watu ambao hawakuwa na dini ama wakristu hata mabaniani anaowasemea mazuri japo wamesahaulika pia na historia ya nchi yetu.
Sijajua kama kweli research anayoifanya ni ya kutaka kujua tulipataje uhuru ama kukuza dhana ya tunaonewa. Ijulikane yeye kasomeshwa katika wakati na kipindi cha huyo anayemnanga.
Ndiyo maana ninaona JF inamkosea haki kuacha thread za huyu nguli katika masuala ya historia za waislamu kuwekwa katika forum ya historia.
Mkuu habari za siku?Utaitaja vipi Historia ya Tanganyika / Tanzania bila kuwataja Waislam? Au huelewi kuwa wao ndio walioanzisha harakati za Uhuru?
Naona unasumbuka sana unapoona Waislam wakitajwa katika historia ya ukweli. Pole sana, ukweli utabaki kuwa ukweli daima.
Walianzishaje, hebu tuongezee ufahamu kidogo!!Au huelewi kuwa wao ndio walioanzisha harakati za Uhuru
Nimesoma kitabu chako "maisha na wakati wa Abdulwahid Sykes" mara mbili na ninakupongeza mno kwa muda uliotumia kusoma,kutafiti na kuandika kitabu.Kwa kweli bila kusoma,kusafiri,kuchambua huwezi kuandika kitabu kama kile.Kuna mtu hapa JF kaniuliza kwa nini kila ninapoandika historia ya TANU lazima nimtaje Abdul Sykes...jibu nilimpa lakini nampa na nyongeza hapo juu...
Mignon ahsante sana. Mie huwauliza wanaokimbilia hoja ya udini kuwa kwani wale wanajopo wa Chuo Cha Kivukoni walipomwondoa Abdulwahid Sykes na wazalendo wengine katika historia ya TANU walifanya hivyo kwa kuogopa kuwa wakimtaja historia itakuwa ya udini?Nimesoma kitabu chako "maisha na wakati wa Abdulwahid Sykes" mara mbili na ninakupongeza mno kwa muda uliotumia kusoma,kutafiti na kuandika kitabu.Kwa kweli bila kusoma,kusafiri,kuchambua huwezi kuandika kitabu kama kile.
Kuna hoja ya udini inaibuliwa mara nyingi lakini haya ni mawazo ya wasomaji yasikuyumbishe.
Natamani ningeweza kusoam na kuandika kama wewe.
Najua ilivyo ngum.Nilifika Mikindani nami ni mpenzi wa mambo ya zamani,nahisi yananiongezea imani.Kwa mfano unakuta nyumba ambayo ilikuwa ya tajiri wa kununua binadamu (sio ng'ombe)lakini leo hayupo!!Mikindani nilionyeshwa gofu ambalo lilikuwa nyumba na ndipo Mwalimu Nyerere alifikia wakati akitafuta Uhuru.Mwenye nyumba hakuogopa utawala wa Mkoloni kumkarimu mgeni huyu.Leo ukimtaja mwenyeji huyo kuwa alikuwa Mwislamu,tayari watu washalipuka.Mignon ahsante sana. Mie huwauliza wanaokumbulia hoja ya udini kuwa kwani wale wanajopo wa Chuo Cha Kivukoni walipomwondoa Abdulwahid Sykes na wazalendo wengine katika historia ya TANU walifanya hivyo kwa kuogopa kuwa wakimtaja historia itakuwa ya udini?
Well said Mkuu coz kuna watu ukitaja Uislam katika harakati za kupigania uhuru huwa wanachukia sana while Waislam ndo nguzo kubwa mpaka uhuru unapatikana. Litakuwa hivyo na litaendelea kuwa hivyo hata kama litapuuzwa.Utaitaja vipi Historia ya Tanganyika / Tanzania bila kuwataja Waislam? Au huelewi kuwa wao ndio walioanzisha harakati za Uhuru?
Naona unasumbuka sana unapoona Waislam wakitajwa katika historia ya ukweli. Pole sana, ukweli utabaki kuwa ukweli daima.
Mkuu Mbase, maadam Maalim Mohammed Said ni Muislamu, ana haki zote kusimulia mchango wa babu zake katika harakati za uhuru.Jamii Forums thread za huyu mwanazuoni mnaziweka mahali si pake hizi ziwekwe katika Forums za dini. Hapa hatuletewi historia bali tunaambiwa masuala ya elimu ahera.
Sijaona hata thread moja ya huyu nguli inayowahusu watu ambao hawakuwa na dini ama wakristu hata mabaniani anaowasemea mazuri japo wamesahaulika pia na historia ya nchi yetu.
Sijajua kama kweli research anayoifanya ni ya kutaka kujua tulipataje uhuru ama kukuza dhana ya tunaonewa. Ijulikane yeye kasomeshwa katika wakati na kipindi cha huyo anayemnanga.
Ndiyo maana ninaona JF inamkosea haki kuacha thread za huyu nguli katika masuala ya historia za waislamu kuwekwa katika forum ya historia.
Hahahaaa yan Wewe ndo wale Ukiskia waislam Unaumiia Lkn Tafuta hotuba ya Nyerere alipohadthia Aliepelekwa Bagamoyo na Akafunga mpk jioni... Hivi unajua kwann alifunga kwann Alisomewa Dua?.. Kwasbb Waislamu walilichukua jambo la Uhuru kama lao Wkaat huo wakristo walikuwa pamoja na ukoloni... Huwez kuwatoa waislam ktk harakat kwasbb ndo walkuwa FrontJamii Forums thread za huyu mwanazuoni mnaziweka mahali si pake hizi ziwekwe katika Forums za dini. Hapa hatuletewi historia bali tunaambiwa masuala ya elimu ahera.
Sijaona hata thread moja ya huyu nguli inayowahusu watu ambao hawakuwa na dini ama wakristu hata mabaniani anaowasemea mazuri japo wamesahaulika pia na historia ya nchi yetu.
Sijajua kama kweli research anayoifanya ni ya kutaka kujua tulipataje uhuru ama kukuza dhana ya tunaonewa. Ijulikane yeye kasomeshwa katika wakati na kipindi cha huyo anayemnanga.
Ndiyo maana ninaona JF inamkosea haki kuacha thread za huyu nguli katika masuala ya historia za waislamu kuwekwa katika forum ya historia.
Walianzishaje, hebu tuongezee ufahamu kidogo!!
Britannica,
Post nzima haikukaa vyema kuanzia kichwa cha habari.
Historia ya TANU huwezi kuiandika kwa mistari miwili.
Historia ya TANU inaanza na African Association mengi
yalipita hadi kufikia kuasisiwa TANU mwaka wa 1954.
Hiyo picha hapo juu inatka katika Nyaraka za Sykes na
mimi ndiye niliyeitia mtandaoni ili watu waione na wasome
historia ya TANU.
Naweka hapo chini niliyoandika katika kitabu cha Abdul
Sykes kuhusu kadi za TANU:
''Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake. Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika. Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion. Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie. Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000. Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa. Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama. Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo. Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7. Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Tosiri kadi nambari 25.''
''Mtemvu alimuelezea Ally kwa ufupi juu ya mkutano wao na Nyerere Morogoro mjini na aliomba apewe mara moja kadi 200 za TANU. Ally aliwaandikia na kuwapa kadi za uanachama wa TANU, Mtemvu na Tambwe na akamwambia mdogo wake Abbas, awaalike wote wawili kwenye mkutano wa uzinduzi wa tawi la TANU la Dar es Salaam ambao ulikuwa ufanyike Jumamosi iliyofuata. Uongozi wa TANU ulipokuwa ukijitayarisha kwa mkutano wa uzinduzi, Ally Sykes alikuwa tayari amekabidhiwa barua ya uhamisho kutoka Dar es Salaam kwenda Korogwe. Kwa hakika hasa, Ally alipewa barua hiyo wiki mbili tu baada ya kuundwa kwa TANU. Hii ilikuwa mara ya pili Ally kupewa uhamisho kama adhabu yake ya kupambana na utawala wa kikoloni.''
''Familia yangu ilifahamiana na Dome Budohi, mmoja wa wanaharakati kutoka Kenya. Wakati ule wakati wa kudai uhuru wa Tanganyika alikuwa akiishi Dar es Salaam. Budohi alikuwa mmoja wa wazalendo walioasisi TANU na kadi yake ya uanachama ni nambari 6 aliyopewa Julai 1954.''
''Mwezi June, makao makuu ya TAA yalitangaza kamati yake ya utendaji: J. K. Nyerere, Rais, Abdulwahid Sykes, Makamu wa Rais; J. P. Kasella Bantu, Katibu Mkuu; Alexander M. Tobias na Waziri Dossa Aziz, Katibu wa pamoja wa muhtasari; Wajumbe wa kamati: Dr Michael Lugazia, Hamisi Diwani, Tewa Said Tewa, Denis Phombeah, Z. James, Dome Okochi, C. Ongalo na Patrick Aoko.''
Hii ndiyo historia ya TAA 1953 kuelekea TANU 1954.
Nadhani suala la kadi sasa limeeleweka pamoja na
historia ya TANU.
Mimi siyo waislamu tu wite wafia dini Nina matatizo nao. Kama umenielewa sijakosoa alichokiandika Bali ni jamvi la siasa na dini wapi na wapi? Mimi ni mtu nisiyeamini dini kwangu dini ni utapeli wa wajanja kuwafanya wengine kuwa watumwa kwa kuwaaminisha uongo. Haiji akilini mwangu Kama kweli waliotuletea dini wanaamini Mungu yupo. Historian inatuonyesha tofauti.Hahahaaa yan Wewe ndo wale Ukiskia waislam Unaumiia Lkn Tafuta hotuba ya Nyerere alipohadthia Aliepelekwa Bagamoyo na Akafunga mpk jioni... Hivi unajua kwann alifunga kwann Alisomewa Dua?.. Kwasbb Waislamu walilichukua jambo la Uhuru kama lao Wkaat huo wakristo walikuwa pamoja na ukoloni... Huwez kuwatoa waislam ktk harakat kwasbb ndo walkuwa Front
Mayalla mbona unanibatiza ukristo bill kuniuliza? Mimi sijajaliwa kutapeliwa Kama wewe kwenye dini namala.Mkuu Mbase, maadam Maalim Mohammed Said ni Muislamu, ana haki zote kusimulia mchango wa babu zake katika harakati za uhuru.
Maadam wahusika wa harakati za uhuru, wako Wakristo na Waislamu, hakuna ubaya wowote, mfia dini mmoja wa Kiislamu kusimulia mchango wa Waislamu katika Uhuru wa Tanganyika. Na nyinyi Wakristo si mpo mnaojua historia, hakuna ubaya mkijitokeza na kueleza the role of Christians, katika harakati za uhuru.
Maalim Mohamed Said, endelea.
P.
Mama umri unakutupa vibayaUtaitaja vipi Historia ya Tanganyika / Tanzania bila kuwataja Waislam? Au huelewi kuwa wao ndio walioanzisha harakati za Uhuru?
Naona unasumbuka sana unapoona Waislam wakitajwa katika historia ya ukweli. Pole sana, ukweli utabaki kuwa ukweli daima.