Mwanahabari Huru
JF-Expert Member
- Mar 9, 2015
- 14,243
- 34,899
Ofisa mtendaji mkuu wa Kampuni ya Mohammed Enterprises Limited (MeTL), Mohamed Dewji ‘Mo’ amesema anamwachia Mungu suala la kampuni hiyo kupokonywa mashamba na mengine kuwekwa chini ya uangalizi na Serikali.
Hivi karibuni, Serikali ilitangaza kufuta umiliki wa mashamba sita yenye ukubwa wa ekari 12,915 yaliyopo Korogwe mkoani Tanga.
Pia, wiki iliyopita bungeni Serikali ilisema mashamba sita yanayomilikiwa na mfanyabiashara huyo bilionea yako chini ya uangalizi na kama atashindwa kutekeleza masharti yatafutwa.
Juzi, Mo akizungumza na Mwananchi mara baada ya kumaliza kuzungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya mwenendo wa timu ya Simba, alisema hayupo tayari kulizungumzia suala hilo la mashamba.
“Kaka naomba uniache tafadhali. Mambo mengine tumuachie Mungu,” alisema Mo kwa kifupi.
Mwezi uliopita, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akiwa ziara wilayani Korogwe alitangaza uamuzi wa Serikali wa kubadilisha mashamba sita kati ya 14 yanayomilikiwa na kampuni hiyo.
Alisema mashamba yaliyofutwa ni yale yaliyopo eneo la Mombo, Mabogo na Kwalukonge wilayani Korogwe.
Naibu waziri huyo alisema uamuzi wa kufuta mashamba hayo umefikiwa baada ya mapendekezo yaliyotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe kutokana na kutoendelezwa kwa muda mrefu.
Pamoja na mashamba hayo kufutwa wiki iliyopita bungeni, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akijibu hoja za wabunge walizozitoa katika mjadala wa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii alisema awali mfanyabiashara huyo alipewa onyo kuhusu mashamba 12 kati ya 21 aliyokuwa akimiliki akitakiwa kuyaendeleza.
Alisema Serikali tayari imefuta hati za mashamba sita na kwamba bado sita ambayo yako kwenye uangalizi.
Waziri huyo alisema Tanzania ina mashamba makubwa 2,000 ya kilimo na ufugaji.
“Haijatokea nikapata agizo kutoka kwa Rais kuwa nifute hati ya shamba la mtu,” alisema Waziri Lukuvi.
Hivi karibuni, Serikali ilitangaza kufuta umiliki wa mashamba sita yenye ukubwa wa ekari 12,915 yaliyopo Korogwe mkoani Tanga.
Pia, wiki iliyopita bungeni Serikali ilisema mashamba sita yanayomilikiwa na mfanyabiashara huyo bilionea yako chini ya uangalizi na kama atashindwa kutekeleza masharti yatafutwa.
Juzi, Mo akizungumza na Mwananchi mara baada ya kumaliza kuzungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam juu ya mwenendo wa timu ya Simba, alisema hayupo tayari kulizungumzia suala hilo la mashamba.
“Kaka naomba uniache tafadhali. Mambo mengine tumuachie Mungu,” alisema Mo kwa kifupi.
Mwezi uliopita, Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Angelina Mabula akiwa ziara wilayani Korogwe alitangaza uamuzi wa Serikali wa kubadilisha mashamba sita kati ya 14 yanayomilikiwa na kampuni hiyo.
Alisema mashamba yaliyofutwa ni yale yaliyopo eneo la Mombo, Mabogo na Kwalukonge wilayani Korogwe.
Naibu waziri huyo alisema uamuzi wa kufuta mashamba hayo umefikiwa baada ya mapendekezo yaliyotolewa na Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe kutokana na kutoendelezwa kwa muda mrefu.
Pamoja na mashamba hayo kufutwa wiki iliyopita bungeni, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi akijibu hoja za wabunge walizozitoa katika mjadala wa taarifa ya Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii alisema awali mfanyabiashara huyo alipewa onyo kuhusu mashamba 12 kati ya 21 aliyokuwa akimiliki akitakiwa kuyaendeleza.
Alisema Serikali tayari imefuta hati za mashamba sita na kwamba bado sita ambayo yako kwenye uangalizi.
Waziri huyo alisema Tanzania ina mashamba makubwa 2,000 ya kilimo na ufugaji.
“Haijatokea nikapata agizo kutoka kwa Rais kuwa nifute hati ya shamba la mtu,” alisema Waziri Lukuvi.