Quemu
JF-Expert Member
- Jun 27, 2007
- 984
- 128
Inaweza kuwa sio Wahindi-Watanzania wote wana mapenzi ya kweli na Tanzania. Lakini bila ya shaka kuna baadhi yao ni wazalendo kutushinda waasili wenyewe.
Kweli kuna sababu ya kuwa na wasiwasi na uzalendo wa Mohamed Dewj kama anavyoonekana kwenye picha hizi mbili (attached)? Aliacha shughuli zake muhimu na kujitokeza kushangilia ushindi wa Taifa stars. Ushindi ambao hauna faida wala maslahi yoyote kwa Mhindi ambaye hana mapenzi ya kweli na Tanzania.
Hakika huyu ni mmoja wa Wahindi wenye 'damu ya Kitanzania.'
Picha kwa hisani ya Global Publishers
(Mods - kwa mara nyingine tena naombeni msaada wenu kubandika hizo picha)