Mohamed Dewj mzalendo halisi!

Quemu

JF-Expert Member
Jun 27, 2007
984
128
3100d1229445541-mohamed-dewj-mzalendo-halisi-mohamed-dewj1.jpg

3101d1229445541-mohamed-dewj-mzalendo-halisi-mohamed-dewj.jpg

Inaweza kuwa sio Wahindi-Watanzania wote wana mapenzi ya kweli na Tanzania. Lakini bila ya shaka kuna baadhi yao ni wazalendo kutushinda waasili wenyewe.

Kweli kuna sababu ya kuwa na wasiwasi na uzalendo wa Mohamed Dewj kama anavyoonekana kwenye picha hizi mbili (attached)? Aliacha shughuli zake muhimu na kujitokeza kushangilia ushindi wa Taifa stars. Ushindi ambao hauna faida wala maslahi yoyote kwa Mhindi ambaye hana mapenzi ya kweli na Tanzania.

Hakika huyu ni mmoja wa Wahindi wenye 'damu ya Kitanzania.'

Picha kwa hisani ya Global Publishers

(Mods - kwa mara nyingine tena naombeni msaada wenu kubandika hizo picha)
 

Attachments

  • Mohamed Dewj1.jpg
    Mohamed Dewj1.jpg
    34.9 KB · Views: 319
  • Mohamed Dewj.jpg
    Mohamed Dewj.jpg
    23.1 KB · Views: 303
Atauza sana bidhaa za viwanda vyake na kutangaza biashara zake zaidi na hii ndio inavyotakiwa kwa wafanyabiashara kitokezeni kudhamini na kutangaza biashara zetu au kazi zetu katika matukio kama haya
 
angekuwa mzalendo angewasaidia wakazi wa singida na asinge uza drugs.. "Negro Please!"
 
Kuuza drugs sio makosa kama ana maduka ya madawa je asiuze au elezea kwa kina ni drugs aina gani ? Nafikiria gharama anazotumia kudhamini stars na jinsi anavyodaiwa jimboni mwake mashule na huduma zingine nyingi sana anazodaiwa na wapiga kura wake
 
angekuwa mzalendo angewasaidia wakazi wa singida na asinge uza drugs.. "Negro Please!"

Duh...hii noma sasa,,kumbe 'MO' naye anauza drugs!!!!!!!!!!..anways lakini jamaa anapenda soka hasa,ni mnazi hasa wa kabumbu so hana budi kupongezwa kwa hili la kuwa msitari wa mbele katika uihamasisha timu yetu ya Taifa pamoja na kutoa misaada ya mara kwa mara ya hali na mali kwa stars...big up 'MO'
 
angekuwa mzalendo angewasaidia wakazi wa singida na asinge uza drugs.. "Negro Please!"

"Kama sentensi yako ni ya kweli, basi inaprove jinsi alivyo mzalendo. Kwa sababu anachofanya yeye hakina tofauti na wanachofanya hao tunaowaona ndio wazawa (wakina sisi)."

Anaweza kuwa hasaidii Singida na anauza drugs kama ulivyohainisha, lakini bado ukweli huko pale pale kuwa aliacha shughuli zake kwenda kushangilia Stars. Jiulize ni "wakina sisi" wangapi ambao wenye 'shughuli zao muhimu' walitenga muda wao siku hiyo kwenda kucheza mdundiko na Stars?
 
Mo ameonyesha mfano mzuri kwa wengine na kama tuna question uzalendo wake basi nadhani neno uzalendo limepoteza maana yake au pengine ili uwe mzalendo lazima uwe na surname ya Mgonja, Yona, Mramba, Karamagi et al
 
....So, all it takes to be a mzalendo is to take off your shirt, to hell with being a honourable MP, and dance to the tune of Mdundiko with Stars Footballers, eh??
 
That is very intresting topic hata manji ameisaidia sana yanga.alishalipia mechi na wananchi waliingia kutazama mechi bure.Does that qualifya to be patriotic.Nadhani muheshimiwa neno uzalendo halielewi maana yake
 
....So, all it takes to be a mzalendo is to take off your shirt, to hell with being a honourable MP, and dance to the tune of Mdundiko with Stars Footballers, eh??

Achana na suala la kucheza mdundiko tu,jamaa alikwenda mpaka SUDAN na mara kibao amekwa akiongozana na Stars inapokwenda nje..na pia amekuwa akimwaga fuba kwa wachezaji wa Stars mara kwa mara..So jamaa anaonesha 'elements' fulani za uzalendo
 
Balantanda uzalendo ni kusapoti soka?
Soka ambayo ilianzia Uingereza na wao bado wanawazomea wachezaji weusi kama monkeys?
Anyways back to the point ni kwamba jiulize kipindi kile cha zamani cha kila mchezaji na mpira wake..Kipindi cha kina Mwameja...Kina Azim Dewji...Zamani walikuwa hata hawasachiwi sijui kuhusu sasa...Lakini nia yao si lazima iwe uzalendo...Inawezekana ni kujtangaza kibiashara...Si unakumbuka mambo ya Bobby Soap?
Sisi waafrika ni budi tubadilike...Mzungu naye si alikuja akajiunga kwenye mdundiko tukampa uhuru wetu?
Sasa kuja kwenye mechi na kucheza mdundiko ni uzalendo...Hivi unajuwa uzalendo ni neno zito?
 
Achana na suala la kucheza mdundiko tu,jamaa alikwenda mpaka SUDAN na mara kibao amekwa akiongozana na Stars inapokwenda nje..na pia amekuwa akimwaga fuba kwa wachezaji wa Stars mara kwa mara..So jamaa anaonesha 'elements' fulani za uzalendo

kwa definition yako wote nchi hii wazalendo! Rostam, EL, manji, Mramba , Yona, Mgonja, maana wote hawa kwa nyakati tofauti maeneo tofauti walitoa misaada tofauti kwa malengo tofauti, amabayo Blatanda unaweza ita uzalendo!

marketing hiyo kaka!!
 
Tatizo letu wabongo tunadhani wazalendo ni tu wale wenye ngozi nyeusi lakini ni Majambazi na Mafisadi kama kina Chenge na Mramba. Hawa washenzi kina Mramba, Yona, Chenge pamoja na kuiba mabilioni umesikia lini wanatoa hizo senti zao kusaidia hata timu ya Taifa?? Huyu jamaa Mohammed Dewji nimemsikia kwa muda mrefu akiwepo kwenye kamati za kuisaidia Taifa Stars na ametoa mchango wa hali na mali kuifikisha timu yetu hapo ilipo. Tumpeni hongera zake kwa hilo, kwenye medani ya michezo hasa soka Rais Kikwete nae anastahili pongezi sana.
 
Kwa mtu kama yeye ofcourse tunaita publicity na kama ni mtoaji thats good also...Lakini kusema hayo ni uzalendo...Si kweli...Na hapo ndo udhaifu wa mwafrika ulipo...Tunatekenywa kiurahisi mno.
Kwani nani kasema hao mafisadi ambao hawajatoa misaada ni wazalendo...Leteni sababu nyingine lakini kusaidia kandanda pekee yake doesn't constitute to patriotism.

Soka ni mchezo na yeye ana mapenzi na mchezo wa soka..Sasa soka ni uzalendo?

Ni rahisi sana kuingiliwa kwa kutumia vigezo kama...I can speak swahili,nasaidia soka kwasababu timu ya soka ya Taifa wanabeba bendera basi wanaliwakilisha Taifa na hapo kina Dewji wanataka kudai ni uzalendo kusaidia the cause...

Sasa kama burudani ya soka na mapenzi yake kwake ndio uzalendo basi tuna shida.
 
Balantanda uzalendo ni kusapoti soka?
Soka ambayo ilianzia Uingereza na wao bado wanawazomea wachezaji weusi kama monkeys?
Anyways back to the point ni kwamba jiulize kipindi kile cha zamani cha kila mchezaji na mpira wake..Kipindi cha kina Mwameja...Kina Azim Dewji...Zamani walikuwa hata hawasachiwi sijui kuhusu sasa...Lakini nia yao si lazima iwe uzalendo...Inawezekana ni kujtangaza kibiashara...Si unakumbuka mambo ya Bobby Soap?
Sisi waafrika ni budi tubadilike...Mzungu naye si alikuja akajiunga kwenye mdundiko tukampa uhuru wetu?
Sasa kuja kwenye mechi na kucheza mdundiko ni uzalendo...Hivi unajuwa uzalendo ni neno zito?

Uzalendo kwa nchi yako uko katika nyanja tofauti na ninaweza kusema hata mtu anaesaidia kuinua michezo kuhakikisha nchi yake inafanikiwa ni Mzalendo. Sio kuingia vitani na kuipigania nchi yako ndio uzalendo pekee. Kuna vitu vingi vitakavyoweza kukufanya uonekane mzalendo kwenye nchi yako, kuna walimu wanaotumia taaluma yao kuinua kiwango cha elimu nchini wao pia ni wazalendo, kuna madaktari wanaotumia udaktari wao kuinua hali ya afya nchini wao pia ni wazalendo, kuna wachezaji soka wanaojitahidi kila siku ili wahahakikishe nchi yao inashinda wao pia ni wazalendo, kuna wachangiaji wa JF ambao wako hapa kila siku kuipigia kelele serikali ifuate mfumo wa haki na upigaji vita rushwa wao pia ni wazalendo, kuna wabunge wetu kina Dr. Slaa wanaotumia bunge kuwakilisha vilio vyetu wao pia ni wazalendo. Ndugu Mushi sielewi wewe kwako uzalendo ni upi lakini nataka nikukumbushe tu uzalendo uko kwenye nyanja mbalimbali. Labda Mushi tupe maana yako ya uzalendo.
 
Heshima mbele wakulu.
Mimi nitafurahi zaidi kama nikiwaona ndugu zetu hawa {watanzania wenzetu] wakijiunga na jeshi la polisi au JWTZ, au tukae wote Mburahati, siku hizi sidhani kama ndugu zetu hawa wanazidi zaidi ya 50 katika watumishi zaidi ya 120,000 wa serikali yetu. na hao hamsini najua labda wapo BOT, Daily News kwenye ITs depts. KAMA KWELI TUPO PAMOJA mimi kipimo changu KIKUU nisikie wanapiga vita ufisadi. Ningemuunga sana mkono Dewji siku ile angekuwepo mahamani anacheza hivyo kufurahia mafisadi kufikishwa mahakamani ili wasiibe hela zaidi za kuhudumia wapigia kura wake, na pengine kuhudumia vizuri zaidi Taifa Stars.
By the way, hongera Taifa Stars.
 
Kwa mtu kama yeye ofcourse tunaita publicity na kama ni mtoaji thats good also...Lakini kusema hayo ni uzalendo...Si kweli...Na hapo ndo udhaifu wa mwafrika ulipo...Tunatekenywa kiurahisi mno.
Kwani nani kasema hao mafisadi ambao hawajatoa misaada ni wazalendo...Leteni sababu nyingine lakini kusaidia kandanda pekee yake doesn't constitute to patriotism.

Soka ni mchezo na yeye ana mapenzi na mchezo wa soka..Sasa soka ni uzalendo?

Ni rahisi sana kuingiliwa kwa kutumia vigezo kama...I can speak swahili,nasaidia soka kwasababu timu ya soka ya Taifa wanabeba bendera basi wanaliwakilisha Taifa na hapo kina Dewji wanataka kudai ni uzalendo kusaidia the cause...

Sasa kama burudani ya soka na mapenzi yake kwake ndio uzalendo basi tuna shida.

UZALENDO ni nini?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom