Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,754
Mojawapo ya kazi ngumu duniani ukiachana na zile zinazotumia nguvu ni hii kazi ya mochwari! Kushinda ama kukesha kwenye chumba kilichojaa miili iliyonyamaa na kutulia tuli....kuandaa mwili wa marehemu ili uweze kuwa na sura inayotazamika mbele ya wafiwa.....lakini kubwa zaidi unapopata tenda ya kunyofoa kiungo/viungo vya marehemu kwa shughuli za kishirikina
Kuna biashara za siri zinaendelea kule...watu wanapiga hela na maisha yanaendelea
Maiti inatisha na kuna watu ni waoga kupitiliza! Hawa hupendwa mno na wahudumu wa mochwari! Mnatoa pesa na nguo ili awasaidie kumuandaa marehemu wenu......wahudumu wasio waaminifu hufanya yao kipindi hiki
Usiku mmoja mochwari si kitu rahisi hata kidogo!
Watakuja wachawi
Watakuja wanga
Watakuja wapiga dili za kitapeli
Watakuja wala nyama za wafu
Watakuja wataka viungo kwa shughwuli wanazojua wao
Watakuja wanaotaka maiti kamili ya mtoto binti kijana mtu mzima nk nk....wote ni wako hawa
Wanga na wachawi watakuja na vitisho hasa kama uko fit kiasi fulani, utafanyiwa michezo mpaka uikimbie mochwari, hawa wengine watakujia live kwa cash money na baadhi watakutisha vyovyote vile
Usiku wa mochwari ni dunia nyingine kabisa. Yenye mambo yasiyoelezeka yakaeleweka kwa urahisi. .ni dunia yenye mtifuano mkubwa wa kiroho na uvutano wa dunia halisi
Pale ndio kituo cha kwanza baada ya roho kutengana na mwili...kwahiyo kuna vurugu mechi kubwa hasa kwa vile vifo vya kishirikina ugomvi dhuluma na zile roho ambazo bado zilikuwa haziko tayari kuachana na mwili....!!! Asikwambie mtu makaburini kuna nafuu kuliko mochwari
Mochwari kuna maiti hununa hucheka hukasirika husogea husonya na mambo mengine mengi ya ajabuajabu lakini muda nwingine yakichombezwa na wachawi na wanga!
Hata hivyo pamoja na changamoto zote hizi, bado inabaki kuwa kazi kama kazi nyingine tu ILA ukimuona mhudumu wa mochwari MHESHIMU sana! Kazi yake imebeba siri kubwa
Kuna biashara za siri zinaendelea kule...watu wanapiga hela na maisha yanaendelea
Maiti inatisha na kuna watu ni waoga kupitiliza! Hawa hupendwa mno na wahudumu wa mochwari! Mnatoa pesa na nguo ili awasaidie kumuandaa marehemu wenu......wahudumu wasio waaminifu hufanya yao kipindi hiki
Usiku mmoja mochwari si kitu rahisi hata kidogo!
Watakuja wachawi
Watakuja wanga
Watakuja wapiga dili za kitapeli
Watakuja wala nyama za wafu
Watakuja wataka viungo kwa shughwuli wanazojua wao
Watakuja wanaotaka maiti kamili ya mtoto binti kijana mtu mzima nk nk....wote ni wako hawa
Wanga na wachawi watakuja na vitisho hasa kama uko fit kiasi fulani, utafanyiwa michezo mpaka uikimbie mochwari, hawa wengine watakujia live kwa cash money na baadhi watakutisha vyovyote vile
Usiku wa mochwari ni dunia nyingine kabisa. Yenye mambo yasiyoelezeka yakaeleweka kwa urahisi. .ni dunia yenye mtifuano mkubwa wa kiroho na uvutano wa dunia halisi
Pale ndio kituo cha kwanza baada ya roho kutengana na mwili...kwahiyo kuna vurugu mechi kubwa hasa kwa vile vifo vya kishirikina ugomvi dhuluma na zile roho ambazo bado zilikuwa haziko tayari kuachana na mwili....!!! Asikwambie mtu makaburini kuna nafuu kuliko mochwari
Mochwari kuna maiti hununa hucheka hukasirika husogea husonya na mambo mengine mengi ya ajabuajabu lakini muda nwingine yakichombezwa na wachawi na wanga!
Hata hivyo pamoja na changamoto zote hizi, bado inabaki kuwa kazi kama kazi nyingine tu ILA ukimuona mhudumu wa mochwari MHESHIMU sana! Kazi yake imebeba siri kubwa