Mnyika, Zitto wamchezesha kwata Naibu Spika

Hii kali '' ni kwelia lichosema Mnyika lakini kachelewa...'' An Ignorant of the law has no excuse, je mwanasheria mkuu analifahamu hilo

Mwaka wa vioja
 
mi natabiri ngumi na makofi yananukia..na adhabu kali kwa wabunge pinzani zitatolewa ili kuwamaliza nguvu
 
kwa hiyo nafasi ya uwakilishi mbunge wa CUF(kura275) amembwaga vibaya mbunge wa chadema(kura47)........?
poleni...subirini nafasi nyingine labda mtapata...!
 
kwa hiyo nafasi ya uwakilishi mbunge wa CUF(kura275) amembwaga vibaya mbunge wa chadema(kura47)........?
poleni...subirini nafasi nyingine labda mtapata...!


Si unajua tena kuna CCM-CUF alliance Bungeni iliyoanzia ndoa yao kule chumbani? Kwa jinsi CCM inavyoweza kuwalambisha pipi vyama inavyoviona dhaifu tukio hili linajirudia: Mwaka 2006 katika kupata mjumbe wa upinzani kwenda Bunge la Afrika, Wabunge karibu wote wlimuunga mkono Phares kabuye wa TLP (RIP) kuliko yule wa CUF -- Fatma Maghimbi.

Hakuna haja ya kutaja kwamba wakati ule CCM na CUF vilikuwa haviendani kabisa na hata Lipimba alisusia mkutano wa NEC wa kuwatangaza washindi wa kura za urais pale Diamond Jubilee Hall. Safari hii mambo yamegeuka, CCM inakiona Chadema ndiyo mpinzani (adui) mkubwa na CUF sasa ni maswahiba. Na utaona kura zote zilizopigwa katika Bungeni Bunge hili baada ya kuapishwa matokeo ya kura yana mwelekeo huo -- yaani CCM-CUF alliance vs CHADEMA.
 
Duu hili linchi ndo nimeamini kabisa kuwa linaendeshaw ki dictatorship! heh! unamtishia mbunge anayefanya kazi yake ati kwa sababu ya kukukosoa ktk kazi yako???, came on spika mdogo!!

  1. A government controlled by one person, or a small group of people. In this form of government the power rests entirely on the person or group of people, and can be obtained by force or by inheritance. The dictator(s) may also take away much of its peoples' freedom.
  2. In contemporary usage, dictatorship refers to an autocratic form of absolute rule by leadership unrestricted by law, constitutions, or other social and political factors within the state.
 
Kitaeleweka sala zetu hazifi zikafa zitaota na mbegu iliyo bora. Mungu yuko!!
 
Hivi jamani naomba kuuliza kwani hakuna vote of no confidence katika bunge maana inaelekea hili bunge litaendeshwa kibabe na kuvuruga vuruga pasina kufuata sheria. Je sheria zinasemaje? Na iko wapi haki ya watanzania? Wanasheria tusaidieni
 
Kuhusu jambo hili vifungu vya kanuni vinasema hivi:

5: (1):
Katika kutekeleza majukumu yake yaliyotajwa katika Ibara ya 84 ya Katiba, Spika ataongozwa na Kanuni hizi na pale ambapo Kanuni hazikutoa mwongozo, basi Spika atafanya kazi kwa kuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamoja na mila na desturi za Mabunge mengine yenye utaratibu wa kibunge unaofanana na
utaratibu wa Bunge la Tanzania.

5: (2):
Spika atawajibika kutilia nguvu Kanuni zote za Bunge, na Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kumwarifu Spika kuwa Mbunge fulani amekiuka Kanuni.

5: (3):
Spika anaweza kumtaka Mbunge yeyote anayekiuka Kanuni hizi kujirekebisha mara moja.

5: (4):
Mbunge yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa Spika anaweza kuwasilisha sababu za kutokuridhika kwake kwa Katibu wa Bunge ambaye atawasilisha malalamiko hayo kwa Spika.

5: (5):
Spika atawajibika kuitisha kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge
na kulijulisha Bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa na Kamati hiyo.

5: (6):
Spika au Naibu Spika hatakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni za Bunge inapokaa kujadili uamuzi unaolalamikiwa
, bali wajumbe watachagua Mwenyekiti wa muda kwa asilimia 50 ya kura za siri.

Tuzichambue.
 
soon wataanza kuwafungia wapiganaji wetu ili waweze kuliendesha bunge kwa mazoea kama walivyozoea
 
ANNA ANNA watanzania hatutaki upumbavu tumechoshwa na Kuibiwa haki zetu we endelea tu na kujipendekeza kwa mafisadi tuone kama ahera utaenda nao....TANZANIA SIO NCHI YA AMANI NI NCHI YA WAOGA NA UOGA UMEANZA KUTUTOKA HIKI NI KIZAZI CHA KUJITOA MUHANGA NYIE FANYENI MAMBO YENU YA KUTOTUMIA AKILI MUONE ....
KWA KWELI TUMECHOKA AMINI USIAMINI TUMECHOKA NA UOGA NDO UNAVYOZIDI KUTUTOKA MAANA TUNA NJAA NA HASIRA....:A S angry:
 
Kuhusu jambo hili vifungu vya kanuni vinasema hivi:

5: (1):
Katika kutekeleza majukumu yake yaliyotajwa katika Ibara ya 84 ya Katiba, Spika ataongozwa na Kanuni hizi na pale ambapo Kanuni hazikutoa mwongozo, basi Spika atafanya kazi kwa kuzingatia Katiba, Sheria nyingine za nchi, Kanuni nyingine zilizopo, maamuzi ya awali ya Maspika wa Bunge pamoja na mila na desturi za Mabunge mengine yenye utaratibu wa kibunge unaofanana na
utaratibu wa Bunge la Tanzania.

5: (2):
Spika atawajibika kutilia nguvu Kanuni zote za Bunge, na Mbunge yeyote anaweza kusimama mahali pake na kumwarifu Spika kuwa Mbunge fulani amekiuka Kanuni.

5: (3):
Spika anaweza kumtaka Mbunge yeyote anayekiuka Kanuni hizi kujirekebisha mara moja.

5: (4):
Mbunge yeyote ambaye hataridhika na uamuzi wa Spika anaweza kuwasilisha sababu za kutokuridhika kwake kwa Katibu wa Bunge ambaye atawasilisha malalamiko hayo kwa Spika.

5: (5):
Spika atawajibika kuitisha kikao cha Kamati ya Kanuni za Bunge
na kulijulisha Bunge kuhusu uamuzi utakaotolewa na Kamati hiyo.

5: (6):
Spika au Naibu Spika hatakuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kanuni za Bunge inapokaa kujadili uamuzi unaolalamikiwa
, bali wajumbe watachagua Mwenyekiti wa muda kwa asilimia 50 ya kura za siri.

Tuzichambue.

Nadhani hizo subsection 4-6 za section 5 zinautata sawa wanapiga kura ya siri kutokuwa na imani na spika lakini kupata asilimia 50 ya kura mh litakuwa gumu hilo je wananchi hawawezi kuliengua bunge kama hawana imani nalo?
 
Big up Zitto and Mnyika. You actually know what your doing in the House. Keep going! No body shall stop you our Excellency MPs.

Mbona vioja bungeni Bunge la 10 vimeanza mapema namna hii? Naona huko tunakoelekea HATUFIKI ASILANI. Nasikia harufu ya DAMU!
Yaani Spika,Naibu wake,Mwanasheria Mkuu na Wabunge wote wa CCM na CUF wavunje KANUNI ZA BUNGE HALAFU WASEME mhe.MB AMECHELEWA KUWASILISHA HOJA SIMPLY BECAUSE NI MB. WA CHADEMA???????????????!!Hapa sipati picha. Natamani nikaingie Bungeni nianze kushusha makonde. Huu uoza wa Bunge hatutakubaliana nao. This is nonsense!

Kwanini kusiwe na vigezo maalumu vya kuwapata Spika na Naibu wake na kigezo mojawapo muhimu na cha kwanza kiwe ni MTU ALIYESOMEA SHERIA?Tunajua kabisa kazi muhimu ya Bunge ni kutunga sheria. Inakuwaje mtu anagombea Uspika na Unaibu wakati hana hata ABC za sheria?
Mpaka sasa Spika na Naibu wake hakuna mwenye Taaluma ya Sheria.Bibi Makinda kasoma IFM mambo ya usimamizi wa Fedha, Ndugai kasoma Mweka mambo ya Wanyama pori. Sasa wapi na wapi Usimamizi wa pesa na Wanyama pori kwenye Kutunga sheria na Kusimamia Kanuni za Bunge? Jibu ni zero!

Tatizo la hawa CCM wanapeana vyeo tu bila kuangalia hata sifa (CV)zinazomruhusu mgombea husika kwenye nafasi husika. Hili bila shaka wanalifanya makusudi ili huyo mtu aendelee kuwa mbumbumbu ili wamtumie kisawasawa.
 
Back
Top Bottom