Uchaguzi 2020 Mnyika: Sakata la Wabunge wa Viti Maalum limehusisha mfumo wa Serikali kufifisha ajenda ya 'Uchaguzi haramu'. Ahoji Nusrat kuteuliwa akiwa gerezani

Waambieni upuuzi wanaofanya umechosha,watumishi wanahitaji stahiki zao.Na si fedha zitumike kuwanunua wakina Mdee.
 
Chadema ndio chama cha Siasa kinachoongoza Barani Africa kwa viongozi wake wakuu kusaliti misimamo na maazimio ya Chama chao!

50% ya Wagombea wao wa Urais wamerudi CCM

Makatibu wakuu wote waliowahi kushika nyadhifa hizo wamerudi CCM i.e Kabourouh, Slaa na Mashinji

Wabunge na wajumbe wa kamati kuu kadhaa wote wamerudi CCM

Mwenyekiti wa Vijana Taifa karudi CCM
Na Sasa Mwenyekiti wa Wanawake anakwaruzana na Mabeberu ya Chama hicho


Chadema watafute chanzo cha Viongozi wake kuamini katika vyeo badala ya Itikadi
Analysis on point
 
Wanandungai 19 leo wanaizika chadema rasmi toka chama kikuu cha upinzani na kuwa chama cha mwisho kabsa cha upinzani endapo kamati kuu ya chadema itakuwa Dhaifu mno kuwakumbatia hao walionyesha dharau kubwa kwa Uongozi wa chadema
 
aliondoka Slaa, aliondoka Zito,
Fukuza wote hao wakakate mauno yao huko...
Tatizo kubwa mbowe na Salum mwalimu wamekula bilion 3 za CCM huku pia wakiwinda ruzuku haramu kupitia hao wabunge 19 wa Ndungai, hapo ndipo penye shida kubwa na pia hao wanandungai wameonyesha dharau kubwa kwa Lisu na mnyika kisa wamepewa vicent na Ndungai na kuahidiwa mgao na mbowe mwenyewe, kuna mkanganyiko mkubwa sasa, mbowe kapagawa yupo mafichoni kaenda kuficha pesa aliyochukua toka CCM kwanza, leo kuba mawili chadema idharaulike au iheshimike zaidi
 
Ni kauli iliyoshiba na yenye mantiki.Ambaye haoni ubatili na uhuni uliofanyika na unaoendelea kufanywa ni kwa utashi wake wa kukana ukweli! Dola iko mikononi mwa "WAHUNI".
 
Ni kweli kama ulivyodai CHADEMA is bigger than individuals who r opportunistic, ila unasahau nyuma ya migogoro yote ni udikteta wa Mbowe, mwenye chama. Aidha Mnyika atafukuzwa au atajiuzuru kwani Mbowe hawezi kukubali kukosa hiyo fedha ya Ruzuku na michango ya hao wabunge ambayo inahitajika sana kukiendesha chama. Labda, labda, labda kama Mnyika ana mipango mbadala ya kupata pesa ya kuendesha chama ikiwa ni pamoja na mshahara wake?
Kwa akili zako CHADEMA ina survive sababu ya ruzuku pekee? More so ruzuku watakayopewa haitozidi 100M kwa mwezi which is peanuts ukizingatia walikua wakipata zaidi ya 2B kwa mwaka. Kwahiyo hta wakiikubali bado haiwezi wasaidia kitu.

Hyo 100M u can simply get from donors na raia kwa mfumo wa michango/kulipia kadi kupitia CHADEMA digital. Na wananchi tutachanga maana tunajua wamekataa hela ya dhulma and itaonyesha seriousness ya chama kuelekea 2025.

Then sio kweli Mbowe kawatuma otherwise asingehitaji kutumia njia za panya. Si mnamuitaga dikteta? Sasa amuogope Mnyika aliyemteua mwenyewe? Amgeitisha press. Angejustify maamuzi kazi kwisha. Ila kudai Mbowe anategemea njia za panya kupitisha maazimio yake ni reasoning ya chini kabisa.

Kma CHADEMA ilivuka kifo cha wangwe,Kesi ya ugaidi wa Lwakatare, kuondoka Zitto na Dk Slaa. Trust me hakuna lingine linaloweza warudisha nyuma ever. Na nchi hii hakuna upinzani nje ya CHADEMA and its more clearer now than ever.
 
Kwa akili zako CHADEMA ina survive sababu ya ruzuku pekee? More so ruzuku watakayopewa haitozidi 100M kwa mwezi which is peanuts ukizingatia walikua wakipata zaidi ya 2B kwa mwaka. Kwahiyo hta wakiikubali bado haiwezi wasaidia kitu.

Hyo 100M u can simply get from donors na raia kwa mfumo wa michango/kulipia kadi kupitia CHADEMA digital. Na wananchi tutachanga maana tunajua wamekataa hela ya dhulma and itaonyesha seriousness ya chama kuelekea 2025.

Then sio kweli Mbowe kawatuma otherwise asingehitaji kutumia njia za panya. Si mnamuitaga dikteta? Sasa amuogope Mnyika aliyemteua mwenyewe? Amgeitisha press..... Angejustify maamuzi kazi kwisha. Ila kudai Mbowe anategemea njia za panya kupitisha maazimio yake ni reasoning ya chini kabisa.

Kma CHADEMA ilivuka kifo cha wangwe,Kesi ya ugaidi wa Lwakatare, kuondoka Zitto na Dk Slaa...... Trust me hakuna lingine linaloweza warudisha nyuma ever. Na nchi hii hakuna upinzani nje ya CHADEMA and its more clearer now than ever.
Nakubaliana na wewe ila unasahau nguvu ya chama ni wanachama. Sijui unajua athari za kuwafukuza viongozi wa BAWACHA uanachama? Je, chama kitabaki salama kweli?
 
Nakubaliana na wewe ila unasahau nguvu ya chama ni wanachama. Sijui unajua athari za kuwafukuza viongozi wa BAWACHA uanachama? Je, chama kitabaki salama kweli?
BAVICHA ilikua ndio nguzo ya CHADEMA enzi za Heche ila walitimuliwa karibu viongozi wote 8 kuanzia Mchange mpaka mwampambana na Shonza. Na tokea hapo vijana waliongezeka mara dufu leo hii kina mchange wameishia wapi?

Slaa na Zitto walikua na zaidi ya 2m followers wa upinzani. Walivyosepa kuna impact yeyote? As long as CHADEMA ni brand watakuja replacements wengi mnoo.

Kuna kina Khadija Mwago, Aisha Madogga, Mama wa chato, Upendo peneza, Moza ally, Amina Saguti, Esther Chisanga, Lucy Owenya, Asia Msangi, Dorcas Francis, Komba, to name a few...... Hao wana replace roster nzima iliyosaliti bila gap yoyote kuonekana.

With time watsahulika tu kma kina Lijualikali na Lwakatare
 
Ikiwa documents zimeghushiwa kwanini wasiende mahakamani ili kupinga uhalali WA kilichotokea?
 
wasipoondolewa uanachama hao warembo
Wanachadema ambao hamukubaliani nao mjiunge chama cha UBWABA
 
Wenawe Mnyika unajisaulisha kipindi kile unaruka ukuta shulee ya loyola ili upate kula si kura leo Halima karuka ukuta bungeni ili nao wapate kula unabweka nini shida nilikuwa simpendi halima Mdee ila kuanzia sasa ni heko kwake hayaaa Huyo Lissu yupo huko Ulaya anakula pancake na nawazungu Mbowe najichana ruzuku tena hili la kuapa wakina Mdee anafaida zake ruzuku nakuchangia kiasi kidogo wabunge ni palepale Wewe mnyika unapakuamkia Asubuhi officini hata kama hakuna cha maana ila upo hapo haya Wakina Mdee wakalee wapi wakaandamane na wasaulike ipo siku utakuja Mshukuru mdeee kacheza karata tatu hata mkizira siewenzenu wala Yaheeh mlizira Corona what Next!!@ Chezea Halima wewe!!

WAMAMAkama wote wameenda kutafuta pesa za maziwa ya Watoto kopo Ya kifuani siku hizi wananyonyo wakubwa Nenda halima wakiwazingua hameni chama tafuteni kichama kidogo kikuzeni kama zzitto
 


Leo Novemba 25, 2020 katibu mkuu wa CHADEMA amezungumza na vyombo vya habari makao makuu ya chama hicho eneo la Ufipa, Kinondoni mada kuu ikiwa uteuzi wa wabunge wa viti maalum ambapo uapisho wao ulifanyika jana bungeni jijini Dodoma jana.

Yafuatayo ni maelezo kwenye mkutano huo kuanzia mwanzo hadi mwisho pamoja na maswali kutoka kwa waandishi wa habari.

PIA, SOMA: Hatimaye Wabunge wa Viti maalumu wa CHADEMA wajitokeza kuapishwa Dodoma. Viongozi wa CHADEMA wakana kupeleka majina yao

=> Ester Matiko: Kama chama kikiona kuna mwingine anafaa zaidi ya Ester Matiko, niko tayari

============​

JOHN MREMA: Mbele yetu katibu mkuu wa chama, John John Mnyika akiwa na mkurugenzi wa Itikadi, Uenezi na mahusiano ya mambo ya nje na msemaji mkuu kwa siku ya leo atakuwa katibu mkuu wa chama.

JOHN MNYIKA: Tarehe 28 Oktoba kulifanyika uchafuzi ulioitwa uchaguzi mkuu ambapo mtakumbuka kati ya mambo yaliyofanyika ni hujuma za wazi za mfumo wa kiserikali ukihusisha tume ya Taifa ya uchaguzi kupika matokeo ya uchaguzi.

Chama cha demokrasia na maendeleo hakijateua wabunge wa viti maalum au wagombe ubunge viti maalum wala hakijawasilisha orodha yoyote tume ya Taifa ya uchaguzi ya uteuzi wa wabunge wa viti maalum.

Kwa katiba ya CHADEMA, mamlaka ya uteuzi wa wabunge yapo kwa kamati kuu ya chama. Kamati kuu ya chama haijawahi kufanya kikao cha kuteua majina ya wabunge wa viti maalum wakati wowote.

Pili katibu mkuu wa chama ambae ndie mwenye mamlaka ya kimawasiliano ya kuwasiliana na tume ya Taifa ya uchaguzi, katibu mkuu wa chama sijawahi kuwasilisha orodha yoyote tume ya Taifa ya uchaguzi ya wanaoitwa waliopendekezwa wabunge wa viti maalum.

Katibu mkuu wa chama sio tu anatakiwa apeleke orodha bali anatakiwa apeleke fomu namba 8(d) kwa kila aliyekuwepo kwenye orodha ikiwa imesainiwa na katibu mkuu. Tume ya Taifa ya uchaguzi ilituletea fomu hizi hapa(Anazonyesha) ili tukishateua kama tungeteua, tupeleke orodha ya majina 113 kwa ujumla tukiwa tumejaza hizi fomu.

Mimi kama katibu mkuu, hakuna fomu yoyote ya mtu yoyote niliyowahi kuijaza popote kuthibitisha uteuzi wa yoyote.

Mchakato huo wote haukufatwa, kwa hiyo kwa tafsiri nyepesi, kilichofanyika ni biashara haramu ya kughushi ambayo imehusisha mfumo wa kiserikali, tume ya Taifa ya uchaguzi na kwakweli niseme vilevile imehusisha hao waliokwenda kuapa bila ridhaa ya chama na bila baraka za chama na bila kupishwa kwa mamlaka halali za chama.

Chama inabidi kichukue hatua, katiba yetu inasema hatua zozote zisichukuliwe bila ya wahusika kuitwa, kujieleza. Sasa kwa kuwa hili jambo ni la dharula, chama kitatumia utaratibu wa dharula katika kushughulika na jambo hili na tutaongozwa na kanuni za chama.

Kwa kuwa mamlaka ya jambo hili ni kamati kuu ya chama, naomba kuwatangazi kwamba tumeitisha kikao cha kamati kuu ya chama maalum, kitafanyika siku ya Ijumaa tarehe 27 hapa jijini Dar es Salaam.

Pamoja na kuwa tutawaandikia wahusika, ili kusitokee kisingizio kwa yeyote kwamba hakuitwa, hakupata taarifa ya kuitwa naomba kutangaza 'Public notice' kupitia vyombo vya habari kwa wanachama wetu 19 walioshiriki kwenda kula kiapo jana tarehe 24 kufika makao makuu ya chama bila kukosa.

Kuna tukio la mwanachama wetu ambae ni kiongozi wa baraza la baraza la vijana la CHADEMA, Nusrat Hanje ambae amesota ndani kwa kesi ya kubambikiziwa kwa siku 133 akiwa mahabusu na leo tarehe 25 mahakama kuu ndio ilikuwa inakutana kutoa uamuzi juu ya rufaa ambayo amekata baada ya kusota ndani kwa muda mrefu.

Kituko kinachoashiria mfumo kuhusika katika huu mchezo, tarehe 23 usiku alikwenda kutolewa gerezani ili kesho yake apelekwe kuapa na alitolewa na mfumo bila hata kuzingatia masharti ya kisheria. Tunashkuru kwamba mwanachama wetu na kiongozi wetu ametoka baada ya kusota ndani kwa muda mrefu lakini mfumo ulimtoa ili kutekeleza malengo yao.

Sasa Ndugai amesema alipelekewa majina tarehe 20 Novemba na tume, Nusrat Hanje alietolewa gerezani tarehe 23 Novemba, uteuzi wa tume unasema umefanyika tarehe 20, fomu yake aliijaza lini, hakimu aliemuapisha alikuwa wapi kabla ya tarehe 20 tume ilipomteua mambo ambayo yanadhihirisha wazi kwamba hili jambo ni kazi ya mfumo.

Lengo la wazi la mfumo ni kutaka kufifisha ajenda ya kwamba Tanzania ilifanya uchaguzi haramu tarehe 28 Oktoba ulioitwa uchafuzi wakati umma ukishinikiza, jamii ya kimataifa ikishinikiza, bunge likionekana la chama kimoja ili kujaribu kulipa uhalali serikali ya illegitimate president Magufuli ikaamua kushiriki huu mchezo haramu wa kuhusisha tume, spika wa bunge na hatimaye tumefika hapa tulipofika.

Nitoe rai kwa watanzania, jambo hili lisitutoe watanzania kwenye mjadala mkubwa na muhimu zaidi kwamba tarehe 28 Oktoba kulifanyika uchafuzi na kwamba sisi tunataka uchaguzi ufanyika upya chini ya tume huru ya uchaguzi.

Sisi tunaotaka hilo tunatengenezewa mazingira ya mjadala kuhama, umma wa watanzania usikubali kuingizwa kwenye mtego wa dola wa kuhamisha mjadala na kufifisha hasira za wananchi.

Kauli iliyotolewa jana wakati wa kuapishwa iliyotaka kujenga ishara kama mwenyekiti wa chama, Freeman Mbowe alihalalisha hili linaloendelea, hii kauli sio ya kweli na mwenyekiti wa chama ndie atakaeongoza kikao cha kamati kuu ya chama kitakachofanyika tarehe 27.

MASWALI NA MAJIBU

MWANDISHI (Halifa-Mwandishi wa kujitegemea):
Swali la kwanza kwa Mnyika, unadhani hili suala litaiacha vipi CHADEMA kama chama kwa sababu kuna hofu, ukizingatia watu walioenda bungeni kuapishwa, kina Mdee, Ester Matiko ni watu wakubwa kwenye chama, unadhani litakiacha chama salama?

Swali la pili, umesema hili suala limetengenezwa na mfumo kwamba kuna hujuma flani unadhani CHADEMA kinafanyiwa, katika mazingira kama hayo unadhani CHADEMA kinapaswa kuchukua hatua gani? Mnakabiliana nalo vipi suala la mfumo kujaribu kuhujumu chama chenu ili kuepusha matukio kama hayo kujirudia siku za mbeleni.

JOHN-Dar Mpya: Swali la kwanza, katibu mkuu umesema sakata zima hili la kuwaapisha kina Halima limekuwa 'engineered' na dola lakini kuna taarifa ambazo mimi binafsi nnazo kwamba majina haya, mchakato mzima huu wa maandalizi ulifanyika ndani ya ofisi ya katibu mkuu aidha ni wewe au wasaidizi wako. Kama kiongozi nilitegemea utaweka pia 'doubt' kwamba dola haiwezi kulikamilisha jambo hili bila kushirikiana na viongozi ndani ya chama maana yake wewe kwenye uongozi mzima wa chama haujaonyesha hata mashaka yoyote yale kwamba inawezekana dola imesaidiwa na either watu ndani ya ofisi yako au ndani ya CHADEMA kwa sababu wewe umejaribu kutuonyesha fomu hapo kwamba fomu za tume umekadhibiwa katibu mkuu lakini what If mtu anajenga hoja kwamba ya msaidizi wako alipitia mlango wa nyuma alienda akazichukua hizo fomu ofisi ya tume akaja akazisaini kwa niaba ya katibu mkuu kwa sababu unavyosema saini ni ya katibu mkuu inatakiwa, what if kuna barua ambazo chama kimekuwa kikifanya mawasiliano na tume kupitia naibu katibu mkuu

Swali la pili, uasi na usaliti ndani ya CHADEMA, hawa watu walioenda kuapa ni viongozi wakubwa ndani ya CHADEMA, mimi naona jambo hili hawa watu hawawezi kuwa wamekwenda bila 'top management' kuwa nyuma yao. Hii 'courage' na 'doubt' yangu inaweza kuwa inasapotiwa na kauli ya Halima jana kwamba alimtaja mwenyekiti, unazungumziaje level ya uasi huu?

REGINA-Mwanahalisi: Kilichofanywa na kina Halima Mdee ndio hichi hicho kilichofanywa na mbunge Aida Khenan lakini hapo katibu mkuu amesema wanaopaswa kuja siku ya Ijumaa ni hao wabunge 19 walioapa jana, vipi kuhusu Aida?

MAJIBU
JOHN MNYIKA:
Nianze na la Aida, nilisema leo nimekuja kuzungumzia walioapa jana, hizi ni kesi mbili zinashahabiana lakini ni case mbili tofauti kwa sababu case ya walioapa 19 kimsingi inahusisha cilevile kughushi orodha ya majina ya chama na mchakato mzima wa fomu.

Suala la Aida linahusisha kukiuka tamko lililotolewa na viongozi wakuu wa chama, haya yote mawili tutayashughulikia na kila moja tutashughulikia kwa namna yake.

Maswali ya Halifa, kwamba chama kitabaki salama, naomba niwahakikishie watanzania chama hiki kitaendelea na kitabaki kuwa salama, kitapita katika mchakato huu kikiwa na nguvu zaidi ya kuendelea kujipanga kushika dola na historia ya CHADEMA inadhihirisha hivyo.

Umenukuu jambo hili limehusisha mfumo, sasa tutachukua hatua gani. Naomba nisizungumze hatua kwa sasa kwasababu kama nilivyosema tunakwenda kufanya kikao cha kamati kuu tarehe 27 na nitoe wito kwa wanachama na viongozi popote pale, milango iko wazi na wadau wa demokrasia kutoa maoni kwa chama juu ya ni hatua gani zikachukuliwe na kamati kuu tarehe 27 kwahiyo sitaki kutoa hukumu.

John, Dar Mpya mpaka ninavyozungumza na nyinyi sijaletewa ushahisi na yoyote juu ya uhusika wa mtu yoyote ndani ya ofisi ya katibu mkuu kushirikiana na mfumo kufanya jambo hili. Jambo ambalo nina hakika nalo moja kwa moja, hao 19 walioenda kuapa walishiriki kwenye huu ubatili na wanaufahamu huu ubatili.

Narudia kusisitiza halina baraka zozote za mwenyekiti Mbowe kwa hiyo ndugu John ulieuliza swali ni vyema ukafatilia na ukaandikana pia ukapata 'quotation' kati ya viongozi wakubwa unaosema wamebariki au wameunga mkono jambo hili, ni kiongozi gani?

Jambo la kuzingatia, kiongozi mmoja mmoja anaweza akawa na mawazo yake binafsi, wapo waliokuwa na maoni kwamba tupeleke majina haraka, wengine wanasema tusipeleke, wapo wanaosema tuendelee na msimamo wetu uleule wa kutopeleka majina, hiki ni chama cha demokrasia na maendeleo, watu wanaweza kuwa na maoni lakini ajitokeze mtu mmoja aseme ni kikao gani kimekaa kikafanya uteuzi wa majina, hakuna mtu atakaekwambia.

Kwa ufupi hawa waliokwenda kuapa, kimsingi walijiteua na wakashirikiana na dola kwenda kuhalalisha huo ubatili, usaliti, uasi na uharamu wa kushiriki kiapo, sasa chama kitachukua hatua gani? Hio sio kazi ya katibu mkuu. Kazi ya katibu mkuu ni kuhakikisha kamati kuu imeitishwa, itafanyika Ijumaa na chama kitaeleza hatua ambazo itachukua, tunawashukuru sana.
Kama ni mfumo
..hao Makamanda ealilishea nini?
Hadi sasa hakuna update ya kikao sio kuhusu Halima ama Mbowe aliyrtajwa na Halima.
 
BAVICHA ilikua ndio nguzo ya CHADEMA enzi za Heche ila walitimuliwa karibu viongozi wote 8 kuanzia Mchange mpaka mwampambana na Shonza. Na tokea hapo vijana waliongezeka mara dufu leo hii kina mchange wameishia wapi?

Slaa na Zitto walikua na zaidi ya 2m followers wa upinzani. Walivyosepa kuna impact yeyote? As long as CHADEMA ni brand watakuja replacements wengi mnoo.

Kuna kina Khadija Mwago, Aisha Madogga, Mama wa chato, Upendo peneza, Moza ally, Amina Saguti, Esther Chisanga, Lucy Owenya, Asia Msangi, Dorcas Francis, Komba, to name a few...... Hao wana replace roster nzima iliyosaliti bila gap yoyote kuonekana.

With time watsahulika tu kma kina Lijualikali na Lwakatare
Kwa hili pia nakubaliana na wewe, japo hutaki kusema wazi, wakati unajua kuwa nyuma ya migogoro yote ndani ya chama ni Mbowe. Hata hao uliowataja kuchukua nafasi ya Halima na wenzake (uteuzi wao una baraka ya Mbowe), hawana ubavu wa kumshauri Mbowe hata akifanya vibaya
 
Kwa hili pia nakubaliana na wewe, japo hutaki kusema wazi, wakati unajua kuwa nyuma ya migogoro yote ndani ya chama ni Mbowe. Hata hao uliowataja kuchukua nafasi ya Halima na wenzake (uteuzi wao una baraka ya Mbowe), hawana ubavu wa kumshauri Mbowe hata akifanya vibaya
Hpn Mbowe si ni dikteta kma mnavyodai kma alibadili gia kwa Lowassa among all people ashindwe kwa hili la mabinti wachache?
Angeitisha press angedai wanawatuma wadada 19 kupambana katiba mpya ipatikane. Nani angepinga?

Ila Mbowe eti amuogope Mnyika ni ujinga kuamini hilo. Angetaka apeleke viti maalum angempa ultimatum tu majina yapelekwe haikua na haja atumie njia za kihuni hivi.

So ntakua mtu wa mwisho kuamini Mbowe ni coward kiasi hiko
 
Kama hujui kuwa nyuma ya migogoro yote ndani ya chama ni Mbowe, M/kiti na mwenye chama, basi subiri matokeo ya kikao cha Kamati Kuu ya chama leo.

Maamuzi ya Mbowe huwa ya mwisho. Hata hili sakata la wabunge wa viti maalumu Mnyika atafukuzwa au kujiuzuru, kwani kujitokeza hadhari kushutumu uteuzi huo ni kama amekalia kuti kavu.
Kitendo cha wale wabunge kwenda bungeni na kuapa mbele ya spika maana yake walikuwa na baraka za mkuu kabisa ndani ya chama.

Wale sio watoto wadogo wafanye jambo kubwa kama lile pasipo kuwa na baraka za ndani ya chama.
 
Wakili msomi haya maswali ni mepesi sana ktk mfumo wa nchi yetu,kuna mambo hufanyika na huwezi hata kuwaza kama yanaweza fanyika ,ngoja tuendelee na ngonjera nyingne mana ni mwendo wa bandika bandua tu
Maswali yafuatayo yanapaswa kujibiwa na Mbowe/ Mnyika:

1. Nani amepeleka Orodha ya Majina ya Wabunge wa Viti Maalum NEC?
2. Orodha hiyo imepelekwa kwa njia gani?...
 
Ameandika hivi kupitia Twitter:

Impunity ya kiwango cha juu kabisa katika taifa letu . Hivi inavumilikaje mtu kuwa mahabusu hajafuata taratibu anatolewa gerezani usiku ,anaapishwa gereji,anakuwa mbunge, halafu waliotenda haya bado wapo ofisi za umaa , halafu yeye na spika wanaitwa waheshimiwa 🤣🤣🤣
 
Back
Top Bottom