Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Hakuna kijana mwenye uwezo mkubwa katika medani za kisiasa katika vyama vyote vya siasa kama Mh John Mnyika. Palipo na ukweli lazima usemwe, palipo na ukweli pia uongo hujitenga. Huwa anajua nini anachokichanganua katika kuchangia miswada mbali mbali hasa bungeni, mwepesi wa kujenga hoja nzito. Mweledi wa kisiasa ambaye huanza kuchambua mada taratibu na umakini mkubwa.
Hana papara wala hakurupuki wakati wa kujibu hoja mbalimbali, mpole anayejiamini. Hutumia busara katika maamuzi na husimamia kile anachokiamini. Jasiri mwenye kuchunguza mambo kwa undani, hana jazba. Hufichua hoja za msingi zilizojificha kiasi mara kadhaa ameweza kuthubutu kusababisha baadhi ya miswaada ya serikali kufanyiwa marekebisho makubwa bungeni.
Pamoja na umri wake mdogo, anafaa kushika nyadhifa za ngazi za juu katika chama na nchi kwa ujumla. Ana sifa nyingi ambazo ukurasa hautatosha kuzibeba kwa wingi wake. Huyu ni JEMBE la uhakika ambalo ni tishio kubwa kwa CCM na Serikali yake na LULU pevu inayopaswa kutunzwa na kuhifadhiwa na chama chake.
Hana papara wala hakurupuki wakati wa kujibu hoja mbalimbali, mpole anayejiamini. Hutumia busara katika maamuzi na husimamia kile anachokiamini. Jasiri mwenye kuchunguza mambo kwa undani, hana jazba. Hufichua hoja za msingi zilizojificha kiasi mara kadhaa ameweza kuthubutu kusababisha baadhi ya miswaada ya serikali kufanyiwa marekebisho makubwa bungeni.
Pamoja na umri wake mdogo, anafaa kushika nyadhifa za ngazi za juu katika chama na nchi kwa ujumla. Ana sifa nyingi ambazo ukurasa hautatosha kuzibeba kwa wingi wake. Huyu ni JEMBE la uhakika ambalo ni tishio kubwa kwa CCM na Serikali yake na LULU pevu inayopaswa kutunzwa na kuhifadhiwa na chama chake.