Serayamajimbo
Senior Member
- Apr 15, 2009
- 191
- 38
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Yusuf Makamba, hakukosea kuwafananisha wanasiasa wa vyama vya upinzani na paka.
Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chadema, John Mnyika kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Kipumbwi wilayani hapa Mkoa wa Tanga katika operesheni Sangara inayoendelea.
Makamba huwa anatufananisha wapinzani na paka sasa sisi hatukatai, sisi kweli ni mapaka tunaotafuta mapanya ambayo ni CCM yanayotafuna fedha za umma, unajua ndani ya nyumba yako yakiingia mapanya lazima ufuge paka ya kuyaua, alisema Mnyika na kuongeza kuwa: wananchi mjitahidi kuongeza idadi ya paka (wapinzani) bungeni ili yasaidie kuyatafuna mapanya (CCM) ambayo yanatafuna rasilimali za nchi.
Aliongeza kuwa panya wa CCM wamekuwa wakitafuna michango inayotolewa na wananchi katika miradi ya maendeleo na fedha za baadhi ya miradi zinazotolewa na wahisani.
Akiwahutubia wakazi wa Kata ya Gare wilayani Lushoto, Mnyika aliwataka Watanzania wasimfananishe hata kidogo Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa na Makamba kwa uelewa wa mambo na utendaji wa kazi zao.
Hivi jamani kwa akili ya kawaida tu unaweza kumfananisha Makamba na Dk. Slaa kwa kitu gani, Dk. Slaa anamzidi Makamba kwa kila kitu, Makamba na mafisadi lao moja wakati Dk. Slaa amekuwa akiyaumbua mafisadi kwa kuanika majina yao, alisema Mnyika.
Mnyika alisema CCM ya wakulima na wafanyakazi ilikufa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na hivi sasa mafisadi yamevamia chama na wanyonge hawana chao.
CHANZO: NIPASHE
Kauli hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Mambo ya Nje wa Chadema, John Mnyika kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Kata ya Kipumbwi wilayani hapa Mkoa wa Tanga katika operesheni Sangara inayoendelea.
Makamba huwa anatufananisha wapinzani na paka sasa sisi hatukatai, sisi kweli ni mapaka tunaotafuta mapanya ambayo ni CCM yanayotafuna fedha za umma, unajua ndani ya nyumba yako yakiingia mapanya lazima ufuge paka ya kuyaua, alisema Mnyika na kuongeza kuwa: wananchi mjitahidi kuongeza idadi ya paka (wapinzani) bungeni ili yasaidie kuyatafuna mapanya (CCM) ambayo yanatafuna rasilimali za nchi.
Aliongeza kuwa panya wa CCM wamekuwa wakitafuna michango inayotolewa na wananchi katika miradi ya maendeleo na fedha za baadhi ya miradi zinazotolewa na wahisani.
Akiwahutubia wakazi wa Kata ya Gare wilayani Lushoto, Mnyika aliwataka Watanzania wasimfananishe hata kidogo Katibu Mkuu wa Chama hicho, Dk. Wilbrod Slaa na Makamba kwa uelewa wa mambo na utendaji wa kazi zao.
Hivi jamani kwa akili ya kawaida tu unaweza kumfananisha Makamba na Dk. Slaa kwa kitu gani, Dk. Slaa anamzidi Makamba kwa kila kitu, Makamba na mafisadi lao moja wakati Dk. Slaa amekuwa akiyaumbua mafisadi kwa kuanika majina yao, alisema Mnyika.
Mnyika alisema CCM ya wakulima na wafanyakazi ilikufa na Baba wa Taifa Mwalimu Julius Nyerere na hivi sasa mafisadi yamevamia chama na wanyonge hawana chao.
CHANZO: NIPASHE