Mnyika, Nape, Mtatiro na Mvungi wanapambana ITV ktk kipima Joto

Kuna hoja katika dondoo yako lakini umechanganya mambo. Mtu yeyote kama ni makini basi atajiunga na chama baada ya kupitia katiba, kanuni na miongozo ya chama hicho na kujiridhisha kuwa anakubaliana nayo, bila ya kujali kuwa katiba hiyo ni nzuri au mbaya. Na ni lazima utambue kuwa utakapoenda kinyume na katiba hiyo ni lazima utapewa adhabu ikiwa pamoja na kufukuzwa. Swali la kujiuliza ni je hawa waliofukuzwa kwenye vyama vyao walikiuka au hawakukiuka katiba, kanuni na miongozo ya vyama vyao. Kama wamekiuka, basi ni halali kabisa kwao kufukuzwa. Kinachogomba hapo ni suala la kufukuzwa uanachama wa chama ukaenda automatic na kufukuzwa ubunge.
Nadhani wewe ndiyo umechangany'a mambo. Ninachozungumzia mimi ni uingiliaji wa vyama kwenye shughuli za serikali, either kuu au za mitaa. Hii inatumiwa kama njia ya kwaadhibu wanachama wenye nafasi za uwakilishi, hawa ndiyo wanachama wnoeta hela au/na umaarufu.Kwa mfano CDM walitaka kumshughulikia Shibuda kwa kupingana na suala la sitting allowance, yaani ingawa kikatiba yao wangeweza,ingekuwa ni jambo linalokandamiza demokrasia.

Sometimes it's not right to do something just because you have the right to.
 
Hivi kwa akili yako wewe nepi, unadhani ndani ya ccm (Chaka Chua Matokeo) kuna mtu mwenye akili aliyesalia baada ya Mwalimu? Tumia akili yako kidogo uliyojaliwa halafu utuambie kama yupo.
nilitegemea sna kungekuwa na matusi na kashfa mpya, lakini hzi ni za siku zote na kwakweli nimeshazizoea sana
 
Jamani mwacheni DC watu akae kimya, nape nikijana makini sana kuliko mnavyodhania. Nape siku zote hutekeleza majukumu yake kwa kujenga chama na kuwatumikia waliomtuma. Nape natarajia anaweza kuwa rais siku moja, nape anatembea kabisa kwenye nyayo za baba yake. nape hana chuki na mtu, kisasi wala majivuno. Nape mdahalo wa jana umefunika sana. unatisha mzee Tatizo ccm haikubaliki tena, mmepoteza dira

Usimdanganye Nape, mwambie ukweli kwamba jana wenzake wamemfunika. Amejitahidi lakini kaacha maswali mengi kuliko majibu. Ni vizuri tukimsaidia ili awe katika nafasi bora zaidi ya kutetea chama chetu, kuliko kumpa maneno mazuri yasio na miguu wala kichwa. Hii ni vita kali, hilo halina ubishi, especially given the fact kwamba yeye ndiye mkuu wa kikosi cha mbele kabisa, kwa nafasi yake. Nape anaweka maslahi ya chama mbele lakini hana support ya kutosha ndani ya Chama. Mdhadhani viongozi wa juu wa Chadema wangekuwa hawapo kwenye mstari mmoja na Mnyika, ingekuwaje? Nyote mmeona kilichotokea baada ya Hamad kuwa mstari tofauti na Mtatiro, kilichomuokoa Mtatiro ni kwamba Seif alikuwa upande wake. Nape angekuwa jasiri angehimiza umuhimu wa kuvunja chama into two, hakuna mbadala wa hilo, kwani hata siasa anayoitetea ya ujamaa na kujitegemea haipo tena kwa vitendo. Hivi sasa ni siasa ya kibepari na ya kutegemea misaada ya wahisani, na pia wawekezaji ili kupata ten percent. Na ni hali hiyo ndiyo inayochangia uwepo wa uadui kati ya Nape na viongozi wenzake.
 
Chama chochote cha siasa kina uwezo wa kumfukuza uanachama mwanchama yeyote, kwa sababu zozote ambazo zitakidhi katiba ya chama hicho

Lakini, utakuwa ni upuuzi mkubwa sana kwa chama chochote cha siasa kumfukuza udiwani au ubunge, au nafasi yeyote aliyopewa mwanachama na wananchi kwa kuchaguliwa. Huu ni upuuzi mkubwa ambao nchi yetu inauendekeza. Enzi ya chama kimoja sawa, ila enzi ya vyama vingi si sawa.
Hao wote waliokuwapo kipima joto na kushabikia ufukuzwaji wa viongozi/wawakilishi wa wananchi bungeni au kwenye halmashauri mbalimbali za serikali za mitaa naona kama ni mapunguwani ambao ni bendera fuata upepo! .
Kitu kingine kinachoudhi ni ukandamizaji wa demokrasia. Iwapo mbunge ana immunity ya kumkosoa rais, waziri mkuu na serikali yote ambayo amekula kiapo kuitumikia, sioni sababu ya yeye kufukuzwa uanachama kwa kumkosoa au kuhoji ufanisi wa kiongozi wake wa chama.
Vilevile, madiwani siyo waajiriwa wa vyama bali ni watumishi wa wananchi waliowawakilisha na wamepewa ridhaa na hao wananchi na siyo vyama vya siasa. Sasa kama wameamua kufanya uamuzi ambao utaleta maendeleo kwa wananchi wanaowawakilisha, iweje vyama viingilie?
Kwani hii nchi inaongozwa na vyama au serikali?

Soby,

Kimsingi, nakubaliana na wewe, lakini hayo yanakuwa na mashiko zaidi katika nchi zilizofanikisha kujenga misingi ya uwajibikaji, uadilifu, utawala wa sheria, n.k. kama unavyoona, siasa zetu Tanzania bado zipo katika kujenga mambo haya, kwani ndio yanayotusumbua kuliko jambo lolote lingine. Tuseme mathalan Chadema au CUF imeshika uongozi wan chi na Kuna Mbunge wa Jimbo moja wapo ambae amepwaya katika sifa hizo hapo juu, tuseme kwa mfano ana rekodi ya kuiba mali ya umma, na kushirikiana na wawekezaji kuingiza nchi katika mikataba mibovu kuhusu matumizi ya rasilimali za taifa, na ni kutokana na bakshishi anazopata katika wizi na uhujumu huu wa uchumi, ndio anajijengea uwezo wa kuwanunua wapiga kura katika jimbo lake, na kushinda kwa kishindo, na kubadilika kuwa Mungu mtu kutokana na haya; Je, hapo viongozi wa chama husika wanafanya nini kukiokoa chama? Wamwache kwa sababu amechaguliwa na wananchi aliowanunua kwa khanga, sukari, sabuni na simu za mikononi, huku kitaifa amewagharimu wananchi kwa kukosesha nchi kodi, mapato n.k, huku vile vile akikigharimu chama chake in terms of kukishushia Heshima na Uhalali mbele ya umma? Nini mawazo yako katika hili.
 
Serikalini kuna sheria za kumuadhibu mtu kiongozi wa aina hiyo. Hata kama chama hakitafanya hivyo. Kwa mfano, akipewa kifungo. Kuhusu hongo kwenye uchaguzi, kuna vyombo vimeundwa kusimamia hongo n.k.
Ninachozungumzia kwa mfano ni mtemvu kuondolewa uanachama kwa sababu amepingana na Magfhufuli.
Au kuondoa uanachama madiwani wa Arusha. I'm not talking about ethics but constitutional suppression of democracy by the politico.
 
Mada hizi japo tamu kuzisikiliza lakini zaweza kuwa kama mipasho, au panzi tunaogombana kwa faida ya kunguru. wanaotoa mfano wa wanachama kufukuzwa wakati wa Mh. mwl. Nyerere, yawapasa wajue kuwa sio kila alichofanya mwl. Nyerere ni sawa. Kwa falsafa zake mwenyewe kwenye vitabu vyake, tunaiona sababu ya kurudishwa vyama vingi ili kukuza demokrasia taifani japo yeye aliviahilisha awali lakini alikubali virudishwe, je sababu hii hatuioni ndiyo ile ile inayowafanya watu wadai kuhojiwa kwa kila jambo? hata wakati wa miiko watu walihojiwa, japo haikuwa mbele ya vyombo vya sheria kwavile miiko haiundi sheria, ila vibaya ingawa zote ni sehemu ya desturi ya jamii yoyote duniani. Nashuri wananchi na vyama vyetu vya siasa tujikague tumekosea wapi katika kuituma serikali yetu na viongozi wetu, pia uimara wa uongozi ndani ya vyama vyetu, kufukuzana si suruhisho tunaongeza nyufa ndani ya taifa letu. Sasa tumesukumwa kwenye kufanya propaganda badala ya siasa, wakifanikiwa kutufikisha kwenye propaganda za visasi tutapiganishwa wenyewe. Vijana na wazee wenye vyeo mbali mbali mnaotjwa kisiasa amkeni, vinginevyo andaeni kikao nami niwadokeze jambo kwani tunaelekea shimoni hata kama mnasikia harufu ya mafanikio yenu si sahihi harufu inawadanganya kaeni mezani, kosa letu sote ni kutojitambua na kukosa siasa ya kitaifa kisa hatuna elimu ya uzalendo, hii ni elimu ya uraia tu haitukomboi kifikra. mimi mgunduzi wa falsafa yetu asilia.
 
tusome histria ya siasa, je mtindo huu mpya? Utatusaidia kutufikisha kwenye lengo mama la uhuru wetu linalozuia tusinyowe, tusinyanyaswe tusitawaliwe tena na kadhalika. Kisha tuone kuwa inafaa mtindo huu uendelee au hapana,tusisifie hoja tuu.
 
Tathimini za baadhi ya members humu zimezingatia zaidi mapenzi kwa mtu binafsi na ushabiki katika vyama. Mdahalo ulilenga zaidi kubadilishana maoni na udhibiti wa nidhamu katika vyama.Nidhahiri hapa majibu hayawezi kufanana kwani asili ya mjadala ilijikita zaidi katika Katiba za vyama ambapo kwa ujumla hazifanani, isipokuwa Katiba mama ambayo ni moja. Ukigusa utendaji wa chama chochote lazima angalizo la katiba yake litizamwe. Kwa msingi huu maoni lazima yatatofautiana katika concept na perception.

Napata shida kama ndio uwezo wetu wa ku-view hauzingatii independent argument na kutafakari uhalali pamoja na applicability yake zaidi ya kuingia na "malice aforethought" kwamba ni ushindani na fulani lazima ashinde kwa kumzidi fulani. hapa mantiki ya hoja lazima ilakuwa mfu. Hili nililitegemea kwani watu waliishaanza kujadili hapa mara baada ya Mnyika kuteuliwa nafasi ya uenezi kuwa Mnyika na Nape nani zaidi.
 
Tathimini za baadhi ya members humu zimezingatia zaidi mapenzi kwa mtu binafsi na ushabiki katika vyama. Mdahalo ulilenga zaidi kubadilishana maoni na udhibiti wa nidhamu katika vyama.Nidhahiri hapa majibu hayawezi kufanana kwani asili ya mjadala ilijikita zaidi katika Katiba za vyama ambapo kwa ujumla hazifanani, isipokuwa Katiba mama ambayo ni moja. Ukigusa utendaji wa chama chochote lazima angalizo la katiba yake litizamwe. Kwa msingi huu maoni lazima yatatofautiana katika concept na perception.

Napata shida kama ndio uwezo wetu wa ku-view hauzingatii independent argument na kutafakari uhalali pamoja na applicability yake zaidi ya kuingia na "malice aforethought" kwamba ni ushindani na fulani lazima ashinde kwa kumzidi fulani. hapa mantiki ya hoja lazima ilakuwa mfu. Hili nililitegemea kwani watu waliishaanza kujadili hapa mara baada ya Mnyika kuteuliwa nafasi ya uenezi kuwa Mnyika na Nape nani zaidi.

Hizi ni zama za siasa za ushindani, na mada ile ndio inayolisumbua taifa, na matokeo ya siasa hizi zita influence sana behaviour ya wapiga kura, 2015. Una hoja, lakini ingekuwa na nguvu zaidi kama mada ile ilikuwa inalenga kwa mfano 'ruzuku' za vyama vya siasa.
 
Back
Top Bottom