Mujumba
JF-Expert Member
- Jan 20, 2011
- 853
- 306
DHANA ya maendeleo kwa wananchi ni moja, kwa maana kuwa maendeleo yanayopiganiwa na serikali kwa wananchi wake kupitia chama tawala, CCM ni sawasawa na maendeleo yanayopiganiwa na vyama vya upinzani katika majimbo yaliyo chini yao.
Hii haina maana kuwa serikali inawajibika kuleta maendeleo katika majimbo ambayo yaliyo chini ya CCM tu, ambacho ndicho kilichounda serikali, bali inawajibika kuhakikisha kuwa wananchi wote, bila kuangalia kuwa ni wa jimbo gani na linaongozwa na chama gani, wanapata fursa sawa za maendeleo.
Hivi wananchi waelewe nini pale serikali ambayo ndiyo yenye jukumu la kuhakikisha kuwa wananchi wananeemeka kutokana na rasilimali walizonazo, inapotaka kuwaletea maendeleo, inakumbana na vikwazo kutoka kwa baadhi ya wabunge wa upinzani, hususan wa chama kikuu cha upinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Hili halina ubishi, kwani mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema, John Mnyika, amenukuliwa katika vyombo mbalimbali vya habari, kwanza akipinga utaratibu wa kuwaondoa wapiga debe katika kituo cha kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha
Ubungo, uliowekwa na serikali ili kuwaondolea wananchi usumbufu.
Serikali ilichukua uamuzi huo, ikizingatia ukweli ulio wazi kuwa wananchi wanapata taabu wanapofika katika kituo hicho, kwanza ya kuibiwa na wapiga debe hao ambao ni wezi wakubwa wa pesa na mali zingine.
Pili, wapigadebe hao huwaibia wananchi kwa kuwatajia nauli, ambayo siyo sahihi. Mara nyingi wanazidisha na kile kilichozidi, wanachukua kwa makubaliano na wenye mabasi. Huu ni ufisadi wa chini chini na usiofaa kuvumiliwa.
Serikali ilipoamua kuwaondoa wapiga debe ili kumaliza tatizo hilo, Mnyika alipinga kwa nguvu zote utaratibu huo, akidai kuwa hiyo ndiyo ajira yao, hivyo waachwe. Hii inaonyesha kuwa Mnyika anataka maendeleo yanayopatikana kwa dhuluma na manyanyaso makubwa. Hiyo haikubaliki!.
Kama hiyo haitoshi, kwa kuzingatia sheria za barabarani na umuhimu wa kupanua barabara za jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya mabasi yaendayo kasi, ilitoa muda kwa watu waliojenga katika hifadhi ya barabara ya Morogoro eneo la Urafiki, kuondoa vibanda vyao.
Muda uliotolewa uliisha na hatua iliyofuatia ni kuvunja kwa nguvu vibanda hivyo, baada ya
wafanyabiashara hao kukaidi amri ya serikali. Mnyika akijua kuwa kilichofanywa na serikali ni utekelezaji wa sheria za ujenzi na barabarani; na hata kama yeye angekuwa waziri wa ujenzi angechukua hatua hizohizo, alilaani hatua hiyo.
Aliwaambia wananchi katika mikutano yake ya hadhara katika jimbo lake, kuwa kilichofanywa
na serikali ni makoa makubwa. Sijui Mnyika anataka maendeleo ya aina gani kwa wananchi wa Tanzania. Ni sahihi nikisema kuwa mbunge huyo, sasa anapinga wananchi hao wasiletewe maendeleo hayo.
Wananchi wa Ubungo walimchagua kwa kishindo, wakiamini atashirikiana na serikali
kuwaletea maendeleo, hasa katika kutatua kero kubwa za wananchi ambazo ni maji, barabara
na usafi, lakini imekuwa kinyume.
Mnyika unataka maendeleo ya aina gani Ubungo? Mbona ahadi zako hujatekeleza hadi moja hadi sasa? Umengangania tu mambo makubwa ya kitaifa, kama vile Katiba Mpya, huku ukisahau kero za msingi za wapiga kura wako wa Ubungo, ulizoahidi utatatua haraka.
Kwa mfano, Jimbo lako la Ubungo ni chafu kupindukia tembelea Manzese, Ubungo,
Mabibo na Tandale, uone harufu kali na takataka vilivyosambaa kila mahali. Uchafu kila
mahali!
Mabibo kuna uvundo na harufu kali ya maji machafu ya mabwawa ya DAWASA. Harufu hii kali, inaathiri afya za wapiga kura wako mchana na usiku. DAWASA hawaweki dawa katika mabwawa hayo kwa muda mrefu sasa.
Mbona hufuatilii hili, wakati afya za wapiga kura wako zikiangamia? Pia, unatakiwa uwe na programu ya kusafisha jimbo lako. Lakini, hili nalo inaonekana siyo kipaumbele chako. Aidha,
maji bado kero kubwa Kimara, Ubungo na Mbezi, lakini pia huonekani kufuatilia, wala kuwa tayari kutatua kero hii sugu.
Kumbuka kuwa hatua ya kuvunja nyumba na mabanda ya biashara Ubungo, ni hatua moja
katika safari ndefu ya kuwaneemesha wananchi, kwa kuondoa kero ya foleni, ambayo jimbo lako ni mhanga namba moja wa foleni hizo.
Kwa mtazamo mmoja, mambo yote hayo yanayofanywa na Mnyika, yanalenga kujinufaisha
kisiasa; na si kuwajali wananchi wa Ubungo, jambo ambalo ni hatari kwa Taifa. Ili
kuthibitisha mtazamo huo wa kujinufaisha kisiasa, badala ya kujali maisha na maslahi ya
wananchi, hebu angalia hili la Mwanza.
Kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Meya jijini Mwanza, Serikali mkoani humo iliwaamuru
wafanyabiashara ndogo (machinga), waondoke katika maeneo yasiyoruhusiwa kufanya
biashara ; na kwenda katika maeneo walikoelekezwa.
Cha kushangaza, wabunge wa majimbo ya Nyamagana na Ilemela mkoa wa Mwanza kupitia Chadema, walikataa amri hiyo ya serikali; na walitaka machinga hao wasiondoke, hali iliyosababisha uvunjifu wa amani, pale polisi walipoingilia kati kutaka kuwaondoa.
Hii inasikitisha, kwa sababu wabunge hao hawakutoa ushirikiano kwa serikali, kuwatafutia mahali wanapoweza kufanya biashara zao vizuri ili waondoke katika eneo hilo, ambalo haliruhusiwi kufanyia biashara.
Lakini, baada ya kufanyika uchaguzi wa Meya na Chadema kushinda, walianza kuwaondoa machinga hao. Kwa nini awali, kabla ya kufanya uchaguzi wa Meya, wabunge hao wa Ilemela na Nyamagana, walikataa machinga hao wasiondolewe, lakini baada ya uchaguzi wa Meya na
baada ya kushinda, waliamua kuwalazimisha waondoke?
Ni dhahiri kuwa walikataa kwa maslahi yao ya kisiasa, lakini sio kwa maslahi ya wananchi. Kama ilikuwa ni kwa maslahi ya wananchi, iweje baada ya wao kukamata halmashauri ya jiji, waamue kuwaondoa?
Nilisema awali kuwa tabia hii imejikita kwa baadhi ya wabunge wa Chama hicho, kwa kuwa sio wote wenye tabia hiyo. Wapo baadhi ya wabunge, ambao wanashirikiana vizuri na serikali, mfano ni Mbunge wa Mpanda Mjini mkoa wa Rukwa kupitia Chadema, Said Arfi.
Arfi amesifiwa na viongozi mbalimbali wa serikali, kuwa anatoa ushirikiano wa hali ya juu
kwa seriikali. Baadhi ya waliompongeza mbunge huyo wa Chadema ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Daniel ole Njoolay.
Imeandikwa na Selemani Nzaro; Tarehe: 21st March 2011 @ 09:48
Hii haina maana kuwa serikali inawajibika kuleta maendeleo katika majimbo ambayo yaliyo chini ya CCM tu, ambacho ndicho kilichounda serikali, bali inawajibika kuhakikisha kuwa wananchi wote, bila kuangalia kuwa ni wa jimbo gani na linaongozwa na chama gani, wanapata fursa sawa za maendeleo.
Hivi wananchi waelewe nini pale serikali ambayo ndiyo yenye jukumu la kuhakikisha kuwa wananchi wananeemeka kutokana na rasilimali walizonazo, inapotaka kuwaletea maendeleo, inakumbana na vikwazo kutoka kwa baadhi ya wabunge wa upinzani, hususan wa chama kikuu cha upinzani, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).
Hili halina ubishi, kwani mbunge wa Ubungo kwa tiketi ya Chadema, John Mnyika, amenukuliwa katika vyombo mbalimbali vya habari, kwanza akipinga utaratibu wa kuwaondoa wapiga debe katika kituo cha kituo kikuu cha mabasi yaendayo mikoani cha
Ubungo, uliowekwa na serikali ili kuwaondolea wananchi usumbufu.
Serikali ilichukua uamuzi huo, ikizingatia ukweli ulio wazi kuwa wananchi wanapata taabu wanapofika katika kituo hicho, kwanza ya kuibiwa na wapiga debe hao ambao ni wezi wakubwa wa pesa na mali zingine.
Pili, wapigadebe hao huwaibia wananchi kwa kuwatajia nauli, ambayo siyo sahihi. Mara nyingi wanazidisha na kile kilichozidi, wanachukua kwa makubaliano na wenye mabasi. Huu ni ufisadi wa chini chini na usiofaa kuvumiliwa.
Serikali ilipoamua kuwaondoa wapiga debe ili kumaliza tatizo hilo, Mnyika alipinga kwa nguvu zote utaratibu huo, akidai kuwa hiyo ndiyo ajira yao, hivyo waachwe. Hii inaonyesha kuwa Mnyika anataka maendeleo yanayopatikana kwa dhuluma na manyanyaso makubwa. Hiyo haikubaliki!.
Kama hiyo haitoshi, kwa kuzingatia sheria za barabarani na umuhimu wa kupanua barabara za jiji la Dar es Salaam kwa ajili ya mabasi yaendayo kasi, ilitoa muda kwa watu waliojenga katika hifadhi ya barabara ya Morogoro eneo la Urafiki, kuondoa vibanda vyao.
Muda uliotolewa uliisha na hatua iliyofuatia ni kuvunja kwa nguvu vibanda hivyo, baada ya
wafanyabiashara hao kukaidi amri ya serikali. Mnyika akijua kuwa kilichofanywa na serikali ni utekelezaji wa sheria za ujenzi na barabarani; na hata kama yeye angekuwa waziri wa ujenzi angechukua hatua hizohizo, alilaani hatua hiyo.
Aliwaambia wananchi katika mikutano yake ya hadhara katika jimbo lake, kuwa kilichofanywa
na serikali ni makoa makubwa. Sijui Mnyika anataka maendeleo ya aina gani kwa wananchi wa Tanzania. Ni sahihi nikisema kuwa mbunge huyo, sasa anapinga wananchi hao wasiletewe maendeleo hayo.
Wananchi wa Ubungo walimchagua kwa kishindo, wakiamini atashirikiana na serikali
kuwaletea maendeleo, hasa katika kutatua kero kubwa za wananchi ambazo ni maji, barabara
na usafi, lakini imekuwa kinyume.
Mnyika unataka maendeleo ya aina gani Ubungo? Mbona ahadi zako hujatekeleza hadi moja hadi sasa? Umengangania tu mambo makubwa ya kitaifa, kama vile Katiba Mpya, huku ukisahau kero za msingi za wapiga kura wako wa Ubungo, ulizoahidi utatatua haraka.
Kwa mfano, Jimbo lako la Ubungo ni chafu kupindukia tembelea Manzese, Ubungo,
Mabibo na Tandale, uone harufu kali na takataka vilivyosambaa kila mahali. Uchafu kila
mahali!
Mabibo kuna uvundo na harufu kali ya maji machafu ya mabwawa ya DAWASA. Harufu hii kali, inaathiri afya za wapiga kura wako mchana na usiku. DAWASA hawaweki dawa katika mabwawa hayo kwa muda mrefu sasa.
Mbona hufuatilii hili, wakati afya za wapiga kura wako zikiangamia? Pia, unatakiwa uwe na programu ya kusafisha jimbo lako. Lakini, hili nalo inaonekana siyo kipaumbele chako. Aidha,
maji bado kero kubwa Kimara, Ubungo na Mbezi, lakini pia huonekani kufuatilia, wala kuwa tayari kutatua kero hii sugu.
Kumbuka kuwa hatua ya kuvunja nyumba na mabanda ya biashara Ubungo, ni hatua moja
katika safari ndefu ya kuwaneemesha wananchi, kwa kuondoa kero ya foleni, ambayo jimbo lako ni mhanga namba moja wa foleni hizo.
Kwa mtazamo mmoja, mambo yote hayo yanayofanywa na Mnyika, yanalenga kujinufaisha
kisiasa; na si kuwajali wananchi wa Ubungo, jambo ambalo ni hatari kwa Taifa. Ili
kuthibitisha mtazamo huo wa kujinufaisha kisiasa, badala ya kujali maisha na maslahi ya
wananchi, hebu angalia hili la Mwanza.
Kabla ya kufanyika kwa uchaguzi wa Meya jijini Mwanza, Serikali mkoani humo iliwaamuru
wafanyabiashara ndogo (machinga), waondoke katika maeneo yasiyoruhusiwa kufanya
biashara ; na kwenda katika maeneo walikoelekezwa.
Cha kushangaza, wabunge wa majimbo ya Nyamagana na Ilemela mkoa wa Mwanza kupitia Chadema, walikataa amri hiyo ya serikali; na walitaka machinga hao wasiondoke, hali iliyosababisha uvunjifu wa amani, pale polisi walipoingilia kati kutaka kuwaondoa.
Hii inasikitisha, kwa sababu wabunge hao hawakutoa ushirikiano kwa serikali, kuwatafutia mahali wanapoweza kufanya biashara zao vizuri ili waondoke katika eneo hilo, ambalo haliruhusiwi kufanyia biashara.
Lakini, baada ya kufanyika uchaguzi wa Meya na Chadema kushinda, walianza kuwaondoa machinga hao. Kwa nini awali, kabla ya kufanya uchaguzi wa Meya, wabunge hao wa Ilemela na Nyamagana, walikataa machinga hao wasiondolewe, lakini baada ya uchaguzi wa Meya na
baada ya kushinda, waliamua kuwalazimisha waondoke?
Ni dhahiri kuwa walikataa kwa maslahi yao ya kisiasa, lakini sio kwa maslahi ya wananchi. Kama ilikuwa ni kwa maslahi ya wananchi, iweje baada ya wao kukamata halmashauri ya jiji, waamue kuwaondoa?
Nilisema awali kuwa tabia hii imejikita kwa baadhi ya wabunge wa Chama hicho, kwa kuwa sio wote wenye tabia hiyo. Wapo baadhi ya wabunge, ambao wanashirikiana vizuri na serikali, mfano ni Mbunge wa Mpanda Mjini mkoa wa Rukwa kupitia Chadema, Said Arfi.
Arfi amesifiwa na viongozi mbalimbali wa serikali, kuwa anatoa ushirikiano wa hali ya juu
kwa seriikali. Baadhi ya waliompongeza mbunge huyo wa Chadema ni Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Daniel ole Njoolay.
Imeandikwa na Selemani Nzaro; Tarehe: 21st March 2011 @ 09:48