Mnyika, Lissu wameianza kazi waliyotumwa

Nadhani baadi yetu tuko kwenye TV zetu tukiangalia kupigwa kura za kumthibitisha Mizengo Pinda kama waziri mkuu.

Ukiacha swali zuri la Mh. JOhn Mnyika kuhusu usiri wa upigaji kura swali kali lilikuwa la Tundu Lissu ambaye alisoma kanuni za bunge kifungu 53 (6a) na (6c).

Amevisoma kwamba hasa kile (6a) kinasema kwamba hoja ikiletwa na serikali ni lazima kwanza ijadiliwe na bunge kama haikupitia kwenye kamati. Ama kiongozi wa upinzani anahusika katika mjadala.

Sasa hoja hii ya umpitisha Waziri mkuu haikupitia utaratibu huo wa vifungu hivi.

Hivyo Mhe. Tundu Lissu alichofanya ni kumuomba Mh. Spika mwongozo kuhusu hilo.

Niaona swali hilo ni kali nikasubiri kuona Mama Makinda akituthibitishia u-genious wake kwenye kanuni za bunge.

Badala yake alichofanya Makinda ni kwanza hakukana ukweli wa hoja ya Tundu Lissu na badala yake akaishia kusema "Jamani hapa tulipofikia hatuhitaji kusomeana tena Kanuni, tuendelee na utaratibu wa kuhesabu kura"

Umeona ambavyo bunge litakavyompelekesha huyu mama yetu akitafunwa na kanuni zilezile ambazo ni msahafu wao.

Ndiyo maana kuna thread niliomba kama kuna mwenye kanuni za bunge atudondoshee tuzichambue na kuhesabu point moja hadi nyingine ya ukiukaji na tuzitungie kitabu cha ukiukaji wa kanuni za bunge ifikapo 2015

Niko naednelea kupata live broadcast.

Ndicho nilichotegemea kutoka kwa spika wetu, UBABE ni mwingi kuliko kufuata msingi wa HOJA! Pia hicho ndicho alichotumwa kukifanya bungeni na chama chake. Shame on them!
 
Mmemwona Spika akitafuta majibu kwa Spika aliopita!!!!!!:yield::yield::yield::yield::yield::yield:
 
Jumla ya kura 328
Zilizoharibika 2
Hapana 49
Ndiyo 277

Pinda waziri mkuu mteule. Kesho anaapishwa Ikulu ya Chamwino
 
Ahahahahahaaaah homeboy bwana eti Anawashutumu chadema kwa kumnunia, lakini kaahidi kufanya kazi na wabunge wote. Lakini kakiri kuwa kipindi hiki kazi ipo!!
 
Kwaio 84.5% ya wabunge wanaona Pinda kataeuliwa kihalali? Parliament inakua kama circus show! Lakini tamati iko karibu!
 
pinda kaliona hili kasema mwaka huu ipo kazi kaisema CHADEMA wazi wazi hanaiogopa bana
 
Kwahiyo oja ya lisu imekufa au?makinda tayari ameshaanza kuzipiga chini oja za wapinzani.
 
Pinda ameanza hotuba ya shukurani. Na katika aya ya pili tu amekiri jinsi CHADEMA walivyomkataa na hata pale wapigapo mikono ya makofi (madeski) upande ule wa CHADEMA uko kimya.

Akasema hiyo ni "viashiria tu kwamba huko tuendako kweli iko kazi".

Lakini ameahidi hatamchukia Mbowe na atatenda haki kwa kila mbunge.

TV yangu iko seating room wakati laptop yangu iko chumbani. Narudi kumsikiliza.
 
Anatoa matumaini kwa wakulima, wafugaji na wavuvi! kwa ajili ya kuleta maendeleo kwa nchi yetu.
 
Sijui kwanini kila mtu anajipendekeza kwa mzee 6? Kama walijua yeye ndiye anayeijua vizuri hiyo kazi kwa nini hawakumpa uspika?
 
Huyu mama kweli hamna kitu!hongera mpiganaji lissu,tunatarajia makubwa zaidi kutoka kwako!!
 
Back
Top Bottom