Nikupateje
JF-Expert Member
- Dec 22, 2009
- 1,334
- 988
Nadhani baadi yetu tuko kwenye TV zetu tukiangalia kupigwa kura za kumthibitisha Mizengo Pinda kama waziri mkuu.
Ukiacha swali zuri la Mh. JOhn Mnyika kuhusu usiri wa upigaji kura swali kali lilikuwa la Tundu Lissu ambaye alisoma kanuni za bunge kifungu 53 (6a) na (6c).
Amevisoma kwamba hasa kile (6a) kinasema kwamba hoja ikiletwa na serikali ni lazima kwanza ijadiliwe na bunge kama haikupitia kwenye kamati. Ama kiongozi wa upinzani anahusika katika mjadala.
Sasa hoja hii ya umpitisha Waziri mkuu haikupitia utaratibu huo wa vifungu hivi.
Hivyo Mhe. Tundu Lissu alichofanya ni kumuomba Mh. Spika mwongozo kuhusu hilo.
Niaona swali hilo ni kali nikasubiri kuona Mama Makinda akituthibitishia u-genious wake kwenye kanuni za bunge.
Badala yake alichofanya Makinda ni kwanza hakukana ukweli wa hoja ya Tundu Lissu na badala yake akaishia kusema "Jamani hapa tulipofikia hatuhitaji kusomeana tena Kanuni, tuendelee na utaratibu wa kuhesabu kura"
Umeona ambavyo bunge litakavyompelekesha huyu mama yetu akitafunwa na kanuni zilezile ambazo ni msahafu wao.
Ndiyo maana kuna thread niliomba kama kuna mwenye kanuni za bunge atudondoshee tuzichambue na kuhesabu point moja hadi nyingine ya ukiukaji na tuzitungie kitabu cha ukiukaji wa kanuni za bunge ifikapo 2015
Niko naednelea kupata live broadcast.
Ukiacha swali zuri la Mh. JOhn Mnyika kuhusu usiri wa upigaji kura swali kali lilikuwa la Tundu Lissu ambaye alisoma kanuni za bunge kifungu 53 (6a) na (6c).
Amevisoma kwamba hasa kile (6a) kinasema kwamba hoja ikiletwa na serikali ni lazima kwanza ijadiliwe na bunge kama haikupitia kwenye kamati. Ama kiongozi wa upinzani anahusika katika mjadala.
Sasa hoja hii ya umpitisha Waziri mkuu haikupitia utaratibu huo wa vifungu hivi.
Hivyo Mhe. Tundu Lissu alichofanya ni kumuomba Mh. Spika mwongozo kuhusu hilo.
Niaona swali hilo ni kali nikasubiri kuona Mama Makinda akituthibitishia u-genious wake kwenye kanuni za bunge.
Badala yake alichofanya Makinda ni kwanza hakukana ukweli wa hoja ya Tundu Lissu na badala yake akaishia kusema "Jamani hapa tulipofikia hatuhitaji kusomeana tena Kanuni, tuendelee na utaratibu wa kuhesabu kura"
Umeona ambavyo bunge litakavyompelekesha huyu mama yetu akitafunwa na kanuni zilezile ambazo ni msahafu wao.
Ndiyo maana kuna thread niliomba kama kuna mwenye kanuni za bunge atudondoshee tuzichambue na kuhesabu point moja hadi nyingine ya ukiukaji na tuzitungie kitabu cha ukiukaji wa kanuni za bunge ifikapo 2015
Niko naednelea kupata live broadcast.