Mnyika, Lissu wameianza kazi waliyotumwa

Nadhani baadi yetu tuko kwenye TV zetu tukiangalia kupigwa kura za kumthibitisha Mizengo Pinda kama waziri mkuu.

Ukiacha swali zuri la Mh. JOhn Mnyika kuhusu usiri wa upigaji kura swali kali lilikuwa la Tundu Lissu ambaye alisoma kanuni za bunge kifungu 53 (6a) na (6c).

Amevisoma kwamba hasa kile (6a) kinasema kwamba hoja ikiletwa na serikali ni lazima kwanza ijadiliwe na bunge kama haikupitia kwenye kamati. Ama kiongozi wa upinzani anahusika katika mjadala.

Sasa hoja hii ya umpitisha Waziri mkuu haikupitia utaratibu huo wa vifungu hivi.

Hivyo Mhe. Tundu Lissu alichofanya ni kumuomba Mh. Spika mwongozo kuhusu hilo.

Niaona swali hilo ni kali nikasubiri kuona Mama Makinda akituthibitishia u-genious wake kwenye kanuni za bunge.

Badala yake alichofanya Makinda ni kwanza hakukana ukweli wa hoja ya Tundu Lissu na badala yake akaishia kusema "Jamani hapa tulipofikia hatuhitaji kusomeana tena Kanuni, tuendelee na utaratibu wa kuhesabu kura"

Umeona ambavyo bunge litakavyompelekesha huyu mama yetu akitafunwa na kanuni zilezile ambazo ni msahafu wao.

Ndiyo maana kuna thread niliomba kama kuna mwenye kanuni za bunge atudondoshee tuzichambue na kuhesabu point moja hadi nyingine ya ukiukaji na tuzitungie kitabu cha ukiukaji wa kanuni za bunge ifikapo 2015

Niko naednelea kupata live broadcast.
 
jamani muwe mnatudokeza kidogo sisi tulio nje ya Tz. Huyo mama lazima ajutie uamuzi wake wa kugombea uspika kipindi hiki ambacho watu wameshafumbuka macho, hakuna kuzibwa midomo tena.
kama uko nje unaweza download player kutoka tv africa utapata itv live na eatv.
Ila itabidi uwachangie paundi5.5 kwa mwezi mambo yatakuwa mswano.
kama hauna paypal unaweza kudownload na kuinstall ntakusaidia login password yangu kwa muda,ila baada ya siku chache ita-expire.
Endelea!
 
Unajua ata JK alisema kumchagua Lissu ubunge ni kheri wamchague Slaa kuwa raisi.
JK alijua Lissu ni jembe tena chapa Rungwe na kamatrekta ni Massey Fergusson tairi kubwa nyuma na mbele MF 350
 
Tafadhali endeleeni kutupa uhondo. Huku mashenzini mbeya tannesco wameamua kuuchukua umeme wao - kata rudisha kata rudisha!! Ndo wawekezaji waje nchi hii!!
 
Duhh! sasa huyo spika hajui mwongozo wala vifungu vya sheria.... naona bunge hili litamwendea pabaya. Kwanini asiombe ushauri wa mwanasheria mkuu wa serikali .... analipwa kwa shughuli hizo!
 
Aanza kwa kuukosoa uchaguzi wa waziri mkuu kwani karatasi zilikuwa na serial numbers kitu ambacho kingesababisha aliyepiga kura kujulikana na hivyo dhana nzima ya USIRI kuondoka
Hivi hawa wabunge wa Sisiem wao hawaoni mapungufu ambayo wenzao wa upinzani wanayaona, maana hawakosoi hata kidogo ingawa kuna makosa ya waziwazi.
 
Hayo ni majembe mapya lazima yanatafuta sehemu za kulima lazima spika awe makini sana na atajikuta nakosolewa sana mpaka ataona ana pwaya.
 
dah noma yani nimetune itv muda nna bahati kweli nikaanza na Mnyika.Guys are confident and flowing with vigour.
Hapa kazi ipo!..I am starting to love this Tundu Lisu guy!

Kwa taarifa yako TINDU LISU ni > / = Slaa
 
Mnamwangalia spika anavyokula mkoba? yaani yuko busy na vitabu nadhani anasoma vifungu alivyoongea TIndU lissu ili aweze kutetea hoja

kazi ipo hili jumba la safari hii labda awe anawabania hawa jamaa la sivyo watampa vichomi sana tu:smile-big:
 
Spika yupo busy anajisomea huku akipatiwa msaada ama kweli hadi bunge liishe itabidi awe na mawani yenye kioo kinene mno
 
Tafadhali endeleeni kutupa uhondo. Huku mashenzini mbeya tannesco wameamua kuuchukua umeme wao - kata rudisha kata rudisha!! Ndo wawekezaji waje nchi hii!!
Poleni sana lakini mtapata taarifa ya kila kitu kinachoendelea kupitia hapahapa JF.
 
Wabunge wa CCM wao wanaona kila kitu ambacho kinafanywa na wana CCM ni sawa wala hawaoni ulazima wa kuhoji so Mkuu usishangae kuona kuwa wako kimya. Mfano Maji marefu unategemea angeweza kuliona hilo???????

Hivi hawa wabunge wa Sisiem wao hawaoni mapungufu ambayo wenzao wa upinzani wanayaona, maana hawakosoi hata kidogo ingawa kuna makosa ya waziwazi.
 
Back
Top Bottom