Henry Kilewo
JF-Expert Member
- Feb 9, 2010
- 899
- 1,084
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Nawasalimu nyote.
Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Kanda maalum ya Dar es salaam, kinapenda kuwajulisha yale yote yaliyojiri kwenye kampeni cha uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya VIJIBWENI iliyomo jimbo la KIGAMBONI ndani ya wilaya ya Temeke.
Zikiwa zimesalia siku mbili za mikutano ya hadhara ya kampeni tunapenda kuwapongeza wakazi wa kata ya vijibweni kwa kuonyesha ushirikiano wa hali ya juu kwa kipindi chote tulichokuwa tunafanya kampeni, wakazi hawa wametupokea vizuri sana na kuonyesha ushirikiano wakutosha na wameonyesha nia kubwa sana ya kuichagua CHADEMA Kupitia kwa Diwani wake Bwana Isaya Mwita.
Vile vile tunapenda kuwaomba ushirikiano wao wauendeleze katika kipindi hiki kifupi kilichosalia cha uchaguzi siku ya Tarehe 01/04/2012, Kwani tumekuwa tukifanya nao kampeni katika mazingira magumu sana ya manyanyaso na vitisho kutoka chama Tawala CCM pamoja na vyombo vya usalama vya taifa hili. Moja yavitisho hivyo ni kauli za mara kwa mara zinazotolewa kwenye mikutano ya hadhara ya chama hicho Tawala ya kuwa, Hata kama Chadema ikishinda CCM itatangazwa washindi then CHADEMA waende mahakamani kudai haki yao. Kutokana na kauli hizo za kufilisika kisiasa, CHADEMA cha makini chenye mgombea makini na hitaji la wakazi wa vijibweni, tunapenda kuwaondoa hofu wale wote wenye nia ya mabadiliko kutokatishwa tamaa na kauli hizo za kijinga. Vile vile Tunawahakikishia ulinzi wa kura zao watakazo piga kuwa zitalindwa kwa hali na mali bila kujali vitisho vya chama hicho.
Kampeni zetu za uchaguzi zitafungwa na Mwenyekiti wa kanda hii ya Dar es salaam ambaye ni Mbunge wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania na muwakilishi wa wakazi wa ubungo Mh. John Mnyika Tarehe 31/03/2012. Vile vile mnyika ameshindwa kwenda Arumeru kutokana na Kesi ya uchaguzi Inayomkabili, Nguvu zote amezielekeza kwasasa kwenye uchaguzi huu mdogo wa udiwani kutokana na ukaribu wa eneo. Tunawaomba wakazi wote wa vijibweni na wale wote wanaopenda mabadiliko kujiunga na sisi siku ya kesho kwenye kufunga kampeni zetu, ambazo zimekuwa na mafanikio makubwa kuliko chama kingine kinachoshiriki uchaguzi huwo bila kujali itikadi za vyama vyao, waje wasikilize sera na siyo matusi na kejeli, kitu ambacho wamekwisha kionyesha na kuvidharau vyama hivyo.
Vile vile tunapenda kuwaambia wananchi kuwa kwasasa taifa linamsiba mkubwa linahitaji mabadiliko kwa haraka sana na harakati hizo za mabadiliko ni lazima zianze sasa. Katika uchaguzi huu wa udiwani CHADEMA tutashinda kwa zaidi ya 82%. Tunawatakia uchaguzi mwema wenzetu wa Arumeru na kwenye kata mbalimbali zinazorudia uchaguzi mdogo.
AHSANTENI KWA USHIRIKIANO NA ENDELEENI KUSIMAMIA UKWELI BILA KUJALI ITIKADI ZA DINI ZENU, KABILA ZENU, HAKIKA UKWELI UTASHINDI DHULUMA, UKWELI UTASHINDA UONGO, UKWELI HAUJAWAHI KUSHINDWA.
Imetolewa leo Tarehe 30/03/2012 na..
HENRY J KILEWO
KATIBU WA KANDA MAALUM YA DSM
MRATIBU MKUU WA UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI (VIJIBWENI) KIGAMBONI/DSM.
SIMU: 0714 225960
Nawasalimu nyote.
Chama cha Demokrasia na maendeleo (CHADEMA) Kanda maalum ya Dar es salaam, kinapenda kuwajulisha yale yote yaliyojiri kwenye kampeni cha uchaguzi mdogo wa udiwani katika kata ya VIJIBWENI iliyomo jimbo la KIGAMBONI ndani ya wilaya ya Temeke.
Zikiwa zimesalia siku mbili za mikutano ya hadhara ya kampeni tunapenda kuwapongeza wakazi wa kata ya vijibweni kwa kuonyesha ushirikiano wa hali ya juu kwa kipindi chote tulichokuwa tunafanya kampeni, wakazi hawa wametupokea vizuri sana na kuonyesha ushirikiano wakutosha na wameonyesha nia kubwa sana ya kuichagua CHADEMA Kupitia kwa Diwani wake Bwana Isaya Mwita.
Vile vile tunapenda kuwaomba ushirikiano wao wauendeleze katika kipindi hiki kifupi kilichosalia cha uchaguzi siku ya Tarehe 01/04/2012, Kwani tumekuwa tukifanya nao kampeni katika mazingira magumu sana ya manyanyaso na vitisho kutoka chama Tawala CCM pamoja na vyombo vya usalama vya taifa hili. Moja yavitisho hivyo ni kauli za mara kwa mara zinazotolewa kwenye mikutano ya hadhara ya chama hicho Tawala ya kuwa, Hata kama Chadema ikishinda CCM itatangazwa washindi then CHADEMA waende mahakamani kudai haki yao. Kutokana na kauli hizo za kufilisika kisiasa, CHADEMA cha makini chenye mgombea makini na hitaji la wakazi wa vijibweni, tunapenda kuwaondoa hofu wale wote wenye nia ya mabadiliko kutokatishwa tamaa na kauli hizo za kijinga. Vile vile Tunawahakikishia ulinzi wa kura zao watakazo piga kuwa zitalindwa kwa hali na mali bila kujali vitisho vya chama hicho.
Kampeni zetu za uchaguzi zitafungwa na Mwenyekiti wa kanda hii ya Dar es salaam ambaye ni Mbunge wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania na muwakilishi wa wakazi wa ubungo Mh. John Mnyika Tarehe 31/03/2012. Vile vile mnyika ameshindwa kwenda Arumeru kutokana na Kesi ya uchaguzi Inayomkabili, Nguvu zote amezielekeza kwasasa kwenye uchaguzi huu mdogo wa udiwani kutokana na ukaribu wa eneo. Tunawaomba wakazi wote wa vijibweni na wale wote wanaopenda mabadiliko kujiunga na sisi siku ya kesho kwenye kufunga kampeni zetu, ambazo zimekuwa na mafanikio makubwa kuliko chama kingine kinachoshiriki uchaguzi huwo bila kujali itikadi za vyama vyao, waje wasikilize sera na siyo matusi na kejeli, kitu ambacho wamekwisha kionyesha na kuvidharau vyama hivyo.
Vile vile tunapenda kuwaambia wananchi kuwa kwasasa taifa linamsiba mkubwa linahitaji mabadiliko kwa haraka sana na harakati hizo za mabadiliko ni lazima zianze sasa. Katika uchaguzi huu wa udiwani CHADEMA tutashinda kwa zaidi ya 82%. Tunawatakia uchaguzi mwema wenzetu wa Arumeru na kwenye kata mbalimbali zinazorudia uchaguzi mdogo.
AHSANTENI KWA USHIRIKIANO NA ENDELEENI KUSIMAMIA UKWELI BILA KUJALI ITIKADI ZA DINI ZENU, KABILA ZENU, HAKIKA UKWELI UTASHINDI DHULUMA, UKWELI UTASHINDA UONGO, UKWELI HAUJAWAHI KUSHINDWA.
Imetolewa leo Tarehe 30/03/2012 na..
HENRY J KILEWO
KATIBU WA KANDA MAALUM YA DSM
MRATIBU MKUU WA UCHAGUZI MDOGO WA UDIWANI (VIJIBWENI) KIGAMBONI/DSM.
SIMU: 0714 225960