Kobello
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 8,635
- 7,918
Nadhani wewe ndiyo unaekosea.Hapo ndio wananchi tunapokosea. Vema kufuatilia na kujua kazi za Mbunge. Wanaohusika na maji ni DAWASCO na barabara ni Halmashauri (au TANROADS kwa baadhi ya barabara kubwa). Anayetakiwa kuwafuatilia hao ni Mkuu wa Wilaya au Mkurugenzi wa Maendeleo wa Wilaya. Ikishindikana kabisa Mkuu wa Mkoa. Serikali ndio ina nyenzo ya kutatua kero hizo. Kazi ya Mbunge ni kuwawakilisha, kuisimamia serikali, shughuli za bungeni n.k. Mnyika ni Mbunge mzuri, naamini pamoja na kuwa hilo sio jukumu lake lakini akilipata atajitolea kufuatilia.
Mbunge na madiwani/meya ni wawakilishi wa wananchi. Kwa hiyo mwananchi hamkabi DC au RC.... hao hukabwa na PM/Rais.
Sisi tunawakaba madiwani na wabunge. Ma-DC na RC hawatuwakilishi wananchi, wanawakilisha serikali kuu. Sasa kama unataka wananchi tuikabe central government, kuna haja gani ya kuwa na representatives?