Mnyika: Diwani wa Sinza amefanya maajabu ni kama mbingu na ardhi ukilinganisha na aliyekuwepo

PAMBA1

Member
Sep 13, 2011
55
26
DIWANI WA KATA YA SINZA AMEFANYA MAAJABU AMBAYO YANAWEZA KULINGANISHWA NA MBINGU NA ARIDHI KWA MIAKA KUMI ALIYOTUMIKIA DIWANI ALIYEKUWEPO MADALAKANI MZEE SALIM MWAKIN"GINDA.AKIONGEA HAYO JANA KWENYE MKUTANO WA HADHARA ULIOFANYIKA MAENEO YA SINZA B VIWANJA VYA SEVEN UP BAADA YA DIWANI WA KATA YA SINZA KUPANDA JUKWAANI NA KUELEZA ALIYOYAFANYA TANGU ACHAGULIWE.DIWANI ALISEMA AMEKUTA UOZO WOTE UNATAJWA UPO KWENYEKATA YA SINZA AMBAO DIWANI ALIYEKUWEPO ALIKUWA AMEGEUZA KAMA DILI. ILE MILADI YA MAENDELEO ILIYOKUWA INALETWA NA HALMASHAURI YEYE ANAONGEA NA WAKANDALASI WALIOPEWA TENDA YA UTENGENEZAJI WA BARA BARA ZA NDANI WANAKULA DILI BADALA YA KUFATA KILICHOKUWEPO KWENYE BOQ YA UTENGENEZAJI WA BARABARA. YEYE ANALETA GARI LA KUKWANGUA BARABARA TU PEKE YAKE LINAKUJA KUKATA MABOMBA NA KUACHA VUMBI.akienda halmashauri anasema tayari barabara imekamilika kumbe imechakachuliwa pesa anatia mfukoni.akiongea hayo diwani alisema alikuta miradi ya utengenezaji barabara ya lion sinza na ile ya kwa lemi karibu na azania guest alisema amekuta barabara hizo zote zinawakandalasi wawili wawili kitu ambacho ni kinyume na taratibu na achilia mbali barabara hizo hazijaanza kutengenezwa pamoja na kuwa na wakandalasi hao wote.diwani alisema barabara hizo aliweza kusimamia wakandalasi watafutwe na waingie site ili kazi ianze mara moja barabara ziliwekwa kifusi na kuwekwa mtandao wa maji ya mvua ambao diwani aliyekuwepo miaka kumi iliyopita hakuwahi kuyafanya hayo hata kukosea kuweka kifusi kimoja.pamoja na hayo diwani alisema alikuta shule zote za kata ya sinza vyoo vimechakaa akakomaa mpaka sasa vyoo vinajengwa shule zote.pamoja na hayo kamanda ameibua mradi wa kulaza mabomba ya mtandao wa maji machafu SEWEGI. NAZANI MNAFAHAMU SINZA HAINA MTANDAO WA MAJI TAKA.KAULI YA MNYIKA BAABA YA HOTUBA YA DIWANI ALIFANANISHA MAMBO ALIYOYAFANYA DIWANI HUYO LIKIWEMO LA KUWA NA KITUO CHA POLISI STATION KATA YA SINZA NI KAMA MBINGU NA ARIDHI YA YALE ALIYOFANYA DIWANI ALIYEKUWEPO KWA KIPINDI CHA MIAKA KUMI IKILINGANISHWA NA HUYU ALIYEKAA MIEZI TISA SASA.
 
Aisee ile barabara pale kwa remmy pembeni ya azania guest toka mwaka 1996 naiona imejaa maji miaka yote mpaka mwaka huu ndo imekuja tengenezwa miaka yote hiyo huwa inajaa maji tuu ikifika wakati wa uchaguzi greda linapitishwa basi hakuna tena. big up sana diwani wetu.
 
Hivi unaongelea Sinza gani? Ile sinza ya kuungana na kwa Mtogore? Mbona chafu tu mifereji ya maji machafu kila kona.
Naona unampenda sana huyo diwani wa Sinza kwa Mtogore mpikie pilao takuletea na kuku wa kienyeji sawa umkaribishe aje kula
 
hivi barabara anajenga diwani au wananchi?
Barabara zimegawanya katika makundi mawili; Kuu hizi hujengwa na serikali kuu kupitia TANROADS. na zile zile za kawaida ambazo hujengwa na halmashauri. Halmashauri huundwa na madiwani hivyo diwanianashiriki katika kupanga viapumbele na kufuatilia utekelezaji wake.....Hata hivyo sina hakika kama ulikuwa hujui au ulikuwa unaleta kejeli.
 
Mbona miye nipo hapa Sinza Palestina mambo bado hayajakaa sawa?
...Soma vizuri post, barabara zimetajwa hapo juu na palestina haijatajwa sasa ulitaka ikae sawa kivipi? Kama unaishi Sinza, na pita bararaba ya kuanzia pale kwa Remmy Azania Guest, kata na ile inayoenda Sinza Catholic church nenda hadi Lion mpaka kufika ktk Lami pale T garden. Mabadiliko yapo makubwa kwa barabara nyingi za sinza kwa upande wa Sinza C,D na E huku maieneo ya Palestina kama sikosei ni Sinza B na huku Mori, Meeda sinza A hakuna mabadiliko bado
 
Hivi unaongelea Sinza gani? Ile sinza ya kuungana na kwa Mtogore? Mbona chafu tu mifereji ya maji machafu kila kona.
Naona unampenda sana huyo diwani wa Sinza kwa Mtogore mpikie pilao takuletea na kuku wa kienyeji sawa umkaribishe aje kula[/QUOTE

Wewe ungewaacha wanaokaa sinza wakachangia na diwani wao.....dalali wako alikudanganya amekupatia chumba na sebule sinza akakuingiza choo cha kike; Hakuna sinza inayoungana na (Tandale) kwa Mtogole. Huko ni Manzese Uzuri; sinza D, inaishia daraja la mto ng'ombe pale uwanja wa TP
 
Ni kweli huyo diwani amejitahidi kulinganisha na huyo gamba aliyekaa miaka 10. Aongeze bidii.
 
Mwaking'inda ndio diwani aliyepita ,kazi yake akishikiana na fisadi Londa aliyekuwa Meya wa Kinondoni ilikuwa ni wizi tu kama anavyofanya Masaburi kule city!!
 
Hivi unaongelea Sinza gani? Ile sinza ya kuungana na kwa Mtogore? Mbona chafu tu mifereji ya maji machafu kila kona.
Naona unampenda sana huyo diwani wa Sinza kwa Mtogore mpikie pilao takuletea na kuku wa kienyeji sawa umkaribishe aje kula

unajidhalilisha!
 
Hahahaha..lol Diwani wa Sinza amefanya maajabu ni kama mbingu na ardhi ukilinganisha na aliyekuwepo!!!
Hii title imeniacha hoi!!
 
Kwani kwa Mtogole ni Sinza?

Sinza ya huyo Diwani ni ya kwa Mtogole eti wenyewe wanaita Sinza D Sinza uzuri, eneo lote ukitoka kwa bibi nyau mpaka hayo maeneo ya Deluxe hotel ni kwa Mtogole tu
 
Hivi unaongelea Sinza gani? Ile sinza ya kuungana na kwa Mtogore? Mbona chafu tu mifereji ya maji machafu kila kona.
Naona unampenda sana huyo diwani wa Sinza kwa Mtogore mpikie pilao takuletea na kuku wa kienyeji sawa umkaribishe aje kula

Ili kuweka taarifa kwa usahihi, maeneo ya Kwa Mtogole ni kata ya Tandale inayoongozwa na magamba na sio Sinza.
 
Hahahaha..lol Diwani wa Sinza amefanya maajabu ni kama mbingu na ardhi ukilinganisha na aliyekuwepo!!!
Hii title imeniacha hoi!!

Hata Barack Obama, hajawahi kufanya maajabu kama ya diwani wa sinza ya Mbingu na ardhi
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom