MBUNGE wa Ubungo, John Mnyika, amesema haitoshi kwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kuweka ukomo wa kukamilika kwa katiba mpya ifikapo mwaka 2014 ,bila kuweka ratiba ya mchakato wa kupata katiba hiyo.
Amesema wananchi wanapaswa kupokea kwa tahadhari taarifa ya Pinda kwa kuwa alipaswa kuitoa bungeni na si katika mkutano nje ya Bunge.
Mnyika alisema hayo jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, kufuatia kauli ya Waziri Mkuu kwamba katiba mpya itazinduliwa Aprili 26 mwaka 2014.
Pinda alisema hayo juzi wakati akifungua semina ya wakuu wa mikoa, wilaya na makatibu tawala, mjini Dodoma.
"Wananchi wawe makini kuhusu kauli ya Waziri Mkuu Pinda, ameweka ukomo lakini hatoi ratiba ya mchakato, ili wananchi wafahamu wanashiriki vipi,"alisema Mnyika.
Alisema hotuba ya Pinda inaonyesha uwa serikali haina uhakika wa lini muswada wa mapitio ya sheria ya marekebisho ya katiba wa mwaka 2011, utawasilishwa bungeni.
"Ni muhimu ukomo huo ukawasilishwa rasmi bungeni kupitia kauli ya serikali kabla muswada wa sheria utakaozingatia ratiba, mipango , maazimio na sheria, " alisema Mnyika.
Mnyika alisema mwanzoni mwa mwaka huu, aliwasilisha hoja binafsi bungeni, kutaka wananchi kuhusishwa katika mchakato wa katiba kuanzia mwanzoni.
Mbunge huyo alisema Pinda alipaswa kutoa kauli bungeni kueleza bayana kama hati ya dharura ya muswada huo iliyowahi kuwasilishwa na serikali kama ilifutwa, ili muswada mwingine uweze kuwasilishwa kwa kufuata taratibu za kawaida kwa mujibu wa kanuni za Bunge.
"Pia kitendo cha wakuu wa mikoa na wilaya kuelekezwa kusimamia mchakato huo wakati sheria haijapitishwa na Bunge kinaonyesha wazi kuwa serikali tayari ina msimamo wake na inataka kulitumia Bunge kuidhinisha uamuzi wake,"alisema Mnyika.
"ikumbukwe kwamba watendaji wamekuwa wakilalamikiwa kwa kutumia madaraka yao vibaya, leo hao ndio wanapewa nafasi za kusimamia katiba mpya, serikali haina dhamira ya kweli katika suala hili," alisisitiza.
Mbunge huyo wa Ubungo, alisema kati ya mambo ambayo wananchi wameanza kuyatolea maoni kuhusu katika mpya ni kutaka kupunguzwa kwa madaraka ya wakuu wa mikoa na wilaya.
"Hawa wakiwa wasimamizi hawatatenda haki," alisema Mnyika.
by Raymond Kaminyoge
Source: Mnyika apingana na Pinda kuhusu katiba
Amesema wananchi wanapaswa kupokea kwa tahadhari taarifa ya Pinda kwa kuwa alipaswa kuitoa bungeni na si katika mkutano nje ya Bunge.
Mnyika alisema hayo jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, kufuatia kauli ya Waziri Mkuu kwamba katiba mpya itazinduliwa Aprili 26 mwaka 2014.
Pinda alisema hayo juzi wakati akifungua semina ya wakuu wa mikoa, wilaya na makatibu tawala, mjini Dodoma.
"Wananchi wawe makini kuhusu kauli ya Waziri Mkuu Pinda, ameweka ukomo lakini hatoi ratiba ya mchakato, ili wananchi wafahamu wanashiriki vipi,"alisema Mnyika.
Alisema hotuba ya Pinda inaonyesha uwa serikali haina uhakika wa lini muswada wa mapitio ya sheria ya marekebisho ya katiba wa mwaka 2011, utawasilishwa bungeni.
"Ni muhimu ukomo huo ukawasilishwa rasmi bungeni kupitia kauli ya serikali kabla muswada wa sheria utakaozingatia ratiba, mipango , maazimio na sheria, " alisema Mnyika.
Mnyika alisema mwanzoni mwa mwaka huu, aliwasilisha hoja binafsi bungeni, kutaka wananchi kuhusishwa katika mchakato wa katiba kuanzia mwanzoni.
Mbunge huyo alisema Pinda alipaswa kutoa kauli bungeni kueleza bayana kama hati ya dharura ya muswada huo iliyowahi kuwasilishwa na serikali kama ilifutwa, ili muswada mwingine uweze kuwasilishwa kwa kufuata taratibu za kawaida kwa mujibu wa kanuni za Bunge.
"Pia kitendo cha wakuu wa mikoa na wilaya kuelekezwa kusimamia mchakato huo wakati sheria haijapitishwa na Bunge kinaonyesha wazi kuwa serikali tayari ina msimamo wake na inataka kulitumia Bunge kuidhinisha uamuzi wake,"alisema Mnyika.
"ikumbukwe kwamba watendaji wamekuwa wakilalamikiwa kwa kutumia madaraka yao vibaya, leo hao ndio wanapewa nafasi za kusimamia katiba mpya, serikali haina dhamira ya kweli katika suala hili," alisisitiza.
Mbunge huyo wa Ubungo, alisema kati ya mambo ambayo wananchi wameanza kuyatolea maoni kuhusu katika mpya ni kutaka kupunguzwa kwa madaraka ya wakuu wa mikoa na wilaya.
"Hawa wakiwa wasimamizi hawatatenda haki," alisema Mnyika.
by Raymond Kaminyoge
Source: Mnyika apingana na Pinda kuhusu katiba