GeniusBrain
JF-Expert Member
- Nov 3, 2010
- 4,315
- 306
Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA John Mnyika amembana Rais Jakaya Kikwete nyumbani kwake Bagamoyo kuhusu utekelezaji wa ahadi za CCM za maisha bora kwa kila mtanzania, wanawake kuwezeshwa na ajira kwa vijana.
Mnyika alifanya hivyo wakati akimnadi mgombea udiwani kwa tiketi ya CHADEMA katika kata ya Magomeni kwenye halmashauri ya Bagamoyo ambapo alisema kwamba badala ya maisha bora wananchi wana maisha magumu kutokana na kasi ya mfumuko wa bei huku ukosefu wa ajira miongoni mwa vijana wa kike na wa kiume ukizidi kuongezeka.
Mnyika amewaomba wananchi kuchagua CHADEMA ili kazi ya kupambana na ufisadi na kutetea rasilimali za taifa kwa sera mbadala iendelee katika halmashauri hiyo ya Bagamoyo yenye tuhuma mbalimbali ambayo madiwani wake wote ni wa CCM.
Mara baada ya mkutano huo wananchi walimsindikiza Mnyika kwa miguu toka kata hiyo ya Magomeni mpaka ofisi za chama hicho za wilaya umbali mrefu kutoka mkutano uliopita ambapo mratibu wa kampeni za CHADEMA katika kata hiyo alitahadharisha rushwa iliyoanza kusambazwa na CCM katika kata hiyo.
serayamajimbo
Kasi ya mfumuko wa bei anao usema mnyika ni upi ? mfumuko wa bei umetoka 19% mpaka sasa 13% , kasi hiyo iko wapi? au yeye hesabu zake anahesabu kinyume nyume? kijana mnyika acha kujitafutia umaarufu wa kisiasa kwa cheap politics