Mnigeria Ayobola Abiola ameweza vipi kuongoza Benki Tanzania?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Ni swali ambalo nilitaka kuliuliza a while ago lakini naona huu ni wakati muafaka. Labda swali liulizwe kwanza kabisa yeye ni nani?

Nashauri watu wa-google na ku-yahoo jina hilo na kujionea wenyewe halafu turudi kulijibu hili swali.
 
Historia haionyeshi sifa nzuri ya watu kutoka taifa ili kuna cases nyingi siyo wote wabaya don't get me wrong but majority duh! hivyo ni muhimu watu kuwa aware na hii bank kabla maafa hayajawafika, mwisho itakuwa kilio.
 
Nina ushahidi kutoka Deloit n'touch walioufanya baada ya kuombwa na BOT (due delegence). Waka waandikia BOT kitengo cha Banking supervision kuwa huyu jamaa hafai, BOT wakishirikiana na wakubwa wakageuza report kuwa jamaa ana faa na kuanzisha bank.

Swali tu ni kuwa bank hio inatumia majengo ya nani na kwa nini?
 
Tanzania sasa imekuwa kichaka cha Mafraud Duniani, Mimi Lawama zangu nazielekeza 1. Usalama Wa Taifa 2. Immigration na Police na 3. BoT na uongozi wake wote. Huu Ufisadi wa kutojali Nchi utaifikisha nchi pabaya zaidi kuliko hapa tulipo.
 
Du kazi kweli kweli BoT wanajua wanahatarisha sana sekta ya fedha ku deal na abiola?pesa chafu na kuzisafisha ndio zitakuwa deal zake
 
Ni swali ambalo nilitaka kuliuliza a while ago lakini naona huu ni wakati muafaka. Labda swali liulizwe kwanza kabisa yeye ni nani?

Nashauri watu wa-google na ku-yahoo jina hilo na kujionea wenyewe halafu turudi kulijibu hili swali.
Mzee Mwanakijiji, kwani Tanzania tunafanya due diligence?. Everything is possible.

Niliomba kajikazi fulani kwa wenzetu, kabla sijakubaliwa wakachukua details zangu zote mpaka biometric na kunicheki, japo nilikuwa cleared wakaniita tena na kutaka maelezo ya mambo fulani ya ajabu yaliyonitokea zamani, nikashangaa!, wenzetu wana details za kila kitu na wana keep records hakuna mfano!.

Ubalozi wa Uingereza huwa una despose properties zake nchini kidogo kidogo, properties hizo ziko kwenye prime area. Kuna tajiri mmoja, anaheshimika sana hapa nyumbani, alishinda bid ya kununua Kasri la Hammaton House alilokuia akiishi Gavana wa UK Zanzibar, next to nyumba ya Karume. Jamaa alikataliwa kuuziwa, kisa baada ya kushinda, walifanya due diligence, wakakuta not all his money ni clean money, wakamkatalia kata kata licha ya kutoa offer kubwa!.

Kama mimi tuu na wewe, tumeweza ku google na kuona madudu ya Ayobola Abiola, haiwezekani BOT hawakuyajua haya, wanajua kila kitu!. Maadamu UBA ni benki yao, mambo yao yanajulikana. Kwa sasa tuna benki 6 zenye Nigerian connection nchini na hata sijui sisi tuna biashara gani kubwa kihivyo na Naigeria hadi zilete benki zao!.

Ama kweli Tanzania ni shamba la bibi, kila mtu kujivunia na kujiondokea!
 
Kukishakuwa na utata juu ya mtu inatakiwa arudishwe kwao maana sekta aliyoshika ni nyeti sana.
Hii ni hatari sana...
 
Kuna tajili mmoja wa kinijeria ambae anasifika kwa utajili wake duniani anaitwa Angote, huyu bwana anakuja fungua kiwanda cha cement huko mikoa ya kusini kwa wakina Anna Abdalla hivyo amewawekea sharti kuwa awe na benki yake ya kupitishia madudu yake wakati akifanya biashara Tanzania!! Gavana wa BOT ni mgonjwa hawezi kusimamia majukumu yake sawa sawa na ndio maana akiulizwa habari hujibu kuwa kuna mtu maalum anayeshuhulikia jambo husika!! You are supposed to be on top of things buddy!!! Kuwachunguza watendaji wakuu wa benki ni moja kati ya kazi muhimu za directorate ya BANK SUPERVISION; yasije yakajirudia yale ya Meridian Biao Bank na Greenland bank enzi za FISADI Idris Rashid
 
Kwa kweli hapa usalama wa taifa mmetuangusaha sana jamani. Hivi hadi haya yote yanatendeka mnakuwa wapi wandugu. Ongezeni juhudi vinginevyo nchi yetu itakuwa kwenye hatari sana. Kataeni kufuatilia mambo ya siasa ili mjikite zaidi kwenye usalama wa taifa letu. Hapa tunawategemea sana jamani. Mambo ya siasa waachieni hao hao wanasiasa msiwatumikie hata kidogo. Wakimbieni na muwakatae kama ukoma.
 
Nyie waswahili mna hulka na mawazo ya kitumwa, huyu jamaa angekuwa mzungu au kaburu msingelalamika mbona benki zenu zote zimechukuliwa na makaburu?.Wanaijeria wanajua sana banking na wana utajiri, angalia banki zao za kimataifa kama zenith bank, UBA etc Tanzania hatuwezi kuwafikia. In 7 years GDP ya nigeria itazidi south afrika.

Grow up guys!
 
Guys, guys, guys.

This is bigger than what you think.

i rember there was a post on this guy something like 12 days ago.

I did post my comment and wont hasitate to share a bit of what i said.

Do you know this bank very well??

Do you know who is banking with them??

Do you know how the MD got is DD (Due dilligence) cleared??

Well take this, the Chairman of the board of this bank is the former CDF,

going by the name Mboma.
 
mbona inaonekana kama mmiliki wa kiwanda cha saruji huko kusini ni mchina? au ndo kujificha manake wachina tunawakubali manake ni wazaramo waliohamia huko kwenye baridi wakatakata ngozi
Kuna tajili mmoja wa kinijeria ambae anasifika kwa utajili wake duniani anaitwa Angote, huyu bwana anakuja fungua kiwanda cha cement huko mikoa ya kusini kwa wakina Anna Abdalla hivyo amewawekea sharti kuwa awe na benki yake ya kupitishia madudu yake wakati akifanya biashara Tanzania!! Gavana wa BOT ni mgonjwa hawezi kusimamia majukumu yake sawa sawa na ndio maana akiulizwa habari hujibu kuwa kuna mtu maalum anayeshuhulikia jambo husika!! You are supposed to be on top of things buddy!!! Kuwachunguza watendaji wakuu wa benki ni moja kati ya kazi muhimu za directorate ya BANK SUPERVISION; yasije yakajirudia yale ya Meridian Biao Bank na Greenland bank enzi za FISADI Idris Rashid
 
Nyie waswahili mna hulka na mawazo ya kitumwa, huyu jamaa angekuwa mzungu au kaburu msingelalamika mbona benki zenu zote zimechukuliwa na makaburu?.Wanaijeria wanajua sana banking na wana utajiri, angalia banki zao za kimataifa kama zenith bank, UBA etc Tanzania hatuwezi kuwafikia. In 7 years GDP ya nigeria itazidi south afrika.

Grow up guys!


Hapo ndo umefikiria mwenyewe? Kwasababu GDP yao, according to you, imeizidi ya South Africa ndo aruhusiwe kufanya kazi nchini hata kama ana rekodi mbaya?
Hapa ameongelewa mtu mwenye rekodi inayomstahili kuwa jela! Nakushauri kula ushibe,pata haja. Pumzika kisha ufikirie tena. Sitaki kusema umetumia....... kufikiria kama alivyosema Mstahiki Meya fulani.
 
Nyie waswahili mna hulka na mawazo ya kitumwa, huyu jamaa angekuwa mzungu au kaburu msingelalamika mbona benki zenu zote zimechukuliwa na makaburu?.Wanaijeria wanajua sana banking na wana utajiri, angalia banki zao za kimataifa kama zenith bank, UBA etc Tanzania hatuwezi kuwafikia. In 7 years GDP ya nigeria itazidi south afrika.

Grow up guys!
Nadhani wewe ndiye unayehitaji ku grow up.
 
Back
Top Bottom