Mnautaka muunganoooo...Hautuutaki!!!

Na kuna wazenji wanaoshabikia kuvunjwa muungano ilhali hata hawajui walioko nyuma ya akina Farid, wamemezeshwa maneno wanayatema bila hata kujua nini dhamira ya dhati nyuma yake

.....waacheni waende............
 
Mimi kwa kweli sijaiona faida ya muungano huo unaoliliwa sana. Zanzibar hasa ndio wenye faida nao zaidi lakini ndio wa kwanza kulalamikia. Kila kijiji in equivalence to Bara kina mbunge, nyadhifa nyingi katika muungano huo wazanzibar wanabebwa sana sababu za kisiasa tu ati kuimarisha muungano. Hapa Bara wazanzibar wamejitwalia ardhi kedekede na vitegauchumi lukuki vinamilikiwa na wao na hatuwasemi tunajua ni wenzetu, lakini nenda Zanzibar kama utaruhusiwa hata kuweka kibadna cha miti kuuza nyanya!!!! Bado mimi naamini usalama wetu Tanganyika ni pale tutakapoachana na Zanzibar tusipigiwe makelele hayo nao wazanzibar wote warudi kwao watuachie bara yetu, hapo ndo watajua kwamba wanafanya makosa kula na kipofu kwa kumpigapiga mikono yake kwenye sahani. Tunavumilia kuwaenzi kina Nyerere tu, Mtikila yuko sahihi saa zote na viongozi wa serikali wanakubaliana naye isipokuwa ni waoga kuchukuwa maamuzi magumu. Zanzibar haitadumu nje ya muungano, wanabwabwaja sana kwa sababu wanalindwa chini ya muungano.
 
jamani naomba muangalie hali halisi ya mtanganyika anaeishi zanzibar kwa sasa hali anayokabiliana nayo ndio utaweza kufanya tathmini ya umuhimu wa muungano.
1.uchomwaji wa maeneo ya biashara mf.baa na maduka ya curio craft. mengi ya maeneo haya yanamilikiwa na watu wa bara.hakuna sehemu iliyochomwa ambayo inamilikiwa na mwenyeji.
2.uchunguzi na uendeshaji wa kesi hizo hadi sasa haueleweki, kwa maana hiyo smz inafahamu kinachoendelea,ila kinachowashinda ni kutamka hadharani,
3.ubaguzi upo wazi wa mtu wa bara,kila kona ya visiwani na hilo lipo wazi.
nadhani wanaoufaidi muungano ni wao zaidi ni wazanzibar.ila hilo hawalioni maana ulichonacho mkononi unakiona hakina thamani ila kikitoweka utaona umuhimu wake.
na kama mmechunguza wanzazibar wengi wanaoishi bara hili suala hili la muungano hawathubutu kamwe kuliongelea maana wanatambua dhahiri athari watakayoipata
 
mimi kila siku najiuliza kwanini bara isiiache zenj na siku tukitengana kila mtu arudi kwao yani wazenj warudi kwao na watanganyika warudi bara kila mtu abake na chake ili baada ya miaka michache tuone nani kapoteza maana you never miss a good thing till its gone ........
 
Mi naona suluhusho pekee ni kuinyima kura CCM, maana wao ndo wanaoukumbatia huu muungano usiyo na tija kwa pande zote mbili.
 
Huyo sheikh alitakiwa aongezewe kesi mpya hapohapo...kuhamasisha wapenzi wake kuuchukia Muungano huku akijua wazi kuwa yuko chini ya ulinzi.

hayo uyasemayo ingekua enzi ya NYERERE ni kizuizini 1:-X.1 bila mjadala lakini dunia imebadilika baba.
 
Waliokuwa wakijibu ni kikundi kidogo cha akina mama ambao hawawezi kuwakilisha maoni ya Wazanzibari wote, iitishwe kura ya maoni upande wa Zanzibar na Tanganyika ili tuweze kufikia maamuzi ya haki.

kwa wazanzibari hicho kikundi kidogo haswa WANAWAKE ogopasana kuliko kundi kubwa la WANAUME hiyo ni ZANZIBAR sio ....ZANZIBARA...ukiona mpaka wanawake wanaongea mbere ya POLICE kuna neno kubwa hapo lolote naliwe...
 
Nyuma ya kina Farid, wako wazanzibar, hata hivyo ni bora kutawaliwa
na YEMEN au OMAN kuliko Tanganyika.

kwani hamkuisikia kauli ya Rais mstafu wa ZANZIBAR.. Amani Karumee?? yeye alisema wale wanao pinga Muungano wasitwe majina ya ajabu etu amehoji Mungano ile kauli ina maana Kubwa ndani yake kwahiyo muungano kwa jumla wa Zanzibar hawautaki...
 
Kwani kuukataa Muungano ni dhambi au kosa kisheria?

Nyuma ya kina Farid, wako wazanzibar, hata hivyo ni bora kutawaliwa
na YEMEN au OMAN kuliko Tanganyika.
Mkuu Vijisenti tambua kuwa makosa mengi ya kisheria ni dhambi. Na ishu ya kutawaliwa na Waarabu wenzao ni kutawaliwa au kuifanya nchi ni ya kiarabu. Na ndio maana nimesikia Zanzibar ni daraja muhimu la mahusiano ya Tanzannia na Omani...... Vile vile kama mnapenda kutawaliwa na Oman mnakuja Tanganyika kufanya nini si mngeenda Oman.
 
Last edited by a moderator:
wanafiki wazanzibar wao wanajua tatizo ni ccm lakini bado tu. Aliyewasemea Dom wanazidi kumuona mbaya
 
Nyuma ya kina Farid, wako wazanzibar, hata hivyo ni bora kutawaliwa
na YEMEN au OMAN kuliko Tanganyika.
Hapo ulipokuwa umejifunika umejifunua bila kujua. Kwa akili hiyo ya mental slave hamtafanikiwa maana agenda yenu iko wazi.
 
Mimi kwa kweli sijaiona faida ya muungano huo unaoliliwa sana. Zanzibar hasa ndio wenye faida nao zaidi lakini ndio wa kwanza kulalamikia. Kila kijiji in equivalence to Bara kina mbunge, nyadhifa nyingi katika muungano huo wazanzibar wanabebwa sana sababu za kisiasa tu ati kuimarisha muungano. Hapa Bara wazanzibar wamejitwalia ardhi kedekede na vitegauchumi lukuki vinamilikiwa na wao na hatuwasemi tunajua ni wenzetu, lakini nenda Zanzibar kama utaruhusiwa hata kuweka kibadna cha miti kuuza nyanya!!!! Bado mimi naamini usalama wetu Tanganyika ni pale tutakapoachana na Zanzibar tusipigiwe makelele hayo nao wazanzibar wote warudi kwao watuachie bara yetu, hapo ndo watajua kwamba wanafanya makosa kula na kipofu kwa kumpigapiga mikono yake kwenye sahani. Tunavumilia kuwaenzi kina Nyerere tu, Mtikila yuko sahihi saa zote na viongozi wa serikali wanakubaliana naye isipokuwa ni waoga kuchukuwa maamuzi magumu. Zanzibar haitadumu nje ya muungano, wanabwabwaja sana kwa sababu wanalindwa chini ya muungano.

No ! Itadumu, mbona rwanda burundi zimedumu na hazikuungana na taifa lolote. Fikra za kijamaa haziwezi kuendelea kudumu. Muungano huu unalindwa tu tamaa za watawala kupenda kuwatawala watu wengi zaidi. Ila zanzibar bila tanganyika inawezekana bila shaka yoyote. Muungano ambao kuungana kwake kumefanyika kijanjajanja hauna vielelezo vya kujitosheleza kisheria. Inatosha sasa tuishi kwa fikra na manufaa ya waliohai aliyepita aliondoka na mawazo yake ! katiba mpya yatosha kuuvunja muungano
 
Muumngano wa Tanzani ni wa muhimu sana na uendelee kuwapo. Isipokuwa kama utata huu unaoibuliwa na wazanzibari ni wa ama
1, Tuwe na muungano wa mkataba au
2. Muungano hatuutaki au
3. Muungano uwe na mipaka
na mengine mengi sana.
Hakuna ulazima wa muungano wa Tanzania ni bora kila mtu arudi kwao kimyakimya.
Tusibembelezane.
Ni vizuri tuwe na nia njema tu.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom