Uchaguzi 2020 Mnataka tuendelee kuwa na Rais wa miundombinu? Ingekuwa miundombinu ndiyo kipaumbele cha mtu wachina wasingekamatwa kwenye makontena wakizamia Ulaya

CreativityCode

Senior Member
Aug 8, 2020
158
653
Huyu mgombea ambaye ndiye Rais amalizaye muda wake na anaomba tena watanzania wampe tena miaka mingine 5 ili aendeleze kipaumbele chake kwenye kununua ndege, kujenga madaraja, kujenga reli, kujenga viwanja vya ndege na yanayofanana na hayo.

Lakini hebu tujiulize ameyafanya hayo miaka yote 5, Je! Mtanzania wa kawaida anayependa kumuita mnyonge amenufaika na nini? zaidi ya kushuhudia ugumu wa maisha kila kukicha?

Rais ambaye unapotaja maendeleo yeye akilini mwake huja flyover, madaraja, reli na midege huyu hatufai.

Rais amabye unapotaja kuboresha afya yeye akilini mwake huja majengo anayoyaita hospitali bila kuangalia soft elements ambazo ndiyo muhimu mfano idadi ya madaktari wanaolipwa vizuri, madawa na vifaa vya matibabu.

Nawakumbusha watanzania kuwa kwa sasa hakuna nchi yenye miundombinu ya kustaajabisha mfano wa flyovers, madaraja, reli duniani kama China lakini raia wake kila kukicha wanazamia kuja Ulaya, kila siku wanakamatwa kwenye makontena. Ukiwauliza tatizo nini ukiwa unafahamu kuwa China ni nchi tajiri kimiundombinu, watakwambia wanahitaji maisha bora na uhuru.

Sasa huyu kila siku yeye anasema anataka kuifanya Tanzania iwe kama Ulaya sijui anajua China iko Ulaya? ni bora angekuwa anasema anataka kuifanya Tanzania kuwa kama China (kitu amabacho nacho hawezi) tungekubaliana naye lakini kwa ubora wa maisha amekwishafeli.

NI WAKATI SASA WANANCHI KUCHAGUA IKIWA MNATAKA RAIS AMBAYE ATAJENGA MIUNDOMBINU AKIBORESHA MAISHA YENU PIA, AU RAIS AMBAYE KWAKE YEYE MAENDELEO NI MIUNDOMBINU PEKEE BILA KUBORESHA MAISHA HALISI YA MWANANCHI NA KUMPATIA UHURU WAKE.

Ni wakati wa kuchagua Tundu Lissu ili ujengewe miundombinu huku maisha yako na uhuru vikiboreshwa ama John Magufuli ambaye tafsiri ya maendeleo kwake yeye ni ujenzi pekee huku akiminya haki za binadamu na kufuta uhuru wa kujieleza.

Jioni njema
 
Kilipofikia chama pendwa kwa sasa!
Egmtp-WWoAE_XGt.jpg
 
"...Wanadamu wapo wenye kashukuru, na wapo wasioshukuru.
Wapo walionufaika kwa hayo wewe unaona yasiyomana.... Ndomana nasema , Hata Mungu kwa wema wake na vyote vizuri alivyoviumba, kuna manyumbu Bado yanamuona hafai."
Unashikuru Nini? Unashukuru kwa kupewa haki yako?
 
Ulitaka serikali ifanye nn labda zaidi ya kuweka miundombinu wezeshi na rafiki ili wananchi wapate wepesi katika shughuli zao??, je hizo hospital zinajengwa na kuachwa tu bila watu na vitendea kazi??? Je ni kweli kwamba serikali imejikita kwenye hivyo vitu tu ulivyovitaja na huku kwenye sekta nyingine hakuna kinachaendelea? People are free to move, to talk and express their feelings and ideas, to worship, vote and being voted, je unataka uhuru gani? Kama unafikiri uhuru ni kutukana au kuvunjia heshima mtu au kikundi cha watu hauko sahihi mkuu, by nature hakuna total freedom, kila kitu kina mipaka. Ukivuka mipaka tu Lazima ukumbane na sheria
 
Kusema hakuna nchi yenye miundombinu kama China ni unadanganya au kutokujua!

Tatizo la China ni Labour market ni cheap. Lakini ndiyo imechangia kuifikisha China hapo ilipo. Kuwa nchi ya pili kiuchumi kuacha USA! M Chinese akifanya kazi Europe au USA ata earn more zaidi ya akifanya kazi hiyo hiyo china!!
 
Jitu linajifanya kushabikia sijui ndege sijui maendeleo ya madaraja wakati ndege hajawahi panda na wala hana gari la kupitisha katika hilo daraja.
Harafu yeye choka mbaya mnyonge anajiita
kila aliyefanikiwa anamuona mwizi na freemason.
kama mkichagua tena mkapimwe akili maana mtakuwa mnamatatizo.
 
Jitu linajifanya kushabikia sijui ndege sijui maendeleo ya madaraja wakati ndege hajawahi panda na wala hana gari la kupitisha katika hilo daraja.
Harafu yeye choka mbaya mnyonge anajiita
kila aliyefanikiwa anamuona mwizi na freemason.
kama mkichagua tena mkapimwe akili maana mtakuwa mnamatatizo.
Unachotaka ni serikali ifanyeje sasa, au kipi kinapaswa kufanyika serikali ionekane bora
 
Back
Top Bottom